14/04/2026
๐๐๐ฟ๐๐ผ๐๐, ๐๐๐๐๐ฟ๐ ๐๐ผ ๐๐ผ๐๐๐๐ฟ๐ ๐๐ผ ๐๐๐ผ๐๐๐ผ
๐๐ฝ๐พ๐ถ๐ฒ๐ผ๐ฑ๐ฒ:๐๐ฎ๐ท๐ผ๐ฎ๐ท ๐ข๐ฑ๐พ๐ถ๐ช
Ufunuo 2:4-5
Lakini nina neno juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza. Basi, kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu.
MAHUBIRI
Nidhamu ya kwanza ni ya kitu cha msingi ambacho kinatokana na mtu mwenyewe na hii ni nidhamu binafsi (self-discipline), ambayo ina uwezo wa kujitawala, kujizuia, na kufanya maamuzi sahihi hata wakati wa mgumu ili kufikia malengo ya muda mrefu. Inahusisha kusimamia hisia, muda, na tabia zako ili kuepuka visingizio na kuleta mafanikio.
Kukosa nidhamu binafsi ndiko chanzo kikubwa cha kushindwa maishani.
Nidhamu ya kwanza inatakiwa Kujidhibiti. Ni uwezo wa kufuata sheria au maagizo uliyojiwekea wewe mwenyewe ili kukuza tabia njema, au nidhamu ya kufanya kazi yako, au biashara yako ili ufikie malengo yako, uliyojiwekea mwenyewe. Hii inatakiwa ujidhibiti.
Nidhamu ya kwanza inahitaji Kuvumilia Magumu: Nidhamu inahitaji utayari wa kufanya kazi ngumu, ukijua kuwa mambo mengi huanza kwa ugumu kabla ya kuwa rahisi.
Nidhamu ya kwanza na tabia zinazotokana na hii k**a vile -nidhamu ya kihisia,
- nidhamu ya kifedha,
-Nidhamu ya kujiendeleza,
-Nidhamu ya mahusiano na watu.
Kimsingi, nidhamu ya kwanza ni uwezo wako wa kuamuru akili na mwili wako kufanya kile unachopaswa kufanywa, na si kile unachojisikia kufanya.
Usiache nidhamu ya kwanza, ndiyo itakungoza kwenye maendeleo yako.
Unamkuta mtu anaacha nidhamu ya kwanza. Watu watakuacha kwenye biashara, kanisani, kazi na hata mambo ya kijamii.
Nidhamu.ya kwanza
- itakufungulia milango
- inadumisha fursa
- inadumisha nafasi uliyokuwa nayo
- itakufanya uwe na uwezo wa kuendelea kwenye kazi
Nidhamu hii inatakiwa kwenye huduma, biashara, ndoa, masomo yako, kazi, jumuiya, mikataba, nk
Nitoe mfano mmoja. Sisi tuna vikoba, lakini kikoba chetu, hatujakiwekea sheria ili watu wawe na nidhamu ya kuleta marejesho kwa wakati.
Wanachama wameachwa ili watumie nidhamu waliyo nayo ya kwanza, ukitoka kwenye hiyo nidhamu kule mwishoni mwingine akichukua 1,000,000 wewe utaisha kuchuku 20,000.
Kwenye vile vya mtaani, watu wanalazimishwa kuwa na nidhamu. Usipoleta rejesho kwa muda, kuna adhabu, ukichelewa kwenye kikao adhabu, usipoudhuria kabisa kwa kutoa udhuru ulipia mawazo ya watu wengine, Hizi adhabu zinamfanya mtu kujidhibiti na kuieshimu nidhamu yake ndani ya vicoba.
Jiulize nidhamu.yako ya kwanza ipoje?
Kijana akiwa na wazazi wake, unafundishwa nidhamu mzuri, ya kwenda kanisani, kutoa sadaka, kufanya kazi, kufanya usafi wa mwili wake, kutoingia kwenye mambo ya kukuletea urahibu k**a kuvuta sigara, kunywa pombe, kuvuta bangi, kutafuta wanaume, kuvaa vizuri, nk. Ngoja akakae mwenyewe, anakuwa mchafu, hafanyi kazi, aendi kanisani, anaanza kunywa pombe, anavuta, nk. Anaacha nidhamu ya kwanza, anaingia kwenye mambo ya kumpotosha.
Ukikuta kwenye ndoa watu wakioana, ule upendo wa kwanza ni wa kimapenzi. Kila wakati ni lazima mume au mke ajue mwingine yupo wapi. Wakitoka wanatoka wote. Wakitembea wamekumbatiana. Wakati mwingine wanavaa nguo zinazofanana. Hii yote ni kwa sababu ya upendo wa kwanza au nidhamu ya kwanza. Ipite miaka mitano, unaweza kukuta kila mtu na lwake.
Ukiacha nidhamu ya kwanza, sahau kufanikiwa. Nidhamu ya kwanza ikipotea kuna tabia mbaya zinaonekana kwa watu. Akikuchelewesha, anaanza kukulaumu fanya haraka tunachelewa ataondoka mwenyewe kanisani, utasikia unanichelewesha.vMwingine wakati mwingine anakwenda kazini, anarudi asubuhi,wakati mwanzo alikuwa akirudi mapema.
Kwenye biashara na kazi ni hivyo hivyo. Ebu fikiria unapoanza biashara senti haipiti pembeni au unapoanza kazi nidhamu unayokuwa nayo, ngoja uzoee, hata boso aliyekupa kazi unaanza kumsema. Haa kazi gani hii.
Roho ya ushujaa inatakiwa ili urudi kwenye nidhamu ya kwanza. Roho ya ushujaa ni hatua ya mwisho ya udhihirisho wa Mungu. Joshua aliambiwa uwe hodari na moyo wa ushujaa,usiogope wala kuona hofu.
Yoshua 1:9
Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.
Hofu ni mlango wa kukuondoa kwenye nidhamu ya kwanza na kukurudisha nyuma. Hofu ni bidhaa inayoweza kuuziwa au kubebeshwa mtu. Kuijua siyo shida bali ulishabebeshwa na wewe ukaikubali.
Watu wanakuzulia hofu ili ushindwa au ukate tamaa. Kuna watu hawajaolewa au kuoa kwa sababu ya hofu. Hawaazishi biashara kwa sababu ya hofu. Hawaokoki kwa sababu ya hofu, na watu watanionaje.
Thamani ya fedha kwa mtu wa Mungu aiwezi kununua hofu.
"Kuna mtu nilisikia akisema hakuna kitu nafanya kinafanikiwa. Nikamuliza hili shati na suruale uliyovaa, umevaa wewe mwenyewe au ulivalishwa. Akasema nimevaa mwenyewe. K**a umevaa basi na vingine unaweza kuvivaa.
Kataa hofu. Huko nje hofu ni bidhaa waambie mimi sichukui. Ukiona mtu amefanikiwa usifikiri ana uwezo sana bali ameshinda hofu. Inua dhamani yako kwenye viwango ambavyo havitanunulia hofu.
Thamini yako ni nini, ni imani yako, uwezo wako kwa Mungu,nk.
Agano la Mungu ni bidhaa inayotufanya tusibebe hofu.
Kuna mtu alisema pembe tatu za tai. Mabawa, mdomo na kucha za tai na macho yake. Macho yake yanaweza kuona hadi ndani ya maji. Tunatakiwa tuwe na macho ya tai yaweze kuona mbali, maisha ya baadaye. Tai kipofu hafai.
Hatakiwi tuone hapa kwenye maisha bali uone mbali. Ukiona karibu wewe hufai.
Mwana wa Mungu hofu kwake ni bidhaa mbovu. Mwombe Mungu afungue mbawa zetu kwa Jina la Yesu. Lazima uwe hodari na kuwa shujaa. Kumbuka haijalishi utakwenda mbali kiasi gani hofu inakunyemelea. Upendo wa biashara unageuka. Hofu ni k**a pumzi unakuzunguka. Yesu alipotakiwa kuokoa ulimwengu alitiwa kwenye mikono ya wanyanganyi. Alisema kuwa kikombe hiki kiniepuke. Hofu ni asili ya maisha hata Yesu alikuwa nayo na uwe mwenye nguvu na hodari ndipo utakaposhinda.
Bibilia inasema umeacha upendo wako wa kwanza. Upendo ni vitendo siyo msisimko.
Usogope huko nje ukiona mambo ya kutisha. Ukiingia kwenye biashara wakikuunikia wanakuogopesha na wewe unaogopa. Wanakuambia nitakuharibia biashara yako. Wewe kimya kimya ingia kwenye maombi, Unasema Mungu niondolee hawa waua ndoto.
Hata k**a umefika mbali kiasi gani hofu itakurudisha chini. Kuna watu wamebeba kitu kikubwa kwa sababu ni waoga wameshindwa kuvionyesha wamekuwa mbilikimo. Hofu inaficha uwezo wako. Inaficha na kuuwa uwezo wa mtu.
Mtu anaweza kuwa na uwezo wa kushindana, watu utakisikia wakisema watanionaje. Wanadogosha uwezo aliyokupa Mungu, usipotumia hupati kitu.
Wewe inafikiri ni kitu gani kilimfanya Daudi amshinde Goliati, ni kwa sababu alishinda hofu ndani yake. Shinda hofu kwenye biashara yako, wewe Unazaje kushindana bila kushinda hofu.
Sema kwa jina la Bwana wa Majeshi nitaliweza hili.
Bwana atanipa kazi, atanipa kipato, Bwana atakuondolea hofu kwa Jina la Yesu.
Unasema sioni mlango, huko nje hakuna huruma, machozi hayasaidii chochote, ni lazima na uchague kwa ushujaa.
Usifikiri ukilia sana watakusaidia, vaa ujasiri wa kutoka hapa ulipo. K**a alivyoambiwa lbrahimu.
K**A UJAWEZA KUWA HODARI BADO UJAANZA KUISHA AHADI ZAKO ALIZOKUAHIDIA MUNGU.
Wale waliotumwa nchi ya ahadi waliona majitu wakaingiwa na hofu. Wawili tu walikuwa hodari. Bila ya kuwa hodari utaweza kuishi maisha yako. Huko nje jitengezee pumzi yako mwenyewe. Ukiona mtu aliyefanikiwa ni mtu aliyeshinda hofu.
Jinsi ya kushinda hofu ni kujiunganisha na Mungu ili uweze kupata njia za kupita katika maisha yako. Ukiwa naye hakuna hofu. Kila aliyejiunganisha na Mungu amejitengezea nguvu ya kushinda hofu na kuleta ushindi ndani yako.
Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu, hata katika maji hayatakugharikisha.
INATAKIWA KURUDI KWENYE YALE MATENDO, UPENDO NA NIDHAMU YAKO YA KWANZA. INATAKIWA UWE HODARO AU SHUJAA KUFIKIA UAMUZI HUO. K**A UJAWEZA KUWA HODARI BADO UJAANZA KUISHA AHADI ZAKO ALIZOKUAHIDIA MUNGU.