Efatha Church-Kigamboni TV

Efatha Church-Kigamboni TV Healing & Deliverance by the Blood of JESUS CHRIST.

Katika mwezi huu wa sita, neema ya Mungu itakutenganisha na kila kilichokuwa kikwazo katika maisha yako. Bwana atakuongo...
01/06/2026

Katika mwezi huu wa sita, neema ya Mungu itakutenganisha na kila kilichokuwa kikwazo katika maisha yako. Bwana atakuongoza katika njia sahihi, ataimarisha hatua zako na kukufungulia milango ya kibali usiyotarajia.
Usiogope changamoto zinazoweza kujitokeza mbele yako, kwa maana Mungu yuko pamoja nawe. Atakupa nguvu mpya, hekima ya kufanya maamuzi sahihi na ushindi katika kila eneo la maisha yako.
Mwezi huu uwe mwezi wa ushuhuda, mafanikio, amani na furaha tele. Mungu atafanya zaidi ya yale uliyokuwa ukiyaomba na kuyatarajia.

Umebarikiwa!





MEZA YA BWANAMungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yak...
31/05/2026

MEZA YA BWANA

Mungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yako ndipo dhambi, magonjwa, shetani wachawi, njaa na hata dhiki zitakukimbia na ndipo utakapoona mema yakikujilia. Ayubu anasema utakusudia neno nao litatimia. Ukilinda imani yako isiyumbe hautasikia njaa wala kiu, maana yake mahitaji yako yatatimizwa.

Haya yote yatatokea kwako k**a utalinda imani yako. Tunapomega mkate na kunywa mvinyo, yale yaliyoshindikana yakawezekane, Biblia inasema “Imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo” mwana wa Mungu Neno hili litatimia kwako, hutaona kiu wala njaa maana mahitaji yako yatatimilizwa, unaenda kula na kunywa vile vitamanikavyo.

Biblia inasema Mungu ndiye uzima wako, baada ya kula na kunywa (meza ya Bwana) ule ugonjwa uliyokukandamiza utaondoka. Kwa mamlaka niliyonayo utaenda kutamka Neno leo na litakwenda kutimia, yule mgonjwa aliyekuwa kitandani kwamba ni mkubwa au mdogo anakwenda kuinuka, kwamba ulikuwa unaumwa na kansa, TB, presha, kisukari au aina yoyote ya ugonjwa leo huo ugonjwa umeondolea maana Bwana amesema amekuja ili sisi tuwe na uzima tele, leo unakwenda kuwa na uzima tele. K**a umekuja hapa ulikuwa na maswali yanayokusumbua umepata majibu yake. Mwanangu wacha ikawe hivyo kwako.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Mwovu hataweza kukugusa mpaka pale utakapoilinda imani yako, ni lazima ujue umeipataje imani yako, watu wengi wanalinda ...
31/05/2026

Mwovu hataweza kukugusa mpaka pale utakapoilinda imani yako, ni lazima ujue umeipataje imani yako, watu wengi wanalinda magari yao, nyumba zao, wake au watoto wao lakini hawalindi imani zao, uko sawa wewe? Linda imani yako kuliko chochote ukilindacho maana ndipo ilipo chemchemi ya uzima wako, linda yale yaliyofanya wewe uitwe mlokole na uwe na nguvu za Mungu linda hicho usiku na mchana.

Waefeso 4:27 “wala msimpe Ibilisi nafasi.”

Wala msimpe Ibilisi nafasi.” tambua kuwa ukimpa tu ibilisi nafasi amekumaliza, unawezaje kumzuia ibilisi asipate nafasi kwako? Kwa kulinda imani yako.

Warumi 8:28 “ Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.”

Watu gani wanampenda? Ni hao wenye imani, hauwezi kumpendeza Mungu k**a hauna imani na imani ni kujua kuwa ulikuwa mwenye dhambi na sasa umeokoka na Je! umeokokaje? Hicho ndicho unapaswa kukilinda. Mungu anafanya kazi na hao wanaompenda ili nini? Ili awape mema.

TANGAZO: Nakutangazia Mungu akakupe mema.

Ukishajua wewe ni nani na uko tayari kufanya kazi na YEYE; ndipo anakuwa tayari kukupa wewe mali.

1 Petro 2:9 “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;”

Lazima uelewe kuwa wewe umechaguliwa na siyo umekataliwa, la! Hata watu wakikusengenya wala usiumie bali jipongeze kwa maana wameona kuna kitu cha tofauti kwako. Mwana wa Mungu wewe umeandaliwa kumiliki yaliyo ya Bwana.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Waamini walio wengi hawaelewi wokovu wao; kwa nini wameokoka? Ni k**a vile umemuajiri mtu katika nafasi fulani na huyo m...
31/05/2026

Waamini walio wengi hawaelewi wokovu wao; kwa nini wameokoka? Ni k**a vile umemuajiri mtu katika nafasi fulani na huyo mtu haelewi wajibu wa hiyo nafasi, ingawa anafanya kazi kila siku. Hiki ndicho kinachowakuta watu wengi ambao wameokoka; ibilisi anawapiga huku na kule maana hawaelewi nafasi zao, kwa nini wameokoka.

1 Yohana 5:18 “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.”

Yohana 16:8 “Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi;”

Dhambi ni nini? Ni kutokumwamini YEYE, tendo lolote linaloitwa dhambi ni matokeo ya kutokujua chanzo cha imani. Ukiwa na imani hata dhambi yoyote itakayokutokea kwa sababu una imani ni rahisi kuiondoa hiyo dhambi pasipo mtu yeyote kuja kukwambie tubu maana unajua umekosea, lakini k**a haujui utaendelea kuitenda hiyo dhambi.

Biblia inasema “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.” Ilinde imani yako kuliko unavyoilinda afya, fedha zako au kuliko kitu kingine unachokijua kwa sababu imani yako ndiyo kila kitu. Ibilisi hana haja na nyumba yako wala fedha zako maana anazo nyingi, bali anashida na imani yako kuliko kitu kingine chochote kile, maana akifanikiwa kuitoa imani yako amekushinda wewe. Yesu alikuja na akafa msalabani kwa ajili yetu, usisahau hilo.

1 Yohana 5:18 “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.”

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa...
31/05/2026

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

Baba anabeba mizigo yote inayohusu watoto, maumivu yote ya watoto, huu ndiyo ubaba; anasimama kwa ajili ya familia yake. Yesu aliye baba wa milele kwetu, alichukua mizigo yetu, maumivu yetu na changamoto zetu zote na akafa nazo msalabani na huu ndiyo ubaba.

Wakolosai 2:14-15 “akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutush*taki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani; akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.”

Yesu k**a baba aliyabeba haya yote kwa ajili yetu mimi na wewe, halafu kuna mtu anasahau kile Yesu Kristo amefanya pale msalabani? Aliyoyafanya Yesu ni kwa ajili yetu.

Wakolosai 2:13 “Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;”
Tulikuwa tumekufa lakini kwa ajili yake leo hii tupo hai.

Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Pasipo Imani hauwezi kumpendeza Mungu, k**a haumpendezi YEYE inamaana kuwa unamkosea; utajuaje hivyo? Kwa maana Biblia inasema “huwapa thawabu wale wamtafutao.”

Wale wanaompendeza Mungu YEYE huwapa mahitaji yao, hii ina maana kuwa wale wasiyompendeza wanateseka na kuzunguka sana, wanaishi na njaa na katika uhitaji ingawa wamezaliwa mara ya pili (wameokoka) kwa nini wanaishi hivyo? Ni kwa sababu hawampendezi YEYE.

Biblia inasema “Kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Hivyo kwanza unapaswa kuelewa kuwa YEYE yupo hai, anakuona na kukutazama, hivyo atatazama kila unachofanya, kile unachokifanya kikimpendeza YEYE anakupa mahitaji ili kukufanya wewe uende mbele, k**a ukifanya vizur

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Nay...
31/05/2026

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Ndiyo maana hata unaposoma biblia Waebrania wote walikuwa wanamuita Ibrahimu baba, kwa nini? Kwa sababu ubaba wa Ibrahimu hautakaa uishe japokuwa yeye amekufa lakini ubaba upo maana huo ubaba ni agano kati ya Mungu na Ibrahimu na huo ubaba utaendelea kuwepo milele. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio yako. Yesu alizaliwa katika ushi

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGUIsaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kif...
31/05/2026

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGU

Isaya 9:6
“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Ndiyo maana hata unaposoma biblia Waebrania wote walikuwa wanamuita Ibrahimu baba, kwa nini? Kwa sababu ubaba wa Ibrahimu hautakaa uishe japokuwa yeye amekufa lakini ubaba upo maana huo ubaba ni agano kati ya Mungu na Ibrahimu na huo ubaba utaendelea kuwepo milele. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio

Leo ni siku yako, furahi kwa maana Bwana ameamua ufurahi, hakuna kitakachokuzuia usifurahi kwa sababu Mungu ameamuru ufu...
31/05/2026

Leo ni siku yako, furahi kwa maana Bwana ameamua ufurahi, hakuna kitakachokuzuia usifurahi kwa sababu Mungu ameamuru ufurahi, katika Jina la Yesu naamuru ufurahi.

Mungu alimuamuru Yesu afe kwa ajili yetu ili mimi na wewe tupate kupatikana, ili wewe uweze kukombolewa, ulipitia maumivu mengi hata haujajua ulikuwa wapi, nguvu za giza, uchawi zilikuwepo ili kukuangamiza, lakini ile nguvu ya mbinguni ikapita kupitia mimi na wewe ukakombolewa, tafadhali usilisahau hilo, kwa maana k**a ukisahau usifikiri utaingia mbinguni; kwa sababu ilimfanya Yesu Kristo afe ili wewe ukombolewe. Yesu hayupo hapa duniani lakini nguvu ile ile iliyomfanya Yesu afe akaniamuru mimi nikombolewe na akanipa hiyo nguvu ili kukufanya wewe ukombolewe, ukisahau hilo kuzimu hakutakuacha salama. Tafadhali haijalishi nini kitatokea usisahau hilo.

Kwa nini Mungu alimtumia Yesu Kristo na siyo Adamu, Musa, wala Eliya, lakini kwa nini Yesu? kwa sababu ni mwana wa Mungu. Nawaona watu wengi wana uchezea wokovu na mpaka wakitambua hilo watakuwa wameshachelewa. Watu wengi wakati walipokuwa wanaokoka wanalia kwa machozi na kusema sitasahau wokovu Bwana, lakini baada ya kitambo kidogo wanasahau na wanaanza kumdhihaki yule aliyewakomboa.

Watu huwa hawaelewi nini maana ya kumdhihaki Roho Mtakatifu, tendo hilo ni la hatari sana zaidi ya kuua, aliyeua anaweza kusamehewa, anayefanya uasherati atasamehewa lakini kumdhihaki Roho Mtakatifu hakuna msamaha. Kwa nini? Kwa sababu wokovu ni kazi ya Roho Mtakatifu ndani ya mtu fulani. Mungu hamtumii malaika, la! Bali anamtumia mtu ambaye alichaguliwa kabla hajazaliwa ili abebe jukumu hilo ili anaposimama anaibeba ile nguvu yote na kuachia vizazi na vizazi, na wale wanayoipokea hiyo nguvu wanaenda na hiyo nguvu na wanaposahau walipotoka hapo ndipo hatari inaanzia. Roho ya mazoea itakupelekea wewe kumkufuru Roho Mtakatifu na hiyo roho ni hatari sana kwako.

OMBI: Bwana nisaidie nitoke katika roho ya mazoea maana nataka nifike mbinguni.

©️ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWI

NENO LA SADAKA Zaburi 100:1-5 “Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa ku...
31/05/2026

NENO LA SADAKA

Zaburi 100:1-5
“Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba; Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu; Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake; Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake; Kwa kuwa Bwana ndiye mwema; Rehema zake ni za milele; Na uaminifu wake vizazi na vizazi.”

Tumfanyie Bwana shangwe maana YEYE ni BABA kwetu. Tuingie nyumbani mwake kwa kushukuru maana ametutendea mema, ndiye anayetupa uwezo na nguvu katika maisha yetu, hajatuacha kamwe katika mwezi huu wa mfungo amekuwa pamoja nasi.

Mshukuru Mungu kwa kumtoa mwanaye mpendwa Yesu Kristo kwa ajili yetu lakini pia akatubariki; kwa maana Yeye ndiye anayetupa nguvu za kufanikiwa.

©️ MTUME ELIAKUNDA MWINGIRA

Ni Jumapili ya kumtukuza Mungu kwa wema wake, rehema zake na upendo wake usio na mwisho. Leo tunainua sauti zetu kwa fur...
31/05/2026

Ni Jumapili ya kumtukuza Mungu kwa wema wake, rehema zake na upendo wake usio na mwisho. Leo tunainua sauti zetu kwa furaha na shukrani, tukimpa heshima anayestahili.

Zaburi 150:6 (SUV) "Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya."

Address

Ungindoni
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church-Kigamboni TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Efatha Church-Kigamboni TV:

Share