Adventist Hope

Adventist Hope Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Adventist Hope, Seventh Day Adventist Church, Dar es salaam, Dar es Salaam.

Huu ni ukurasa maalumu wa Adventist hope Ministry ukiwa na lengo kuu la kukufikishia machapisho yote ya neno la Mungu yanayoandaliwa na idara mbalimbali ndani ya taasisi yetu. .

ANZA NA BWANA 🌅MIANGA KATIKA ULIMWENGUWAFILIPI 2:15, SUVMpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasi...
21/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

MIANGA KATIKA ULIMWENGU

WAFILIPI 2:15, SUV
Mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaoonekana kuwa k**a mianga katika ulimwengu.

Mungu anakusudia kudhihirisha kanuni za ufalme wake kupitia kwa watu wake. Anakusudia kuwatenganisha na mila, mazoea, na vitendo vya kidunia ili katika maisha yao na tabia zao wafunue kanuni zake... Tabia ya Mungu itakuwa imewasilishwa katika ulimwengu pale ambapo ulimwengu utakuwa umeona wema, rehema, haki na upendo wa Mungu katika kanisa lake. Wakati sheria ya Mungu itakapokuwa imeelelezwa hivyo katika maisha, ulimwengu pia utatambua ya kwamba wale wampendao, wamchao na kumtimikia Mungu ni bora kuliko watu wengine wote.

Waadventista wa Sabato, wanapaswa kuwa kielelezo kuliko watu wengine wote katika utauwa, kuwa watakatifu mioyoni na kwenye mazungumzo yao. Hawa wamekabidhiwa kweli zilizo takatifu ambazo mwanadamu amewahi kupewa. Kila kipaji cha neema na uwezo na ufanisi kimetolewa kwa ukarimu mkubwa. Hawa wanadumu katika kutazamia marejeo ya Kristo katika mawingu ya mbinguni, jambo ambalo limekaribia sana. Kwa hawa, kutokuweka mwonekano kwamba imani yao ni nguvu inayoweza kutawala katika maisha kunamdhalilisha Mungu kwa kiasi kikubwa.

Kwa sababu ya kuongezeka kwa nguvu ya majaribu ya Shetani, nyakati tunazoishi ni za hatari zaidi kwa watoto wa Mungu, na hivyo tunahitaji kujifunza kwa Mwalimu Mkuu bila kukoma, ili tuweze kuchukua kila hatua kwa uhakika na katika haki. Matukio ya ajabu yanafunguka mbele yetu; na katika wakati k**a huu ushuhuda hai unapaswa kubebwa maishani mwa watu wajiitao kuwa ni wa Mungu, ili ulimwengu upate kuliona hilo katika kizazi hiki, wakati uovu unapotawala kila upande, bado wapo watu wanaoweka pembeni nia zao na kutafuta kutenda mapenzi ya Mungu-watu ambao ndani ya mioyo yao sheria ya Mungu imeandikwa...

Counsels to Parents, Teachers, and Students, p. 321, 322 (Ellen Gould White)

ANZA NA BWANA 🌅MWENENDO MZURI1 PETRO 2:12, SUVMwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watend...
16/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

MWENENDO MZURI

1 PETRO 2:12, SUV
Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.

Mungu anategemea ya kwamba wale walichukualo jina la Kristo wamwakilishe Yeye. . . Wanapaswa kutakaswa, kusafishwa, kufanywa watakatifu, wakiwasilisha nuru kwa wote wanaokutana nao. . .

Wafuasi wa Kristo wanapaswa kujitenga na dunia katika kanuni na utashi wake, lakini hawapaswi kujiweka pembeni na dunia. Mwokozi alijichanganya na watu wakati wote, siyo kwa makusudi ya kuwatia moyo kufanya kinyume na mapenzi ya Mungu, bali kuwainua na kuwaadilisha. “Najiweka wakfu mwenyewe,” alitamka, “Ili na hao watakaswe.” (Yohana 17:19). Hivyo Mkristo anapaswa kuishi na watu, ili mwonjo wa upendo wa kimbingu uwe k**a chumvi na hivyo kuilinda dunia isiharibike...

Hitaji letu kuu ni nguvu ya maisha yaliyo ya juu, yaliyo safi, na adiIifu. Ulimwengu unasubiri kuona aina ya matunda yanayotoka kwa Wakristo... Mivuto inayokubaliana na dini ya kibiblia na ile isiyokubaliana nayo, inaendelea kuoeneshwa kwa mawazo ya wote ambao tunapaswa kuwavuta.

Mungu na malaika wanatazama. Ni shauku ya Mungu kwamba, watu wake waoneshe katika maisha yao, ya kuwa kuna faida katika kuwa Mkristo kuliko kuwa wa dunia, waoneshe kwamba wanatenda kazi katika ngazi iliyo ya juu, tena takatifu. Anatamani kuwaona wakidhihirisha kuwa ukweli ambao wameupokea umewafanya kuwa watoto wa Mfalme wa mbinguni. Anatamani kuwafanya wawe mifereji ambayo kupitia kwayo aweza kumwaga upendo wake usio na kifani na rehema yake. - Maranatha, p. 112 (Ellen Gould White)





Follow Channel Yetu Kupata Masomo Haya Kila Siku: https://whatsapp.com/channel/0029VaFZEGaK0IBb1L7Rel1Y

ANZA NA BWANA 🌅MZABIBU NA MATAWIYOHANA 15:5, SUVMimi ni mzabibu; ninyi ni matawi; akaaye ndani yangu nami ndani yake, hu...
14/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

MZABIBU NA MATAWI

YOHANA 15:5, SUV
Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi; akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.

Mwisho umekaribia! Mungu analiita kanisa kuweka tayari yale ambayo yamesalia. K**a watendakazi pamoja na Mungu, mnawezeshwa na Bwana kuingia kwenye ufalme pamoja na wengine mnaowaleta. Ninyi ni mawakala wa Mungu walio hai, mifereji ya nuru kwa ulimwengu, na mnazingirwa na malaika wa mbinguni wakiwa na utume toka kwa Kristo ili kuwatunza, kuwaimarisha, na kuwainua mtendapo kazi ya kuokoa roho. . . - Letters and Manuscripts — Volume 12 (1897), Ms 151, 1897, par. 42

Simameni mkiwa mmejitenga kwa kuwa tofauti na ulimwengu, na wala msiwe wa ulimwengu, bali mkiakisi miali angavu ya Jua la Haki, mkiwa safi, watakatifu, wasio na mawaa, na kwa imani mkiibeba nuru katika njia zote kuu na vichochoro vya dunia. - An Appeal to Our Churches in Behalf of Home Missionary Work, p. 19.3 (Ellen Gould White)

Hebu makanisa yaamke kabla ya kuchelewa milele. Hebu kila mshiriki awe makini na kazi yake binafsi na kuthibitisha jina la Bwana aliloitiwa. Hebu imani na utauwa wa dhati uchukue nafasi ya uzembe na kutokuamini. Imani inapokuwa imeshik**ana na Kristo, kweli italeta amani rohoni, na huduma za kidini hazitadorora na kukosa mvuto. . . Unapodumu katika kuishi Kikristo k**a unavyojiita, kila siku utakuwa na uzoefu mpya na mkubwa na wenye dhambi wataongolewa. . . - Testimony Treasures, vol. 3, p. 70.2 (Ellen Gould White)

Laiti wote wangeamka na kuushuhudia ulimwengu ya kwamba imani yao ni imani iliyo hai, ya kwamba suala zito la muhimu sana IinaikabiIi dunia, kwamba Yesu anakuja upesi. Hebu watu washuhudie kwamba tunaamini ya kuwa tumo katika kingo za ulimwengu wa milele. - Testimonies for the Church, vol. 6, p. 437.3 (Ellen Gould White)





Follow Channel Yetu Kupata Masomo Haya Kila Siku: https://whatsapp.com/channel/0029VaFZEGaK0IBb1L7Rel1Y

ANZA NA BWANA 🌅NJIA NYEMBAMBAMATHAYO 7:13,14, SUVIngieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na nj...
13/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

NJIA NYEMBAMBA

MATHAYO 7:13,14, SUV
Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

Kristo anatuita tuingie kupitia njia nyembamba, ambapo kila hatua inamaanisha kujikana nafsi. Anatuita tusimame katika jukwaa la ukweli wa milele, kisha tupambane, naam, tupambane kwa dhati, kwa ajili ya imani ambayo ilitolewa kwa watakatifu. . . - Our High Calling, p. 172.4 (Ellen Gould White)

Tunapozidi kukaribia wakati ambapo wakuu na mamlaka na uovu wa kiroho katika mahali palipoinuka vitakapokuwa pamoja katika vita kamili dhidi ya kweli, wakati nguvu ya Shetani ya udanganyifu itakapokuwa kubwa kiasi kwamba, hata k**a ingewezekana, angedanganya hata walio wateule, mtazamo wetu unapaswa kufanywa kuwa wa makini zaidi kutokana na kuangaziwa na uungu, ili tusibaki katika kutojua mbinu za Shetani. . . Kwa kutupatia ushirikiano wa malaika watakatifu, Mungu ametupatia uwezo wa kuifanya kazi yetu iwe ya mafanikio yaliyotukuka. Lakini mara chache sana, k**a hili lipo, ambapo mafanikio huwa yanakuja wakati juhudi zinakuwa zimegawanyika. Mvuto wa umoja wa wote walio washiriki wa kanisa unahitajika. - Maranatha, p. 110.3 (Ellen Gould White)

Kanisa leo linahitaji watu ambao k**a Henoko, wanatembea na Mungu, wakimfunua Kristo kwa ulimwengu. Washiriki wa kanisa wanahitajika kufika katika kiwango cha juu. Wajumbe wa kimbingu wanasubiri kuwasiliana na wale ambao wamezamisha nafsi zao hata zisionekane, wale ambao maisha yao ni utimilifu wa maneno, “lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu: na uhai nilio nao sasa katika mwili ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.” - The Review and Herald December 4, 1900, paragraph 12





Follow Channel Yetu Kupata Masomo Haya Kila Siku: https://whatsapp.com/channel/0029VaFZEGaK0IBb1L7Rel1Y

ANZA NA BWANA 🌅JITWIKE MSALABA WAKOLUKA 9:23, SUVMtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wak...
13/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

JITWIKE MSALABA WAKO

LUKA 9:23, SUV
Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku anifuate.

Dhambi ambayo imezoeleka kwa kiasi kikubwa kuliko zote, tena ambayo hututenganisha na Mungu huku ikizaa madhara ya kiroho yaliyo makubwa na yanayoambukiza, ni ile ya ubinafsi. Hakuna namna ambayo mtu aweza kumrudia Bwana k**a sio kwa kujikana nafsi. Kwa kweli hatuwezi kufanya lolote sisi wenyewe; lakini. Mungu akitutia nguvu, twaweza kuishi tukitenda mema kwa wengine, na kwa njia hii kukataa uovu wa ubinafsi. Hatuhitaji kwenda nchi za ugenini ili kuonesha shauku yetu ya kutoa vyote kwa Mungu, na kuishi maisha yenye faida na yasiyo na ubinafsi. Twapaswa kufanya haya katika mazingira ya nyumbani, kanisani mwetu, kati ya wale tunaoshirikiana nao wakati wote na wale tunaofanya nao biashara. Hapo hapo katika maisha ya kawaida ya kila siku ndipo ambapo tunapaswa kuikana nafsi. - Counsels for the Church, p. 80.2 (Ellen Gould White)

Paulo alisema, “ninakufa kila siku.” Kinachopelekea kutufanya washindi ni nafsi zetu kufa kila siku katika shughuli zile ndogo za maisha. Tunapaswa kusahau nafsi katika kutamani kutendea wengine mema. Wengi wamepoa katika kupenda wengine. Badala ya kutimiza wajibu wao kwa uaminifu, wanatafuta anasa kwa ajili yao wenyewe. - In Heavenly Places, p. 233.4 (Ellen Gould White)

Kazi iliyo kuu kuliko zote ipaswayo kufanyika hapa duniani ni kumtukuza Mungu kwa kuishi kulingana na tabia ya Kristo. - Reflecting Christ, p. 313.2 (Ellen Gould White)





Follow Channel Yetu Kupata Masomo Haya Kila Siku: https://whatsapp.com/channel/0029VaFZEGaK0IBb1L7Rel1Y

ANZA NA BWANA 🌅CHAGUENI LEO!YOSHUA 24:15, SUVChagueni hivi leo mtakayemtumikia. Leo, dunia imekuwa kichaa: hali ya kucha...
12/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

CHAGUENI LEO!

YOSHUA 24:15, SUV
Chagueni hivi leo mtakayemtumikia.

Leo, dunia imekuwa kichaa: hali ya kuchanganyikiwa imewakumba wanaume na wanawake, inawaendesha kasi kuelekea katika uharibifu. Kila aina ya mazoea mabaya inatawala, na watu wamepumbazwa na uovu kwa kiasi kikubwa hata kutoweza kusikiliza maonyo na miito. . .

Bwana anasema kwa wote duniani, “Chagueni hivi leo mtakayemtumikia.” Wote wamo katika kufanya maamuzi kwa ajili ya hatima yao ya milele. Watu wanapaswa kuamshwa watambue uzito wa wakati uliopo na ukaribu wa siku rehema itakapofikia mwisho. . .

Mungu hamwambii mwanadamu ya kwamba bado miaka mitano, au kumi au ishirini hadi kufungwa kwa historia ya dunia hii. Hawezi kumpa mtu kisingizio chochote ili acheleweshe maandalizi ya kumlaki ajapo. Hatampa mtu sababu ya kusema k**a yule mtumwa mbaya, “Bwana wangu anakawia kuja;” kwani hili linapelekea mtu kuzembea katika nafasi na fursa alizopewa ili kujiandaa kwa ajili ya siku ile kuu. Kila mmoja anayedai kuwa mtumishi wa Mungu anaitwa kuhudumu kwa ajili yake kila siku kana kwamba ni siku yake ya mwisho...

Hebu tafakari juu ya kuja upesi kwa Mwana wa Adamu katika mawingu ya mbinguni akiwa na mamlaka na utukufu mkubwa. Usiiahirishe siku hiyo mawazoni mwako. . .

Hapa ndipo ulipo mzigo mkubwa wa kubebwa na kila mtu. Je, dhambi zangu zimesamehewa? Je, Kristo anayebeba mzigo wa dhambi, ameichukua hatia yangu? Je, mimi ninao moyo safi, uliosafishwa na haki ya Yesu Kristo? Ole wa roho ile isiyotamtafuta Kristo k**a kimbilio. Ole wao wote ambao kwa namna yoyote wanatoa mawazo toka katika kazi, na kusababisha udhaifu wa roho yoyote wakali huu. . .

ANZA NA BWANA 🌅VAA SILAHA ZA NURUWARUMI 13:12, SUVUsiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya g...
11/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

VAA SILAHA ZA NURU

WARUMI 13:12, SUV
Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.

Wakati huu, tunapaswa kuwa na shabaha moja mbele yetu - kuwekeza kila alichokitoa Mungu kwa ajili ya kupandikiza kweli katika mioyo ya watu. . .Ni wajibu wa kila Mkristo kupambana kwa uwezo wote alio nao ili kusambaza ujuzi wa ukweli.

Mungu amesubiri kwa muda mrefu, na bado anangoja, kuwa na wale ambao ni wake kwa njia ya uumbaji na pia ukombozi. Shauku yake ni kwamba waisikilize sauti yake, wamtii Yeye k**a watoto wenye upendo na wanyenyekevu, ambao tamaa yao ni kuwa karibu naye, na kung’aa kutokana na mwonekano wake juu yao. Tunapaswa kupeleka ujumbe wa malaika yule wa tatu kwa ulimwengu na kuwaonya watu dhidi ya ibada ya mnyama na sanamu yake, na kuwaelekeza kuchukua nafasi zao katika safu ya wale “wazishikao amri za Mungu, na kuwa na imani ya Yesu.” Mungu hajafunua kwetu wakati ujumbe huu utakapofungwa, au wakati rehema itakapokwisha.... Ni wajibu wetu kusubiri na kufanya kazi na kungoja, kutenda kazi kila wakati kwa ajili ya roho za watu walio katika uangamivu....

Sasa, hivi sasa, ni wakati wa kukesha, kufanya kazi, na kungoja. . . . Mwisho wa mambo yote umekaribia. . . Roho wa Bwana anafanya kazi ya kuchukua ukweli wa Neno lilovuviwa na kulitia ndani ya kila roho ili wale wajiitao kuwa wafuasi wa Kristo wawe na furaha iliyo takatifu, ambayo itawawezesha kuambukiza wengine. . .

Lipo hitaji la kuwa na ushuhuda, ulio wa kina zaidi, ulio na nguvu zaidi unaohusu ukweli k**a unavyoonekana katika utauwa halisi wa wale wanaodai kuuamini.





Follow Channel Yetu Kupata Masomo Haya Kila Siku: https://whatsapp.com/channel/0029VaFZEGaK0IBb1L7Rel1Y

ANZA NA BWANA 🌅PIGENI KELELE!YOELI 2:1, SUVPigeni tarumbeta katika Sayuni, pigeni na kelele katika mlima wangu mtakatifu...
09/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

PIGENI KELELE!

YOELI 2:1, SUV
Pigeni tarumbeta katika Sayuni, pigeni na kelele katika mlima wangu mtakatifu; wenyeji wote wa nchi na watetemeke; kwa maana siku ya BWANA inakuja.

Mambo yahusuyo mahitaji yetu ya milele yanapaswa sasa kutawala mawazo yetu. Hatuwezi kuyapa mambo ya mbinguni nafasi ya pili... Tunazo hukumu za Mungu, Zinatoa onyo la dhati kabisa zikisema; “mwe tayari; kwa maana saa msiyoijua Mwana wa Adamu yuaja.”

Wapo wengi, wengi sana makanisani mwetu wanaojua kidogo sana maana halisi ya ukweli wa wakati huu. Natoa wito kwao wasidharau utimilifu wa dalili za nyakati, zinazoonesha wazi kabisa ya kwamba mwisho umekaribia. Ni wengi sana ambao hawajatafuta wokovu wa roho zao ambao watatoa kilio hiki cha kusikitisha; “Mavuno yamepita, wakati wa hari umekwisha, wala sisi hatukuokoka”!

Tumo katikati ya matukio yafungayo historia ya dunia hii. Unabii unatimia kwa kasi. Saa ya rehema inapita upesi. Hatuna muda - hatuna wasaa wa kupoteza. Hebu tusikutwe tumelala katika zamu zetu. Hebu asiwepo atakayesema moyoni mwake au katika matendo yake, “Bwana wangu anachelewa kuja.” Hebu ujumbe wa marejeo ya Kristo hivi karibuni utoe onyo kwa maneno yaliyo dhahiri. Hebu muwashawishi waume kwa wake kila mahali watubu, na waikimbie ghadhabu inayokuja. Tuwaamshe wapate kufanya maandalizi mara moja; kwani hatujui zaidi juu ya kile kitakachofuata. Wachungaji na walei na waende katika mashamba yenye mazao yaliyoiva tayari...

Bwana anakuja upesi, na tunapaswa kukutana naye kwa amani. Na tukusudie kutenda yote kulingana na uwezo wetu kuweka nuru kwa wale wanaotuzunguka. Hatupaswi kuwa na huzuni, bali kuchangamka, na tunapaswa kuwa na Bwana wetu Yesu daima mbele zetu... Tunapaswa kuwa tayari na kusubiri ujio wake.

ANZA NA BWANA 🌅MSHUHUDIE KILA MTUYOHANA 3:16, SUVKwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pek...
08/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

MSHUHUDIE KILA MTU

YOHANA 3:16, SUV
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, hali awe na uzima wa milele.

Je, kwa nini wote wanaodai kumpenda Mungu hawatafuti namna ya kuwaangazia majirani na washirika wao, ili wasiendelee kudharau wokovu huu mkuu? Kristo alijitoa ili afe kifo cha aibu na chenye maumivu makali, roho yake ikipitia taabu kuu kwa ajili ya kuokoa roho zinazoangamia. Naam! Kristo anao uwezo, na yupo tayari, tena ni shauku yake, kuokoa wote watakaomjia!

Ongea na roho zilizo katika hatari na zielekeze kumtazama Yesu msalabani, akifa kwa makusudi ya kumfanya aweze kusamehe. Nena na mwenye dhambi moyo wako ukiwa umejaa wema na upendo wa Yesu wenye huruma. Hebu nena kwa dhati kabisa; lakini Iisisikike hata neno moja la ukali au kutoka kwa yule anayejaribu kuiongoa roho akiielekeza kumtazama Yesu kwa ajili ya uhai.

Kwanza kabisa, iweke roho yako wakfu kwa Mungu. Unapoendelea kumtazama Mpatanishi wetu aliyeko mbinguni, moyo wako utavunjika-vunjika. Baada ya hapo, ukiwa na moyo uliolainishwa na kunyenyekezwa, unaweza kuwaelekeza wadhambi wanaotubu sasa ukiwa na ufahamu fika wa uwezo wa upendo unaookoa. Hebu sali na watu hawa, ukiwaleta kwa imani chini ya msalaba; unganisha mawazo yao na yako, na kaza jicho la imani pale unapopaswa, pale kwa Yesu, abebaye dhambi zote.

Ukiweza kuwaelekeza waache kutazama umaskini wao, na nafsi zao zenye dhambi na badala yake wamtazame Mwokozi, ushindi utakuwa umepatikana. Wao wenyewe, watamtazama Mwanakondoo wa Mungu azichukuaye dhambi za ulimwengu. Wataona Njia, Kweli na Uzima. Jua la Haki litang’aza miali yake angavu mioyoni. Mkondo wenye nguvu wa upendo unaokomboa utamiminika katika roho iliyojeruhiwa na yenye kiu, na mwenye dhambi ataokolewa na Yesu Kristo.





Follow Channel Yetu Kupata Masomo Haya Kila Siku: https://whatsapp.com/channel/0029VaFZEGaK0IBb1L7Rel1Y

ANZA NA BWANA 🌅MBINU YA KUWAFIKIA WATUISAYA 59:9, SUVTwatazamia nuru, na kumbe! Latokea giza; twatazamia mwanga, lakini ...
06/05/2026

ANZA NA BWANA 🌅

MBINU YA KUWAFIKIA WATU

ISAYA 59:9, SUV
Twatazamia nuru, na kumbe! Latokea giza; twatazamia mwanga, lakini twaenda katika giza kuu.

Wapo wengi ambao hata ingawa wanasoma Maandiko, hawaelewi yanachokimaanisha hasa. Duniani kote, watu wanatazama mbinguni kwa shauku kubwa. Sala, machozi na maswali yanayotoka katika roho za watu yanatamani nuru, neema, na Roho Mtakatifu. Wengi wamo katika ukingo wa ufalme, wakisubiri kukusanywa. - The Acts of the Apostles, p. 109.1 (Ellen Gould White)

Kila mahali kuna mioyo iliayo kwa ajili ya kile wanachokihitaji. Wanatamani uwezo utakaowapa ushindi dhidi ya dhambi, nguvu itakayowakomboa toka katika utumwa wa uovu, uwezo ambao utawapa afya, uhai na amani. Wengi ambao waliwahi kujua nguvu ya neno la Mungu, wamedumu kuwa mahali ambapo Mungu haheshimiki, na sasa wanautamani uwepo wa Mungu. - Counsels on Health, p. 25.2 (Ellen Gould White)

Leo, dunia inahitaji kile ilichokihitaji takriban miaka elfu mbili iliyopita - ufunuo wa Kristo. Kazi kuu ya matengenezo inahitajika, na ni kwa neema ya Kristo tu kazi ya urejeshwaji, kimwili, kiakili na kiroho inaweza kukamilishwa. - Counsels on Health, p. 25.2 (Ellen Gould White)

Mbinu ya Kristo peke yake ndiyo iwezayo kuleta mafanikio katika kuwafikia watu. Mwokozi alichangamana na watu kwa namna iliyoonesha kupenda mafanikio yao. Aliwahurumia, aIijishughuIisha na mahitaji yao, na alipata kibali kwao. Kisha akawaalika akisema, “Nifuateni.” - Gospel Workers (1915 ed.), p. 363.2 (Ellen Gould White)
Tembelea what’s app channel yetu kupata somo kamili na masomo zaidi





Follow Channel Yetu Kupata Masomo Haya Kila Siku: https://whatsapp.com/channel/0029VaFZEGaK0IBb1L7Rel1Y

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 23:00
Tuesday 09:00 - 23:00
Wednesday 09:00 - 23:00
Thursday 08:00 - 23:00
Friday 08:00 - 23:00
Saturday 08:00 - 23:00
Sunday 08:00 - 23:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Adventist Hope posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Adventist Hope:

Share