27/08/2022
Yeremia 18: 1-6.
1 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa BWANA, kusema,
2 Ondoka, ukashuke mpaka nyumba ya mfinyanzi, na huko nitakusikizisha maneno yangu.
3 Basi nikashuka mpaka nyumba ya mfinyanzi, na tazama, alikuwa akifanya kazi yake kwa magurudumu.
4 Na chombo kile, alichokuwa akikifinyanga, kilipoharibika mkononi mwake yule mfinyanzi, alikitengeneza tena kuwa chombo kingine, k**a alivyoona vema yule mfinyanzi kukifanya.
5 Ndipo neno la BWANA likanijia, kusema,
6 Ee nyumba ya Israeli, je! Siwezi mimi kuwatendea ninyi vile vile k**a mfinyanzi huyu alivyotenda? Asema BWANA. Angalieni, k**a udongo ulivyo katika mkono wa mfinyanzi, ndivyo mlivyo ninyi katika mkono wangu, Ee nyumba ya Israeli.
Sisi ni chombo cha udongo mbele ya mikono ya Mungu wetu atak**a tumeharibika kiasi gani anaweza kutufinyanga tena vile apendavyo Yeye.
Haijalishi maisha yameharibu umbo lako kiasi gani, Mungu anaweza kukufinyanga tena.
Haijalishi mahusiano yamevuruga muonekano wako kiasi gani Mungu anaweza kukufinyanga tena.
Haijalishi umevunjika moyo kiasi gani, Mungu anaweza kukufinyanga tena hali wewe ni chombo cha udongo kwenye mikono yake na Yeye ni mfinyanzi.
K**a vile plastic urudishwa kiwandani na kuundwa tena kitu kingine, K**a vile chuma urudishwa kiwandani na kuyeyushwa na kuundwa kitu kingine vyote havina usemi mbele ya muundaji
Je wewe umeharibika kiasi gani Mungu asiweze kukufinyanga tena na kukuunda tena vile apendavyo Yeye?
Hivyo ndiyo atakavyo kufinyanga na kukuunda tena vile apendavyo Yeye ukirudi kwake na kunyenyekea mbele zake haijalishi umevunjika moyo kiasi gani.....
Wewe rudi kwenye mikono yake Mungu wetu tena na umpe nafasi akufinyange tena vile apendavyo. Hakuna jambo lisilowezekana kwake.