ZGA-DAR

ZGA-DAR We preach Christ and Him crucified.

MKESHA WA VIJANA – MAISHA YA MKRISTO! β€œKuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii…” (Yakobo 5:16b)πŸ“ Mahali:...
21/04/2026

MKESHA WA VIJANA – MAISHA YA MKRISTO!

β€œKuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii…” (Yakobo 5:16b)

πŸ“ Mahali: ZGA Dar es Salaam
πŸ“… Ijumaa, 24 April 2026
⏰ Muda: Saa 3 usiku – Saa 7 usiku

πŸ“² Scan QR code kujisajili au click Link hii https://forms.gle/AKSUU2d2shpSQYUR9
πŸ“ž Mawasiliano: 0717551871

Usikose! Mualike na rafiki yako πŸ‘‡

12/04/2026

Wapendwa wetu,

Tunaomba radhi kuwataarifu kuwa hatutaweza kurusha ibada ya leo moja kwa moja kutokana na changamoto za kiufundi. Tafadhali endeleeni kuwa nasi wakati mwingine tutakaporejea hewani.

Mungu awabariki sana.

21/02/2026
20/02/2026
Tarehe 4–6 Machi 2026 tutakusanyika kwa Kongamano la BUILD – wakati wa kurudi kwenye msingi.Wachungaji wote na viongozi ...
20/02/2026

Tarehe 4–6 Machi 2026 tutakusanyika kwa Kongamano la BUILD – wakati wa kurudi kwenye msingi.

Wachungaji wote na viongozi wa makanisa mnakaribishwa kwa moyo wote kuhudhuria. Huu ni mwito wa kujengwa upya, kuimarishwa, na kulirudisha kanisa katika msingi sahihi wa Kristo.

Karibuni.

Tulibarikiwa sana Jumapili hii katika uwepo wa Bwana, baada ya kumuabudu kwa kina, Mchungaji Elly Mpule alilitia moyo Ka...
10/02/2026

Tulibarikiwa sana Jumapili hii katika uwepo wa Bwana, baada ya kumuabudu kwa kina, Mchungaji Elly Mpule alilitia moyo Kanisa la Mungu juu ya uhai na umuhimu wa Ujazo wa Roho Mtakatifu.
Tulihimizwa kukumbuka kwamba β€œWote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.” K**a vile katika Agano la Kale wana wa Israeli walivyoongozwa na nguzo ya moto usiku na wingu mchana kuelekea Kanaani, ndivyo na sisi katika Agano Jipya tumeitwa kuongozwa na Roho wa Mungu, si kwa hisia, si kwa akili, bali kwa uongozi wa Roho Mtakatifu.

Ujumbe ulitukumbusha pia kuwa kuusulubisha mwili na kufa kwa nafsi kuna matokeo makubwa katika ufalme wa rohoni.
K**a vile Yesu Kristo alivyoutoa uhai wake msalabani na kuwa sababu ya wokovu wetu, ndivyo nasi tunaitwa kuitoa miili yetu kuwa dhabihu iliyo hai, hii ndiyo ibada ya kweli.

Mambo yote ya Agano la Kale β€” ishara, miujiza, dhabihu na kuhani kuingia patakatifu kwa damu ya mwanakondoo β€” yote yalikuwa vivuli vya mambo mema yajayo katika Agano Jipya. Leo sisi, k**a ukuhani wa kifalme, tuna fursa ya kutoa dhabihu za rohoni kwa Mungu na kuishi maisha yanayoongozwa na Roho Mtakatifu.

πŸ‘‰ Katika Agano Jipya, Roho wa Mungu si chaguo β€” ni lazima. Yeye ndiye anayetuongoza, kumfunua Kristo, na kututia katika kweli yote ya Mungu.


22/01/2026

"AGENDA YETU NI YESU KRISTO"

Ni muhimu kufahamu ukweli huu wa msingi:
Mungu haweki upako wake kwenye maji, wala mafuta, wala mchanga.
Upako wa Mungu unakaa mahali pawili tu πŸ‘‡

1️⃣ Kwa Yesu Kristo β€”
Mungu amemtia Yesu mafuta. Ndiyo maana jina Kristo maana yake ni Mtiwa Mafuta (The Anointed One). Ndani yake ndiko kuna ukamilifu wote wa Mungu.

2️⃣ Kwa moyo wa mwanadamu (Kanisa) β€”
Mungu ameweka mafuta yake ndani ya mioyo ya waaminio, yaani kanisa lake. Sisi ni hekalu la Roho Mtakatifu; si vitu vya nje, bali ni mioyo iliyomtii Kristo.

πŸ‘‰ Agenda yetu si vitu, si ishara za njeβ€”
AGENDA YETU NI YESU KRISTO,
na Kristo akae mioyoni mwetu kwa imani.





Mkutano wa Jenga Watu Wake utafanyika hapa Dar es Salaam kuanzia tarehe 4–6 Machi πŸ™Mkutano huu utahudumiwa na Mchungaji ...
22/01/2026

Mkutano wa Jenga Watu Wake utafanyika hapa Dar es Salaam kuanzia tarehe 4–6 Machi πŸ™

Mkutano huu utahudumiwa na Mchungaji Miki Hard, ukiwa na lengo kuu la kuimarisha watu wa Mungu na kuimarisha kanisa lake kwa fundisho la kweli.
πŸ‘‰ Ni wakati wa kuimarisha watu wake, kuimarisha kanisa lake.

Save the date!

13/01/2026

🌟 SHUKRANI ZA DHATI KWA WAZAZI WAPENDWA – KAMBI YA WATOTO INUKA UANGAZE 🌟

Kwa mioyo iliyojaa shukrani, tunatoa pongezi na asante za dhati kwa wazazi wote kwa imani, uaminifu na upendo mkubwa mliouonyesha kwa kuwaruhusu watoto wenu kushiriki katika Kambi ya Watoto Inuka Uangaze πŸ™πŸ‘§πŸ½πŸ‘¦πŸ½

Kwa neema ya Mungu, siku zote za kambi zimekuwa za thamani na zenye matokeo ya kudumu. Tumeona watoto wakikua kiroho, wakijengwa kimaadili, wakijifunza nidhamu, ujasiri na mshik**ano, huku wakifundishwa kuishi k**a mwanga wa Kristo nyumbani, shuleni na katika jamii zao.

Kambi hii imekuwa baraka si kwa watoto pekee, bali pia kwa kanisa kwa ujumla, kwani tunaona kizazi kinachoinuka kikiwa na misingi imara ya imani, upendo na hofu ya Mungu 🀍

πŸŽ₯ Tunakualika kutazama highlight video hii uone kwa macho yako mwenyewe kile ambacho Mungu ametenda katika maisha ya watoto wetu.
Tunaomba muendelee kuwa karibu nasi katika safari hii ya malezi, na msisite tena kuwaruhusu watoto wenu kushiriki katika kambi na programu k**a hizi siku zijazo.

Hakika, kuwekeza kwa mtoto leo ni kujenga kanisa na jamii ya kesho ✨
Mungu awabariki sana kwa ushirikiano na imani yenu πŸ’›





Address

Ubungo, Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ZGA-DAR posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to ZGA-DAR:

Share