IJUE KWELI YA MUNGU

IJUE KWELI YA MUNGU Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from IJUE KWELI YA MUNGU, Church of Christ, Dar es Salaam.

Naam,
zaidi ya hayo, Nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi kwa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa k**a mavi ili nipate Kristo;
Wafilipi 3:8

Endelea kufurahia zawadi ya MAISHA aliyokupa Mungu. Ekupa kusema Maneno haya Katika MAISHA1. MAISHA magumu2. MAISHA maba...
10/12/2023

Endelea kufurahia zawadi ya MAISHA aliyokupa Mungu. Ekupa kusema Maneno haya Katika MAISHA
1. MAISHA magumu
2. MAISHA mabaya.
3. Kwanini Mungu amenipa maisha haya.

Hakikisha unajinenea Maneno mema na yanayosadifu utukufu wa Mungu. Kumbuka: 7 Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.
Mithali 23:7a

Kila sekunde Moja ya maisha imejaa utukufu wa Mungu. Mungu hubariki wale wenye shukrani Mbele zake. Yapende na uyafurahie maisha yako, hiyo ni zawadi Mungu amekupa. Mungu hatoi zawadi mbaya Kwa awapendao.

Hakikisha Kila wakati unakua na furaha(filipi 4:4). Furaha ni tiba ya asili ambayo Mungu ameweka ndani yetu.

Mungu akubariki sana, uwe na wakati mwema.

Nahumu 1:9 Mnawaza nini juu ya Bwana? Yeye atakomesha kabisa; mateso hayatainuka mara ya pili.
05/07/2023

Nahumu 1:9 Mnawaza nini juu ya Bwana? Yeye atakomesha kabisa; mateso hayatainuka mara ya pili.

JINSI MKULIMA WA VIJIJINI NEW YORK NA MHUBIRI WA KAWAIDA WA BAPTIST  ALIVYOINGIZA UZUSHI WA KUPOTEZA NDANI YA ‘DHEHEBU L...
22/08/2022

JINSI MKULIMA WA VIJIJINI NEW YORK NA MHUBIRI WA KAWAIDA WA BAPTIST ALIVYOINGIZA UZUSHI WA KUPOTEZA NDANI YA ‘DHEHEBU LA KIKRISTO’ NA YAKADUMU HATA LEO.(Part ONE)

Na Shemasi Jimmy 0659 611 252 Hallelujah watu wa Mungu, hakika tunakila sababu ya kumshukuru Mungu kwa wema na ukuu wake katika maisha yetu. Basi sifa na utukufu vina yeye hata milele. Leo tutaangalia jinsi mafundisho potofu yalivyoingia katika baadhi ya madhehebu ya kikristo kupitia mlango wa unabii wa Daniel.

Neno la Mungu linasema,’’ Mambo ya siri ni ya BWANA, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria hii’’ kumb 29:29. Ni wazi kua hakuna mwanadamu mwenye hekima ya kutoa tafasiri ya jambo ambalo halijafunuliwa na Mungu kupitia neno lake takatifu. Mambo yote ambayo Mungu imempendeza sisi tuyajue aliweza kuyatolea tafasiri ndani ya biblia. Ukisoma kwa utulivu kitabu cha nabii Danieli utagundua kua ni moja kati ya vitabu vigumu ambavyo si jambo rahisi kwa mwanadamu kupata tafasiri ya maono na doto kwa kutumia hekima zake. Iimpendeza Mungu kutufunulia badhi ya mambo ndani ya kitabu hicho, na baadhi ya mambo yamefanywa kua SIRI ya Mungu. Mfano wa baadhi ya mambo ambayo Mungu hakuyatolea ufafanuzi ni pamoja na:-
-majuma 70(Dan 9:24)
-majuma 62(Dan 9:25)
-siku 2300(Dan 8:14)
-siku 1290(Dan 12:11)
-siku 1335(dan 12:12)
BAADHI YA MAFUNDISHO YANAYOFUNGAMANISHWA NA UNABII WA DANIEL(AYA HIZO JUU) NI PAMOJA NA-
-Huduma ya patakatifu pa mbinguni
-wanafundisha pia kua Yesu aliingia patakarifu pa mbinguni tarehe 22.10.1844

Chimbuko la mapotovu hayo ni the Great disappointment(kukata tamaa kubwa) iliyoasisiwa na mkulima wa matunda na mwinjiristi wa kujitolea wa kanisa la babtisti aliyejulikana k**a Willium Miller.
Great disappointment katika harakati ya Millerite ilikuwa majibu ambayo yalifuata tangazo la mhubiri wa Baptist Miller kwamba Yesu Kristo atarudi Duniani kufikia 1844, kile alichokiita Advent. Uchunguzi wake wa unabii wa Danieli 8 wakati wa Ufufuo Mkuu wa Pili ulimpeleka kwenye hitimisho kwamba "utakaso wa patakatifu" wa Danieli ulikuwa utakaso wa ulimwengu kutoka kwa dhambi wakati Kristo angekuja, na yeye na wengine wengi walijiandaa, lakini Oktoba 22, 1844, walikuja na wakakatishwa tamaa.

Matukio haya yalifungua njia kwa Wasabato waliounda Kanisa la Waadventista Wasabato. Walisema kwamba kile kilichotokea Oktoba 22 haikuwa kurudi kwa Yesu, k**a vile Miller alifikiria, lakini kuanza kwa kazi ya mwisho ya Yesu ya upatanisho, utakaso katika patakatifu pa mbinguni, kuelekea kurudi mara ya pili.

MILLER ALIDAI UJIO WA PILI WA KRISTO ULIKUWA KARIBU

Kati ya 1831 na 1844, kwa msingi wa ujifunzaji wake wa Biblia, na haswa unabii wa Danieli 8: 14 - "Mpaka siku elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa" - William Miller, mkulima wa vijijini New York na Mhubiri wa kawaida wa Baptist, alitabiri na kuhubiri kurudi kwa Yesu Kristo duniani. Mafundisho ya Miller yanaunda msingi wa kitheolojia wa Seventh-day Adventism. Mada nne zilikuwa muhimu sana:
1. Matumizi ya Miller ya Biblia;
2. eskatolojia yake;
3. mtazamo wake juu ya ujumbe wa malaika wa kwanza na wa pili wa Ufunuo 14; na
4. Harakati ya miezi ya saba ambayo ilimalizika na "Kukata tamaa Kubwa".

ungana nami tena panapo majaliwa siku ya kesho kwa mwendelezo wa habari hii. Mungu akubariki kwa kutumia muda wako wa thamani kusoma chapisho hili.

JINA BALOKOLE LILIVYOTUMIKA K**A DHIHAKA JUU YA WAKRISTO WA MWANZO NCHINI UGANDA KISHA KUGEUKA UTAMBULISHO WA WAAMINI WA...
20/08/2022

JINA BALOKOLE LILIVYOTUMIKA K**A DHIHAKA JUU YA WAKRISTO WA MWANZO NCHINI UGANDA KISHA KUGEUKA UTAMBULISHO WA WAAMINI WA MADHEHEBU YA KIPROTESTANTI A.MASHARIKI

Na @ shemas Jimny 0659 611 252
Bwana sifiwe wapendwa, neno la Mungu linasema, Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa (mit 12:1a). Tumepewa neema ya kuiona siku ya leo ili tuyafanye mapenzi ya Mungu. Karibu tujifunze.

Je, umewahi kusikia neno MLOKOLE/WALOKOLE? Leo tutazama juu ya asili na chimbuko la neno WALOKOLE. Kwanini linatumika Afrika mashariki tuu na si kwingineko duniani.Ungana name shemasi wako katika simulizi hii.Neno hilo linalotumika k**a utambulisho wa wafuasi wa madhehebu ya kiprotestanti Afrika Mashariki .

Asili yake ni nchini Uganda na chanzo chake ni vuguvugu la mageuzi la kikristo lililoanzishwa na Simioni Nsibambi mwaka 1930’s. Mwanzoni mwa miaka ya 1930 kipindi cha vugu vugu la mageuzi la kikristo, jina hili lilitumika k**a dhihaka kwa wakristo hao wa mwanzo nchini Uganda kutokana na mfumo wa ibada na maombi uliokua ukitumiwa na wafuasi wao, mfano kunena kwa Lugha, maombi ya kukemea na kulia. Mfumo huu ulionekana wa kipekee na wa ajabu kwa jamii ya wasioamini kwani hawakuzoea kuona ibada za mfumo huo.

Balokole(walokole) ni vuguvugu la mageuzi la Kikristo la Kiafrika lililoanzishwa na Simeon Nsibambi na John E. Church katika miaka ya 1930. Balokole waliibuka ndani ya Vuguvugu la Uamsho la Afrika Mashariki lililotaka kuyafanya upya makanisa ya Kiprotestanti nchini Uganda, Kenya, Tanganyika, na Ruanda-Urundi. Licha ya mizizi yake ya kitheolojia katika harakati za uamsho wa Magharibi wa karne ya kumi na nane na kumi na tisa, Balokole ilibadilika kuwa vuguvugu la asili la Kiafrika. Neno Balokole linaweza kutafsiriwa k**a "waliookolewa" au "waliochaguliwa".

Vuguvugu la Balokole lilikosoa matabaka yaliyoanzishwa ndani ya Kanisa la Uganda na kutilia shaka maadili yaliyoenea au viwango viwili. Balokole waliunda udugu wenye usawa, wakafuata sheria za usafi, kuungama dhambi zao hadharani na kukiri uzoefu wao wa kuongoka, ambao walielewa kuwa ni kujitenga na nafsi zao za dhambi za zamani na kupokea maisha mapya kutoka kwa Mungu. Walisisitiza umuhimu wa Ubwana wa Kristo juu ya maeneo yote ya maisha.

Balokole nchini Uganda si tu wa Vuguvugu la Uamsho wa Afrika Mashariki bali pia Wakristo wa Kipentekoste waliozaliwa mara ya pili ambao wana sala zao za Jumapili au za kila siku kutoka kwa makanisa ya Kipentekoste ambayo yanaongozwa na Wachungaji, ambao nyakati fulani huitwa 'Maaskofu'. Wakristo waliozaliwa mara ya pili wa East Africa Revival Movement walitokana na Kanisa la mapema la Waprotestanti wa Uganda ambao waliitwa Wakristo 'waliolala'. Vuguvugu la Uamsho la Afrika Mashariki Kuzaliwa Mara ya Pili Wakristo leo wanaitwa 'Abalokole Abazukuffu' likimaanisha 'Amka Kuzaliwa Mara ya Pili'. Bado wanaendelea na huduma zao za kawaida kutoka kwa kanisa la kianglikana lakini wanafanya ushirika kutoka sehemu zilizotengwa ambapo kwa kawaida kuna mzee katika imani.

Mungu awabariki nyote mliotumia Muda wenu wa thamani kusoma ujumbe huu. Bwana akakufanye Baraka na si laana, ukue na kustawi katika jina la Yesu, amina

18/07/2022
4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu. Zaburi 115:45 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho laki...
23/04/2022

4 Sanamu zao ni fedha na dhahabu, Kazi ya mikono ya wanadamu.
Zaburi 115:4

5 Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,
Zaburi 115:5

6 Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,
Zaburi 115:6

7 Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake.
Zaburi 115:7

8 Wazifanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia.
Zaburi 115:8

Address

Dar Es Salaam
12106

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when IJUE KWELI YA MUNGU posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to IJUE KWELI YA MUNGU:

Share