deogratiuslukanda

deogratiuslukanda Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from deogratiuslukanda, Religious organisation, Goba, Dar es Salaam.

Karibu sana kwenye Ibada Maalum ya Shukrani na Urejesho baada ya kumaliza Mfungo wa Siku 40!Huduma ya IRCT - HEMA LA UPA...
14/02/2026

Karibu sana kwenye Ibada Maalum ya Shukrani na Urejesho baada ya kumaliza Mfungo wa Siku 40!

Huduma ya IRCT - HEMA LA UPATANISHO inakualika wewe na familia yako katika ibada ya Jumapili ya kipekee ya kumshukuru Mungu kwa ushindi, maombi yaliyojibiwa, na neema mpya iliyoachiliwa juu yetu.

πŸ“ Goba Kulangwa, Mtaa wa Mariga Road, barabara ya njia nne – Madale
πŸ‘€ Uongozi wa Kanisa: Apostle Deogratius Lukanda
πŸ“ž 0765695805

Usikose! Njoo upokee neno, upako na mwelekeo mpya baada ya siku 40 za maombi.
Mlete na mwenzako – Mungu ana jambo lako Jumapili hii! πŸ”₯πŸ™
Muda ni saa Tatu na nusu Asubuhi - mpaka saa saba mchana

pita tutakuwa mubashara kupitia Upatanisho radio -Sauti ya Ushindi.
kwa kubonyeza link hii πŸ‘‰
Listen to Upatanisho Radio -

Listen to Upatanisho Radio online

MAOMBI YA MFUNGO WA SIKU 40SIKU YA 23OMBEA SAFARI ZAKO ZOTE NA KATAA AJALI ZOTE MWAKA HUUπŸ“– β€œWakatanga-tanga toka taifa h...
27/01/2026

MAOMBI YA MFUNGO WA SIKU 40

SIKU YA 23

OMBEA SAFARI ZAKO ZOTE NA KATAA AJALI ZOTE MWAKA HUU

πŸ“– β€œWakatanga-tanga toka taifa hata taifa,
toka ufalme mmoja hata kwa watu wengine.
Hakumwacha mtu awaonee,
hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao.
Akisema, Msiwaguse masihi wangu,
wala msiwadhuru manabii wangu.”
Zaburi 105:13–15

---

UTANGULIZI

Mwaka huu hakuna hata mmoja wetu atakayekosa safari.
Tutafanya safari za barabarani, angani, na majiniβ€”iwe ni safari fupi au ndefu.

Ndiyo maana leo, siku ya 23 ya mfungo wetu,
tunasimama mbele za Mungu kuzikabidhi safari zetu zote.

---

UHALISIA WA KIROHO

πŸ”΄ Kuna ajali ambazo hazitokei kwa bahati mbaya,
bali huandaliwa na shetani na mawakala wake
kwa lengo la kuharibu, kuumiza na kuangamiza maisha ya watu.

πŸ“– β€œAjali yako imekujia, wewe ukaaye katika nchi hii;
majira yamewadia, siku ile inakaribia;
siku ya fujo, wala si ya shangwe.”
Ezekieli 7:7

---

MSIMAMO WETU KATIKA MAOMBI

βœ… Tunakataaa ajali zote za:

Barabarani

Angani

Majini

βœ… Tunatangaza:

Ulinzi wa Mungu katika kila safari

Malaika wa Bwana watutangulie

Hakuna kuguswa, hakuna kudhurika

πŸ“Œ Safari zako zote zipo chini ya damu ya Yesu Kristo.

---

UNGANA NASI KUPITIA

🎧 Upatanisho Radio (Live)
πŸ‘‰ https://onlineradiobox.com/tz/upatanisho/

---

RATIBA YA MAOMBI

πŸ”₯ Maombi ya Vita
πŸ• 01:00 AM – 02:00 AM

πŸŒ… Maombi ya Amka na Bwana
πŸ•• 06:00 AM – 07:00 AM

🍽 Maombi ya Lunch Hour
πŸ•§ 12:30 PM – 01:30 PM

πŸŒ‡ Maombi ya Jioni
πŸ•” 05:00 PM – 06:30 PM

---

MTUMISHI WA MUNGU

Apostle Deogratius Lukanda
πŸ“ž +255 765 695 805

πŸ› MAOMBI YA MFUNGO WA SIKU 40πŸ“… SIKU YA 22πŸ”₯ OMBA HEKIMA YA KI-UNGU> β€œBora hekima, basi jipatie hekima; naam, kwa mapato y...
26/01/2026

πŸ› MAOMBI YA MFUNGO WA SIKU 40

πŸ“… SIKU YA 22

πŸ”₯ OMBA HEKIMA YA KI-UNGU

> β€œBora hekima, basi jipatie hekima; naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.”
Mithali 4:7

πŸ“Œ Maana ya Hekima ya Ki-Ungu

Hekima ni kujua jambo sahihi la kufanya kulingana na Neno la Mungu na kulitenda.

Ni uwezo wa kuenenda kwa kutumia maandiko katika masuala ya maisha ya kila siku.

Hekima ya ki-Ungu humweka mtu juu ya mazingira anayopitia, haongozwi na hali bali huliongoza jambo.

> β€œBasi, tazama, nimefanya k**a ulivyosema. Tazama, nimekupa moyo wa hekima na wa akili; hata kabla yako hapakuwa na mtu k**a wewe, wala baada yako hatainuka mtu k**a wewe.”
1 Wafalme 3:12

---

πŸ“» Ungana Nasi Kupitia Upatanisho Radio

πŸ”— https://onlineradiobox.com/tz/upatanisho/

---

⏰ RATIBA YA MAOMBI

πŸ”Ή Maombi ya Vita
πŸ•– Saa saba usiku – saa nane usiku

πŸ”Ή Maombi ya Amka na Bwana
πŸ•› Saa kumi na mbili asubuhi – saa moja kamili asubuhi

πŸ”Ή Maombi ya Mchana
πŸ•‘ Saa sita na nusu mchana – saa saba kamili mchana

πŸ”Ή Maombi ya Jioni
πŸ•š Saa kumi na moja jioni – saa kumi na mbili na nusu jioni

---

πŸ™ Karibu sana tuombe pamoja
Hii ni siku ya kupokea hekima ya ki-Ungu kwa maamuzi sahihi, ushindi na uongozi wa Roho Mtakatifu.

Apostle Deogratius Lukanda
πŸ“ž +255 765 695 805

MFUNGO WA MAOMBI YA SIKU 40     SIKU YA 20KUHARIBU KILA NGUVU INAYOKUZUIA KUWA NA MATOKEO πŸ”₯Watu wengi wanafanya kazi, wa...
24/01/2026

MFUNGO WA MAOMBI YA SIKU 40

SIKU YA 20

KUHARIBU KILA NGUVU INAYOKUZUIA KUWA NA MATOKEO πŸ”₯

Watu wengi wanafanya kazi, wanaomba na wana ndoto kubwa, lakini hawana matokeo β€” si kwa sababu hawajitahidi, bali kuna nguvu za rohoni zinazowazuia.

πŸ“– Isaya 10:27 β€” nira itaondolewa kwa sababu ya kutiwa mafuta.
πŸ“– Zekaria 4:6 β€” si kwa uwezo wala kwa nguvu, bali kwa Roho wa Mungu.

πŸ‘‰ Mungu hakukuita uwe bila matokeo (Yohana 15:16).
πŸ‘‰ Kila nguvu ya kuchelewesha, kufunga, na kushindwa inahitajika kuharibiwa, si kuvumiliwa.

πŸ”₯ Leo:

vizuizi vinaondolewa

nira zinavunjika

msimu wa matokeo unaanza

Unaweza kuungana nasi kwenye maombi haya kupitia Upatanisho radio kwa kubonyeza link hii
https://onlineradiobox.com/tz/upatanisho/

RATIBA YA MAOMBI

Maombi ya vita, Usiku wa manane
01:00 - 07:00 AM

Amka na Bwana
06:00 - 07:00 AM

Lunch hour
12:30 - 13:30 PM

Maombi ya Jioni
17:00 - 18:30 PM

Huu ni mwaka wa KUANZA, KUONEKANA NA KUONGOZA

NA: APOSTLE DEOGRATIUS ABEL LUKANDA
+255765695805/0658695805

Listen to Upatanisho Radio online

πŸ•ŠοΈ MAOMBI YA MFUNGO WA SIKU 40πŸ“… SIKU YA 10πŸ”₯ KUSHUGHULIKIA ROHO YA UKIWA, UTUPU NA GIZA β€œHapo mwanzo Mungu aliziumba mbin...
14/01/2026

πŸ•ŠοΈ MAOMBI YA MFUNGO WA SIKU 40

πŸ“… SIKU YA 10

πŸ”₯ KUSHUGHULIKIA ROHO YA UKIWA, UTUPU NA GIZA

β€œHapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. 2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji”.

πŸ“– Mwanzo 1:1–2

πŸ“Œ UFUNUO WA KIMAANDIKO

πŸ”Ή Ukiwa
Ni hali ya kukosa mpangilio, kusudi, na uzima unaoonekana.

πŸ”Ή Utupu
Ni hali ya kukosa uhai, maudhui, na tija.

πŸ”Ή Giza
Ni hali ya kukosekana kwa ufunuo, nuru, na utambuzi wa kiroho.

➑️ Lakini hata katikati ya hali hizi zote, Roho ya Mungu alikuwepo – ishara kwamba mabadiliko yako karibu.

🀲 KARIBU KUSHIRIKI MAOMBI

IRCT – HEMA LA UPATANISHO
πŸ“ Goba Kulangwa, Mtaa wa Mariga Road, Barabara ya Madale

Pia unaweza kuungana nasi kupitia Upatanisho radio
https://onlineradiobox.com/tz/upatanisho/

⏰ RATIBA YA MAOMBI

πŸ•• Amka na Bwana
06:00 – 07:00 Asubuhi

πŸ•§ Lunch Hour Prayer
12:30 – 13:30 Mchana

πŸ•” Maombi ya Jioni
17:00 – 18:30

πŸŒ™ Maombi ya Vita ya Usiku wa manane
01:00 – 02:00

🌿 KAULI YA MWAKA

MWAKA WA
KUANZA β€’ KUONEKANA β€’ KUONGOZA
πŸ’ͺ Kwa matokeo ya Mwaka 2026

NA:
Apostle Deogratius Lukanda
πŸ“ž +255 765 695 805
πŸ“ž +255 658 695 805

πŸ™ Karibu uungane nasi katika maombi haya ya kina kwa ajili ya
kuondoa ukiwa, kujazwa utupu, na kutawanywa kwa giza kwa NURU ya Kristo.

Listen to Upatanisho Radio online

13/01/2026

MAOMBI YA MFUNGO WA SIKU 40

Leo ni siku ya 9

Prayer point

πŸ› OMBA MUNGU AKUPE AKILI NA UFAHAMU WA KI-UNGU – 2026

πŸ”Ή Akili ni uwezo wa kufikiri, kukumbuka, kuchambua na kufanya maamuzi sahihi.
πŸ”Ή Ufahamu ni uelewa wa ndani na utambuzi wa maana, hali au ukweli wa jambo.

βˆ† Mtu anaweza kuwa na akili nyingi lakini akakosa ufahamu wa kina, au akawa na ufahamu mzuri hata k**a elimu yake si kubwa.

πŸ‘‰ Kwa mantiki hiyo, unamhitaji Mungu akupe akili na ufahamu wa ki-Ungu, ili uweze:

Kubuni kwa hekima

Kuwaza kwa mwelekeo sahihi

Kufanya maamuzi yanayoendana na kusudi la Mungu

Kutekeleza yale Mungu anayakuhitaji uyafanye mwaka huu 2026

β€’ Neno la Mungu linasema:

> β€œBasi Daudi akatoka kwenda kila mahali alikotumwa na Sauli, akatenda kwa akili; Sauli akamweka juu ya watu wa vita; jambo hili likawa jema machoni pa watu wote, na machoni pa watumishi wa Sauli pia.”
1 Samweli 18:5

β€’ Daudi hakutenda kwa nguvu peke yake, bali kwa akili na ufahamu alioupata kutoka kwa Mungu.

---

⏰ KARIBU UUNGANE NASI KWENYE MAOMBI

πŸ“» Kupitia Online [email protected]
Listen to Upatanisho Radio - https://onlineradiobox.com/tz/upatanisho/
πŸ•°οΈ Ratiba ya Maombi:

πŸ₯— Lunch Hour β†’ 12:30 – 13:30 Mchana

πŸŒ† Maombi ya Jioni β†’ 17:00 – 18:30

βš”οΈ Maombi ya Vita ya Usiku β†’ 01:00 – 02:00

πŸ™ Usikose nafasi hii ya kuomba na kupokea akili na ufahamu wa ki-Ungu kwa ushindi wa mwaka 2026.

Apostle Deogratius Lukanda
+255765695805/0658695805

πŸ”₯ MFUNGO RASMI WA MAOMBI YA SIKU 40 πŸ”₯πŸ¦… MWAKA WA KUANZA, KUONEKANA NA KUONGOZAMwaka wa kubadilishwa hatima na mwanzo mpya...
03/01/2026

πŸ”₯ MFUNGO RASMI WA MAOMBI YA SIKU 40 πŸ”₯

πŸ¦… MWAKA WA KUANZA, KUONEKANA NA KUONGOZA
Mwaka wa kubadilishwa hatima na mwanzo mpya wa kinabii

πŸ“– β€œWakati ule nitayabadilisha majaliwa yenu.”
β€” Sefania 3:20

πŸ“£ HUDUMA YA IRCT – HEMA LA UPATANISHO

Linawatangazia waumini wote na wapendwa wote:

πŸ™ MAOMBI YA SIKU 40 (FAST & PRAYER)

πŸ—“ Kuanzia:
πŸ“… Tarehe 5 Januari 2026

⏰ Muda:
πŸ•š Saa Kumi na Moja Jioni (kila siku)

πŸ“ Mahali:
Huduma ya IRCT – Hema la Upatanisho
πŸ“Œ Goba Kulangwa
πŸ“Œ Mtaa wa Mariga Road
πŸ“Œ Barabara ya Madale

πŸ”₯ Lengo la Maombi

πŸ”Ή Kubadilishwa hatima
πŸ”Ή Mwanzo mpya wa kiroho
πŸ”Ή Kufunguliwa milango mipya
πŸ”Ή Kuingia kwenye mwaka wa kuanza, kuonekana na kuongoza

πŸ“– β€œWatumainio Bwana watapata nguvu mpya; watapaa kwa mabawa k**a tai.”
β€” Isaya 40:31

πŸ¦… MWITO

Njoo uungane nasi katika maombi haya ya siku 40,
uachilie yaliyopita, upokee nguvu mpya, na uanze mwaka kwa ufunuo na mamlaka.

LAKINI PIA UNAWEZA KUJIUNGA KWENYE GROUP LETU LA MAOMBI KWA KUBONYEZA LINK HII πŸ‘‰ https://chat.whatsapp.com/BB6uQlDi0IE6P6AwMTWEk2

---

Apostle Deogratius Lukanda
General Overseer – IRCT
πŸ“ž +255 765 695 805 / +255 658 695 805

TANZANIA MPYA INAZALIWA  OKTOBA 29 si tarehe ya kawaida. Ni siku yenye alama ya kihistoria na kiroho kwa Taifa letu. Kun...
23/10/2025

TANZANIA MPYA INAZALIWA

OKTOBA 29 si tarehe ya kawaida. Ni siku yenye alama ya kihistoria na kiroho kwa Taifa letu. Kuna jambo KUBWA litakalotokea katika nchi yetu β€” ni wakati wa kuomba juu ya Tanzania!

Kumbuka:
Tarehe 29 Oktoba 1964, jina TANZANIA lilizaliwa rasmi baada ya 26 Aprili 1964 Tanganyika na Zanzibar kuungana na kuunda Jamhuri mpya.
Tarehe 29 Oktoba 1995, Watanzania walishiriki uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi, ishara ya mabadiliko makubwa katika historia ya kisiasa ya nchi yetu.

Kwa hiyo, 29 Oktoba ni siku ya kiroho ya mabadiliko ya mifumo, siasa, na hatma ya taifa.

Unapoomba katika majira haya, omba mapenzi ya Mungu yatimizwe juu ya Tanzania. Kwa kufanya hivyo, unashiriki moja kwa moja katika kuizaa TANZANIA MPYA β€” Tanzania aitakayo Mungu.

Ninaiona Tanzania Mpya:
Tanganyika ikiwa na mipaka yake halali,
Zanzibar ikiwa na mipaka yake halali,
Nchi moja, yenye haki, amani na utukufu wa Mungu.

--- β€œTazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani”.
Isaya 43:19


Subscribe and comment
29/07/2025

Subscribe and comment

29/05/2025
29/05/2025

Bwana Yesu asifiwe! Karibu sana Tarehe 31 May 2025, siku ya jumamosi, kuanzia saa mbili kamili Asubuhi mpaka saa kumi na mbili jioni, Viwanja vya Mnazi Mmoja, njoo tuizae Tanzania mpya na haya ni majira sahihi ya wewe kuomba uliyepo Dar es salaam usipange kukosa kabisa, kwa wewe uliye mbali na una rafiki, ndugu au Jamaa mualike aweze kufika kwenye maombi haya.

Ni siku Tano za Kuinuka Tena na Mtumishi wa Mungu Ap Ronald Odongo kutoka Uganda. Mimi tayari nipo Kahama Town kwa ajili...
13/10/2024

Ni siku Tano za Kuinuka Tena na Mtumishi wa Mungu Ap Ronald Odongo kutoka Uganda. Mimi tayari nipo Kahama Town kwa ajili ya semina hii Nichukue nafasi kukukaribisha karibu sana uweze kushiriki, hautabaki k**a ulivyo, ni tarehe 16 - 20 October kuanzia saa kumi mpaka saa kumi na mbili jioni kwenye Kanisa la International Reconciliation church of Tanzania (IRCT) Nyakato karibu na Makaburi

Address

Goba
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when deogratiuslukanda posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share