Adonai El Ohim Mungu Mkuu AEM

Adonai El Ohim Mungu Mkuu AEM Maono ya AEM:
1. Kuhubiri injili duniani kote, kufundisha mafundisho yenye uzima kutoka kwa walimu mb

28/05/2026

Warumi 8:14

Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.

▪️Kuongozwa na Roho wa Mungu si tu katika mambo ya kiroho tu, yaani, katika huduma, kazi, biashara, mahusiano, masomo n.k
▫️Sasa basi kuokolewa ina maana kuwa unakua mwana wa Mungu. Kuwa mwana wa Mungu, hii ina maana kwamba Mungu ndiye Baba yako, unayepaswa kumtegemea, unayepaswa kumtii na kumuheshimu.
▪️Heshima na utii kwa Mungu k**a Baba ni jambo la lazima kwako.
▫️K**a sisi ni wana wa Mungu, matendo yetu yanapaswa kuwa ya ki Mungu, yaani watu wamuone Mungu kupitia sisi.
▪️Sisi k**a wana wa Mungu hatuyaepuki maisha matakatifu, tunapaswa tuishi maisha matakatifu ili kumdhihirisha Mungu kwenye maisha yetu.
▫️Kuwa mwana wa Mungu maana yake serikali ya mbingu ndiyo inawajika kukutunza na kukuhudumia.
▪️K**a tumeokolewa na sisi ni wana wa Mungu, tupendane, tusihukumiane bali tuombeane.
▫️Sifa kuu ya mwana wa Mungu ni upendo, upendo huumia na wanaoumia, upendo hufurahi na wanaofurahi, upendo auhesabu mabaya.
▪️Sisi ni wana wa nuru tuwe nuru, watu waondoke gizani kupitia sisi.

Shalom Shalom 🙏🏾

Ev. Elisha Samson
+255 716 472 317
+255 759 007 009

08/05/2026

Kutoka 8:7

Waganga nao wakafanya mfano wa hayo kwa uganga wao; na kuwaleta vyura juu ya nchi ya Misri.

▫️Kitabu cha kutoka kinaelezea namna ambavyo Mungu aliwakomboa wana wa Israeli, kwahiyo kitabu hiki ni cha ukombozi. Lakini pia kinatupa picha ya ukombozi wa mwanadamu unavyokuwa.
▪️Jambo la kutoka katika mateso au vifungo halijawahi kuwa rahisi hata kidogo, kuna vita, lawama, kutengwa na usipokua makini unaweza ukatamani ubakie kwenye hali hiyo hiyo usitoke.
▫️Lakini ukiwa na uvumilivu lazima utoke na utauona ushindi katika maisha yako.
▪️Wakati wa ukombozi wa Israeli, Mungu alikua akiipiga nchi ya Misri, alikua akifanya pigo na wachawi wa Misri nao wanafanya vivyo hivyo, hii ni ajabu kweli. Kumbe shetani naye anauwezo wa kufanya k**a afanyavyo Mungu YEHOVA, ndiyo maana shetani naye amepewa cheo cha mungu wa dunia hii.
▫️Kumbe wakati mwingine moyo wa Farao ulikua mgumu kwasababu aliona k**a hata wachawi wanaweza k**a Mungu, aliona k**a mapigo ya Mungu si kitu. Lakini pia wana wa Israeli wengine walikatishwa tamaa na wachawi maana waliona k**a huyu Mungu hawezi kuwasaidia k**a anaweza kufanya mambo ambayo wachawi pia wanaweza kuyafanya. Wanaona k**a mbona miujiza hii hii ndiyo wachawi wa Misri wanafanya, wao walikua sehemu ambayo mapigo hayakuwapata, hawakujua kwamba badala ya tatizo kutatuliwa tatizo liliongozeka.
▪️Farao alisahau kwamba wachawi walikua wanaongeza matatizo balada ya kutatua tatizo, maana Mungu alipoleta vyura na wachawi nao wakafanya vyura, waliongeza idadi ya vyura badala ya kupunguza vyura.
▫️Ni upofu tu wa Farao, shetani alimpofusha, akaona k**a tatizo limetatuliwa kumbe tatizo limeongezeka.
▪️Tunapaswa kujua kwamba katika wakati wa kutoka uchawi unatumika kuwazuia watu wasitoke. Wakati wa kutoka kuna miujiza feki inayowazuia watu wasitoke. Katika Kutoka kuna ushirikina unaowazuia watu wasitoke.
▫️Uchawi umewafanya watu waogope na kuwa na hofu, wanahisi k**a Mungu hatoweza kuwasidia.
▪️Kwa ushawishi wa ushirikina, wakati wa kutoka watu wameenda kwa waganga, ili wapate kutoka walipo.
▫️Ni kweli uchawi upo lakini, unapaswa ujue kwamba uchawi haujawahi kumaliza tatizo, bali umeongeza tatizo, usiogope wala kuwa na hofu.
▪️Ni kweli kuna watu wameenda kwa waganga wakahisi k**a wamepata ufumbuzi wa tatizo, kumbe wameenda kuongeza matatizo mengine kwenye maisha yao.
▫️Wakati mwingine miujiza feki, umesababisha watu kubaki palepale bila kutoka, badala yake matatizo yamekua matatizo.
▪️Wakati wa kutoka unapaswa kumsubiria Mungu pekee, bila kuangalia miujiza gani inafanyika, bila kuangalia ni uchawi gani unatumika. Ndiyo unapaswa kusubiri maelekezo ya Mungu wakati anashuka kuja kukuokoa dhindi ya mkono wa Farao. Amini damu ya Yesu itakutoa hapo ulipo na utafika Kanani salama.

Shalom Shalom 🙏🏾

Ev. Elisha Samson
+255 716 472 317
+255 759 007 009

28/04/2026

TAFAKARI YA SIKU

SOMO: KUKAMILISHWA KUWA K**A YESU.
📖Waefeso 4:12-13

Kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; kopo8 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;

▪️Yesu ni njia ya uhakika ya kutufikisha kwenye hatma yetu, baraka na mbinguni.
▫️Lakini katika njia hii amewaweka watu wa aina tofauti tofauti kwaajili ya kuifanyakazi moja.
▪️Ametoa huduma mbalimbalu kwa kusudi la kuwafanyawatu wakamilishwe katika kumjua Yesu ambaye ndiye njia ya kweli na uzima.
▫️Biblia inasema katika Waefeso 4:11 'Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;' wengine ina maana kwamba katika huduma hatufanani na Mungu hata Mungu hataki tufanane, maana hatutakamilisha kazi yake.
▪️Kusudi la kukamilisha kazi ya Kristo limewekwa kwenye huduma tofauti tofauti katika kanisa.
▫️Mitume, manabii, waalimu, wainjilisti na wachungaji, wamewekwa kwaajili ya kulikamilisha kwa kila mtu na huduma aliyopewa.
▪️Hakuna huduma iliyobora zaidi ya huduma nyingine, hakuna huduma iliyokuu zaidi ya huduma nyingine. Maana kila huduma ina kazi yake ambayo kazi hiyo huduma nyingine haina.
▫️Hizi huduma ni k**a vifaa vinavyohitajika kwenye ujenzi, mchanga, saruji, tofali, n.k. Ni vifaa tofauti lakini vinakamilisha kazi moja ambayo baadae itaitwa jina moja na itafaa.
▪️Kwahiyo kanisa linahitaji hizi huduma. Lakini cha kusikitisha ni kwamba huduma hizi siku hizi ni k**a zimetengeneza ufa. Kuna mafundisho ya wachungaji, mitume, manabii, waalimu na wainjilisti. Aliye kwa mtume ni tofauti na aliye kwa nabii, vivyo hivyo kwa mwalimu na mwinjilisti.
▫️Tumegawanyika, kuna huduma kuu, kuna huduma ndogo. Huyu anamuona yule, huyu kwangu, huyo huku. Ubinafsi umetawala, kanisa badala ya kukamilishwa limetengeneza vibanda vibanda.
▪️Kanisa tegemezi kwenye huduma, huyu bila mchungaji, huyo bila nabii, huyu bila mtume, huyu bila mwalimu au mwinjilisti humuoni Mungu.
▫️Uponyaji, baraka, miujiza inatokea ili kuukamilisha mwili wa Kristo.
▪️Yesu anataka aonekane ndani ya mkristo. Maana sisi si wa Paulo wala wa Kefa, wala wa Apolo, sisi ni wa Kristo. Yesu anataka lijengwe kanisa moja kupitia huduma zake.
▫️Tunapaswa tuzitumie huduma hizi ili ulimwengu uone NJIA yaani Yesu Kristo. Yesu wakujue wewe Mungu wa kweli na Yesu ulimtuma... Huu ndio uzima wa milele Yohana 17:3.
▪️Kamilishwa kwa kumjua Yesu, usigawanywe na waliopewa kazi ya kuukamilisha, wao wanapojiona bora sisi tumwangalie Yeye aliyewafanya kuwa walivyo. Tusigawanywe, tuwe makini na mafundisho ya tukudumaza ila tuk**ate yale yanayotukamilisha.
▫️Nataka niwe k**a Yesu. Nitakua k**a nitamjua, katikati ya huduma tutamjua Yesu HALELUYA!

Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.

🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi

Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/

Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]

THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO

ZANZIBAR

MUNGU AKUBARIKI

SHALOM SHALOM ✋

24/04/2026

Yohana 14:6

Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.

▪️Watu wengi wamekua wakiangalia wapi wanaelekea bila kuzingatia njia wanayopitia kuelekea huko wanapopaswa kuelekea. Wao wanatamani wafike tu hata kwa kutumia njia za mkato ambazo zinaweza kuwapoteza wasifike kule wanapotakiwa kufika.
▫️Wengi wamejikuta wanapita njia ambazo zimewachosha wamekatatamaa na hatimaye wameacha safari.
▪️Wana wa Israeli hawakufika Kanani kwasababu walitaka wafike tu bila kuzingatia njia sahihi ya Mungu.
▫️Yesu ndiye njia, wala si mwanadamu aliyepata nafasi kwenye huduma yake. Yesu ndiye anaweza kutufikisha kwenye hatma ya maisha yetu. Tuna dini na madhehebu mbali mbali, lakini hayo siyo njia inayoweza kutupeleka, yanaweza yakawa ni ya kweli lakini yasiwe na uzima maana hata madhehebu yana historia zake ambazo nyingine zimewapoteza watu.
▪️Ili uweze kufika unapaswa uijue njia, kwahiyo tunapaswa tumjue Yesu zaidi ya dini au dhehebu letu, tunapaswa tumjue Yesu zaidi ya watumishi wa Yesu.
▫️Kumjua Yesu ndiyo uzima wa milele wenyewe, mafundisho tunayoyapokea tunapaswa tuzingatie kwamba yanatuwezesha kumjua Yesu na tuweze kumfuata.
▪️Yohana 17:3 "Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma."
▫️Usipomjua Yesu unapaswa utambue kwamba hauwezi kufika kwenye kusudi la Mungu wala hatma yako.
▪️Lakini pia usitamani kumjua Yesu kwa namna ambayo mtu mwingine anamjua, maana kila mtu ana namna ya kumjua Yesu, na katika namna hiyo kusudi ni kufika kwenye kusudi moja.
▫️Mjue sana Yesu ili uwe na uhakika maana kwa Yeye unauhakika na unapoenda.

Mungu akubariki.

Shalom Shalom 🙏🏾

Ev. Elisha Samson
+255 716 472 317
+255 759 007 009

23/04/2026

Kutoka 1:17

Lakini wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, wasifanye k**a walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri, lakini wakawahifadhi hai wale wanaume.

▫️Ili Musa azaliwe, ilihitajika wawepo wazaliza wacha Mungu ambao hawatatii kauli ya uuaji ya Farao.
▪️Kwa namna moja ama nyingine, ili Mungu atimize kusudi lake la kuwaokoa wana wa Israeli, ilipaswa Musa azaliwe, na ili Musa aishi, ilipaswa wawepo wazalisha waaminifu.
▫️Ili mpango wa Mungu utimie kwenye maisha yako, unapaswa uwe na wazaliza waaminifu k**a Shifra na Pua kwenye maisha yako. Watakao simama kinyume na amri ya ulimwengu wa giza, inayotaka kuua kile Mungu alichokiweka ndani yako.
▫️Amini nakwambia, katika maisha haya wapo wazalisha katika hospitali ambao ni maajenti wa kuzimu, wanaosimama kuhakikisha watoto wenye ndoto na waliobeba hatima za watu hawaziliwa hai.
▪️Kwahiyo unapokua hospitali omba Mungu awalete wazalisha waaminifu ambao mpango wa shetani hautafanikiwa.
▫️Kwenye biashara yako wapo wazalisha ambao wameagizwa kikamilifu kuhakikisha haustawi unaishia hapo hapo ulipo, unaona mafanikio kwenye ulimwengu wa roho lakini mafanikio hao yanakufa. Omba mpendwa katika jina la Yesu Mungu awalete wazalisha wacha Mungu watakaofanya kinyume na washirikina na roho za hasara.
▪️Kazini kwako wapo pia wazalisha maajenti wa kuzimu waliotayari kwaajili ya kuhakikisha hapigi hatua yoyote, wanaweza kuonekana k**a wanakusaidia kumbe lengo lao kuua kile kilichopo ndani yako kisiweze kuzaliwa. Oh omba kwa jina la Yesu Kristo, Mungu alete wazalisha waaminifu watakao kaidi amri ya Farao, mwenye wivu ambaye ameapa hataki wewe ufanikiwe.
▫️Iwe ni hospitali, Kazini, kwenye biashara, katika jina la Yesu Kristo, Mungu ataleta wazalisha wacha Mungu, ambayo watahakikisha Musa wa kututoa utumwani anazaliwa, Musa wa kutuvusha bahari ya shamu anazaliwa. Musa ambaye atanyoosha mikono yake katika kila vita tutashinda. Hii itafanyika katika jina la Yesu Kristo aliyehai.

Shalom Shalom 🙏🏾

Ev. Elisha Samson
+255 716 472 317
+255 759 007 009

21/04/2026

TAFAKARI YA SIKU

SOMO: MUNGU KWANZA.
📖Waebrania 11:17-19

Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee; naam, yeye aliyeambiwa, Katika Isaka uzao wako utaitwa, akihesabu ya kuwa Mungu aweza kumfufua hata kutoka kuzimu; akampata tena toka huko kwa mfano.

▫️Imani si jambo rahisi, na halijawahi kuwa rahisi k**a watu tunavyodhania. Tunapoangalia imani ya Ibrahim k**a mfano kwenye maisha yetu, tunapaswa tutambue kwamba Ibrahimu alikua ni mwanadamu k**a mimi na wewe.
▫️Wengi wetu teichukua hii habari kwa kufumdishia bila kuiangalia kwa udani zaidi na kutafakari na kuvaa viatu vya Ibrahimu.
▪️Kabla ya kuelezea ugumu wa kufanya maamuzi k**a ya Ibrahimu, tunapaswa kujua kwamba Ibrahimu ana historia ya kumtii Mungu katika mazungira ambayo mimi na wewe leo hii siyo rahisi kuyakubali. Alitii kwenda nchi ambayo haijui na hajawai kuiona hajui atakutana na nini na atafanya nini maana hana historia nayo, yaani nchi ambayo hajui ikoje pengine hata kuisikia hajawahi kuisikia, aliwaacha ndugu zake, dada, kaka n.k ambao wengekua msaada k**a angepata shida au tatizo lolote katika maisha yake k**a ambavyo wengi tuna mtazamo huo.
▫️Mpendwa katika Bwana, mambo ya imani siyo ya kuyachukulia kawaida kawaida.
▪️Biblia inasema kwamba Ibrahimu alikubali kumtoa mwanaye wa pekee. Kwanini Biblia inasema mzaliwa wa pekee? Kwani si Ibrahimu alikua na Ishmaeli. Hii ina maana kwamba mapenzi ya Ibrahimu yalikua kwa Isaka, alikua mtoto pekee ambaye Ibrahimu alikua ameweka tumaini na matarajio kwake.
▫️Unafikiri k**a Ibrahimu aliambiwa amtoe Isaka lilikua jambo jepesi. Ni kweli alikua anaamini kwamba Mungu anaweza kumfufua, lakini kumbuka mwanadamu anaingalia leo yake, tumaini la baadae mara zote linaweza kumuweka njia panda na pengine akakata tamaa. K**a alizaa na mjakazi, ina maana kuna wakati alijaribiwa kwasababu uvumilivu ulimshinda na pengine aliona k**a ahadi ya Mungu inachelewa. Ndiyo Ibrahimu alikua mwanadamu pia, wewe unafikiri k**a angemtoa sadaka Isaka, ingechukua muda gani mpaka Isaka kufufuliwa kwa mujibu wa imani yake? Hilo ni fumbo.
▪️Kwanini Mungu anataka Ibrahimu amtoe mwanae wa pekee, kwanini hii ilikua ni kipimo cha imani kwa Ibrahimu? Kwasababu Mungu aliuona upendo mkubwa wa Ibrahimu kwa Isaka mwanae. Kwahiyo alitaka ajue k**a Isaka amechukua nafasi ya Mungu kwenye moyo wa Ibrahimu?
▫️Kwahiyo kile kitendo cha Ibrahimu kukubali kumtoa Isaka, ilitosha kumuonesha Mungu kwamba hakuna kitu chochote kwenye maisha ya Ibrahimu kinaweza kuchukua nafasi ya Mungu.
▪️Kumbe kwenye maisha yetu tusipokua waangalifu kuna watu au vitu vinaweza kuchukua nafasi ya Mungu, na k**a vikichukua nafasi ya Mungu basi ujue iko siku Mungu anaweza kukujaribu na k**a hautakubali unaweza kuvipoteza.
▫️K**a Ibrahimu asingemtii Mungu kwa kumtoa Isaka kwasababu zozote zile, basi Mungu angeweza kumharibu Isaka, na pengine Isaka angekua tanzi kwa Ibrahimu, angekua mateso kwa Ibrahimu na hata angetafuta msaada asingeupata.
▪️Tunapaswa tutambue kwamba Mungu anapaswa kuwa wa kwanza kuliko kitu chochote kwenye maisha yetu, na k**a kazi, mume, mke, mzazi, biashara zikichukua nafasi ya Mungu kwenye maisha yetu vinaweza kugeuka sumu kwenye maisha yetu na mwisho wa siku tukapoteza amani maishani mwetu.
▫️Tunapompa nafasi Mungu ya kwanza kwenye maisha yetu basi atatuzidisha na kutuongeza kwa namna ya ajabu.
▪️Ndiyo maana mwanzo 12:15-18, Mungu anaapa kumzidisha, na kumuongezea maana alijitoa kwaajili ya Mungu.
▫️Vilevile hata kwetu sisi k**a vitu vitachukua nafasi ya Mungu basi Mungu ataapa kuviondoa au kuvipunguza kwasababu Mungu ni Mungu mwenye wivu. Si rahisi, omba neema ya Mungu akusaidi kujikana na kuubeba msalaba.

Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.

🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi

Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/

Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]

THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO

ZANZIBAR

MUNGU AKUBARIKI

SHALOM SHALOM ✋

17/04/2026

TAFAKARI YA SIKU

SOMO: USIMTEGEMEE MWANADAMU.
📖Kutoka 1:8

Basi akainuka mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu.

▫️Kuna wakati ukiishi kwa kumtegemea mtu, siku huyo mtu akiondoka na akatokea mtu mwingine unaweza ukapata shida.
▪️Mwanadamu anahitaji kumtegemea Mungu pekee.
▫️Siku zote kumtegemea mwanadamu kunakufanya mtu awe na kiburi na dharau kwa watu wengine.
▪️Lakini pia unapomtegemea mwanadamu kwa nafasi yake, nafasi yake siyo ya kudumu kuna wakati atatoka katika nafasi hiyo. Matokeo yake utaishi kwa taabu na shida, utaishi kwa kusimangwa na watu. Nafasi ya huyo ikichukukiwa na mtu mwingine unaweza kupata shida na mahangaiko.
▫️Akainuka Farao asiyemjua Yusufu, akaanza kuwatendea mabaya, hii ni kawaida ya maisha akiinuka mwingine asiyemjua unayemjua, unaweza kupata shida na unaweza ukapoteza nafasi yako.
▪️Kitu pekee kitakachokufanya wewe usipate shida atakapoinuka Farao asiyemjua Yusufu ni wewe kumtegemea Mungu pekee. Mungu ndiye anadumu milele, Mungu ndiye hufanyika msaada kwenye maisha wakati wowote.
▫️Ukimtegemea Mungu hautakua mtumwa wa wanadamu, ni watu wangapi wamefanya mambo yasiyompendeza Mungu kwasababu ya kuwategemea wanadamu. Ukimtegemea Mungu una uhakika wa kufanikiwa popote hata k**a hapo watakukataa, tena kukataliwa kwako kwa kukataa kuwategemea wanadamu ndiyo njia yako ya kwenda katika kilele cha mafanikio yako.
▪️Mungu ndiye Yehova-Yire (Mungu atupaye), yaani tunapata vitu ambapo tuna uhitaji. Lakini Mungu ni ELISHADAI (MTOSHELEZI), yaani kwake kuna uhakika wa kila kitu, kwahiyo ukimtegemea Mungu hauwezi kuna na hofu pale ambapo kuna upungufu.

Mungu akubariki na uwe na tafakari njema.

🔗Usisahau kubonyeza hapa halafu bonyeza LIKE ili uendelee kuwa nasi-https://www.facebook.com/Adonaielohi

Instagram: https://www.instagram.com/adonaielohi/

Ev. Elisha Samson
☎+255716472317
☎+255759007009
📧 [email protected]

THE FREE PENTECOSTAL CHURCH OF TANZANIA (FPCT)
TOMONDO

ZANZIBAR

MUNGU AKUBARIKI

SHALOM SHALOM ✋

16/04/2026

Luka 12:2

Lakini hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa, wala lililofichwa ambalo halitajulikana.

▫️Siri ni kitu ambacho kipo ndani ya mtu bila mtu mwingine kujua wala kufahamu nini kilichopo ndani ya mtu huyo.
▪️Siri ni mambo yanayotendeka kwa uficho bila watu kujua.
▫️K**a ni siri mtu mwingine ni ngumu kukifahamu. Na hata k**a akijaribu kukitafuta ili akijue anaweza kutumia akili nyingi, anaweza kuingia katika hali ya kujiumiza moyo wake na asipate majibu kabisa mwisho wa siku akapata magonjwa ya msongo wa mawazo na moyo, kwasababu unatafuta jambo la siri.
▪️Watu wengi katika dunia hii wameingia kwenye matatizo kwasababu ya kutafuta mambo ya siri, mambo wanayoyahisi, mambo yaliyoyasikia ambayo hawana uhakika nayo.
▫️Watu wengine wamefanya maamuzi ya kuwagharimu maisha yao na pengine kupata hasara zisizo na sababu kwasababu ya mambo ya siri. Nasisitiza siri maana yake ni jambo ambalo halijawa wazi hata k**a unahisi kwamba upo sahihi lakini k**a halijawa wazi hilo ni siri. K**a halijawa wazi inawezekana k**a utajaribu kutaka kulitafuta unaweza kudanganyika.
▪️Lakini pia kuna watu ambao wanafanya mambo mabaya kwa siri ili kuwaficha watu. Wengine pia wanafanya mambo mazuri kwasababu ili kuwaficha watu ili iwe surprise kwao.
▫️Biblia inasema kwamba hakuna jambo la siri ambalo halitawekwa wazi, liwe zuri au baya. Umejipangaje? Maana watu wengi wamepoteza maisha yao kwasababu ya mambo ya siri kuwa wazi na hatimaye kupata mshtuko, na kuna watu wamepoteza wapendwa wao kufanya mambo kwa siri, baada ya siri zao kujulikana uaminifu wao umetiliwa shaka, wengine kupelekea kutoaminiwa kabisa. Shida siyo zuri au baya, shida ni siri.
▪️Tunapaswa kujua kwamba siri zetu kwa Mungu ziko wazi, maana sifa ya Mungu ni Mungu aonaye sirini na k**a Yeye anaona sirini basi Yeye ndiye anaziweka wazi siri zote. Chochote unachokifanya basi unapaswa kujua kwamba Mungu wa mbinguni anakuona, wanadamu unaweza kuwaficha lakini siyo Mungu. Unapaswa kujua Mungu anaona sirini, unapojificha Yeye anaona, mipango yako yote Yeye anaijua, mawazo yako Mungu anayajua. Kwahiyo uwe unafahamu kwamba usifanye lolote baya unafikiri unamficha Mungu hapana, chukua tahadhali geuka. Lakini pia kwanini uumize moyo wako kwa kutafuta mambo ya siri usiyoyajua? Yesu anasema yoyote yaliyofanywa kwa siri yatawekwa dhahiri, kwanini uwe na hofu na mipango yao wanaifanya gizani juu yako? Hata k**a ukiijua unaweza usibadirishe chochote maana ukizijua siri zao bado wanaweza wakatafuta namna ya kukuficha ili mipango yao itimie. Unachopaswa kujua kwamba iko siku mambo ya siri yatawekwa wazi. ▫️Je, siku mambo yako ya siri yakiwekwa wazi, nini kitatokea? Aibu, maumivu au la? Mungu k**a anaona sirini basi tujitafakari tunayoyafanya sirini, lakini pia usiwe na presha, usiwe na mawazo (stress) juu ya mambo ya siri kwasababu iko siku yatawekwa wazi.
▪️Haijalishi wamepanga nini sirini, au wanafanya nini sirini. Wewe mwambie Yesu, mipango yao haitofanikiwa na iko siku wataumbuka na kuwa vichwa chini.

Mungu akubariki.

Shalom Shalom 🙏🏾

Ev. Elisha Samson
+255 716 472 317
+255 759 007 009

Address

Kijichi
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Adonai El Ohim Mungu Mkuu AEM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Adonai El Ohim Mungu Mkuu AEM:

Share