Power in the word of God

Power in the word of God Karibu tujifunze neno la MUNGU litakalobadiilisha maisha yako kila siku Created by Sigfrid

BARAKA 12 KWA AJILI YA MWEZI OCTOBERBwana Yesu asifiwe mpendwa wangu hongera sana kwa kuona mwezi mpya Mungu amekupa mwe...
01/10/2024

BARAKA 12 KWA AJILI YA MWEZI OCTOBER

Bwana Yesu asifiwe mpendwa wangu hongera sana kwa kuona mwezi mpya

Mungu amekupa mwezi wa kufanikiwa katika mambo yote

Mimi k**a mtumishi wake nipo hapa kukutamkia Baraka katika mwezi huu mpya

1. Ninakuombea mwezi huu ukawe mwezi wa kufanikiwa sana na kuinuliwa ,

2. Mwezi huu Kila jambo Ambalo ulitamani Mungu akutendee mwezi wa Tisa basi naungana nawe katika kuomba kwamba mwezi huu Bwana asikupite

3. Nakuombea Kila waliokuzuia miezi yote Tisa iliyopita basi umeingia mwezi mpya huu na VIZUIZI vimekuachia kwa jina la Yesu Kristo

4. Ninakutangazia kwamba kutokea mwezi huu na miezi miwili iliyobaki mbele maono Yako kuhusu mwaka huu yatimie kwa jina la Yesu

5. Kila mpango mbaya kutoka kwa adui kuhusu wewe ninaufuta kwa damu ya Yesu Kristo .

6. Kila mash*taka waliyokush*taki kuzimu Mimi ninasimama na damu ya Yesu ambayo ni damu ya utetezi ninafuta Kila sh*taka kwa jina la Yesu

7. Ninageuza Kila aibu waliyokuandali naifanya kuwa utukufu mkubwa kwa jina la Yesu

8. Mwezi huu nakutangazia kukutana na yule mtu ambaye ametumwa kukuvusha kwenye eneo la uchumi kwa jina la Yesu

9. Habari zako zivume kwa sifa njema na wengi wakisikia wamtukuze Mungu unayemuamini kwa jina la Yesu

10. Nakuombea Kila sadaka utakayotoa kwa Mungu ndani ya mwezi huu hataenda Bure Bali utavuna Sawa sawa na ahadi za Mungu kwako kwa Jina la Yesu

11. Ninasimama k**a kuhani mbele za kiti Cha neema Cha Mungu kwa ajili Yako wewe usomaye hapa kwamba Kila uharibifu uliopangwa kwako hata k**a ni kwa uhalali Niko hapa kuomba rehema za Mungu zikufunike na zikutenge na uharibifu wote

12. Ninakuombea mwezi wa kumi huu uwe ni mwezi wa kurejeshewa Kila kilichopotea kwa miezi yote Tisa iliyopita kwa jina la Yesu

Ninakuandikia haya mwanangu usomaye Kwa Upendo mtupu usio na hata chembe ya unafiki kutoka ndani kabisa ya moyo wangu.

Ninatamani kuona maisha Yako yakiwa yamejaa shuhuda nyingi za ushindi mkuu .

Ukiwa umesoma hayo kwa Imani basi itoshe kusema umebarikiwa na hakuna kukulaani . Andika hapo *nimebarikiwa*

Umebarikiwa sana kupitia Mimi mtumishi wa Mungu na mtumishi wako SIGFRID CHUWA

0683111586

IPO NGUVU NDANI YAKOWaefeso 3:20 Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawaz...
06/03/2024

IPO NGUVU NDANI YAKO

Waefeso 3:20 Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu;

Mara nyingi watu wameomba Kwa kutumia Hilo andiko hapo juu lakini hawakuona matokeo Kwa kiwango kile ambacho walitarajia unajua ni Kwanini?
Watu wengi wanapotafakari Hilo andiko wao huishia hapo kuliko
Lakini Paul hakuishia tu kwamba Mungu anaweza kufanya Bali aliendelea kusema ni Kwa kadiri ya nguvu inayotenda kazi ndani yetu

Kumbe kiwango Cha nguvu ndani ya mtu ndicho kitaamua Mungu atafanya jambo kubwa kiasi gani .
Ni kweli tunaomba na kuombewa lakini lazima ujue nguvu ya kufanya Mambo makubwa ipo ndani Yako tayari . Hii inamaanisha uweza wa Mungu unafanya kazi Kwa ushirika wa karibu kabisa na uweza ambao tayari upo ndani ya mwombaji .
Mtu anapokuombea maana yake ni nguvu ya Mungu inashuka kushirikiana na nguvu iliyopo ndani Yako Kisha unaona matokeo .

Hii nguvu inayotenda kazi ndani Yako inaitwa Imani
Najua umekutana na watu wengi ambao wakikuombea majibu yasipotokea yeye atakuambia huna Imani lakini muujiza ukipatikana atakuambia yeye ananguvu nyingi rohoni . Hapo swala la Imani limeishaje? Mbona hajakuambia unayo Imani ndio maana muujiza umetokea?

Matendo ya Mitume 14:9
Mtu huyo alimsikia Paulo alipokuwa akinena; ambaye akamkazia macho na kuona ya kuwa ana imani ya kuponywa,
:10 akasema kwa sauti kuu, Simama kwa miguu yako sawasawa. Akasimama upesi akaenda.
Umeona? Paulo amekutana na mtu kiwete lakini biblia inatuambia alimwona kuwa anayo Imani ya kuponywa hivyo Imani ya kiwete ikakutana na nguvu za Mungu ndani ya Paulo kiwete akasimama
Kila unaoosemama kuomba neno lolote mbele za Mungu hakikisha umetambua Kuna nguvu ndani Yako inayotakiwa kushirikiana na na nguvu za Mungu ili Mambo yafanyike
Hii itakusaidia hata kushinda uovu maana nguvu ya kushinda inaanzia ndani Yako tunaweza kukuwekea mikono kichwani mpaka kichwa kikawa na upara lakini k**a Bado nguvu iliyopo ndani Yako haijahusika yaani Bado hutaki kutumia nguvu iliyopo ndani hamna matokeo yoyote ..
1 Yohana 5:15
Na k**a tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba.

Kumbe lazima mtu ujue ya kwamba tayari unazo haja ulizomwomba Kwa kuwa amekusikia maana yake lazima kuamini

Leo nakuombea kiwango Cha nguvu iliyopo ndani Yako kiongezeke na mambo makubwa yaanze kutokea Kila uombapo Kwa Jina la Yesu

Pst SIGFRID CHUWA
0683111586

Mara nyingi tumepita kwenye changamoto na hata tulipo jaribu kujiuliza kwanini tunapita jibu la Kwanza tulilipata kwenye...
29/07/2022

Mara nyingi tumepita kwenye changamoto na hata tulipo jaribu kujiuliza kwanini tunapita jibu la Kwanza tulilipata kwenye biblia ya kwamba mkono wa Mungu umeondoka kwetu tena ni Kwa sababu ya njia zetu sio nzuri mbele zake..

Isaya 59:1-2
Tazama, mkono wa BWANA haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
[2]
lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.

Ni kweli uovu ni Moja Kati ya sababu za watu kupitishwa kwenye magumu lakini haitoshi kusema Kila tunapopita huko sababu ni dhambi au mkono wa Mungu umeondoka kwetu, Ivi umewahi kujiuliza k**a ndivyo ViP Yusuf alipopita gerezani ni dhambi Gani alifanya? Kuna wakati ukitafakari Kwa kina unagundua magumu hayaji Ili kutuhakikishia anguko letu katika dhambi ila yanakuja kutuhakikishia kuwa Yupo Mungu anayeweza kufanya Mambo Kwa mkono wenye nguvu..
Sio Kila magumu ni njia ya kukurudisha nyuma au ni ishara ya kukosa uwepo wa Mungu maishani mwako Hapana.
Mark 4:37-39
[37]
Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.
[38]
Naye mwenyewe alikuwapo katika shetri, amelala juu ya mto; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?
[39]
Akaamka, akaukemea upepo, akaiambia bahari, Nyamaza, utulie. Upepo ukakoma, kukawa shwari kuu.
Ukisoma vizuri hiyo sura utagundua Yesu alikuwepo katika mashua na Bado dhoruba inawapiga. Lakini zaidi sana utajua sababu ya dhoruba sio kwamba safari haikuwa na kibali Hapana ila sababu ya dhoruba ni Kwa kuwa waliamua kuvuka ng'ambo nyingine.

Mark 4:35-39
[35]
Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.
[36]
Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye.

Unaona? Kabla ya safari Yesu alikuwa kwenye mashua ndani ya Bahari akihubiri lakini hatuoni upepo Wala Dhoruba ikitokea popote ni mpaka walipoamua kwenda ng'ambo . kumbe wakati mwingine Dhoruba ipo kwa kuwa umeamua kuvuka ng'ambo nyingine lengo la dhoruba ni kukuzuia usifike kwenye hatma ya safari uliyoianza . Lakini pia utagundua maisha ya mtu ni safari na Kila mtu anayo hatma kubwa mbele ya safari yake lakini adui anajaribu kuchezea akili Yako Ili kukurudisha ulipotoka maana anajua kufanikiwa kwako ndio kushindwa kwake .
Mark 5:1-3
[1].
Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi.
[2]
Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;
[3]:
makao yake yalikuwa pale makaburini; wala hakuna mtu ye yote aliyeweza kumfunga tena, hata kwa minyororo;
Hapo ni baada ya kufika ng'ambo wanakutana na mtu mwenye Pepo na Yesu anamfungua Yule mtu na anakuwa huru , unaweza ukaona Kuna uhusiano mkubwa Kati ya dhoruba na kazi aliyoenda kukutana nayo ng'ambo je, ingekuaje k**a wangeamua kurudi walipotoka eti Kwa kuogopa kuzama ? Hatima uliyo nayo ni kubwa isikatishwe na dhoruba kemea upepo na uendelee na safari . Lipo kundi kubwa ng'ambo linakusubiri ushinde hiyo dhoruba Ili wapate kuwa huru . kufunguliwa Kwa huyu Mgerasi kulitegemea sana mafanikio ya Yesu kuishinda dhoruba na kufika ng'ambo.
Acha kujihukumu wewe unalo kusudi chagua kuvuka ng'ambo na sio kurudi nyuma. Je, umewahi kujiuliza ingekuaje k**a Yusuf asingepita Gerezani angefikaje, Ikulu? Na je, story ya Yusuf ingekuwa na mvuto gani bila mke wa Potifa kumtamani? Kila aliyefika kwenye hatma anayo story (in every Glory there's a story) kaa Kwa utulivu story yako inaandikwa usikubali story ikavutia mwanzo alafu mwisho ikachukiza ni heri ionekane Sasa kuwa Haina mvuto lakini mwisho itamvutia msomaji ..
K**a Yusuf angeulizwa Kwa muda huu upo Gerezani tukupe msaada gani yeye angeomba apewe mwanasheria ila amsaidie kupata haki yake maana hukumu aliyonayo sio ya haki. Lakini je, angekuwa amepata msaada kweli? Jibu ni Hapana maana K**a angeshinda Kesi angerudi Uraiani na Bado angeendelea kuwa mtumwa Kwa haki maana Kwa kipindi kile utumwa ilikuwa ni biashara halali . je,angepataje kuonana na farao? Na vip Ile ndoto yake ingetimiaje?
Hivyo usitafute sana njia ya kukimbia matatizo bali tafuta njia ya kushinda huku ukitazama hatma kubwa unayoiendea . Mungu anakupenda kuliko unavyofikiri na anampango mzuri tu na wewe yaan atakufikisha mbali Ione Kanaan yako Bwana aliyokuahidi bila kujali umepita jangwani Kwa muda Gani wewe ndelea kuamini Kanaan ipo. Wewe sio wa Kwanza kupita hapo ulipo Sasa wengi walipita wengine walirudi nyuma lakini waliovumilia walipata nguvu mpya nao wakapaa Kwa mbawa mpaka ng'ambo yenye hatma kubwa..
Isaiah 40:31
[31]
bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa k**a tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia...

Hivyo usiogope unapoona Mambo hayaendi dhoruba inakuja Kwa Kasi jambo la msingi hakikisha Yesu yupo ndani ya Mashua k**a ndio basi safari ni salama Songa mbele ufike ng'ambo

Sigfrid Jerome Chuwa
0683111586

BWANA NA NGUVU ZAKE ..(SHEMU 01)1nyakati 16:10 Jisifuni kwa jina lake takatifu; Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.11 ...
09/10/2021

BWANA NA NGUVU ZAKE ..(SHEMU 01)
1nyakati 16:10 Jisifuni kwa jina lake takatifu; Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.

11 Mtakeni Bwana na nguvu zake; Utafuteni uso wake siku zote.
Hapo tunaona kumtak Bwana na Nguvu zake
Nguvu za Mungu ni uweza wa kiungu anaouachia Mungu mwenyewe kwa watu wake ili kufanya mambo ambayo kibinadamu yasingewezekana lkn kwa nguvu za Mungu yanawezekana .
Nguvu za Mungu ndani yake zimebeba mambo mengi ambayo mwanadam peke yake asingeweza lkn kwa nguvu hizo yanawezekana mf. Uponyaji wa kiungu, miujiza, na matendo yote ya ishara na maajabu, hivi vyote vipo ndani ya Nguvu za Mungu yaani pasipo nguvu za Mungu haviwezekani.,
Mdo 1:
8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

Umeona hapo? Anasema tutapokea nguvu lkn nguvu hizo haziji peke yake bali zinaletwa na Roho mtakatifu. Hivyo hatuwezi kupata nguvu za Mungu pasipo kuwa na
MUNGU yaan ili uweze kuwa na uponyaji ni lazima utafute nguvu za Mungu na hizo Nguvu hazipatikani bila kuwa Roho wa Mungu basi. Ili uweze kudumu katka nguvu za Mungu lazima umtafute Mungu.
Isaya 55:6
Mtafuteni Bwana, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu;
Mara nyingi tumekuwa na maisha yanayojirudia yaan unaombewa na mtumishi huyu unakaa sawa baada ya cku chache mambo yanaanza upya tena kwa ugumu zaidi hapo shida ni kwamba nguvu za Mungu zipo juu ya mtumishi lkn kwako hazipo hivyo anapokuwekea mikono anaachia nguvu juu yako ambazo zinaenda kupambana na nguvu ya adui inayotenda kazi katka hilo tatizo sasa unapoachana nae huyo mtumishi ile nguvu inaenda na wewe lkn kwakuwa wewe huna mahusiano na yule mtoa nguvu(Roho mt) itakaa na ww kwa mda mchache na baadae itakuacha na Adui atapata nafasi kwa nguvu na atakushambulia zaidi maana ameshajua kuna mahali ukienda anashindwa .
Wafilipi 4:
13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.
Mara nyingi tumeutumia huu mstari bila kuuchunguza vzri huwezi kuyaweza mambo yote bila kuwa na nguvu ya kufanya uweze na huwezi kuwa na nguvu bila kuwa na ushirika mzuri na yeye akutiaye nguvu . Hivyo ni lazima kumtafuta Bwana mwenye nguvu ili atupe nguvu ya kuyaweza mambo yote..
Ukimtafuta Bwana anakuja na nguvu zake na ndani ya Nguvu zake kuna uweza wa kufanya yote yasiyowezekana. Unapozunguka huko na huko kutafuta muujiza juu ya tatizo lako ebu jiulize unamtafuta Bwana au unatafuta yaliyomo ndani ya Nguvu za Bwana
Maana ikiwa ndivyo basi hakuna faida maana aliyemtafuta Bwana amepata na nguvu zake na vyote vilivyo katika Nguvu za Bwana lakini ukitafuta vilivyo katka nguvu za Bwana huwa havidumu bali nguvu ikiondoka navyo vinaenda..

Tukutane sehemu ya 2 ambapo tutaangalia namna ya Kumtafuta Bwana..

Mungu akubariki sana
Call: 0712220381
0683111586

23/06/2021

Matendo ya Mitume 17
29 Basi, kwa kuwa sisi tu wazao wa Mungu, haitupasi kudhani ya kuwa Uungu ni mfano wa dhahabu au fedha au jiwe, vitu vilivyochongwa kwa ustadi na akili za wanadamu.
Hapo tunamwona Paul anaonya watu kuhusu kumfananisha Mungu na vitu vnavyoonekana navyo ni kazi ya mikono ya wanadam,. Ndugu unapoenda mbele za Mungu hakikisha umeondoa Kila fikra uliyonayo kuhusu kumfananisha Mungu. Mungu afanani na dhahabu, fedha wala sanamu yoyote uliyowahi kuiona jitahd sana kumuweka Mungu katka kundi hilo ya kwamba hafananishwi na chochote.. Hii itakusaidia sana kumwona Mungu akikutendea kwa kiwango cha juu sana maana umemtofautisha na vitu vingine vinavyoabudiwa

22/06/2021

IPO NGUVU KATIKA KUJUA
Shalom karibu jifunze pamoja nami.....
Mwanzo 3:
5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa k**a Mungu, mkijua mema na mabaya.

6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.

Hapo tunaona shetani anamdanganya Eva kwamba wakila tunda watajua mema na mabaya, lkn jambo la kujiuliza ni kwamba mtu akijua mabaya inasaidia nini? Maana Mungu alipoumba Kila kitu alikiona ni chema akampa mwanadam amiliki na kutawala Sasa wanataka kujua mema yapi? Hapo utagundua shetani alitaka kumjulisha mwanadam mabaya ili wawe pamoja kwenye ubaya. Na hii ndio sababu baada ya mwanadam kula tunda matokeo yake hakuna jema lililotokea Bali yote yalikuwa mabaya. Hii hata kwenye maisha ya kawaida inatufundisha hivyo ulivyo sasa ni matokeo ya kile ulichokijua,; mf“k**a usingejua sukari ni tamu leo usingependa kuilamba” Kuna mtu leo ndoa yake ina shida kwa sababu alianza kazi ya kuchunguza mabaya ya mwenzie siku zote ukitafuta ubaya wa mtu ni lazma uupate maana hakuna mtu aliye na ukamilifu wa kutosha kumpendeza Kila mtu.. Ndugu yangu tafuta sana yaliyo mema maana hata dhambi inayokutesa leo ni kwa sababu ulitafuta kujua, ni vyema sana ukichagua vitu vya kujua ili usiingie kwenye mabaya kuna vitu hata usipovijua hautapungukiwa na chochote. Pia tafuta sana kumjua Mungu ili uwe na uzima yaan mtu akishamjua Mungu anakuwa na uhakika wa mambo mema tu.
Yohana 17:
3 “Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma”
Kumbe ukimjua Mungu unakuwa na uzima wa milele na ndani ya uzima hakuna mateso lkn unapojua mabaya ndani yake kuna maumivu...

MUNGU AKUBARIKI SANA
ni mm
SIGFRID CHUWA
0712220381 .

22/06/2021

UMEUMBWA KWA
KUSUDI
Mhubiri 3:1 “Kila jambo na majira yake na wakati wake, kwa Kila kusudi chini ya mbingu”.

Bwana Yesu asifiwe mwana wa Mungu' karibu tujifunze neno la MUNGU.
Somo linasema umeumbwa kwa Kusudi, hii inamaana kuwa hakuna mtu aliyeumbwa kwa bahati mbaya na ndio maana ukisoma Mhubiri 3:1 ameongelea mambo matatu ya msingi: majira, wakati na Kusudi ambapo haya yakifanyika kwa usahihi jambo linakuwa na mafanikio sahihi. Binadamu yeyote ameumbwa na Mungu kwa majira sahihi, wakati sahihi na makusudi sahihi,
Yeremia 1:
4 Neno la Bwana lilinijia, kusema,
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa” .
Hapo tunamwona Yeremia hakujua k**a aliumbwa kwa kusudi gani alipopewa kazi na Mungu yeye akajua Mungu amekosea kumbe Mungu alimuumba kwa Kusudi hilo. Ndugu yangu nikwambie ukweli kwamba hakuna bahati mbaya katka kuumbwa hivyo kataa kuishi kwa bahati mbaya. Kabla hujaja kwenye tumbo la Mama ulikuwa kwa Mungu k**a Roho isiyo na Mwili hivyo wazazi wako walitengeneza Mwili Mungu akakutuma Duniani kutimiza kusudi ukavaa mwili ndani ya tumbo la mama ukazaliwa kwa njia hiyo . Shetani ni mwongo anatazama kusudi lako tokea mbali anagundua utakuja kuwa nani baadae anaona umetumwa kuharibu kazi zake anaanza kukushambulia ili usitimize kusudi '.
Kutoka 1:
15 “Kisha mfalme wa Misri akasema na wazalisha wa Waebrania, mmoja jina lake aliitwa Shifra, na wa pili jina lake aliitwa Pua;
16 akasema, Wakati mwazalishapo wanawake wa Kiebrania na kuwaona wa katika kuzaa, ikiwa ni mtoto mwanamume, basi mwueni, bali ikiwa ni mtoto mwanamke, na aishi.”

Hapo farao ametambua kuna mtu atakuja kuwakomboa wana wa Israeli ametangaza watoto wasiachwe hai na kumbe ndani ya watoto hao ndio Musa anazaliwa, Unaona ni jinsi gani sababu kubwa ya mateso yako sio hivyo unavyooneka Sasa Bali vile kesho yako ilivyo kubwa
Na lengo ni kukuchelewesha au kukuzuia kabisa usifanye kusudi lililokuleta Duniani.
Mda mwingine Shetani anakuweka kwenye kazi flani ambayo anajua hutaweza kutimiza kusudi kwa wakati.. Mf “unakuta Mungu alipokuumba amekuwekea vipawa kwamba ukija Duniani uwe milionea ili uwasaidie Yatima Sasa shetani akiona hilo kusudi anaanza kukushambulia unaanza kuona Kila biashara unafanya hela hupati,..
Matendo ya Mitume 22:
8 “Nikajibu, Wewe u nani, Bwana? Akaniambia, Mimi ni Yesu Mnazareti, ambaye wewe unaniudhi.

9 Na wale waliokuwa pamoja nami waliiona ile nuru, lakini hawakuisikia ile sauti ya yule aliyesema nami.

10 Nikasema, Nifanye nini, Bwana? Bwana akaniambia, Simama, uingie Dameski, na huko utaambiwa habari za mambo yote yaliyoamriwa uyafanye” .
Huyo aliitwa sauli kazi yake alikuwa askari aliyepewa kitengo cha kulitesa kanisa la MUNGU kumbe shetani alikuwa amejua alitumwa kuhubiri injili na kukuza kanisa kwa kiwango cha juu sana akamweka kuwa wa kulitesa kanisa. Hapo tunajifunza yupo mtu anafanya mambo mabaya k**a Wizi, Ulevi, Ukahaba, na mengine k**a hayo si kwa kupenda ni shetani ametazama hatma yake akajua madhara yake akaamua kumpeleka huko.. Yesu alipomtokea Sauli aliamua kumfanya upya na kumrudisha kwenye Kusudi na jina akam'badilisha akaitwa PAUL leo hii ukiongelea injili kwa mataifa unamwongelea Paul maana yeye ndio aliyeihubiri tujiulize ingekuaje k**a Paul angeendelea na lile kusudi la shetani ambalo ni kuharibu kanisa leo hii tungekuwa wap? Kuna mtu unakusudi kubwa tu lkn shetani anakuingiza kwenye dhambi ambayo inakutesa na kila ukijaribu kuiacha inakushinda lengo lake ni ww uishi nje ya kusudi la MUNGU.. Ndugu tafuta sana kuishi ndani ya kusudi la Mungu mafanikio sio kumiliki vitu vnavyoonekana kwa macho Bali nikuyajua mapenzi na makusudi ya Mungu na kuyatimiza kikamilifu hapo tunasema umefanikiwa,
Yohana 4:
34 Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake. Jiulize je, hapo ulipo ni Mahali sahihi? Vp maisha unayoishi ndio kusudi la MUNGU kukuleta Duniani? Vp Yesu akirudi leo utavikwa taji kwa kazi aliyokutuma kufanya? Ndugu yangu hakuna jambo lisilo na Kusudi hata pesa uliyonayo k**a isipofanya kusudi la Mungu ni kazi Bure, hata kazi uliyo nayo k**a sio kusudi la Mungu hutapata matokeo.. Hivyo tafuta sana kuyatimiza kusudi la Mungu..
Maombi...
>Mwombe Mungu akujuze kusudi la yeye kukuumba.
>Kataa Kila kusudi la adui katka maisha yako.
>kataa Kila mpango wa Adui unaozuia usitimize kusudi
>Mwambie Mungu akupe wasaidizi watakaosaidiana na wewe kutimiza kusudi. Paul alikutanishwa na Anania akayajua mapenzi ya Mungu.
>Kataa Kila mahusiano ambayo adui ameyaleta kwako ili kuzuia Kusudi la MUNGU.
Ndugu hukuumbwa kwa bahati mbaya Mungu amekuleta Duniani ili umuwakilishe kwenye Kusudi flani hajakuleta ili uwe masikin k**a ilivyo Sasa wala mlevi, ila anataka kwa wewe watu waseme hakika Mungu yupo. Hivyo tafuta sana kuyatimiza yaliyokuleta ili siku zako zikiisha upokee malipo ya kazi yako..
Mungu akubariki sana ni mimi mwalimu
Sigfrid chuwa
Kwa maombi na ushauri unaweza kunipata kwa cm
0712220381 au
0748637804

Neno la MUNGU lina Nguvu hata kuangusha ngomeZaburi 294 Sauti ya Bwana ina nguvu; Sauti ya Bwana ina adhama;5 Sauti ya B...
22/06/2021

Neno la MUNGU lina Nguvu hata kuangusha ngome
Zaburi 29
4 Sauti ya Bwana ina nguvu; Sauti ya Bwana ina adhama;

5 Sauti ya Bwana yaivunja mierezi; Naam, Bwana aivunja-vunja mierezi ya Lebanoni;

6 Airusha-rusha k**a ndama wa ng'ombe; Lebanoni na Sirioni k**a mwana-nyati.

7 Sauti ya Bwana yaipasua miali ya moto;

8 Sauti ya Bwana yalitetemesha jangwa; Bwana alitetemesha jangwa la Kadeshi.

9 Sauti ya Bwana yawazalisha ayala, Na kuifichua misitu; Na ndani ya hekalu lake Wanasema wote, Utukufu.
Karibu tujifunze neno la MUNGU litakalobadiilisha maisha yako kila siku

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Power in the word of God posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share