27/03/2026
*MAKAVAZI YA USHUHUDA NA SHUHUDA ZA BWANA NI URITHI WETU NA VIZAZI VYETU. [ZAB 119:111]*
*"UJUMBE WETU, UHURU WETU NA VIZAZI VYETU."*
_"...tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru..."[Yn 8:32 SUV]_
Shalom Taifa la Kweli ya Kristo Yesu iliyofunuliwa kwetu na Roho Mtakatifu katika Ujumbe wa Uana na Ufalme wa Mungu tulionao. Hongereni nyote kwa kuendelea kudumu katika Kweli hii huku mkiendelea kutafiti ndani yake kila siku.
Ninapenda kumshuhudia Mungu Baba kwenu kwa ajili ya Ujumbe wa Uana na Ufalme wa Mungu wa Taifa la Bwana Pete ya Muhuri jinsi ambavyo kupitia Ufahamu wa Ujumbe huu umekuwa hifadhi yangu na uzao wangu na vizazi vyangu dhidi ya kila hila, uongo na uharibifu wowote. Ujumbe huu umekuwa ulinzi na usalama kwangu na vizazi vyangu vyote. Ujumbe huu umekuwa Wokovu hata katika nyumba ya Baba na mama yangu wa kimwili. Ujumbe huu umekuwa uhuru wetu ndani ya Kristo hata kutufanya kuwa wanufaika wa Baraka zote zilizo katika Ujumbe huu. Ujumbe huu ambao ni mafanikio na ustawi wetu kwa vizazi hata vizazi.
Ninakumbuka katika Ibada ya tarehe 8/3/2026 Bwana Mwenyewe alimtumia Mwana na Urithi wake kutuongoza ombi hili;
*"kumshukuru Yeye (Mungu Baba) kwa ajili ya Kweli yake (Ujumbe wa Uana na Ufalme wa Mungu) ambayo ni ulinzi na usalama na hifadhi yetu dhidi ya kila uongo, hila na uharibifu, udanganyifu. Kweli ambayo imetufanikisha, imetustawisha, imetuinua."*
Hakika baada ya ombi hili siku tano mbele yaani 13/3/2026, Bwana alinifunulia jinsi ambavyo kupitia Kweli hii (Ujumbe wa Uana na Ufalme wa Mungu) amekomesha uzao wote wa hila, uongo na uharibifu vilivyokuwapo kabla yangu katika familia ya kimwili na sasa ameanza rasmi kizazi chake kipya na mimi. Kizazi cha Wana wa Mkono wa Kuume wa BABA ambao ni waendelezaji wa Maono ya Ufalme wa Mungu Baba hapa duniani.
Ama kwa hakika, mimi na uzao wangu wote na vizazi vyangu vyote tunaungana na Watakatifu wote Mbinguni na duniani kusema ya kwamba tumekombolewa na kuwekwa huru na Kristo milele!
Shalom!
Na,
Mwana wa Mungu,
Taifa la Bwana Pete ya Muhuri (Hag 2:23),
Dar es salaam, Tanzania.
@2026.