T.A.G Lighthouse Revival Temple- Tegeta

T.A.G Lighthouse Revival Temple- Tegeta Lighthouse Revival Temple is a Tanzania Assemblies of God church located at Tegeta Nyuki Bus station

TAG LIGHTHOUSEMhbr.JEREMIAH OGWAN*Somo.  UMEBADILISHWA ILI KUBADILISHA WENGINEKitabu.  WARUMI 12:1-2Tarehe.  23/08/2026 ...
24/08/2026

TAG LIGHTHOUSE
Mhbr.JEREMIAH OGWAN*
Somo. UMEBADILISHWA ILI KUBADILISHA WENGINE
Kitabu. WARUMI 12:1-2
Tarehe. 23/08/2026

💥*Kubadilishwa ni Nini?* Kubadilishwa ni kutoka sehemu/hali moja kwenda Hali nyingine mpya

*Imani Isiyo na Matendo Ni Mfu
Mabadiliko ya kweli hayaishii tu kwa mtu kusema "nimeokoka", bali lazima yaonekane wazi kupitia tabia, matendo, na jinsi unavyoishi na wengine. Mungu ameweka uwezo mkubwa ndani yako; hupaswi kubaki umekaa bure.

Njia 3 za Kudhihirisha Mabadiliko Katika Maisha Yako

1.Yatoe Maisha Yako Kikamilifu kwa Mungu_ (Surrender Your Life to God)

-Kujitoa kwa Mungu lazima kuwe kwa 100%(completely), sio nusu nusu(Partially).

-Kuchagua njia ya Mungu na kukataa njia/mashinikizo mengine ya kupelekea dhambi.

-Yatoe maisha yako, wazo lako, na njia zako zote mikononi mwa Mungu.

-Mtume Paulo anatukumbusha kutoa miili yetu kuwa dhabihu inayompendeza Mungu kwa sababu ya huruma zake kwetu.

2.Badilishwa Fikra/mawazo na Nia Yako (Be Transformed in Your Mind)_

-Ruhusu Mungu abadilishe namna unavyofikiri, kuishi na kuamini.

-Mabadiliko huanzia ndani (kile unachofikiri ndio kitazaa matarajio)

-Chukua Hatua: K**a hauna kazi au biashara au chanzo chochote Cha kipato, mtegemee Mungu huku ukiamka kwenda kutafuta fursa, kujifunza ujuzi mpya, na kufanya kazi kwa uaminifu.

-Acha mtazamo wa hofu na kujiona huna mtaji au uwezo. Mungu ameweka kitu ndani yako—kionyeshe nje.

3.Onyesha Upendo, Unyenyekevu na Msamaha_ _Ishi ukiwa na ushawishi Kwa wengine_
-Mabadiliko ya kweli huanzia ndani ya moyo na kutoka nje kupitia unyenyekevu, upendo, na msamaha kwa wengine.

-Tumia nguvu na mwili wako kutumika kanisani na kwenye jamii bila kusubiri kulipwa pesa au kuombwa. Utayari wako wa kutumika ndio unaowavuta wengine kwa Kristo.

-Mungu amekupa uwezo na huruma zake ili uwe mwanga. Amka, badili fikra zako, na ukawabadilishe wengine!

We are so excited to welcome all to our English Services, we are believing that worshipping is beyond our language barri...
16/08/2026

We are so excited to welcome all to our English Services, we are believing that worshipping is beyond our language barriers , but we can fellowship and reaching out the International community.

06/08/2026

Karibu sana kwenye Mkutano wa Injili hapa Tegeta

*IBADA YA JUMATANO*EV.SAMUEL NSHATSI KICHWA: MOYO WA INJILI MATENDO 17:16-18 UTANGULIZI - Mtume Paulo ambaye hapo mwanzo...
05/08/2026

*IBADA YA JUMATANO*
EV.SAMUEL NSHATSI

KICHWA: MOYO WA INJILI
MATENDO 17:16-18

UTANGULIZI
- Mtume Paulo ambaye hapo mwanzo aliitwa Sauli , mtu aliyepambana sana kuzima nguvu ya Injili ya Yesu Kristo ( Soma Matendo 7-8).
- Akiwa safari kwenda kuwaua wanafunzi wa Yesu , ili Injili nayo ife alikutana na Yesu mwenye Injili yake ( Soma Matendo 9)
- Yesu ndio aliyekuja duniani kutafuta kile kilichopotea , kazi yake kuu hapa duniani ni Kutafuta kile kilichopotea
- Alipomaliza kazi hiyo ,alifanya jamii ya waaminio ambao ni kanisa ( Mathayo 16:13-18)
- kanisa lipo duniani kufanya kazi aliyotumwa Yesu hapa duniani ( Yoh 20:21)
- Kazi hiyo n kutafuta kile kilichopotea , hili ndio kusudi kuu la uwepo wa kanisa hapa duniani.
A.KABLA YA KUWAPA AGIZO KUU ,YESU ALILIPA KANISA MAZOEZI KWANZA ( MATHAYO 10:5-7)

1.Alipowaita , akawapa agizo la kwenda kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israel
2.Ni majirani zao , wale walio karibu yao , Injili huanza na waliopo karibu
3.Kazi walizopewa ni
a.Kuhubiri Ufalme
b.Kupooza wagonjwa ( Kuponya)!
c.Fufueni wafu
d.Kutakasa wenye ukoma
e.Kutoa pepo

B.KAZI YA INJILI ILITAKIWA KUENDELEZWA NA KANISA ( Matendo 17:16-18).

👆🏻 Tutaendelea Ijumaa @⁨all⁩

Karibu  katika mkutano wa Injili .....!
30/07/2026

Karibu katika mkutano wa Injili .....!

Vijana na wote mnakaribishwa sana
10/07/2026

Vijana na wote mnakaribishwa sana

08/07/2026

Karibu katika ibada za Jumapili! Mungu yupo Mahali hapa ,tunamwabudu katika roho na kweli

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255719234615

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when T.A.G Lighthouse Revival Temple- Tegeta posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share