Kivule SDA Church

Kivule SDA Church Karibu Mpendwa! Huu ni ukurasa rasmi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Kivule - Dar es salaam

Inukeni, mkafyeke miti, mkajenge nyumba hii, nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana." Hagai 1:8Tarehe 30/05/20...
27/05/2026

Inukeni, mkafyeke miti, mkajenge nyumba hii, nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana." Hagai 1:8

Tarehe 30/05/2026 ni Sabato Maalumu ya Majengo! Tunakukaribisha kwa upendo mwingi kuja kujumuika nasi katika ibada hii ya kipekee. Tukutane tukiwa na mioyo ya utayari kusikiliza neno la Mungu, lakini pia kuweka mbegu itakayozaa baraka maishani kwa kuchangia ujenzi wa nyumba ya Bwana.

Baraka za Mungu zinatusubiri tunapochangia kazi yake. Karibu sana, mwalike na mwingine!

Inapendeza k**a nini kuona mkono wa Bwana ukituma watumishi wake! Tarehe 09 May,2026, itakuwa Sabato ya pekee kwetu k**a...
06/05/2026

Inapendeza k**a nini kuona mkono wa Bwana ukituma watumishi wake! Tarehe 09 May,2026, itakuwa Sabato ya pekee kwetu k**a familia ya Waadventista Wasabato Kivule tunapomuaga mpendwa wetu, Mchungaji James Kibiti.

Tunamshukuru Mungu kwa muda aliombatana nasi k**a mshiriki, na sasa tunamkabidhi mikononi mwa Bwana anapoenda kuchunga kundi la kondoo wa Mungu.

Katika Sabato hii, tutatafakari somo lenye nguvu: "Tumaini Katikati ya Ukimya Mzito" Hata katika nyakati ambazo hatuoni hatua za Mungu waziwazi, Yeye bado yupo kazini.

Karibuni sote tujumuike kumuombea na kumpa heri katika utumishi wake mpya.

Habari mpendwa! Kanisa la Waadventista wa Sabato Kivule linapenda kukualika katika mfululizo wa mikutano ya injili inayo...
30/03/2026

Habari mpendwa! Kanisa la Waadventista wa Sabato Kivule linapenda kukualika katika mfululizo wa mikutano ya injili inayofanyika hapa Kivule, Matemebele ya pili. Neno kuu ni "Uwe Tayari, Yesu Anakuja Tena."

Ni wakati wa kufarijiwa na kupata matumaini mapya katikati ya changamoto za dunia. Njoo tusikie ujumbe huu wa pekee utakaobadilisha maisha yako

πŸ“Mahali: Kivule, Matembele Ya Pili
⏰ Muda: Kila saa 9:00 Alasiri - Saa 12:00 Jioni
πŸ“† Tarehe 28/03 - 11/04, 2026

Karibu sana, umwalike na mwenzako!πŸ™πŸ½

Kuwa na rafiki mwema ni utajiri, lakini kuwakutanisha marafiki zako na rafiki wa kweli ni baraka isiyo kifani.Tunakukari...
25/02/2026

Kuwa na rafiki mwema ni utajiri, lakini kuwakutanisha marafiki zako na rafiki wa kweli ni baraka isiyo kifani.

Tunakukaribisha katika Sabato ya Wageni na Marafiki hapa Kanisa la Waadventista wa Sabato - Kivule. Njoo tujionee utajiri wa urafiki wa Yesu Kristo kwa pamoja. Tunakusubiri Jumamosi hii!!

"Ushindi Ni Hakika" ni kichwa cha hubiri ya Sabato hii. Kanisa la Waadventista Wasabato Kivule tunakualika katika Ibada ...
03/10/2025

"Ushindi Ni Hakika" ni kichwa cha hubiri ya Sabato hii. Kanisa la Waadventista Wasabato Kivule tunakualika katika Ibada ya Sabato Tarehe 04/10/2025, tushiriki pamoja na mibaraka tele toka kwa Muumba wetu
Alika jirani, rafiki, ndugu na jamaa tushiriki pamoja Ibada ya Sabato, pia tutakuwa live kupitia akaunti yetu ya Youtube. Karibu sana!


Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliyowapa ninyi, ya kwamba Bwana Yesu usiku ule aliotolewa, alitwaa mkate. (1 Wakori...
26/09/2025

Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliyowapa ninyi, ya kwamba Bwana Yesu usiku ule aliotolewa, alitwaa mkate. (1 Wakorintho 11:23)
Kanisa la Waadventista Wasabato Kivule tunakuwaalika kwa moyo mkunjufu katika ibada ya sabato ya meza ya Bwana, tushiriki pamoja kwa maombi na tafakari.

Karibu katika Ibada ya Sabato kesho katika Kanisa la Waadventista wa Sabato Kivule. Mungu wetu amepanga baraka kwaajili ...
19/09/2025

Karibu katika Ibada ya Sabato kesho katika Kanisa la Waadventista wa Sabato Kivule. Mungu wetu amepanga baraka kwaajili yetu sote.


Moto unaowaka , ukumbusho wa uwepo wa Mungu. Katika kumjua yeye kuna amani kamilifu. "Utanijulisha njia ya uzima; Mbele ...
23/05/2025

Moto unaowaka , ukumbusho wa uwepo wa Mungu. Katika kumjua yeye kuna amani kamilifu. "Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako ziko furaha tele; Na katika mkono wako wa kuume Mna mema ya milele" (Zaburi 16:11)

Furaha yangu ni kumjua Bwana. Kanisa la Waadventista wa Sabato Kivule tunakualika siku ya kesho baada ya Sabato kuungana na vijana mtaa wa Kivule kushiriki pamoja Kambi ya moto tukifurahia uzoefu wa kumjua Bwana. Nyote mnakaribishwa!!


Mahubiri ya Vijana: "Furaha yangu ni kumjua Bwana"Jiunge nasi Mei hii kwa mfululizo wa Mahubiri ya Vijana yasiyosahaulik...
02/05/2025

Mahubiri ya Vijana: "Furaha yangu ni kumjua Bwana"

Jiunge nasi Mei hii kwa mfululizo wa Mahubiri ya Vijana yasiyosahaulika yenye mada kuu "Furaha yangu ni kumjua Bwana" kuanzia Tarehe 10-31 Mei, 2025, saa 10 kamili jioni mpaka saa 12 jioni, tutachunguza maana halisi ya kupata furaha katika kumjua Mungu kwa undani, kibinafsi, na kwa ukaribu.

Katika ulimwengu uliojaa maasi, mfululizo huu utatukumbusha kwamba furaha yetu kuu inatokana na kuelewa na kuona upendo wa Mungu, uwepo wake, na kusudi lake kwa maisha yetu. Kupitia jumbe za kutia moyo, ibada ya dhati, na nyakati za kutafakari, tutagundua jinsi kumjua Bwana kunaleta utimilifu wa kweli, amani, na nguvu.

Huu ni mwaliko wa kuimarisha uhusiano wako na Kristo, kupata furaha katika ukweli wake, na kuwezeshwa kuishi kwa ujasiri kwa ajili yake. Alika marafiki zako, na ujitayarishe kwa mabadiliko katika maisha yako.

Tia alama kwenye kalenda yako - Mei 10-31, 2025!!




An evening where melodies become prayers and voices rise in unity. We at Kivule SDA Church invite you this Friday to joi...
24/04/2025

An evening where melodies become prayers and voices rise in unity.

We at Kivule SDA Church invite you this Friday to join us as we lift our heart and hands, guiding one another closer to the presence of God through powerful praise and heartfelt worship

Address

KIVULE SDA CHURCH
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kivule SDA Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share