10/02/2026
Tulibarikiwa sana Jumapili hii katika uwepo wa Bwana, baada ya kumuabudu kwa kina, Mchungaji Elly Mpule alilitia moyo Kanisa la Mungu juu ya uhai na umuhimu wa Ujazo wa Roho Mtakatifu.
Tulihimizwa kukumbuka kwamba βWote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.β K**a vile katika Agano la Kale wana wa Israeli walivyoongozwa na nguzo ya moto usiku na wingu mchana kuelekea Kanaani, ndivyo na sisi katika Agano Jipya tumeitwa kuongozwa na Roho wa Mungu, si kwa hisia, si kwa akili, bali kwa uongozi wa Roho Mtakatifu.
Ujumbe ulitukumbusha pia kuwa kuusulubisha mwili na kufa kwa nafsi kuna matokeo makubwa katika ufalme wa rohoni.
K**a vile Yesu Kristo alivyoutoa uhai wake msalabani na kuwa sababu ya wokovu wetu, ndivyo nasi tunaitwa kuitoa miili yetu kuwa dhabihu iliyo hai, hii ndiyo ibada ya kweli.
Mambo yote ya Agano la Kale β ishara, miujiza, dhabihu na kuhani kuingia patakatifu kwa damu ya mwanakondoo β yote yalikuwa vivuli vya mambo mema yajayo katika Agano Jipya. Leo sisi, k**a ukuhani wa kifalme, tuna fursa ya kutoa dhabihu za rohoni kwa Mungu na kuishi maisha yanayoongozwa na Roho Mtakatifu.
π Katika Agano Jipya, Roho wa Mungu si chaguo β ni lazima. Yeye ndiye anayetuongoza, kumfunua Kristo, na kututia katika kweli yote ya Mungu.