01/01/2024
NENO LA MWAKA 2024
Mwaka 2024 ni Mwaka wa KUMILIKI VYA KWAKO
Kumbu kumbu la Torati 1:21 “Tazama, Bwana, Mungu wako, ameiweka nchi mbele yako; haya panda, itamalaki, k**a Bwana, Mungu wa baba zako, alivyokuambia; usiogope wala usifadhaike.”
Kila kilicho chema ni sehemu ya fungu lako kwa sababu Kristo alikifia kwa hiyo ni chakwako.
Yakobo 1:17 “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.”
Mungu hawezi kukataa wewe kuwa nacho kila kilicho chema, Mungu yupo kukuhakikishia kwamba utakuwa nacho. Mungu tayari amefanya maamuzi kwako kwamba ukapate kila kilicho chema.
Chochote kilicho chema unaweza kukitaja maana umepewa, chochote kilicho chema ambacho kimeinuliwa kinatoka juu (Mbinguni), unastahili kukipokea, chochote ambacho kipo chini ambacho hakijakidhi viwango na hakina thamani ni kitu cha duniani lakini chochote kilicho kizuri na kina thamani maana yake kinatoka juu ni pamoja na wewe kwa maana wewe ni wa thamani. Chanzo chako ni juu. Chochote chenye thamani kinatoka juu.
Kila zawadi njema na zawadi kamili inatoka juu
Siku ya kwanza Mungu alipokwenda kwa Waebrania na alipotaka kuwatoa alitaka kuwaonesha ni jinsi gani alivyo mzuri, aliwaandalia chakula na wakala; hivyo waliona ni jinsi gani Mungu alivyo mzuri. Tumeanza mwaka huu kwa tafrija ili muone ni jinsi gani Mungu ni mzuri, Yeye ametupa chakula ili kutuamuru sisi twende tukamiliki milki yetu.
Mwanangu huu ni wakati wako wa Kumiliki milki Yako.
© Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira