Adonai El Ohim Mungu Mkuu AEM

Adonai El Ohim Mungu Mkuu AEM Maono ya AEM:
1. Kuhubiri injili duniani kote, kufundisha mafundisho yenye uzima kutoka kwa walimu mb

SOMO: UJUE ULIMWENGU WA ROHO. (Utendajikazi wake na matokeo yake kwenye maisha)....15.NAMNA YA KUSHUGHULIKA NA ULIMWENGU...
19/08/2026

SOMO: UJUE ULIMWENGU WA ROHO. (Utendajikazi wake na matokeo yake kwenye maisha)....15.

NAMNA YA KUSHUGHULIKA NA ULIMWENGU WA ROHO KATIKA KULETA MATOKEO.

NAMNA YA KUSHUGHULIKA NA ULIMWENGU WA ROHO KATIKA KULETA MATOKEO.

Mungu akubariki kwa kuendelea kuwa mvumilivu kwa somo hili ambalo limekua lefu sana ila lengo ni kutaka upate maarifa ya kina kuhusu mambo ya rohoni.

Leo tutamalizia mfano wa mwisho katika somo letu.

Yesu Kristo alitabiriwa kuzaliwa, kufa na kufufuka tangu mwanzo wa mwanadamu kuasi.

Unakumbuka kwamba Mungu alisema kwa uzao wa mwanamke nyoka atapondwa kichwa na nyoka atauponda uzao wa mwanamke kisigino. Mwanzo 3:14,15.

Hapa ulimwengu wa roho tayari ulikua umeshatengeneza mpango wa Yesu kuzaliwa kuteswa, kufa na kufufuka, hii pia ilikua ni kanuni ya ulimwengu wa roho kumkomboa mwanadamu. Maana ulimwengu wa roho pia una kanuni, sheria na taratibu zake katika kukamilisha mpango wake (Hili ni somo lingine k**a Roho akinipa mafunuo tutajifunza).

Kwahiyo Yesu alipaswa kuwa uzao wa mwanamke, uzao wa mwanamke maana yake mtoto atakayezaliwa bila tendo la ndoa, maana unapaswa ujue uzao ni wa mwanaume mwanamke ana uzazi.

Pia kwenye Isaya inaonesha ni mwanamke gani atakayeleta huu uzao, maana hata aliyezaa k**a atazaa bila mwanaume pengine tungesema ndiye yule ulimwengu wa roho ulisema, lakini ulimwengu wa roho ukatoa ni mwanamke gani mwenye hiyo sifa ya kuzaa uzao wa kumponda kichwa nyoka (shetani), sifa hiyo ilikua ni BIKIRA (Isaya 7:14). Hapa tunapaona uthibitisho wa kile kitakachotokea, hapa tunapata kitu kingine kuhusu ulimwengu wa roho kwamba unasifa ya kuelekeza jambo gani litatokea, kwahiyo mambo ya ulimwengu wa roho yanatabia ya kuthibitisha ili kitakachotokea kiwe sahihi. Ulimwengu wa roho unazungumza, unahitaji masikio na macho ya rohoni ili shetani asikuchanganye. Lakini la nyongeza hapa ni kwamba Mika aliona mpaka sehemu atakayozaliwa Yesu (Bethlehem), manabii tofauti ila wanaona kitu kimoja. Hapa tunaona ulimwengu wa roho unaendelea kuthibitisha kile ambacho kilichokuwepo kwenye ulimwengu huo, kwahiyo kila kitu kilikua kilishafanyika, lakini ulimwengu wa roho unatabia ya kujifunua ili kwamba kikitokea tofauti na hapo hata k**a kinafanana fanana ila k**a kuna utofauti hata sehemu basi ujue kwamba hiko siyo shetani anataka kukupotosha.

Sasa somo lijalo tutaangalia Sababu na Matokeo, maana hapa tumeangalia chanzo.

Kumbuka kwamba hii mifano ni michache kati ya mingi inayoelezea kuzaliwa, kufa na kufufuka kwa Yesu, kumbuka pia Biblia nzima inamuelezea Yesu.

Tafadhali toa maoni yako umejifunza nini na umepata ufunuo gani katika somo hili, k**a ulipitwa na masomo ya nyuma tafadhili nitafute WhatsApp kwa namba hapo chini ili nikutumie masomo ya nyuma.

Shalom Shalom 🙏🏾

Ev. Elisha Samson
+255 716 472 317
+255 759 007 009

18/08/2026

TAFAKARI YA SIKU

SOMO:
📖UNAWEZA UKAWA UMEKUFA ILA UNAISHI.

Mambo ya Walawi 10:1-2
Na Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mtu chetezo chake, wakatia moto ndani yake, wakatia na uvumba, nao wakatoa moto wa kigeni mbele ya BWANA, ambao yeye hakuwaagiza. Kisha moto ukatoka hapo mbele za BWANA, nao ukawala, nao wakafa mbele za BWANA.

▫️Wapo wakina Abihu na Nadabu ndani ya kanisa bila wao kujijua, kuna wakati wametumia moto wa kigeni ambao umewaua wamekufa lakini wanaonekana k**a wanaishi.
▪️Hawa walikua makuhani wa Mungu, na waliwekewa mafuta yaani wakfu kwaajili ya kutumika madhabahuni, lakini wakazoelea madhabahu.
▫️Wakaacha maagizo ya Mungu na kufanya kwa akili zao. Kitu ambacho ni machukizo mbele za Mungu.
▪️Si kwamba walikua wanatarajia k**a hayo yangetokea, maana waliona ni kawaida kwenye taratibu zao za ibada, pengine walikua wanahisi Mungu atafurahia ubunifu wao, kumbe matokeo yake ikawa ni kifo kwenye maisha yao.
▫️Hapa tunapata fundisho kutoka kwao kwamba hatupaswi kufanya kwa mazoea mambo ya ki Mungu, maana yale yanakwenda kwa maelekezo ya Mungu mwenyewe, kile alichoagiza tunapaswa kukifanya, tusione k**a tunahitaji kuboresha au kurekebisha. Ndiyo maana kwenye kitabu cha Ufunuo wa Yohana 22:18-19, inatoa onyo kuzidisha au kupunguza kwenye maelekezo ya Mungu(Neno la Mungu), ataongezewa mapigo au atapunguziwa kwenye ufalme wa Mungu.
▪️Kumbe haihitaji kwenye mambo ya Mungu au maelekezo ya Mungu, kuongeza au kupunguza yale ambayo Bwana ametuelekeza.
▫️Ilikua agano la kale wakati wa Abihu na Nadabu, lakini yanatufundisha hata sasa maana 1 Wakorintho 10:11 inaeleza kwamba haya yaliwatokea wale ili yawe mafundisho na maonyo kwetu sisi katika agano jipya.
▪️K**a tunakubali kwamba agalo la kale lilikua kivuli basi tujue kwamba Mungu ni yule yule, aliyefanya kwa kina Abihu na Nadabu basi anafanya hata sasa, ndiyo maana aliweka tahadhali kwenye ufunuo na wakorintho ili tujue kwamba, k**a tutaingiza moto wa kigeni kwenye kazi ya Mungu basi tutakufa, na kwasababu ni wakati wa neema unaweza ukawa unaishi lakini umekufa kiroho. Ndiyo maana hofu imeondoka, watu wanafanya mambo ndani ya kanisa k**a watu wa mataifa. Ndiyo maana neno la Mungu limegeuzwa, wakati mwingine limeongezewa, limewekewa ubunifu, watu wamekufa kabisa kiroho, humuoni tena Roho Mtakatifu ndani ya watu, unauona ubunifu, watu hawaguswi tena kwasababu wamekufa.
▫️Lakini kwasababu neema ya Mungu ipo tunaweza kugeuka, hatujachelewa, waimbaji, wachungaj, walimu, wainjilisti, mitume, manabii, wakristo na wote walio katika njia hii ya Yesu Kristo, tunaweza kugeuka, tukatubu ili Bwana atutumia, maana Yeye ni ufufuo na uzima. Atafufua tena kazi yake katikati ya miaka hii.
▪️Geuka, wewe uliyeacha kufuata maagizo ya Mungu, kumbuka ni wapi ulijikwaa ugeuke ukatende mambo ya kwanza, wewe ambaye husikii tena hukumu ya ndani katika maisha yako unaweza rudi tena kwa Kristo akuhuishe tena maana siku zimeisha.

Aliye na sikio na asikie ujumbe huu ambao Bwana ameureta jioni ya leo.

Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.

🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi

Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/

Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]

THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO

ZANZIBAR

MUNGU AKUBARIKI

SHALOM SHALOM ✋

14/08/2026

TAFAKARI YA SIKU

SOMO: JIHADHALI USIANGUKE.
📖1 Wakorintho 10:12

Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.

▫️Aliyesimama ndiye yupo kwenye hatari kubwa ya kuanguka.
▪️Aliyesimama anahitaji kuchukua tahadhali zaidi maana yupo kwenye hatari ya kuanguka.
▫️Aliyeanguka kashaanguka, ina maana yupo chini anahitaji kuinuka.
▪️Hapa tunapata onyo na tahadhali kwenye maisha yetu ya kiroho, wengi wamesimama na wanahisi wapo salama na hawawezi kuanguka, ni kweli upo salama lakini kuna hatari kubwa ya wewe kuanguka.
▫️Tunapaswa tujue kwamba walioanguka si kwamba walipenda, bali walidhani wamesimama hawawezi kuanguka, sasa wameanguka. Ina umiza sana kuona mtu aliyesimama, mwenye huduma kubwa Mungu alimtumia kaanguka.
▪️Wengine wameanguka na misemo ikawepo mingi, tulijua kwamba huyu ataanguka. Uliedhani umesimama angalia usije ukaanguka.
▫️Ukijua kwamba ukisimama una hatari ya kuanguka, unapaswa utachukua tahadhali usianguke. Tunapowaona watu walioanguka tusiwabeze maana adhaniaye amesimama aangalie asianguke.
▪️Aliyesimama anapaswa aishi kwa unyenyekevu, kila anapoona wanaoanguka, anapaswa arudi magotini kumwambia Bwana nitie nguvu nisije kuanguka.
▫️Waliosimama wanapaswa wachukue muda mwingi kuwaombea walioanguka na wenye hatari ya kuanguka.
▪️Ukifurahia anguko la mwenzako, aliyeanguka anakungoja uanguke afurahi. Na k**a tukiishi hivyo maana yake tutaombeana maanguko.
▫️Anguko la mwanakwaya mwenzako ni anguko la kwaya, tunapaswa tuombeane sisi kwa sisi ili tusianguke ili kwaya isiingie doa. Anguko la mtumishi, ni anguko la watumishi maana wapo watakaokosa uaminifu kwa watumishi, tuwaombee watumishi Mungu aendelee kuwasimamisha imara.
▪️Usiingie kiburi kwasababu wameanguka wengi wewe upo salama, katika maanguko mengi unapaswa uombe ili usiwe miongoni mwao walioanguka.
▫️Biblia katika mstari huu, tunapewa maonyo na mahusia juu ya maisha yetu ya kiroho, tujue kwamba k**a kuna kusimama basi kuna kuanguka, tuishi kwa kujilinda, maana kuendelea kwako kusimama ni sifa na utukufu kwa Bwana Yesu wa majeshi.
▪️Walioanguka wakasimama wasijisahau wakadhani wamesimama waangalie wasije kuanguka tena.
▫️Walioanguka ni wakati wao kusimama, na wahakikishe wanajilinda wasianguke, wasiangalie waliozomea walipoanguka, wasiangalie waliowacheka walipoanguka na wala wasiwaombee mabaya watesi wao. Ni wakati wakusema usifurahi juu yangu eee adui yangu, niangukapo nitasimama. Lakini pia wakumbuke mwenye haki huanguka mara saba akaenda. Mpendwa simama.

Adhaniaye amesimama na angalie asije kuanguka, Mungu akusimamishe mwambani na uwe imara katika UTII na UNYENYEKEVU.

Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.

🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi

Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/

Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]

THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO

ZANZIBAR

MUNGU AKUBARIKI

SHALOM SHALOM ✋

12/08/2026

TAFAKARI YA SIKU

SOMO: MAISHANI KUNA KUANGUKA NA KUSIMAMA.
📖Mithali 24:16

Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena;
Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.

▫️Kuanguka ni sehemu ya maisha ya mwanadamu, unaposimama basi jua kabisa unaweza ukaanguka.
▪️Hapa sizungumzii kwenye mambo ya kiroho, ila pia kwenye mambo ya rohoni unapoona umesimama basi uwe makini kwamba unaweza kuanguka. Kwahiyo usijikweze, hii tutaitazama katika tafakari au inada ijayo.
▫️Kwahiyo kwenye mambo ya kimwili yaani haya maisha ya kawaida, mwanadamu kuanguka ni jambo la kawaida, na wala tusilichukulie kwa ukubwa ikakufanya umlaumu Mungu, ukaona k**a Mungu amekuacha au kukususa kabisa.
▪️Unapaswa kusimama na kuanguka ni sehemu ya maisha ya mwanadamu.
▫️Leo unaweza ukawa na afya tele kabisa, lakini kesho unaweza ukawa mgomjwa mahututi.
▪️Na hii imewekwa makusudi na Mungu ili watu wakifunze, ili watu wawe wanyenyekevu, hii imewekwa ili tujue kwamba maisha yanaweza kubadirika wakati wowote ili tujipange, kiakili na kisaikolojia.
▫️Asiyetaka kuanguka mara nyingi ameishia kwenye presha, magonjwa ya moyo n.k.
▪️Asiyekubali kuanguka ina maana kwamba siku akianguka hatoweza kuinuka.
▫️Asiyekubali kuanguka ni mtu ambaye anaweza kuwakashifu na kuwaona hawana akili wanaoanguka.
▪️Asiyekubali kuanguka, ni mtu anayeangalia alipoanguka, ni mtu wa lawama, visasi na uchungu siku zote. Atakua anaishi na watu mioyoni mwake, kila siku atakua ni wa kunyooshea vidole watu anaowaona k**a maadui zake ambao pengine anahisi ni chanzo cha anguko lake, mtu k**a huyu kuinuka itamchukua muda sana.
▫️Biblia katika Mithali 24:16 (BHN), leo inatuonesha waovu huangamia waangukapo, anguko lao mara nyingi limekua ndiyo mwisho wao, hawana namna ya kuanguka.
▪️Waovu waangukapo ndiyo tunasikia wamejinyonga, wamekunywa sumu, wameua au kufanya tukio ambalo litagharimu maisha yao.
▫️Mtu mwenye haki, mtu mwema, ni yule ambaye anakubali kwanza kwamba kuna kuanguka. Lakini pia anapoanguka anajua kwamba kuna kusimama tena.
▪️Huyu mtu anapoanguka anainuka, anawaambia waovu wanaofurahia anguko lake kwamba niangukapo nitasimama tena Mika 7:8.
▫️Huyu mtu anapoanguka habaki chini, anasimama na kuanza upya. Akianguka anajifunza kwamba kuna kuanguka atakaposimama anakua imara.
▪️Huyu mtu ni mtu wa msamaha siku zote, awaangalii waliomuangusha k**a maadui bali anawaona k**a daraja lililomfikisha hapo alipofika.
▫️Huyu mtu ajinyongi kwasababu anajua Mungu ndiye ainuaye waangukao.
▪️Mpendwa katika Bwana, unapaswa kujua kwamba k**a umesimama basi unaweza kuanguka, kuanguka si kwa watu wadhaifu, hata walioimara wanaanguka, kwahiyo usiogope na wala usitishwe na kuanguka.
▫️Shetani mara zote amewatega watu na kuwapoteza, kwasababu siraha kubwa ya shetani ni kukutishia kukuangusha k**a usipofuata kile anachotaka.
▪️Kwahiyo k**a kuna kuanguka basi ujue kuna kusimama pia.
▫️Usiogope kuanza upya, usikae hapo ulipo, songa mbele, shetani asikudanganye na kukutisha. Mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena, haijalishi ni mara ngapi unaanguka uwe na imani kwamba utasimama, na hautabaki k**a ulivyokua.
▪️Usiogope kuanguka kwasababu, tunajifunza kutokana na anguko la kwanza.
▫️Wenye kiburi ni watu wasiojua kwamba kuna kuanguka, ni wajinga tu.
▪️Ukijua kuna kuanguka utanyenyekea na kujishusha. Maisha ni kuanguka na kusimama.

Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.

🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi

Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/

Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]

THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO

ZANZIBAR

MUNGU AKUBARIKI

SHALOM SHALOM ✋

07/08/2026

TAFAKARI YA SIKU

SOMO: ENDELEA KUMWITA YESU, ATASIKIA.
📖Marko 10:47-48
Naye aliposikia ya kwamba ni Yesu Mnazareti, alianza kupaza sauti yake, na kusema, Mwana wa Daudi, Yesu, unirehemu. Na wengi wakamkemea ili anyamaze, lakini alizidi kupaza sauti, Mwana wa Daudi, unirehemu.

▫️Bartimayo alisimamia kile anachokihitaji, alisimama na msimamo wake mpaka apokee.
▪️Watu walimzuia, hawakutaka aendelee kupaza sauti yake, lakini msimamo wa Bartimayo ulikua ni ule ule, kwamba Yesu mwana wa Daudi unirehemu.
▫️Ni kweli alikua anapiga kelele na walikua hawataki amsumbue Yesu, au pengine walikua wanaona k**a hana hadhi ya kuhudumiwa na Yesu.
▪️Mpendwa katika kumwita Yesu, usikubali kunyamanzishwa.
▫️Simamia msimamo wako wa kuendelea kumwita Yesu kwa nguvu zako zote.
▪️Kile unachokihitaji mtu asikunyamanzishe kwa namna yoyote.
▫️Wengi wamenyamanzishwa na miujiza, wakaacha kumwita Yesu.
▪️Wengine wamenyamanzishwa kwa kukatishwa tamaa.
▫️Mpendwa Bartimayo hakutaka kunyamanzishwa kwasababu hakutaka kuendelea kuwa kipofu na ombaomba.
▪️Wengi wamebaki vipofu na ombaomba kwasababu walikubali kunyamanzishwa.
▫️Usinyamanzishwe, kuna msaada wa kumwita Yesu, tunamwita Yesu kwa njia ya maombi. Wengi wamekua ombaomba na vipofu kwasababu walikubali kunyamanzishwa na watumishi wanaotaka kuwafanya mateka, wameshindwa kuwa waombaji sasa wamegeuka kuwa waombewaji.
▪️Mpendwa katika Bwana, Bartimayo alipomwelezea shida zake Yesu hakua kipofu tena, hakua ombaomba tena.
▫️Tumia sauti yako kumwita Yesu, watu wasikufundishe namna ya kuomba, wakikwambia unaomba vibaya wapuuze, hao wanataka kukuzuia usimfikie Yesu. Kumbuka unamwita Yesu, siyo wao.
▪️Endelea kuwa na msimamo wa kuendelea kumwita Yesu, atakusikia na kuponya, hautaendelea kuwa kipofu na ombaomba.

Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.

🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi

Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/

Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]

THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO

ZANZIBAR

MUNGU AKUBARIKI

SHALOM SHALOM ✋

27/07/2026

Yohana 14:12

Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.

▫️Msisitizo wa Yesu Kristo katika andiko hili, ni kutaka kuonesha kwamba Yeye ni mwaminifu, na kile anachokisema ni hakika.
▪️Tunapaswa tujue kwamba imani ya mkristo yeyote ni kumwamini Yesu, kuamini anachosema na kuamini anachotenda, ukifanya hivyo basi utaona matokeo kutoka kwa Mungu.
▫️Kristo anataka tuifanyekazi yake ile ambayo ametuachia hapa duniani.
▪️Ili kuifanyakazi ya Bwana Yesu, tunapaswa tuamini juu ya yale aliyoyasema, halafu tuyaishi.
▫️K**a tunayaamini yale anayoyasema, tunapaswa tumwamini Yeye, kwamba anauwezo wa kutuwezesha kwa kila gumu ambalo tunaliona kwenye maisha yetu.
▪️K**a tuna mwamini Yeye, basi tuamini kazi anazozitenda.
▫️Hii inakamilisha imani yetu na kile tunachoamini, hii inatufanya tuwe na uwezo wa kufanya yale ambayo Bwana Yesu alifanya.
▪️Bila imani hauwezi kufanikiwa katika chochote katika mambo yako ya kiroho. Hivyo mpendwa katika Bwana, hatuna budi kusimama na imani hii.
▫️Uwezo wa mkristo upo katika kile anachoamini, ukitenganisha hata kimoja kati ya hivi vitatu yaani kuamini maneno ya Yesu, pili kumwamini Yesu mwenyewe na mwisho kuamini kazi zake, hauwezi kuona matokeo yoyote kwenye maisha yako.
▪️Ahadi ya Kristo ni sisi kutenda zaidi yake kwa kuendelea kumwamini.

USIMUWEKEE YESU MIPAKA, WEWE AMINI TU.

Shalom Shalom 🙏🏾

Ev. Elisha Samson
+255 716 472 317
+255 759 007 009

18/07/2026

TAFAKARI YA SIKU

SOMO: USIACHE, USICHOKE WALA USIKATE TAMAA.
📖Luka 11:9

Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.

▪️Yesu anatoa msisitizo wa maisha ya mwanadamu ya kila siku. Mwanadamu ana uhitaji, na suluhisho la majibu yetu ni Mungu wetu aliyembinguni.
▫️Unapaswa ujue kwamba Mungu ni ELISHADAI na pia YEHOVA-YIRE, Mungu ni mtoshelezi na pia ni mpaji.
▪️Jambo gumu hapa ni lini atakupatia?
▫️Swali hili linajibiwa kwamba hakuna ajuaye, ndiyo maana Biblia inasisitiza imani, kwasababu imani yetu ndiyo inaamua ni lini tupate. K**a ukikatamaa basi, ujue kwamba hautopata kile ambacho Mungu amekusudia kukupa.
▪️Katika imani kuna jambo tunaambata nalo la kutokukata tamaa, katika kutokata tamaa kuna jambo la muhimu la uvumilivu.
▫️Kutokata tamaa na kuvumilia ni jambo la msingi katika imani.
▪️Na imani ni kuamwamini kwanza Mungu yupo, ukiamini kwamba yupo, basi ujue kwamba anasikia, na k**a anasikia unapaswa ujue kwamba atajibu, lini na namna gani kwenye imani haimuhusu mwombaji.
▫️Kwahiyo imani kwa Mungu inatuhakikishia kwamba Mungu anaweza yote.
▪️Ndiyo maana hapa Yesu anafumdisha jambo la msingi na muhimu kwamba wewe omba tu, iko siku utapewa, wewe yafuta tu iko siku utaona, bisha tu wewe jua iko siku utafunguliwa.
▫️Hapa inahitaji uvumilivu, kwahiyo wewe suala la kuomba, kutafuta au kubisha halina ukomo ni suala la uvumilivu na imani juu ya Mungu wetu.
▪️Umeomba bila majibu usichoke omba, ongeza juhudi maana Mungu ni mtoshelezi na mpaji.
▫️Nik**a umetafuta kumsikia Mungu, kumuona, ni k**a unahisi watu wanadanganya wanaposema wamemsikia, huoni uwepo wa Mungu, usichoke wewe endelea kutafuta kwa wakati wake utauona usitoke kwenye line ya ki Mungu.
▪️Milango imekua migumu, haifunguki kabisa, ukiangalia wengine ni k**a wao wana funguo zao, kila wanapobisha wanafunguliwa. Mungu anachelewa kukufungulia ili akuimarishe, jambo linalochelewa lina thamani kubwa.
▫️Mambo yakiwa hayapo kwenye mamlaka yako, hauwezi kusema umechelewa au umewahi, Yeye mwenye mamlaka ndiye anajua wakati gani ni sahihi kwake kukupa kile unachopaswa kukipata.
▪️Hata Yesu alipoulizwa kwa habari ya siku za mwisho akasema hajui kwasababu hayo yapo kwenye mamlaka ya Mungu.
▫️Usiwe na hofu wala usikate tamaa. Yesu anatufundisha:-
1. Kuomba bila kukoma.
2. Kutafuta bila kuchoka.
3. Kubisha bila kukata tamaa.

Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.

🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi

Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/

Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]

THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO

ZANZIBAR

MUNGU AKUBARIKI

SHALOM SHALOM ✋

13/07/2026

TAFAKARI YA SIKU

SOMO: USIMTEGEMEE MWANADAMU.
📖Kutoka 32:1

Hata watu walipoona ya kuwa Musa amekawia kushuka katika mlima, wakakusanyana wakamwendea Haruni, wakamwambia, Haya! Katufanyizie miungu itakayokwenda mbele yetu, kwa maana Musa huyo aliyetutoa katika nchi ya Misri hatujui yaliyompata.

▫️Israeli ilikua inamuangalia Musa k**a mtu anayewaunganisha na Mungu.
▪️Somo la Mungu kuwatoa Misri kwa mkono mkuu ilikua nikutaka waweze kumjua Yeye, ili kupitia wao Mungu ajulikane kwa mataifa, taifa la Israeli Mungu hakulichagua kwa bahati mbaya, aliwachagua wawe k**a wainjilisti wakuwahubiria watu habari zake. Na ili uweze kuhubiri, unapaswa umjue yule unayepaswa kumuhubiri.
▫️Zaburi 46:10 "Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu,
Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi." Hii inatufundisha kwamba ukimjua Mungu, kupitia kumjua atakuzwa.
▪️Miujiza aliyoifanya Mungu kupitia Musa, alitaka si Musa aabudiwe bali kupitia miujiza ile wana wa Israeli wamjue Mungu.
▫️Musa alipotumwa na Mungu alimuuliza watajuaje k**a Wewe Mungu umenituma, Mungu alimuonesha muujiza ili atakapowaambia ni Mungu amemtuma wamwamini.
▪️Kitu ambacho hakikutarajiwa ni kwamba, Israeli badala ya kumjua Mungu na kumtegemea, wakamwona Musa k**a mtu anayewasemea kwa Mungu, hivyo wakaanza kumtegea, ndiyo maana walipomuona harudi wakamwambia Haruni awatengenezee sanamu.
▫️Hii haukutokea kwa bahati mbaya, kwasababu mioyo yao ilikua tegemezi kwa Musa, walimuona k**a Musa ndiye msemaji wao kwa Mungu na ndiye mleta taarifa kutoka kwa Mungu.
▪️Walimuona k**a muwakilishi wao kwa Mungu, ndiyo maana ilikua rahisi wao kutengeneza mungu wa ndama ili wamwabudu, kwasababu waliona k**a ndiye mungu wanaoweza kumfikia.
▫️Kanisa la leo tunapaswa tujifunze kwamba Mungu haitaji umtegemee mwanadamu, Mungu anataka umjue kupitia watumishi wake, miujiza ikifanyika usimuone mtumishi muone Mungu.
▪️Hasara ya kumtegemea mwanadamu ni kwamba siku asipoonekana ni rahisi kuabudu miungu, ni rahisi kurudi nyuma kuitumikia miungu ulioiacha.
▫️K**a watumishi tunapaswa kuwafanya watu wamjue Mungu, na wamtegemee Mungu, miujiza inapofanyika wanapaswa wajue ni Mungu siyo wewe ili wamtukuze Mungu kwasababu mtumishi hafanyi kwa nguvu zake.
▪️K**a vile Musa alivyokua anamtafuta Mungu ndivyo ambavyo wewe unapaswa umfuate.
▫️Mjue Mungu kupitia mtumishi wake siyo mfuate Mungu kwa mtumishi wake.

Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.

🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi

Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/

Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]

THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO

ZANZIBAR

MUNGU AKUBARIKI

SHALOM SHALOM ✋

Address

Kijichi
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Adonai El Ohim Mungu Mkuu AEM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Adonai El Ohim Mungu Mkuu AEM:

Shortcuts

Share