28/04/2026
TAFAKARI YA SIKU
SOMO: KUKAMILISHWA KUWA K**A YESU.
📖Waefeso 4:12-13
Kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; kopo8 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;
▪️Yesu ni njia ya uhakika ya kutufikisha kwenye hatma yetu, baraka na mbinguni.
▫️Lakini katika njia hii amewaweka watu wa aina tofauti tofauti kwaajili ya kuifanyakazi moja.
▪️Ametoa huduma mbalimbalu kwa kusudi la kuwafanyawatu wakamilishwe katika kumjua Yesu ambaye ndiye njia ya kweli na uzima.
▫️Biblia inasema katika Waefeso 4:11 'Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;' wengine ina maana kwamba katika huduma hatufanani na Mungu hata Mungu hataki tufanane, maana hatutakamilisha kazi yake.
▪️Kusudi la kukamilisha kazi ya Kristo limewekwa kwenye huduma tofauti tofauti katika kanisa.
▫️Mitume, manabii, waalimu, wainjilisti na wachungaji, wamewekwa kwaajili ya kulikamilisha kwa kila mtu na huduma aliyopewa.
▪️Hakuna huduma iliyobora zaidi ya huduma nyingine, hakuna huduma iliyokuu zaidi ya huduma nyingine. Maana kila huduma ina kazi yake ambayo kazi hiyo huduma nyingine haina.
▫️Hizi huduma ni k**a vifaa vinavyohitajika kwenye ujenzi, mchanga, saruji, tofali, n.k. Ni vifaa tofauti lakini vinakamilisha kazi moja ambayo baadae itaitwa jina moja na itafaa.
▪️Kwahiyo kanisa linahitaji hizi huduma. Lakini cha kusikitisha ni kwamba huduma hizi siku hizi ni k**a zimetengeneza ufa. Kuna mafundisho ya wachungaji, mitume, manabii, waalimu na wainjilisti. Aliye kwa mtume ni tofauti na aliye kwa nabii, vivyo hivyo kwa mwalimu na mwinjilisti.
▫️Tumegawanyika, kuna huduma kuu, kuna huduma ndogo. Huyu anamuona yule, huyu kwangu, huyo huku. Ubinafsi umetawala, kanisa badala ya kukamilishwa limetengeneza vibanda vibanda.
▪️Kanisa tegemezi kwenye huduma, huyu bila mchungaji, huyo bila nabii, huyu bila mtume, huyu bila mwalimu au mwinjilisti humuoni Mungu.
▫️Uponyaji, baraka, miujiza inatokea ili kuukamilisha mwili wa Kristo.
▪️Yesu anataka aonekane ndani ya mkristo. Maana sisi si wa Paulo wala wa Kefa, wala wa Apolo, sisi ni wa Kristo. Yesu anataka lijengwe kanisa moja kupitia huduma zake.
▫️Tunapaswa tuzitumie huduma hizi ili ulimwengu uone NJIA yaani Yesu Kristo. Yesu wakujue wewe Mungu wa kweli na Yesu ulimtuma... Huu ndio uzima wa milele Yohana 17:3.
▪️Kamilishwa kwa kumjua Yesu, usigawanywe na waliopewa kazi ya kuukamilisha, wao wanapojiona bora sisi tumwangalie Yeye aliyewafanya kuwa walivyo. Tusigawanywe, tuwe makini na mafundisho ya tukudumaza ila tuk**ate yale yanayotukamilisha.
▫️Nataka niwe k**a Yesu. Nitakua k**a nitamjua, katikati ya huduma tutamjua Yesu HALELUYA!
Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.
🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi
Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/
Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]
THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO
ZANZIBAR
MUNGU AKUBARIKI
SHALOM SHALOM ✋