02/01/2022
Kila unacho hitaji kipo tayari tokea mwanzo Mungu Alisha kuungamanisha nacho.kama ni uhai wako Roho wa Mungu anaishi ndani yako.soma Mw 2:7.Kama ni mahitaji yako ya kila siku.Soma Mw 1:29.Kama ni kumiliki na kutawala,vipotayali maana kwa kusudi Hilo uliumbwa.Soma Mw 1:26.Kama ni baraka Alisha kubariki.Soma Mw 1:28.Waefeso.1:3-5.Kama ni magonjwa amesema hatatia magonjwa juu yako.Soma kut.15:26.kut.23:25-26.Kama ni Adui.Mungu amesema atakuwa adui wa adui zako.kut.23:22.Kama ni vikwazo Mungu anasema uwe hodari na moyo wa ushujaa,usiogope Wala usihofu;kwa maana Bwana Mungu wako,yeye ndie anaye kwenda pamoja Nawe,hatakupungukia Wala hatakuacha.Soma kumb.31:6Kama ni kushindana Hakuna wa kukushinda.Soma.Joshua.1:5.Kama ni uchawi wewe huna wa kukuloga.Soma Hesabu.23:23(Kuanzia leo Nataka utambue Jambo Hili yakwamba Mateso na Maumivu yote unayoyapitia Adui yako siyo shetani Wala siyo Mungu;Bali ni (Akili yako mwenyewe)Nakuombea kwa Jina la Yesu Kristo Akili yako ifunguke ili upate kufanya maamuzi sahihi.maana Aina ya Maisha unayotaka kuishi yako ndani ya Maamuzi yako.Fanya uchaguzi sawasawa Hakika utashinda.Soma kumb.30:19-20.kumb.11:26-28.Na
Nakutabiria mafanikio makubwa mwaka2022.Nakupenda Mungu wangu akubariki.