T.A.G Lighthouse Revival Temple- Tegeta

T.A.G Lighthouse Revival Temple- Tegeta Lighthouse Revival Temple is a Tanzania Assemblies of God church located at Tegeta Nyuki Bus station

22/05/2026

Nguvu ya Roho Mtakatifu

Karibuni sana katika wiki ya Pentekoste.....!
16/05/2026

Karibuni sana katika wiki ya Pentekoste.....!

Rev.Ezekiel Mwakajwanga and church leadership are so excited to announce the inauguration of English services , we are b...
09/05/2026

Rev.Ezekiel Mwakajwanga and church leadership are so excited to announce the inauguration of English services , we are believing church is multiculturalism organisation which is designed to reach the global community, so whoever you are and You feel to join us , please never histate to come or communicate with us. Be blessed & welcome to this powerful service!

Mchungaji Kiongozi wa TAG Lighthouse Revival Temple, Rev.Ezekiel Mwakajwanga aliongoza mamia ya Waombolezaji katika ibad...
07/05/2026

Mchungaji Kiongozi wa TAG Lighthouse Revival Temple, Rev.Ezekiel Mwakajwanga aliongoza mamia ya Waombolezaji katika ibada ya kuuaga mwili wa Mama na Bibi , Wellu Mkumbo Nagunwa aliyezaliwa mwaka 1928 na maisha yake yote Bibi huyu aliyatoa kwa Yesu , ikiwepo kuanzishwa kanisa la TAG sebuleni kwake , akiwa Ulemo - Singida.Bibi huyo amekuwa akihudumiwa na kanisa la Lighthouse, msiba huo ulidhuriwa na Watumishi mbali mbali akiwepo Mzee Dkt.Titus Mk**a, Dkt.Samwel Mollel - Makamu Mwangalizi wa Seksheni ya Uhuru , Mch.Kipolozi wa KKKT ushirika wa Tegeta Wazo na Waombolezaji wengi.
Bwana alitoa na Bwana ametoa ,jina lake libarikiwe!

Ushirika wa Wanaume (CMF) , wakihudumu na kuadhimisha siku yao , hakika ilipendeza sana
04/05/2026

Ushirika wa Wanaume (CMF) , wakihudumu na kuadhimisha siku yao , hakika ilipendeza sana

13/04/2026

Miongoni mwa mafundisho na mifano ya mwisho , Rev.Gregory Mallonga

MHBR.EV. SAMUEL NSHATSI SOMO.        USIFUKIE TALANTA YAKOKITABU.      Mathayo 25:14-30TAREHE.    12/04/2026Utangulizi  ...
13/04/2026

MHBR.EV. SAMUEL NSHATSI
SOMO. USIFUKIE TALANTA YAKO
KITABU. Mathayo 25:14-30
TAREHE. 12/04/2026
Utangulizi
Mambo makubwa matatu ambayo *YESU* aliyafanya sana Katika huduma yake
1️⃣Alihubiri (luka 4:18)
2️⃣Alitenda miujiza mingi (Aliponya) (Marko 10:46-52)
3️⃣Alifundisha
Kitabu Cha (mathayo 24:1 mpaka mathayo 25:6) Yesu Alifundisha mambo makubwa mawili Kwa mifano

↪️*Mifano* ni hadithi fupi na rahisi ambazo zimebeba kweli au fundisho moja au Siri moja ya kiroho

*Kwanini Yesu alitumia mifano?*
➡️Ni Kwa sababu alitaka watu wafunuliwe na wazijue Siri za ufalme wa Mbinguni (mathayo 13:10-12)
➡️Ni Kwa sababu alitumia kutoa tahadhari au kuonya (mathayo 24)

*Mifano mitatu inayopatikana katika kitabu Cha mathayo 25*
1️⃣*Wanawali 10* watano wapumbavu na watano wenye akili (Mathayo 25:1-13):
Mfano huu unafundisha umuhimu wa kuwa macho na tayari wakati wote kwa kurudi kwa Kristo.
2️⃣*TALANTA*(Mathayo 25:14-30)
Mfano huu unahimiza kutumia vipawa na fursa tulizopewa na Mungu kwa uaminifu.
3️⃣*Mfano wa Kondoo na Mbuzi* (Mathayo 25:31-46)
Mfano unaoelezea kuhusu hukumu ya siku ya mwisho

➡️Mfano wa *TALANTA* Yesu Alifundisha k**a tahadhari (tahadhari maana yake mbele Kuna hatari)
*Talanta ni kitu chochote ambacho Mungu ameweka Kwa mtu ili kitumike Katika huduma yake*
💥Vipengele vya somo la talanta (mathayo 25:14-30)
1️⃣Mtu aliyetaka kusafiri (kwenda na kurudi)
2️⃣Akawaita watumwa wake watatu
3️⃣Kila mtu mmoja akampa talanta kulingana na uwezo (wakwanza akampa 5 wapili akampa 2 watatu akampa moja) aliwapa taranta bure
4️⃣baada ya kuwapa talanta Akasafiri
5️⃣ Mwenye talanta Tano akazipeleka kwenye biashara na wapili akafanya ivo ivo ila uyu watatu aliyepata talanta moja akaifukia talanta
6️⃣ Bwana alivyorudi aliwaita watumwa wote akitaka hesabu ya Kila mtumwa aliyempa talanta

💥*Leo Hii Bwana akirudi atahitaji hesabu ya talanta aliyokupa (usifukie Talanta Yako)*
🎯Yule Bwana Aliyefukia talanta Wale wenzake walipongezwa Kwa kuambiwa
1️⃣mtumwa mwema na mwaminifu,
2️⃣ukiwa mwaminifu Kwa madogo Mungu atakuinua Kwa makubwa
🎯 Mambo matatu ambayo Aliyefukia talanta Alianza kuyanena
1️⃣Alianza kulaumu (Bwana wewe ni mtu mgumu, wavuna usipopanda,wakusanya usipotawanya)
2️⃣Alianza kutoa visingizio( niliogopa nikaificha ardhini talanta yako)
3️⃣Kutokuzaa baada ya kuficha talanta

*HITIMISHO*
💥*Mfano huu wa talanta unaonyesha kweli moja, kwamba nafasi yako Katika ufalme wa Mbinguni inategemeana na uaminifu wa huduma, karama na kipawa alichowekeza Kwako* Amen..........

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255719234615

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when T.A.G Lighthouse Revival Temple- Tegeta posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share