Fanuel Kijoji

Fanuel Kijoji page hii ni kwa ajili ya mafundisho ya Neno la Mungu na mambo mengine yayohusiana nayo.

Faragha za wanafunzi wa kikristo au Christian Unions ( CU ) zimekuwa na nafasi kubwa ya kupenyeza injili katika taasisi ...
20/12/2022

Faragha za wanafunzi wa kikristo au Christian Unions ( CU ) zimekuwa na nafasi kubwa ya kupenyeza injili katika taasisi za elimu ya juu ambapo ndio kiwanda cha kutengeza wataalamu mbali mbali katika nchi hii.

Faragha za wanafunzi wa kikristo zimekuwa na mchango mkubwa katika kueneza injili katika maeneo ambayo makanisa mengi imekuwa vigumu kufika.

Faragha za wanafunzi zimekuwa kitovu cha mafunzo ya neno la Mungu kwa vitendo. Program za mafunzo kwa vitendo k**a vile uinjilisti , maombi n.k ni moja ya program ambazo zimekuwa changamoto sana katika makanisa mengi.

Kwa hiyo kuna kila sababu kwa makanisa kushurikiana na hizi faragha za wanafunzi katika kueneza injili na kuandaa watumishi.

Uhitaji wa kifedha, walezi na waalimu ni mkubwa sana katika hizi fellowship . Kimbilio pekee la hizi fellowship Ni makanisa ya mahali pamoja , associate members na waamini wengine.

Saidiana na MUNGU kuandika historia njema ya maisha yako.Mungu ndiye mtunzi ila wewe ndiye mwandishi,  andika kile alich...
25/11/2022

Saidiana na MUNGU kuandika historia njema ya maisha yako.

Mungu ndiye mtunzi ila wewe ndiye mwandishi, andika kile alichokusudia , usizitegemee akili zako mwenyewe.

Only 45 days!!Don't plan to miss
24/10/2022

Only 45 days!!
Don't plan to miss

  Kupima.Sio kila huduma ( ministry )  inayoinuka / kanisa linalochipuka ni feki.Kuna kitu kipya  ambacho hakipo mahali ...
19/05/2022

Kupima.

Sio kila huduma ( ministry ) inayoinuka / kanisa linalochipuka ni feki.
Kuna kitu kipya ambacho hakipo mahali unaposali Unaweza kujifunza.

Vile vile sio kila huduma inayoinuka au kanisa linalochipuka ni la kuaminika.
Wengine feki wanataka kutumia ujinga k**a kigezo cha kuwatumikisha watu.

Jifunze kupima.
Ndio alisema tutawambua kwa matunda yao.

Lakini embu jiulize , vipi k**a wewe ndio hilo shamba?
Upo tayari kusubiri matokeo?
Upo tayari kusubiri uone ni zao gani litamea ndio ufanye maamuzi ?
Vipi k**a yatakuwa matokeo hasi.

Wengi wameona isiwe kesi , wameamua kujiaminisha kuwa hakuna jipya Kwenye hizi huduma na haya makanisa.

Je ni kweli?

Jibu ni hapana.

Yapo mengi ya kujifunza ambayo pengine Mfumo / msingi wa kanisa / kusanyiko / dhehebu ulilopo huwezi kujifunza au hairuhusiwi kufundisha kutokana na sababu za kimapokeo ( Dogmas )
Kwa hiyo Ukiona kuna huduma imeinuka nje ya kusanyiko ulilopo pengine pioneer wake alikuwa mtu wa kwenu ila ameamua kuanzisha hiyo huduma pembeni kidogo ,embu punguza spidi kidogo , weka hisia pembeni , tafakari katika misingi ya neno , kabla hujaanza kuzungumza kinyume na huyo mtumishi , kabla hujaanza kumwita majina ya ajabu ajabu , feki , msaliti , mlafi wa madaraka ,mpenda fedha n.k

Vile vile tafakari kwa kina kabla hujaanza kutoa support yako ya kifedha n.k

Kwa sababu kwa kusaidia huduma feki itajiungamanisha na madhara pasipo kujua , vile vile kwa kusaidia huduma ya kweli utajipatia thawabu mbele za Mungu.

Kwa sababu billia inasema:
Mathayo 10:40-42
[40]Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma.

Vile vile kanisa la thiaira lilionywa kuhusu manabii wa uongo:
Ufunuo wa Yohana 2:20-23
*Lakini nina neno juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yezebeli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu. ]Nami nimempa muda ili atubu, wala hataki kuutubia uzinzi wake. Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake; nami nitawaua watoto wake kwa mauti.
Kwa hiyo ni vyema ukajua kupima kila huduma katika misingi ya neno ili uweze kunufaika na huduma ambazo Mungu anaziinua.Kwa mtu aliyeoka , na Roho mtakatifu yupo active ndani atajua tuu hapa kuna kitu hakipo sawa.Roho mtakatifu ni mwaminifu ataku alert tuu.
Tatizo ni kwamba k**a haupo vizuri Kwenye neno na umdhaifu rohoni Hisia zinaweza kukuzidi kete ukajikuta unampotezea Roho mtakatifu.Na hawajamaa feki wanajua sana kucheza na hisia za watu hawajagi kichwa kichwa , they are professional killers in the spirit
Ulimwengu wa sasa unapiga hatua sana katika eneo la maarifa.
Sio elimu - Dunia tuu , maarifa ya kiroho yanaongezeka kwa kasi sana.
Madamu ule Mwisho haujafika , Bado kuna vitu vingi sana hatujavijua , Bado kuna kweli nyingi sana zitazidi kufunuliwa.
Madamu hutajifikia katika ule ukamilifu , hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo basi kuna mengi sana ya kujifunza.

Kwa nini ipo hivi ?
Kwanza ni hatari sana kupokea huduma inayoinuka katika ya kusanyiko bila kuwa na uhakika wa hiyo huduma.
Pili , madhehebu / makanisa / huduma zilizopo ni kazi ya Mungu ambayo kwa sehemu fulani inajumuisha utashi wa kibinadamu yaani pioneers.Kwa hiyo inaweza kuhitaji mabadiliko makubwa sana ya kimfumo ili kuondoa hicho kiasi cha utashi kilichotumika kitu ambacho wengi hawawezi kuvumilia kwa sababu zisizo na mashiko kiroho ( sababu binafsi ).Na kwa sababu hawapotayari kubadili hiyo misingi ni ngumu sana hizi huduma mpya kufanikiwa katikati ya hilo kusanyiko kwahiyo wengi

Je , kiwango cha utashi wa kibinadamu kilichotumika kinafanana dhehebu moja na jingine?
Jibu ni hapana
Kiwango cha utashi kilichotumika kinatokana na kiwango cha ufahamu alichokuwa nacho huyo pioneer kipindi anaanza hiyo huduma.kwa hiyo haiwezekana ukakuta kuna dhehebu lipo perfect 100 % ingawa yametofautiana level of perfection kutokana na bidii yayoweka katika kulisoma na kulifafanua neno , kumtafuta Mungu Na hatua ya ukuaji kiroho ( growth stage which has nothing to do with the age ).

Kitu pekee ambacho Unaweza kufanya ili kuhakikisha hubaki nyuma kiufahamu , ni kijikita katika kusoma na kulifafanua neno katika nuru ya Yesu Kristo yaani kazi ya msalaba.
Update your mind day after day

Hapa lazima utahitaji waalimu waliojikita kutoa mafundisho ya kitume ili wakutengenezee msingi imara , kwa kufanya hayo utajijengea uwezo mzuri wa kuchambua huduma inayoinuka kila siku.
Kwa nini mafundisho ya kitume?
Waefeso 2:20 biblia yasema:
[20]Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.

Mitume katika kutufundisha , manibii katika kututhibitisha.

Yaani Mitume kwanza , manabii baadae.

Shalom.

Aliyemgonjwa , asimkimbie tabibu.Yesu , tabibu wa kweli.
19/03/2022

Aliyemgonjwa , asimkimbie tabibu.
Yesu , tabibu wa kweli.

TULIA KWA BWANA muendelezo........Biblia inasema  2 Petro 3:9Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, k**a wengine wanavyokud...
17/03/2022

TULIA KWA BWANA
muendelezo........

Biblia inasema
2 Petro 3:9
Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, k**a wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.

Madam upo hai , bado lipo tumaini kwako. Usimkimbie Mungu , rudii atakupokea. K**a yule mwanampotevu alipokelewa na Baba yake kwa furaha si zaidi kwa baba yetu aliyembinguni.

Neno la Mungu lasema
Luka 15:7
Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu.

Ni Mungu wa rehema kwa sababu tupo sisi tunaohitaji rehema zake ili tuendelee kuwa Karibu yake.

Unajua tofauti kubwa kati ya Peter na Yuda ni kwamba ingawaje wote walikosea , ( Peter alimkana Yesu , Yuda alimsaliti Yesu ) Yuda alijiona Mr perfect , kwamba hawezi kujishusha , hawezi kunyenyekea ili asemehewe , mwisho aliamua kujiadhibu , akajidhuru mwenyewe.
Lakini Peter alijua hakuna tumaini kwa mwingine isipokuwa katika Yesu Kristo awezaye kusamehe , akanyenyekea akasemehewa maisha yakaendelea.

Ingawaje unachangamoto za kitabia na za kimwenendo , kuwa mpole , nyenyekea , tulia kwa Mungu hapo ndipo ulipomsaada wako.
Yeye atakufundisha , atakubadilisha na kukupa mwenendo mpya.
Ni yeye ndiye aliyeianzisha kazi njema moyoni mwako , na ndiye atakayeikamilisha.
Usiache ibada , usiache HUDUMA , isiwakimbie wanakulea kiroho.

Usiwe k**a Mr perfect , utakuja kujidhuru.

TULIA KWA BWANA.Ingawaje tunajaribu kuenenda vile impendezavyo Mungu , bado kuna mahali huwa tunalikoroga.Uhalisia upo h...
17/03/2022

TULIA KWA BWANA.

Ingawaje tunajaribu kuenenda vile impendezavyo Mungu , bado kuna mahali huwa tunalikoroga.

Uhalisia upo hivi unavyozidi kumkaribia Mungu ndivyo unavyozidi kujiona kuwa wewe si mkamilifu na unamuhitaji Mungu zaidi ya hapo.

K**a ilivyokuwa kwa Nabii Isaya kabla hajamuona Mungu kutika maono alikaza kusema Ole wenu , Ole wako, lakini alipomuona Mungu kauli yake ilibadilika kutoka ole wenu kuwa Ole wangu.

Mwanadamu hajawahi kuwa mkamilifu na hatowahi kuwa mkamilifu ndio maana hatuhesabiwi haki kwa matendo , Bali kwa kuiamini kazi ya msalaba.( Yesu Kristo )

Yaani yupo aondoaye dhambi katika yeye sisi tumefanywa wakamilifu mbele za Mungu.

Isikusumbue sana kuona kuwa bado unachangamoto za kitabia na za kimwenendo , mshukuru Mungu vile ulivyoleo alafu mwamini Mungu kuwa katika Yesu Kristo anaweza kukubadilisha na kukufanya uishi vile impendezavyo.
Ikusumbue kuona unachangamoto za kitabia na za kimwenendo alafu umeacha ibada , umeacha kusoma neno , umeacha kushiriki vipindi vya maombi , yaani hata ukiwaona wanaokulea kiroho unawakimbia.
Kimsimgi hiiyo ni mbinu ya adui kukuweka mbali na suluhisho la changamoto zako.

Uliona wapi mgonjwa anamkimbia daktari ?
( Ni kwenye wodi ya wagonjwa wa akili pekee utakutana na hizi kesi )

Hatak**a unahesabika kuwa umekengeuka au umeasi kanisa au umesimamishwa HUDUMA za kanisa , au umetengwa na kanisa vyote hivyo visikufanye ukae mbali na tabibu ya moyo wako.

Neno moja nikwambie msaada wako upo katika Bwana Pekee , aliyeziumba mbingu na nchi , yeye hawezikukuchoka , yeye hawezikukukana , yeyehawezi kukutupa.

Madam upo hai bado unayonafasi katika ufalme wake .
Biblia yasema

Ezekieli 33:11
[11]Waambie, K**a mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?

Inaendelea.........

Note!
25/01/2022

Note!

Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni  mwetu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu; Bei...
24/01/2022

Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwetu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;
Being confident of this very thing, that he which hath begun a good work in us will perform it until the day of Jesus Christ:
Amen!
Wafilipi 1:6

21/01/2022

Doctrinal issues!
Mkristo anapaswa kukua kiufahamu hata kufikia level ya kuweza kupima fundisho katika kwa nuru ya Yesu kristo yaani neno la Mungu ( kweli iwekayo huru )

20/01/2022

Muziki

Uhuru Dei!
19/01/2022

Uhuru Dei!

Address

Ubungo
Dar Es Salaam

Telephone

+255688246745

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Fanuel Kijoji posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Fanuel Kijoji:

Share