Wanaume Waombaji & Wanawake Waombolezaji

Wanaume Waombaji & Wanawake Waombolezaji Kuutafuta uso wa Mungu kwa viwango vya kipekee na kusaidia wengine kumtafuta na kumjua Mungu.

Heri ya Krismasi!Huduma ya Wanaumbe Wombaji na Wanawake Waombolezaji inakutakia heri katika siku hii kuu ya adhimisho la...
25/12/2025

Heri ya Krismasi!

Huduma ya Wanaumbe Wombaji na Wanawake Waombolezaji inakutakia heri katika siku hii kuu ya adhimisho la kuzaliwa kwa Bwana Yesu Kristo, Mwokozi wa Ulimwengu.

"Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia" - LUKA 2:14.

Tuakupenda sana.

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08-15 OKTOBA 2025USHUHUDA WA SABAShalom Mtumish...
29/10/2025

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08-15 OKTOBA 2025

USHUHUDA WA SABA

Shalom Mtumishi.

Namshuhudia Mungu kwa uponyaji alioachilia kwenye goti langu la mhuu wa kulia, yangu tumeanza maombi ya Yeriko sisikii pakiuma tena hata ninapokunja goti hapaumi K**a ilivyokuwa.

Pia namshukukulu Mungu ameonekana katika biashara yangu wikii nimepata nimepata wateja sio k**a ilivyokuwa hapo kabla ya maombi.

Asante sana Mtumishi Mungu akubariki Sana.

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08-15 OKTOBA 2025USHUHUDA WA SITAShalom Mtumish...
29/10/2025

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08-15 OKTOBA 2025

USHUHUDA WA SITA

Shalom Mtumishi.

Namshukuru MUNGU kupitia maongozi yako kwenye maombi haya ya Yeriko niliona k**a nitashindwa kulingana na ratiba ya kazi iliyokuwa mbele yangu lakini Mungu amenionekania kwa kusogeza ratiba hiyo mbele na hivyo tutakuwa tumemaliza maombi.

Mimi mwenyewe nilikuwa sijui nilipewa taarifa jioni siku ya Jumatatu muda mfupi kabla ya maombi kuanza ya ratiba kusogezwa mbele, pia kukawa na upangwaji wa jukumu jingine lilitolewa jana nalo namshukuru Mungu sijapangwa.

Namrudishia Bwana Mungu wa mbinguni sifa, heshima na utukufu siku zote.

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08-15 OKTOBA 2025USHUHUDA WA 5Shalom mtumishi. ...
28/10/2025

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08-15 OKTOBA 2025

USHUHUDA WA 5

Shalom mtumishi.
Namshukuru Mungu kwa wema wake na uaminifu wake katika maisha yangu. Mwaka huu umekuwa mwaka wa vita vikubwa sana kwangu, lakini katika yote hayo Mungu hajaniacha.

1. MUNGU AMERUDISHA HESHIMA YANGU

Kutosemeshwa kwa miaka mitano haikuwa jambo rahisi, hasa kwa watu ambao kiasili nilipaswa kuzungumza nao karibu kila siku. Ilikuwa kipindi cha upweke, maumivu, na maswali mengi moyoni.

Kulikuwa na watu waliokuwa wamenidharau, wakanisemea maneno ya uongo, wakanitukana, na wengine wakaniangalia k**a sifai chochote.
Lakini ninamshukuru Mungu wa rehema, kwa sababu hao hao waliokuwa wakinicheka na kunidharau, Mungu amewagusa na kubadilisha mioyo yao na sasa wameanza kuniambia tena, tena kwa heshima na utulivu mkubwa.

Kupitia hili nimejifunza kwamba Mungu pekee ndiye hurejesha heshima ya mtu.
Wakati wa Mungu ukifika, hakuna mtu, hali, wala nguvu yoyote inayoweza kuzuia kile alichokusudia kukifanya.

2. MUNGU AMEFUNUA SIRI KUPITIA MAOMBI

Wakati wa Maombi ya Yeriko, nilisukumwa rohoni kumuweka binti anayenisaidia kazi nyumbani katika agenda ya maombi, ingawa sikupanga kufanya hivyo.

Baada ya maombi, alijitahidi kutoroka, lakini majirani walimk**ata. Nilipopigiwa simu na kurudi nyumbani, nikagundua alikuwa amenibia pesa. Mungu alinifungua macho na kunilinda dhidi ya udanganyifu huo.

Kupitia tukio hili, nimejifunza jambo muhimu: tunapaswa kuwaombea wale wote tunaishi nao, kwa sababu maombi yetu yanaweza kuwasaidia, kuwakomesha waovu, na kufungua njia za wema ambazo hatuwezi kuzifanikisha wenyewe.

Hii ni ishara ya nguvu ya Mungu, yeye hufunua siri zilizofichika na hutoa ulinzi kwa wale wanaomtegemea.

3. MUNGU AMEANZA KUFUNGUA MILANGO YA UJENZI

Nilimlilia Mungu kuhusu suala la ujenzi wa nyumba yetu, nikaomba atufungulie milango na avunje vizuizi vyote vilivyokuwa vinatukwamisha.
Kwa kweli Mungu ni mwema! Kwa uweza wake, kazi imeanza kufanyika kwa kasi, na tunaendelea kuona maendeleo katika ujenzi wetu hatua kwa hatua.

4. MUNGU AMENIPA WEPESI NA UHURU WA KIROHO

Kwa muda mrefu nilitamani sana kunyoa nywele zangu, lakini haikuwa rahisi. Nilipomaliza maombi, nikaanza kukumbuka mambo ya zamani ambayo nilidhani ni ya kawaida, kumbe yalikuwa na mizizi ya kiroho.

Miaka miwili iliyopita nywele zangu mbili zilikatika, nikaunganishiwa. Baada ya muda nikaanza kukosa amani, nywele zikaanza kudumaa, kukosa nuru, na hatimaye kuharibika (zilioza kabisa). Nilihisi kutaka kunyoa lakini sikuwa na kibali; hata familia yangu hawakutaka nisifanye hivyo.
Nilianza kwa kupunguza nusu kwa nusu, kisha nikaendelea kusuka kwa kipindi cha miaka miwili, nilisuka mara moja tu kwa kila mwaka.

Wakati wa Maombi ya Malango mwezi Septemba 2025, hisia za kunyoa nywele zikaongezeka zaidi. Nilifumua nywele na kuendelea kutafakari, lakini nilipoanza Maombi ya Yeriko, nikasikia msukumo mkubwa rohoni wa kuzitoa kabisa.
Hatimaye niliamka na kutoa dreadlocks zote, na nilishangaa kuona wepesi usio wa kawaida na amani ya ajabu rohoni mwangu.

Kupitia hili, nimejifunza jambo kubwa sana kuhusu nywele, kwamba si kila kitu kinachoonekana cha kawaida ni cha kawaida. Mungu hutumia mambo madogo kutufundisha masomo makubwa ya kiroho.

Kwa kweli Mungu ni mwaminifu.
Ameonyesha upendo, ulinzi, na nguvu zake katika maisha yangu.
Utukufu, heshima, na sifa zote zimrudie Mungu wetu milele.

SHUHUZA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08 MPAKA 15 OKTOBA 2025USHUHUDA WA NNEShalom,Na...
25/10/2025

SHUHUZA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08 MPAKA 15 OKTOBA 2025

USHUHUDA WA NNE

Shalom,

Namshukuru Mungu kwa ulinzi wake. Katika maombi ya Yeriko na haya ya kuliombea taifa yanayoendelea sasa nimeuona mkono wa Bwana kwa namna ya ajabu kabisa.

Mimi nina utaratibu wa kuwaombea ulinzi na kibali na neema ya kumjua Bwana ndugu, na marafiki zangu wote. Sasa tarehe 21 Oktoba rafiki yangu mmoja ambaye tunashirikiana kibiashara alipata ajali ya gari katika eneo la Dumila mkoa wa Morogoro.

Yeye pamoja na watu wengine 4 walikuwa wanasafiri kutoka mkoa wa Geita kuelekea Dar es Salaam kikazi. Ghafla tairi ya nyuma ya gari waliyokuwa wanasafiri ilipasuka na kusababisha kubiringita mara kadhaa.

Yeye pamoja na wenzako wote walitoka salama isipokuwa majeraha kadhaa tu madogo, ingwa mmoja wao alihitaji uangalizi wa huduma ya kitabibu. Ukitazama gari lilivyoharibika na namna walivyotoka salama ni mkono wa Mungu pekee tu.

Mungu anajibu maombi yetu tunayoomba tusichoke wala kuacha, sisi tumepewa neema ya kusimama k**a walinzi kwa ajili ya familia, watu wetu na taifa kwa ujumla.

Shalom.

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08 MPAKA 15 OKTOBA 2025USHUHUDA WA TATUShalom M...
25/10/2025

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08 MPAKA 15 OKTOBA 2025

USHUHUDA WA TATU

Shalom Mtutmishi.

Namshukuru Mungu kwa maombi ya malango mwezi wa tisa ametenda atatenda na anaendelea kutenda. Uliposema tuombee wanaume niliwaombea kaka zangu kati yao mmoja nilimuombea apandishwe cheo kazini. Namshukuru Mungu baada ya maombi alinipigia simu akaniambia dada naona mwaka huu kwangu imekuwa na Baraka sana kwangu niliomba kwenda kusoma miaka mitatu iliyopita nilikataliwa ila nimeletewa barua hapa natakiwa kwenda kusoma PHD na pia kazini naona mabadiliko nimepanda cheo.

Namtukuza Mungu ametenda

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZAYERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08 - 15 OKTOBA 2025USHUHUDA WA PILIShalom Namshu...
24/10/2025

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZAYERIKO YALIYOFANYIKA KUANZIA TAREHE 08 - 15 OKTOBA 2025

USHUHUDA WA PILI

Shalom

Namshukuru Mungu sana kwa matendo makuu aliyonitendea kupitia maombi ya malango ya mwezi wa Tisa 9 .

Siku ya kwanza kuanzia maombi ya malango mwezi wa Tisa yalikuwa magumu sana upande wangu maana nilijishauri sana Kuhusu kufunga kwani nilikuwa naumwa mfungo ulipoanza nilikuwa na maumivu makali sana upande wa kulia chini ya mbavu kiuno maumivu yalikuwa ya muda mrefu.

Nakumbuka siku Ile Mtumishi alisisitiza sana wanaofunga Danieli Mimi nikasema nafunga Danieli safari hii Mtutmishi akasema msijihurumie K**a una umwa kweli sawa au una miaka 55 ukiangalia na Mimi Nina miaka hiyo nikawaza sana tulipoanza mfungo nikasema wewe shetani sikia hayo maubili Yako nayajua, nikasema kwa sauti mtu hataishi kwa mkate ila kwa neno la Mungu nikafunga uji
Katika maombi yangu siku ya pili nilijiombea afya yangu uponyaji pia nilisema naomba nipate Dr wa kugundua tatizo maana nilishapima ultrasound mara 3 na x-ray mara 2 majibu yakaja tofauti mara ya mwisho nilvyopimwa majibu nikaambiwa kongosho Kuna infection niliogopa sana .

Siku ya 5 ya maombi usiku niliumwa maumivu makali sana nikaanza kuwaza niache kufunga uji nifunge Daniel asubuhi nilpoamka nikasema tena mtu hataishi kwa mkate ila kwa neno la Mungu nik**alza siku nane zote tulivyomaliza mfungo nikarudi tena Dr mwingine kabisa ambaye ni specialrist wa magonjwa ya ndani
Yani namtukuza Mungu nikamwelezea Dr akanisikiliza tu hakunipima kipimo chochote wala dawa yoyote hakunipa akaniambia mama huna ugojwa wowote dawa Yako ni mazoezi tu siku Ile akanifanyia mazoezi maumivu yote nliyokuwa naumwa kipindi Cha mwaka mzima sikuyasikia nimepona kabisa.

Namshukuru Mungu sana πŸ™πŸ½

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA TAREHE 8 - 15 OKTOBA 2025USHUHUDA WA 1Shalom Mtumishi, Napenda...
24/10/2025

SHUHUDA ZA MAOMBI YA KUVUNJA KUTA ZA YERIKO YALIYOFANYIKA TAREHE 8 - 15 OKTOBA 2025

USHUHUDA WA 1

Shalom Mtumishi,

Napenda kushukru Mungu kunijibu ombi langu kati ya maombi yangu ya Yeriko, Asifiwe Mungu milele, nilimuomba anisaidie na kunikinga na roho za mauti ninazoziota ndotoni nilikuwa naota sana watu waliokufa, mazishi ya watu hata siwajui majeneza na makaburi ila baada ya kuanza maombi ya Yeriko namshukru sana Mungu sioti tena hizo ndoto.

Asante sana Mungu wangu, nakushukru sana mtumishi kuniombea maana ili tatizo nakumbuka nilikuambia pia.

Mungu azidi kukuinua kwa ajili ya wahitaji wengineπŸ™πŸΌπŸ™πŸΌπŸ§ŽπŸΎβ€β™€πŸ§ŽπŸΎβ€β™€β€β€

NJOO ULE, UKUE SEHEMU YA 84KUYAINGIA MALANGO YA BWANAUkitaka kufanikiwa kuziingia Nyua za BWANA (Heavenly Courts) na Mal...
14/10/2025

NJOO ULE, UKUE SEHEMU YA 84

KUYAINGIA MALANGO YA BWANA

Ukitaka kufanikiwa kuziingia Nyua za BWANA (Heavenly Courts) na Malango yake (Heavenly Gates) zingatia mambo 11 yafuatayo;

Toba. Inamaana gani kwako? Inakuletea hali ya hofu? Au inakuletea hali ya furaha? Umeshawahi kujikuta kwenye hali ya uka...
22/09/2025

Toba.

Inamaana gani kwako?

Inakuletea hali ya hofu?

Au inakuletea hali ya furaha?

Umeshawahi kujikuta kwenye hali ya ukavu wa kiroho ukajisikia kuwa mtupu, haijalishi nini unafanya?

Iwe ni kwenda kanisani kwa ujumla, au kusali kwa kujilazimisha, chochote unachokifanya juu ya mambo ya rohoni huvutiwi nayo, hata kuomba kwako ni pasipo kuwa na msukumo wa ndani na kuishia kujisikia vibaya?

K**a ndivyo hiki ni kitabu kitakachokufaa. Kitabu cha Toba cha mwandishi Mai Godfrey ni cha kipekee na chenye kukupa mwanga kwa habari ya Toba.

Msomaji utakutana na kitabu chenye utaratibu muhimu wa kufanya toba, unaomsaidia mtu yeyote kuweza kuutafuta uso wa Mungu. Kitabu hiki kinaweza kuwasaidia wakristo na wasiowakristo kumjua Mungu wa kweli kwa namna tofauti baada ya kufanya toba. Ni muongozo unaoweza kutumika tena na tena, iwe ni kwa ajili ya toba tu au kwa ajili ya maombi mazuri ya kupambana na vita vya kiroho na kufunguliwa. Muongozo wake utakusaidia kuweza kuomba kwa nguvu na mamlaka na kuweza kuona matokeo unayotamani kuyapata unapoomba.

Ndani ya kurasa hizi, msomaji na muombaji, utakutana na shehena kubwa ya sala zenye maelezo ya kina juu ya huduma ya mwandishi, mpangilio wake, dira yake, pamoja na shuhuda zenye uzito wa majibu ya maombi. Unapokitumia kitabu hiki, unatengeneza mahusiano yako na Mungu, pamoja na watu wanaokuzunguka. Miujiza iliyokuwa inaonekana haiwezekani, mara itaonekana kuwezekana.

Anza safari yako ya kuwa muombaji mzuri leo!

SHUHUDA ZA MAOMBI YA MALANGO YALIYOFANYIKA TAREHE 08-15 JUNI 2025USHUHUDA WA SABAShalom,Napenda kumshuhudia Mungu Kwa ku...
19/06/2025

SHUHUDA ZA MAOMBI YA MALANGO YALIYOFANYIKA TAREHE 08-15 JUNI 2025

USHUHUDA WA SABA

Shalom,

Napenda kumshuhudia Mungu Kwa kunifanyia njia pasipo na njia. Tulikuwa na ratiba ya kuanza mitihani ya chuo tar 9-15/6 ambayo ilitoka tangu mwezi wa 3. Nikawa nawaza tar hizo pia ni za malango ya mwezi wa 6, na nina siku 3 natakiwa kuingia asubuhi na jioni na kipindi cha jioni kinaanza saa 9-12. Yaani nikawa naendelea kujiuliza nitamwomba mtumishi niingie Kwa zoom na nitatembea na earphone na naweza kutoka dk10 kabla ili nijiunge lakini shida ikaja mazingira, wapi nitakaa ili niweze kusali Kwa utulivu bila miingiliano ya watu.

Nikamwambia Mungu maombi ya malango haya ni ya muhimu sana kwangu kutoka na changamoto ninazopitia, wewe wajua namna gani nitashriki. Tar 5 /6 akaja rafiki yangu akaniambia mitihani imehahirishwa mpaka tar 16/6.
Hivyo ninmshukuru Mungu Kwa kunipa nafasi ya kushiki maombi ya malango haya.

SHUHUDA ZA MAOMBI YA MALANGO YALIYOFANYIKA TAREHE 08-15 JUNI 2025USHUHUDA WA SITA (06)Shalom Mtumishi.Jumapili nilianza ...
18/06/2025

SHUHUDA ZA MAOMBI YA MALANGO YALIYOFANYIKA TAREHE 08-15 JUNI 2025

USHUHUDA WA SITA (06)

Shalom Mtumishi.

Jumapili nilianza na maombi ya toba na niliiweka kampuni yetu pia.
Mwaka jana December tuliambiwa kampuni itafungwa Juni 2025 tusipoongeza uzalishaji. Tuliendelea kumsihi Mungu ili atuonekanie.

Tunapata orders tunashindwa maana mkurugenzi mtendaji na (ndo mwenye duka) hataki kuweka mtaji na hayuko tayari kusaidia anataka kuifunga.

Kuna order kubwa tulipata na mzigo umefika kwa Distributor hivyo tunatakiwa kulipa ili tupewe mzigo. Tulijaribu njia zote za kupata pesa ilishindikana na huyu ni mteja wetu mzuri anayetupa biashara.

Cha kushangaza Jana mkurugenzi mmoja aliwapigia bank walipie order hiyo tu, wamekubali na leo hii process zinaendelea ili tupewe mzigo toka kwa distributor.
Kila mmoja amebakia anashangaa kwa jinsi ilivyowezekana ndani ya muda mfupi na ikafanikiwa.

Kweli njia ya Mungu haichunguziki maana malipo yake yamefungua milango ya kupewa mizigo mingine kwa orders zilizopo.

Namshukuru Mungu maana ametuonekania na kila mmoja amefurahi.

Address

Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wanaume Waombaji & Wanawake Waombolezaji posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Wanaume Waombaji & Wanawake Waombolezaji:

Share