27/05/2026
Inukeni, mkafyeke miti, mkajenge nyumba hii, nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana." Hagai 1:8
Tarehe 30/05/2026 ni Sabato Maalumu ya Majengo! Tunakukaribisha kwa upendo mwingi kuja kujumuika nasi katika ibada hii ya kipekee. Tukutane tukiwa na mioyo ya utayari kusikiliza neno la Mungu, lakini pia kuweka mbegu itakayozaa baraka maishani kwa kuchangia ujenzi wa nyumba ya Bwana.
Baraka za Mungu zinatusubiri tunapochangia kazi yake. Karibu sana, mwalike na mwingine!