21/05/2026
ANZA NA BWANA 🌅
MIANGA KATIKA ULIMWENGU
WAFILIPI 2:15, SUV
Mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaoonekana kuwa k**a mianga katika ulimwengu.
Mungu anakusudia kudhihirisha kanuni za ufalme wake kupitia kwa watu wake. Anakusudia kuwatenganisha na mila, mazoea, na vitendo vya kidunia ili katika maisha yao na tabia zao wafunue kanuni zake... Tabia ya Mungu itakuwa imewasilishwa katika ulimwengu pale ambapo ulimwengu utakuwa umeona wema, rehema, haki na upendo wa Mungu katika kanisa lake. Wakati sheria ya Mungu itakapokuwa imeelelezwa hivyo katika maisha, ulimwengu pia utatambua ya kwamba wale wampendao, wamchao na kumtimikia Mungu ni bora kuliko watu wengine wote.
Waadventista wa Sabato, wanapaswa kuwa kielelezo kuliko watu wengine wote katika utauwa, kuwa watakatifu mioyoni na kwenye mazungumzo yao. Hawa wamekabidhiwa kweli zilizo takatifu ambazo mwanadamu amewahi kupewa. Kila kipaji cha neema na uwezo na ufanisi kimetolewa kwa ukarimu mkubwa. Hawa wanadumu katika kutazamia marejeo ya Kristo katika mawingu ya mbinguni, jambo ambalo limekaribia sana. Kwa hawa, kutokuweka mwonekano kwamba imani yao ni nguvu inayoweza kutawala katika maisha kunamdhalilisha Mungu kwa kiasi kikubwa.
Kwa sababu ya kuongezeka kwa nguvu ya majaribu ya Shetani, nyakati tunazoishi ni za hatari zaidi kwa watoto wa Mungu, na hivyo tunahitaji kujifunza kwa Mwalimu Mkuu bila kukoma, ili tuweze kuchukua kila hatua kwa uhakika na katika haki. Matukio ya ajabu yanafunguka mbele yetu; na katika wakati k**a huu ushuhuda hai unapaswa kubebwa maishani mwa watu wajiitao kuwa ni wa Mungu, ili ulimwengu upate kuliona hilo katika kizazi hiki, wakati uovu unapotawala kila upande, bado wapo watu wanaoweka pembeni nia zao na kutafuta kutenda mapenzi ya Mungu-watu ambao ndani ya mioyo yao sheria ya Mungu imeandikwa...
Counsels to Parents, Teachers, and Students, p. 321, 322 (Ellen Gould White)