TAG ICC King'azi B

TAG ICC King'azi B Religious matters

Karibu Uabudu nasi, tutafurahi sana kukuona
25/04/2026

Karibu Uabudu nasi, tutafurahi sana kukuona

24/03/2026
12/01/2026
MAMBO YANAYOTOKEA PAPO HAPO MTU WA MUNGU ANAPOTENDA DHAMBI📖Mwanzo 3:1-24📍Kutengwa na Mungu (Kifo cha kiroho)Mtu wa Mungu...
12/01/2026

MAMBO YANAYOTOKEA PAPO HAPO MTU WA MUNGU ANAPOTENDA DHAMBI

đź“–Mwanzo 3:1-24

📍Kutengwa na Mungu (Kifo cha kiroho)

Mtu wa Mungu anapotenda dhambi tu, hutengwa na Mungu

Kitendo cha kutengwa na Mungu ndio kifo cha kiroho ndani ya mtu.

Ikumbukwe kwamba:

"Kifo cha kiroho hutangulia kifo cha kimwili, na kifo cha kimwili anachokutana nacho mwanadamu sasa ni Matokeo ya kifo cha kiroho alichokutana nacho Adamu pake Edeni".

đź“–Mwanzo 2:17
[17] walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, "kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika."

Adamu alipotenda dhambi pale pale alitengwa na Mungu(kufa kiroho).

Nuru na giza havikai pamoja, Dhambi ni giza na utakatifu ni nuru, shetani alipopewa nafasi kwa ruhusa ya Adam ndipo Mungu alijitenga naye automatic

Mwanadamu akapoteza ushirika wake na Mahusiano yake ya karibu na Mungu

📍Kupoteza sura ya Mungu ndani yako.
Mwanadamu aliumbwa kwa sura na mfano wa Mungu kwa namna alivyo kuwa kabla ya dhambi.

đź“–Mwanzo 1:26, 1Petro 2:17

Ukamilifu wa Kiungu ulikuwa ndani yake, aliwa,a katika ukamilifu wa Kiungu, alienenda katika ukamilifu wa Kiungu, aliamua katika ukamilifu wa Kiungu.

Kabla ya dhambi, Adamu anafanya kazi ukamilifu ya kutoa majina kwa viumbe vyote na anagindua hakuna wa kufanana naye

Baadaye Mungu alimtia katika Usingizi mzito asijitambue, akamuondolea sehemu ya ubavu na kumuumba Eva kutoka katika mifupa na nyama zake , akamweka karibu yake akaondoka

Adamu alipokuja kuamka katika Usingizi wake alipimuona tu Eva, akatambua huyu ni nyama katika zangu na mifupa katika yangu,

Anasema ataitwa mwanamke kwa sababu alitoka kwa mwanaume, Tena akampa na jina ataitwa Hawa (Eva) mama wa wote walio hai

Sasa ukiangalia hapa, unagundua Adamu alikuwa moamilifu katika njia zake kwa sababu akili, ufahamu na mawazo yake yalikuwa makamilifu hivyo alikuwa anaona mambo k**a Mungu alivyoyafanya ingawa wakati Mungu anafanya yeye hakuwepo.

Dhambi ilipokuja ilimfarakanisha mtu na sura ya Mungu ndani yake, ndipo kukatokea gap kubwa sana kati ya Sura na Mungu na mwanadamu.

Hata imekuwa mawazo ya Mungu na mwanadamu vimeachana patefu sana, njia za mwandamu na ufahamu wake vimeachana mbali na sana na alivyo Mungu kwa sababu sura ya Mungu haipo Tena ndani ya mwanadamu.

Hivi ndivyo inavyotokea kwa mtu wa Mungu anapotenda dhambi, Kuna kuwa na muachano mkubwa sana kati yake na Mungu katika mtazamo, mawazo na njia. [Isaya 55:8-9]

📍Kupoteza Haki na Mamlaka.
Mungu ni mtawala wa mbingu na nchi, alipomfanya mwanadamu kwa sura na kwa mfano wake alimweka awe mtawala wa nchi.

Hivyo mwanadamu alikuwa na Haki pamoja na mamlaka ya kutawala nchi kwa sababu ya sura na mfano wa Mungu aliokuwa amepewa.

Lakini, baada ya anguko Adamu alipoteza Haki na Mamlaka ya kutawala nchi kwa sababu alikuwa mateka wa shetani kuqnzia hapo akawa mtumwa wake

Kila mtenda dhambi ni mtumwa wa dhambi

Ikumbukwe kwamba:

Dhambi unaweza kushinda kabla hujatenda kwani wewe unakuwa na nguvu na dhambi inakuwa DHAIFU kwako, lakini dhambi ukiisha kutenda tayari imekushinda na wewe ni mateka na mtumwa wake kwani I akuwa na nguvu dhidi yako nawe unakuwa DHAIFU dhidi yake.

Badala ya kutawala mwanadamu anakuwa mtumwa wa dhambi chini ya shetani

Ndiomaana mtu akitenda dhambi mara moja ni rahisi zaidi kutenda Tena na tena, na zaidi sana ni rahisi KUONGEZA na dhambi nyingine nyingi juu yake.

Daudi alitenda dhambi ya kuzini na mke wa Uria, ikazaliwa dhambi ya uongozi haraka, mara ikazaliwa dhambi ya kuua hapo hapo, akamuua Uria

Hii ndio kuwa mtumwa wa dhambi chini ya shetani, unaweza kutumiwa kufanya dhambi yoyote k**a shetani apendavyo.

📍Hukumu ya Mungu huanzia papo hapo.

Adamu alihukumiwa pale pale katika bustani ya Eden, Mungu alitamka hukumu zake kwa Adamu, Eva na kwa nyoka

Wakati mtu anasubiri kifo cha kimwili, akishatenda dhambi papo hapo anahukumiwa na matokeo ya hukumu huanza kufanya kazi kuanzia hapo

Adamu alifukuzwa kwenye bustani ya Eden,

Ardhi ililaa iwa kwa ajili yake

Akazidishiwa taabu, mzigo na ugumu wa maisha

Kwamba itamgharimu jamsho na MAUMIVU ili aweze kula na kunywa

📍Kuondokewa na utukufu wa Mungu.

Utukufu ni vazi la Kiungu ambalo huwavika na kuwafunika watu wa Mungu

Utukufu wa Mungu ni uwepo wa Mungu, nuru ya Mungu na kibali cha kiungu juu ya mtu.

Utukufu wa Mungu k**a vazi, hufunika aibu na madhaifu au mapungufu ya mwanadamu.

Utukufu wa Mungu, hufunika maisha ya mtu wa Mungu na kila kitu chake na afanyacho hufunikwa nao, hivyo huonekana kiutofauti hata k**a ni cha kawaida sana

Adamu na Eva walikuwa uchi wote wawili, lakini kwa kuwa walifunikwa na utukufu wa Mungu hawakuoneana haya

Lakini walipotenda dhambi, ndipo utukufu wa Mungu ukajitenga nao Ikawa ni k**a mtu aliyevuliwa nguo mbele ya watu.

Wote wawili wakajikuta wako uchi, wakaoneana haya wakakimbia na kushona majani ili kuficha aibu yao.

Mtu akitenda dhambi, uwepo na utukufu wa Mungu hujitenga na kuondoka na hapo ndipo aibu ya mtu huwa peupe na kufuatana naye huonekana wazi kwa kila mtu.

📍Kuondokewa ulinzi wa Mungu.

Mungu huwalida watu wake kwa ulinzi wake ili wasivamiwe na nguvu za falme na mamlaka nyingine.

Lakini dhambi hutendeka kwa hiari ya mtu mwenyewe kwa Ushawishi wake, dhambi ikishatendeka hufukuza ulinzi wa kiungu na kufungua milango ya uvamizi wa nguvu za giza.

Utukufu wa Mungu na uwepo wa Mungu huondoka pale dhambi inapoingia na kuchukua nafasi kwenye maisha ya mtu

Uwepo wa Mungu na utukufu wa Mungu ni kinga, ni boma, na ulinzi wa Kiungu juu ya mtu wa Mungu wakati wote awapo Mtakatifu.

Dhambi inapochukua nafasi kwenye maisha ya mtu ndipo uwepo na utukufu wa Mungu hutoweka na kujitenga mbali, mtu huwa k**a mji ulioachwa wazi wezi na wavamizi huingia k**a wapendavyo.

Uvamizi wa nguvu za giza k**a vile mapepo huwa rahisi sana kwa mtu ambaye ameondokewa uwepo na utukufu wa Mungu kwa sababu ulinzi wake umeondolewa.

Dhambi humwondolea mtu utiisho na nguvu za Mungu, na kumfanya kuwa mtu wa kawaida sana asiye na madhara kwenye ulimwengu wa roho wa giza.

Hivyo basi;

Ni muhimu mnoo kutunza utakatifu ulio nao kwa sababu ndio uzima wako, sura ya Mungu kwako, ndio nguvu yako, ndio HAKI na mamlaka yako, ndio ulinzi na usalama wako.

Mungu akubariki sana, karibu icc

Pst. Simon Mwamakimbula
Tag - icc king'azi - Mungu Kwanza
Sunday, 11 January 2026

Simu: +255755153801

01/01/2026

Mkesha WA mwaka mpya 2026 hapakanisani

29/12/2025

Mvua ikinyesha walio WA MUNGU IBADA k**a kawa

NEEMA YA MUNGU ILIKUWA NI KUBWA SANA SIKU YA LEO KHERI MWISHO KULIKO MWANZO HAKIKA IMEKUWA SIKU YA BARAKA SANA TUMEUONA ...
29/06/2025

NEEMA YA MUNGU ILIKUWA NI KUBWA SANA SIKU YA LEO KHERI MWISHO KULIKO MWANZO HAKIKA IMEKUWA SIKU YA BARAKA SANA TUMEUONA MKONO WA MUNGU MUNGU AWABARIKI WOTE TULIOFIKA KARIBUNI NA WAKATI MWENGINE ASANTE

29/06/2025

SHALOM LEO TAR 29/06/2025 TUMEHITIMISHA KWA KISHINDO SEMINA YA MOTO WA UAMSHO HAPA TAG ICC King'azi B TUNA MSHUKURU SANA MUNGU KWA MATE DO YAKE MAKUU

NEEMA YA MUNGU NI  KUBWA SANA TUMEMTUKUZA MUNGU SANA HAKIKA MKONO WAKE UMEKUWA NI MKUBWA SANA JUU YETU KARIBUNI NA KESHO...
28/06/2025

NEEMA YA MUNGU NI KUBWA SANA TUMEMTUKUZA MUNGU SANA HAKIKA MKONO WAKE UMEKUWA NI MKUBWA SANA JUU YETU KARIBUNI NA KESHO TUABUDU PAMOJA ASANTE

28/06/2025

SHALOM LEO IKIWA SIKU YA NNE YA SEMINA YA MOTO WA UAMSHO HAPA KANISANI TAG ICC King'azi B HAKIKA TUNAENDELEA KUMUONA MUNGU AKITUTENDEA KARIBU SIKU YA KESHO MUNGU AKUBARIKI SANA

Address

KING'AZI
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 11:00 - 17:00
Tuesday 16:00 - 18:00
Wednesday 15:30 - 18:00
Thursday 16:00 - 18:00
Friday 16:00 - 18:00
Saturday 14:30 - 17:00
Sunday 08:00 - 12:30

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAG ICC King'azi B posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to TAG ICC King'azi B:

Share