ZGA-DAR

ZGA-DAR We preach Christ and Him crucified.

IBADA YA JUMAPILI | KUMSIKILIZA ROHO MTAKATIFU"Si kwa uwezo wala kwa nguvu, bali ni kwa Roho Yangu," asema Bwana wa maje...
22/07/2026

IBADA YA JUMAPILI | KUMSIKILIZA ROHO MTAKATIFU

"Si kwa uwezo wala kwa nguvu, bali ni kwa Roho Yangu," asema Bwana wa majeshi. β€” Zakaria 4:6

Jumapili iliyopita tulibarikiwa na Neno la Mungu kupitia Ndugu Charles Washoma, akitukumbusha kuwa muujiza mkuu ambao Mungu amefanya ni kutuokoa, na si hivyo tu bali kutufanya kuwa watoto Wake na kufanya makao Yake ndani yetu kwa njia ya Roho Mtakatifu.

Sisi ndio hekalu la Mungu. Hivyo, maisha yetu yanapaswa kuwa mahali patakatifu ambapo Roho wa Mungu anakaa kwa uhuru. Kila tunachosema, kusikia na kufanya kinapaswa kuonyesha uwepo wa Roho wa Mungu anayekaa ndani yetu.

K**a Israeli walivyokutana na upinzani wakati wa kujenga hekalu baada ya kutoka Babeli, nasi hukutana na changamoto katika safari yetu ya imani. Lakini ushindi haupatikani kwa nguvu zetu wala uwezo wetu, bali kwa kumruhusu Roho Mtakatifu aongoze kila hatua ya maisha yetu.

Kumsikiliza Roho wa Mungu kuna gharama, kwa sababu mara nyingi hutuelekeza kinyume na matakwa ya mwili wetu. Hata hivyo, ndani ya utiifu huo ndipo kuna amani, ushindi na mapenzi kamili ya Mungu.

Bwana anatualika leo tusimhuzunishe Roho Mtakatifu, bali tujifunze kutambua sauti Yake, kuisikiliza na kuitii kila siku. Hapo ndipo tutaishi maisha yanayompendeza Mungu na kutimiza kusudi Lake.

πŸ“– Marejeo ya Neno:
β€’ Zakaria 4:6
β€’ Yohana 14:25–26
β€’ Warumi 12:1
β€’ Wagalatia 5
β€’ 1 Wafalme 19:11–13
β€’ Matendo ya Mitume 18

SUNDAY SERVICE | LISTENING TO THE HOLY SPIRIT

β€œNot by might nor by power, but by My Spirit,” says the Lord Almighty. β€” Zechariah 4:6

Last Sunday, we were greatly blessed by the Word of God through Brother Charles Washoma, who reminded us that the greatest miracle God has performed is not only saving us, but also making us His children and choosing to dwell within us through the Holy Spirit.

We are now the temple of God. Therefore, our lives are meant to be a holy dwelling place where the Holy Spirit lives freely. Everything we say, hear, and do should reflect the presence of the Holy Spirit who dwells within us.

Just as the Israelites encountered opposition while rebuilding the temple after returning from Babylon, we too face challenges in our journey of faith. Yet our victory does not come through our own strength or ability, but by allowing the Holy Spirit to lead and direct every step of our lives.

Listening to the Holy Spirit comes at a cost because He often leads us in ways that are completely contrary to the desires of our flesh. Nevertheless, it is through that obedience that we find peace, victory, and the perfect will of God.

Today, the Lord calls us not to grieve the Holy Spirit, but to learn to recognize His voice, listen to Him, and obey Him every day. It is through this that we will live lives that please God and fulfill His divine purpose for us.

πŸ“– Scripture References:

Zechariah 4:6
John 14:25–26
Romans 12:1
Galatians 5
1 Kings 19:11–13
Acts 18

IBADA YA JUMAPILI "Nitalijenga Kanisa Langu..." β€” Mathayo 16:18Kanisa la Kristo halijengwi na mawazo ya mwanadamu, vipaw...
16/07/2026

IBADA YA JUMAPILI

"Nitalijenga Kanisa Langu..." β€” Mathayo 16:18

Kanisa la Kristo halijengwi na mawazo ya mwanadamu, vipawa, uzoefu wala elimu. Linajengwa na ufunuo ambao Mungu mwenyewe hutoa. Tunaweza kujikuta tunafanya mambo mengi ndani ya kanisa, lakini yasiyokuwa mapenzi ya Mungu ikiwa msingi wake si ufunuo wa Kristo.

Kupokea wokovu ni mwanzo wa safari, si mwisho wake. Mungu anatuita kuingia katika mchakato wa kila siku wa kujengwa, kubadilishwa tabia, na kufananishwa na Kristo. Ndipo mapenzi Yake yanapoanza kuonekana wazi katika maisha yetu.

K**a alivyotukumbusha ndugu Vicent Ngabo, Ufalme wa Mungu si matokeo ya hekima ya kibinadamu, bali ni ufunuo wa Mungu unaofanya kazi ndani ya maisha ya mwamini. Kila hatua ya ukuaji wetu wa kiroho inaanza pale tunapomruhusu Kristo aendelee kutujenga.

"kila kipawa kilicho kamili hutoka juu..." β€” Yakobo 1:17

Tunaomba Neno hili liendelee kuzaa matunda ndani yetu, kuwa Kanisa linalosimama juu ya msingi wa Kristo na ufunuo, si juu ya juhudi zetu wenyewe.

πŸ“–
β€’ Mathayo 16:18
β€’ Yakobo 1:17

SUNDAY SERVICE

β€œI will build My Church…” β€” Matthew 16:18

The Church of Christ is not built on human ideas, talents, experience, or intellectual knowledge. It is built upon the revelation that God Himself gives. We may find ourselves doing many things in the church, yet they may not be in accordance with God's will if their foundation is not the revelation of Christ.

Receiving salvation is only the beginning of the journeyβ€”it is not the destination. God calls us into a lifelong process of being built, transformed, and conformed to the likeness of Christ. It is through this process that His perfect will becomes increasingly evident in our lives.

As Brother Vicent Ngabo reminded us, the Kingdom of God is not the product of human wisdom or academic knowledge, but of God's revelation actively at work in the life of every believer. Every stage of our spiritual growth begins when we allow Christ to continue building and shaping us.

β€œEvery good and perfect gift is from above…” β€” James 1:17

Our prayer is that this Word will continue to bear lasting fruit in our lives, making us a Church firmly established on the foundation of Christ and His revelation, rather than on our own efforts and human understanding.

πŸ“– Scripture References:

Matthew 16:18
James 1:17

Jumapili hii tulibarikiwa kusikia Neno la Mungu kupitia Mch. Damas Makuza, ambaye alitukumbusha juu ya maisha yaliyotole...
08/07/2026

Jumapili hii tulibarikiwa kusikia Neno la Mungu kupitia Mch. Damas Makuza, ambaye alitukumbusha juu ya maisha yaliyotolewa, kwamba huduma ya kweli haianzi madhabahuni, wala kwenye vipawa vyetu, bali inaanza pale mtu anapoanza kuichukua barabara ya msalaba.

Akitoa mfano wa Martha ambaye alimtumikia Yesu kwa bidii, lakini alijikuta akinung'unika kwa sababu dada yake hakumsaidia. Hii ni onyo kwetu sote kwamba tunaweza kuwa na bidii kubwa kanisani, lakini tukakosa uhai wa Kristo ndani yetu.

Kanisa la Kristo halijengwi na uwezo wa kibinadamu, elimu, au uzoefu. Linajengwa na watu ambao wamezifia nafsi zao wenyewe sasa wanaishi maisha ya Kristo. Hapo ndipo huduma inakuwa yenye nguvu, yenye matunda, na yenye kumletea Mungu utukufu.

Mtume Paulo anatukumbusha kwamba tukiwa katika mwili tuko mbali na Bwana; ndiyo maana kila siku tunaitwa kuiacha asili ya mwili na kuishi kwa Roho, ili uhai wa Yesu udhihirike katika nafsi zetu zipatikanazo na mauti.

πŸ“–: Warumi 16:1| 2 Wakorintho 5:6–10| 2 Wakorintho 4:11

RUDI SASA | KAMBI YA VIJANA YA JIMBO 2026 "Nitaondoka na kwenda kwa Baba yangu..." β€” Luka 15:18Kwa neema ya Mungu, kambi...
07/07/2026

RUDI SASA | KAMBI YA VIJANA YA JIMBO 2026

"Nitaondoka na kwenda kwa Baba yangu..." β€” Luka 15:18

Kwa neema ya Mungu, kambi ya vijana ya jimbo 2026 yenye kauli mbiu "RUDI SASA" iliyofanyika tarehe 1–2 Julai 2026 katika Sea Eagle Ocean Front Resort, Kigamboni imehitimishwa kwa mafanikio makubwa.

Zaidi ya vijana 128 walikusanyika kwa siku mbili za kipekee za kujengwa kiroho, kuimarisha ushirika na kufurahia uwepo wa Mungu.

Tulibarikiwa kuwa na vipindi mbalimbali vilivyogusa maisha ya vijana, ikiwemo:
Kusifu na kuabudu, Mafundisho yenye kujenga na Neno la Mungu, Workshops mbalimbali, Makundi rika, Kuogelea na michezo mbalimbali, Ushirika wa pamoja.
Lakini zaidi ya yote, tuliona mkono wa Mungu ukitenda kwa namna ya pekee.

Vijana zaidi ya 6 walimpokea Yesu Kristo k**a Bwana na Mwokozi wa maisha yao.
Vijana 8 walibatizwa, wakichukua hatua ya imani na kuanza maisha mapya ndani ya Kristo.

Tunamshukuru Mungu kwa kila mshiriki, viongozi, waandaaji na kila aliyechangia kufanikisha kambi hii. Tunaamini mbegu zilizopandwa zitaendelea kuzaa matunda katika maisha ya kila kijana.

RUDI SASA haikuwa kauli mbiu tu, bali ilikuwa mwaliko wa kurejea kwenye kusudi la Mungu na kuishi maisha yanayomtukuza Yeye.

πŸ“Έ Tazama baadhi ya matukio yaliyotokea katika kambi yetu ya mwaka huu.

29/06/2026

Kuna jambo zuri linakuja.
Tunajiandaa kwa Kambi ya Vijana ya Jimbo 2026 β€” siku mbili za Neno, ushirika, na uwepo wa Mungu. K**a mwana mpotevu, ni wakati wa kurudi nyumbani kwa Baba.

πŸ“– Kauli mbiu: Luka 15:18

πŸ“ Mahali: SeaEagle Ocean Front Resort

πŸ—“οΈ Tarehe: 1 – 2 Julai 2026

Karibu sana, Tuonane SeaEagle Ocean Front.

MKESHA WA VIJANA – MAISHA YA MKRISTO! β€œKuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii…” (Yakobo 5:16b)πŸ“ Mahali:...
21/04/2026

MKESHA WA VIJANA – MAISHA YA MKRISTO!

β€œKuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii…” (Yakobo 5:16b)

πŸ“ Mahali: ZGA Dar es Salaam
πŸ“… Ijumaa, 24 April 2026
⏰ Muda: Saa 3 usiku – Saa 7 usiku

πŸ“² Scan QR code kujisajili au click Link hii https://forms.gle/AKSUU2d2shpSQYUR9
πŸ“ž Mawasiliano: 0717551871

Usikose! Mualike na rafiki yako πŸ‘‡

12/04/2026

Wapendwa wetu,

Tunaomba radhi kuwataarifu kuwa hatutaweza kurusha ibada ya leo moja kwa moja kutokana na changamoto za kiufundi. Tafadhali endeleeni kuwa nasi wakati mwingine tutakaporejea hewani.

Mungu awabariki sana.

21/02/2026
20/02/2026
Tarehe 4–6 Machi 2026 tutakusanyika kwa Kongamano la BUILD – wakati wa kurudi kwenye msingi.Wachungaji wote na viongozi ...
20/02/2026

Tarehe 4–6 Machi 2026 tutakusanyika kwa Kongamano la BUILD – wakati wa kurudi kwenye msingi.

Wachungaji wote na viongozi wa makanisa mnakaribishwa kwa moyo wote kuhudhuria. Huu ni mwito wa kujengwa upya, kuimarishwa, na kulirudisha kanisa katika msingi sahihi wa Kristo.

Karibuni.

Address

Ubungo, Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ZGA-DAR posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to ZGA-DAR:

Shortcuts

Share