04/09/2026
*HEKO MWALIMU IMANI*
1. Kijana mtanashati, sifa zende kwa mkeo,
Tena umejizatiti, kufanya maendeleo,
Una wako mkakati, kumwinua mwenye cheo,
Heko Mwalimu Imani, jaliwa miaka mingi.
2. Mwalimu Neno la Mungu, unafundisha upeo,
Umefunikwa na wingu, kwa ya wokovu chapeo,
Kwako twashiba mafungu, kwa yetu maendeleo,
Heko Mwalimu Imani, happy birthday yako.
3. Ujaliwe naye Mungu, alokufikisha leo,
Uzidi pata mafungu, hata ya upendeleo,
Na wote wenye kiwingu, wakingwe na mwenye cheo,
Heko Mwalimu Imani, happy birthday yako.
4. Miongoni mwa vijana, ni msafi wa upeo,
Pamba zako twaziona, nzuri k**a kipepeo,
Ni mtumishi wa Bwana, mfano wa kwetu leo,
Heko Mwalimu Imani, happy birthday yako.
5. Kingine kizuri kwako, unyenyekevu ni cheo,
Unafanya kazi zako, pote penye matokeo,
Kuchagua siyo zako, mtumishi wa kileo,
Heko Mwalimu Imani, happy birthday yako.
6. Lengo lako lile kuu, juzi jana hata leo,
Ni kwamba Mungu mkuu, ajulikane upeo,
Watu ulimwengu huu, wayaache mapokeo,
Heko Mwalimu Imani, happy birthday yako.
7. Na hizo huduma zako, tunazipenda upeo,
Na hizi salamu kwako, ziwe kwako kichocheo,
Zidi mwaga maandiko, utaona matokeo,
Heko Mwalimu Imani, happy birthday kwako.
8. Heri tunakutakia, wa Mungu upendeleo,
Uzidi mtumikia, mwovu umtoe ngeo,
Na kwa yako familia, uyapate matoleo,
Heko Mwalimu Imani, happy birthday kwako.
9. Hivi kwako soda gani, inao upendeleo,
Au ni juisi gani, utakayokunywa leo,
Nitajie bei gani, utapata matoleo,
Heko Mwalimu Imani, happy birthday kwako.
10. Zidi kumtumikia, Mungu ndiye mwenye cheo,
Azidi kubarikia, upate maendeleo,
Hadi uweze fikia, kinachokufaa cheo,
Heko Mwalimu Imani, happy birthday kwako.
*(3 Yohana 1:2, Kumbukumbu la Torati 28:1-13)*
Na Lwaga Mwambande (KiMPAB)
23/5/2024