25/06/2023
UFUFUO NA UZIMA PUGU.
BABA YETU: ASKOFU ELIDADI GWITEGO
TAREHE: 25/6/2023
SOMO: IBADA YA MIUNGU NA FAMILIA ILIYO MILIKIWA.
-Familia tulizo tokea ni familia zilizo kuwa zikiabudu miungu. Na familia hizo zilikuwa zikimilikiwa na iyo miungu kwa kuwa kila kitu walicho kuwa wakikiomba na kukifanya lazima wafanye kupitia miungu wanayo iabudu. Na ndipo hapo izo familia zikamilikiwa na miungu mingine na kuwa mali za mashetani.
-Na sisi tumezaliwa katika familia ambazo zilimilikiwa.
Ufunuo wa Yohana 2:13
[13]Napajua ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani; nawe walishika sana jina langu, wala hukuikana imani yangu, hata katika siku za Antipa shahidi wangu, mwaminifu wangu, aliyeuawa kati yenu, hapo akaapo Shetani.
-Hapa tunaona katika maandiko kuwa tunatokea katika familia ambazo shetani alipata nafasi ya kuendesha maisha yao.
-Ila katika yote tunaweza kusambalatisha kwa kutumia upanga wa Rohoni kwa kufyeka na kuteketeza unaweza kuharibu madhabahu zote ambazo walikuwa wanatumia watu wa zamani katika miungu yao na kuweka Madhabahu ya Mungu wa kweli. Ambayo inaweza kuharibu na kusimamisha agano ambalo Mungu aliliweka kwa watu wake.
-Tunapaswa kushika sana jina la Mungu wetu na upanga wa rohoni kwakuwa upanga wake unamakali pande zote mbili hakuna adui ambae ataweza kusimama mbele yako.
-Tunapaswa kuwa waaminifu ndani ya bwana wetu na kubeba upanga wa rohoni ili kuweza kushindana na maadui katika ulimwengu wa rohoni.
-Wakolosai 1:13
[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
-Mwanzoni tulizaliwa katika familia zinazo abudu miungu, tulipo mwamini Yesu kuwa bwana na mwokozi wetu akatuamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana wa pendo lake ambae katika yeye tuna msamaha wa dhambi. Lazima kujua kuwa kabla ya kuokoka ulikuwa katika familia ambayo inaongozwa na shetani kupitia miungu ya mababu zetu na baada ya kuokoka unaingia katika ukoo wa Yesu na umeokolewa katika dhambi.
- Katika hali ya kimwili bado ni mwana familia ila katika upande wa rohoni mtu unakuwa upo katika wokovu wa Yesu kristo ambako hakuna nguvu za giza kuna kukombolewa, kufutiwa dhambi na kuwa na uhakika wa maisha ya milele kwakuwa utakuwa unaishi maisha ya wokovu ambayo Mungu amewaandalia wale wote walio kubali kuwa wana wake. Kwa kutumia silaa za vita za rohoni ambazo huteketeza yale maagano yote ambayo mababu zetu walikuwa wakiyaishi kabla ya kumkubali na kumpokea bwana wetu Yesu kristo.
-Na katika kuamishwa katika ulimwengu wa giza na kwenda katika ulimwengu wa nuru lazima uwe na silaa za kuwashinda watu wa ulimwengu wa giza kwakuwa bado watakuwa wanakutafuta kwakuwa mwanzo walijimilikisha maisha yako. Hivyo unapaswa kuvaa silaa za rohoni jina la Yesu na damu ya Yesu juu ya upanga ukatao kuwili ili kuweza kuwashinda katika kweli.
-Ufunuo wa Yohana 5:9-10
[9]Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,
[10]ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.
-Mungu amekufanya uwe kuhani na uwe mmiliki na katika maombi utakayo kuwa unaomba unaomba kanakamba wewe ni mmiliki wa pendo la Yesu kwaiyo chochote kilichopo duniani unapaswa kumili.
-Maandiko yote yaliyopo katika kitabu kitakatifu cha biblia hayafanyi kazi kwa sababu yameandikwa ila yanafanya kazi kwakuwa watu wameyajua na kuyaelewa sawa sawa na maandiko yanavyo sema kwa kuamini kwako.
-Anae sikia na kuyafanyia kazi atainuka na kumea sawa sawa na maandiko yanavyo sema. Na mtu atakae soma na kuacha k**a yalivyo hato badilika kamwe.
Waamuzi 6:12-13
[12]Malaika wa BWANA akamtokea, akamwambia, BWANA yu pamoja nawe, Ee shujaa.
[13]Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu, ikiwa BWANA yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliyotuhadithia baba zetu, wakisema, Je! Siye BWANA, aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa, naye ametutia katika mikono ya Midiani.
-Tunaona Gideon anafaham ya kuwa kuna vitu ukiwa na Mungu haviwezi kukupata.
Mungu yupo na sisi ila watu wake hawajui k**a Mungu yupo nao. Unapaswa ujue kuwa Mungu yupo na wewe ili kila unacho kiomba kipate kibali mbele zake ndipo anapo tenda kazi zake.
-Watu wengi walio okolewa na damu ya Yesu hukata manaa sana kwa sababu ya roho za mizimu zinazo endelea kutenda kazi ndani yake.
Waamuzi 6:12,25-26,28
[12]Malaika wa BWANA akamtokea, akamwambia, BWANA yu pamoja nawe, Ee shujaa.
[25]Ikawa usiku uo huo BWANA akamwambia, Mtwae ng’ombe wa baba yako, yaani ng’ombe wa pili, wa miaka saba, ukaiangushe madhabahu ya Baali, aliyo nayo baba yako, ukaikate Ashera ile iliyo karibu nayo;
[26]ukamjengee BWANA, Mungu wako, madhabahu juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; ukamtwae yule ng’ombe wa pili na kumtoa awe sadaka ya kuteketezwa, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata.
[28]Hata watu wa mji walipoondoka asubuhi na mapema, tazama, madhabahu ya Baali imebomolewa, na ile Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na yule ng’ombe wa pili ametolewa sadaka juu ya ile madhabahu iliyojengwa.
-Katika madhabau za kimiungu ikivunja lazimaa uyapenyaa zaidi.
-mizimu na majoka yakishapigwa haku kitu ambcho kitaweza kunyanyuka tena katika maisha yako.
- Na baada ya kutoka katika kuabudu ibada ya mizimu na kuwa katika nuru vifungo vyote vinakatika katika biashara, katika afya katika masomo katika uchumi na katika famili kwa ujumla. Kumiliki na kutawala kunakuwa ndani yenu na kuishi kusudi la Mungu duniani linapata kutimia.