Stawi Ministries

Stawi Ministries Karibu katika ukurasa wa huduma ya Stawi. Huduma hii ni kwa ajili ya kufundisha Neno la Mungu

26/10/2025

Nira ni kifaa kinachotumiwa kumshurutisha mnyama atii kwa lazima. Vifaa vingine vinavyotumika kutiisha kwa lazima ni pamoja na kulabu, na hatamu.
Kulabu na hatamu hufungwa kwanye pua na shingo.

Bwana Yesu alitumia mfano wa vifaa hivyo kuonyesha vile mtu anavyotakiwa kusaidiwa kutii. Pia, mitume wa Bwana Yesu waliichukulia ile torati ya Musa k**a nira. Kwa sababu inaulazima. Ni lazima mtu aitii torati. Asiyeitii torati huadhibiwa.

Lakini Bwana Yesu alileta nira nyingine tofauti na hatamu na kulabu na nira ya Musa. Aliielezea nira hiyo kuwa ni laini, inayomsaidia mtu kutii, badala ya kumlazimisha. Nira ya Bwana Yesu inamfanya mtu apende kutii, moja kwa moja toka moyoni mwake.

Tuendelee kujifunza...

23/10/2025

Kuishi moyoni

15/10/2025

Mambo ya ROHONI

14/10/2025

Dunia ina uhitaji mkubwa wa Mungu. Yaani, Mungu aonekane, akitenda kazi hapa duniani. Dunia ina uhitaji mkubwa wa kazi za Mungu. Watu wajue kuwa yupo Mungu anayemiliki, kutawala na kutiisha hapa duniani.

Sasa, ili hayo yatokee, itakuwa tu ni kwa kupitia watu waliofunuliwa na Mungu. Watu watakaotawala, kumiliki na kutiisha mazingira yao na mambo yao ndio watakaomdhihirisha Mungu hapa duniani. Hata sasa, kutawala, kumiliki na kutiisha ni nadra sana kwa watu.

Tuendelee kujifunza...

13/10/2025

Pale unapopokea maarifa moja kwa moja toka kwa Mungu pasipo kupitia kujifunza kwa elimu ya kidunia. Unafahamu mambo, unaelewa, unapambanua kwa namna isiyotokana na elimu ya dunia. Hapo unakuwa umepokea ufunuo toka kwa Mungu

06/10/2025

Mungu akijidhihirisha kwako utakuwa na ushuhuda wa kudumu

05/10/2025

MUNGU AMEJIDHIHIRISHA KWA WATU KWA NAMNA NYINGI

Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njianyingi.......
Waebrania 1:1 (a)

Mungu hujitokeza kwenye maisha ya mtu binafsi. Kule kujitokeza kwenye maisha ya mtu binafsi kunaitwa Ufunuo wa Mungu.

Enzi hizo, Mungu alipojitokeza kwa watu binafsi, walifanya ukumbusho kwa kuweka alama au kutajia watoto wao majina yaliyoelezea kile alichokifanya Mungu kwenye maisha yao.

Mfano, "Hata sasa Mungu ni Ebenezer", ilitokana na mtu aliyetokewa na Mungu akaamua kufanya ukumbosho wa mahali alipotokewa na Mungu na kupatajia jina hilo la Ebenezer.

Tuendelee kujifunza zaidi......

01/10/2025

Ujuzi mwingi, au maarifa huleta majivuno.

Mtume Paulo alizilinganisha credeintials zake zote na mavi. Pia, ameeleza kwenye 2 Wakorintho 8:1 kuwa, ujuzi, (maarifa) huleta kiburi. Mtu mwenye maarifa huwa anavimba kichwa. Huwa anayategemea yale maarifa. Huwa anajiona kuwa bora kuliko wengine kwa sababu ya maarifa aliyo nayo.

Lakini ndo trend ya siku hizi. Tuendelee kujifunza

30/09/2025

Mtume Paulo Alifunuliwa Siri za Mungu

29/09/2025

UFUNUO WA NENO LA KRISTO

Ufunuo ni haki ya kila mwana wa Mungu. Usipokuwa na ufunuo wa Neno la Kristo utaishi maisha ya kubahatisha sana. Na, ninafahamu kuwa wapo wapendwa wengi sana wanaoishi maisha ya kubahatisha kijumlajumla. Wanapapasapapasa k**a vipofu, na kupoteza muda mwingi sana wakihangaika huku, na kule, juu na chini, ili kupata kile ambacho Mungu alikwisha wapatia, au alikwishakiachilia bure.

Tuendelee kujifunza pamoja

28/09/2025

WITO WA MTUME PAULO

27/09/2025

Wito wa Kufundisha
Agizo kuu la Bwana Yesu ni kwenda ulimweni kwote kuwafanya mataifa wote kuwa wanafunzi wake.

Address

P. O Box 12345
Dar Es Salaam
0255

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255768979282

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Stawi Ministries posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Stawi Ministries:

Share