10/08/2026
**UJUMBE WA SHUKRANI**
**“Bwana ndiye aliyekuwa upande wetu; mioyo yetu inasema: Asante.”**
Ndugu, jamaa, marafiki, waumini na wadau mbalimbali,
Kwa unyenyekevu mkubwa, tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja wenu aliyesimama nasi katika kipindi hiki kigumu cha majonzi kufuatia ajali iliyosababisha kuondokewa na ndugu zetu na kuwaacha wengine wakiwa majeruhi.
Tunatambua kwamba maneno hayawezi kutosha kueleza namna tunavyothamini upendo, faraja, mshikamano na msaada mlioendelea kutupatia. Katika wakati ambao mioyo yetu ilikuwa imejaa huzuni na maswali mengi, uwepo wenu, sala zenu, salamu za pole, michango yenu na msaada wenu wa aina mbalimbali vimetupa nguvu na kutukumbusha kwamba hatuko peke yetu.
Kwa namna ya pekee, tunatoa shukrani kwa Taasisi mbalimbali za Serikali kwa ushirikiano, uratibu na huduma mlizotoa katika kipindi hiki cha majonzi na katika kushughulikia madhara yaliyotokana na ajali hiyo.
*ASANTENI SANA KWA UPENDO WENU, FARAJA YENU, MAOMBI YENU NA MSHIKAMANO WENU.*