17/12/2023
KUTIANA MOYO.
6 Wakasaidiana, kila mtu na mwenzake, kila mtu akamwambia ndugu yake; Uwe na moyo mkuu. (Isaya 41:6)
7 Seremala akamtia moyo mfua dhahabu, na yeye alainishaye kwa nyundo akamhimiza yule apigaye fuawe, akiisifu kazi ya kuunga, akisema, Ni kazi njema; naye akaikaza kwa misumari isitikisike. (Isaya 41:7).
ππΎKwenye maisha tunatakiwa kutiana moyo na kushirikiana siyo kukatishana tamaa.
ππΎKila mtu hapa Duniani anafaida ila asipotiwa moyo faida yake haionekani.
ππΎMungu ametuumba na vipawa/Karama tofauti tofauti Ili katika uo utofauti tumtukuze yeye.
ππΎKatika maisha Kuna nyakati tofauti tofauti ambazo katika hizo, Kuna wakati wa huzuni,kukata tamaa,kuchoka na katika nyakati hizo tunatakiwa kutiana moyo.
ππΎTusiwe watu wa kukusoa tu, kulaumu tu Bali wambie wengine YESU ANAKUPENDA, UTAVUKA, BWANA HAJAKUACHA......
WhatsApp
https://chat.whatsapp.com/CYYsFKMWcgh0gOPEDgc8S3
Telegram.
https://t.me/spiritualbreakfast
Meja William
0757215614.