10/11/2021
PAMBANO KUU
Kwa namna fulani hatujui ni kwa nini hasa dhambi ilizuka katika viumbe vikamilifu vya Mungu, na kwamba dhambi hiyo ikawa ni mwanzo wa kile tunachokielewa k**a "Pambano kuu". Hata hivyo tunajua jambo moja, na tunalijua vizuri sana pia kwamba : k**a wanadamu tumenasa katikati ya pambano hili kuu. Ni pambano ambalo kati yetu hakuna awezaye kulikwepa.
Ufunuo 12 : 7-9, Biblia inasema kulikuwa na vita mbinguni. Hatujui vita mbinguni inamaanisha nini; yaani, hatujui ni aina gani ya mapambano halisi yaliyopiganwa zaidi ya kutupwa shetani na malaika zake. Ukweli ni kwamba Biblia haisemi chochote kuhusu matokeo ya kimwili ya mgogoro huu uliotokea mbinguni badala yake inashughulika na matokeo yake ya kiroho hapa duniani
Katika kiini cha vita siku zote huwa kuna swala linalogombaniwa, linaweza kuwa masuala ya mipaka, maslahi ya kiuchumi, kitamaduni au itikadi kali. Vita ya mbinguni k**a inavyoelezwa na unabii wa ufunuo licha ya kutopiganwa kwa zana za kidunia, haijapungua katika ukali. Ni vita ya kiroho, ikiwa na taswira za kimaadili na kisheria. Suala linaloshindaniwa ni sheria ya Mungu.
Shetani si msh*taki wa ndugu tu pia ni msh*taki wa Mungu. Amekuwa akidai kuwa sheria za Mungu si za haki na ni za kidhalimu. Jambo hili sasa ni lazima liamuliwe katika uwanja wa vita wa ulimwengu ambao ni utii wa mwanadamu. Wakati ibilisi anatumia udanganyifu, kupotosha ukweli, kupiga vijembe, kulazimisha uharibifu na silaha zingine za aina hiyo, silaha aliyoichagua Kristo ni upendo
Pambano kuu lilikuja duniani wakati Shetani alipowadanganya Adam na Hawa kwa ulaghai na udanganyifu, akageuza utii wao kutoka kwa Mungu kwenda kwake mwenyewe. K**a wangeendelea kuwa waaminifu kwa kile ambacho Mungu alikuwa amewaambia, k**a wangetii maagizo yake rahisi, dunia hii tunayoijua pamoja na maumivu yake, majaribu na mateso visingekuwepo kamwe.
Katika kushughulikia hili janga, Mungu ambaye alikuwa ameliona hili likitokea "kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu (Efe 1: 4), aliandaa mpango wake wa wokovu. Ni ule ambao tunaujua k**a mpango wa ukombozi na si mwingine zaidi ya kumtoa mwanaye pekee kuja kurejesha imaya iliyokuwa imeporwa kutoka kwa Adam na Hawa. Yesu alifaulu mahali ambapo Adam alishindwa.
Yesu alipata ushindi dhahiri pale msalabani, sikuzote changamoto imekuwa ni mahali tunapoweka utii wetu, upande ulioshinda au upande ulioshindwa. Pambano bado linapamba moto na udanganyifu upo siku zote, vita juu ya mioyo na akili zetu inaendelea kwa hiyo tumaini na ombi letu ni kwamba kwa neema ya mungu tuujue udaganyifu wa shetani na hivyo itusaidie siyo tu kumchagua Kristo, gali pia kuendelea kuwa naye kwani, k**a alivyoahidi "atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokoka" (Mt 24 : 13).
MUNGU AKUBARIKI UNAPOTAFAKARI UJUMBE HUU