20/01/2026
1 Wathesalonike 5:18
Kila jambo unapaswa kumwambia Mungu asante.
Kila changamoto unayokutana nayo sio mwisho wa maisha yako.
1 Mambo ya nyakati 29:10-12
Daudi alikuwa anapitia changamoto nyingi lakini aliendelea kumhimidi Mungu.
Kumshukuru Mungu kwa kila jambo maana utamuona katika kila jambo. kila unachopitia Mungu ameruhusu kwa maana yote kwa yote ni yake.
Danieli 2:23
Danieli alimshukuru Mungu kwa Hekima na uwezo.
Mungu anapendezwa sana na shukrani zetu.
Mungu anaruhusu mabaya yatokee ili tujue kumtafuta.
Zaburi 103:1-5
Mungu atakurejeshea vyote vilivyo potea.
Kila kitu unachopitia uantakiwa kujifunza na kutafakari umekosea wapi.
1 Wakorintho 1:4-5
Imetupasa kumshuru Mungu kwa maana ni kwa neema tu.
Hakuna aliyetajirika bila kupitia changamoto.
Usiwe mtu wa kukiri udhaifu kwa kuwa Mungu anajambo jipya juu ya maisha yako.
Mungu yupo teyari kubadilisha maisha yako. Usipende faida tu, penda hasara wala usipende kupokea tu penda na kutoa.
Wakolosai 3: 15, wafilipi 4:6,11-12
Mapito yakiwa magumu ujue kuwa mazuri yanakuja.
Kila jambo limeruhusiwa na sio mwisho wako, kwa maana kila jambo ni nyakati za Mungu.
Wafilipi 2: 14-15
Tutende mambo ya Mungu bila manuniko wala mashindano.