02/08/2022
SOMO: “SADAKA INAPOTUMIKA KUTENGENEZA MAISHA YA FAMILIA YALIYOFUNGWA NA SADAKA” (Sehemu ya pili)
MWL. CHRISTOPHER MWAKASEGE.
SIKU YA PILI 22 JULAI 2022, TABORA
LINK YA SOMO LA HILI YOUTUBE
👉🏼https://youtu.be/Km-flK5j_CU
NAMBA ZA KUTUMA SADAKA, MAOMBI NA SHUHUDA
👉🏼https://bit.ly/Sadaka-Maombi-Shuhuda
UTANGULIZI
LENGO LA SOMO
Kutumia mbinu za ki Biblia ili kujinasua toka kwenye vifungo vibaya vya maisha vinavyotokana na sadaka.
1Wafalme 12:26-27
“Yeroboamu akasema moyoni mwake, Basi ufalme utairudia nyumba ya Daudi. K**a watu hawa wakipanda kwenda kutoa dhabihu katika nyumba ya BWANA huko Yerusalemu, ndipo mioyo ya watu hawa itamrudia bwana wao, yaani Rehoboamu, mfalme wa Yuda; nao wataniua mimi, na kumrudia Rehoboamu, mfalme wa Yuda.”
Alikuwa akijua siri iliyoko kwenye sadaka jinsi ambavyo inaweza kuk**ata moyo wa mtu na kuushikilia na kuusukuma kufanya vitu ambavyo yule mwenye huo moyo hakuwa hata amekiwazia. Lakini kuna nguvu zilizowekwa ndani ya sadaka ambavyo si watu wengi sana wanajua.
Leo nataka tuangalie kipengele hiki UHUSIANO WA SADAKA NA MWILI KIMAISHA
soma 1Wafalme 18:30,36-39
Kwa kujifunza jambo hili la Uhusiano wa sadaka na mwili kimaisha tuangalie mambo kadhaa ili uweze kuelewa kirahisi:-
JAMBO LA KWANZA
SADAKA INAWEZA KUTAWALA NA KUFUNGA MAENEO KADHAA YA MTU NA FAMILIA YAKE
1Wafalme 18:38
“Ndipo moto wa BWANA ukashuka, ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa, na kuni, na mawe, na mavumbi, ukayaramba yale maji yaliyokuwamo katika mfereji.”
Hii inaelezea jinsi ambavyo Eliya alitengeneza ile madhabahu na vitu alivyokuwa ameweka. Ukisoma vizuri utaona jinsi ambavyo alichukua mawe 12 yakiwakilisha watoto 12 wa Mzee Yakobo au kuwakilisha kabila 12 za Taifa la Israeli, pamoja na kwamba waliokuwa chini ya Rehoboamu walikuwa 10 lakini alikuwa anataka kutuonyesha ya kwamba kitu kilichofanyika pale kilikuwa kikigusa na wale wengine ambao hawakuwepo katika ile idadi. Kwa hiyo alikuwa akitafuta namna ya kuwakilisha kitu kizima mbele za Bwana.
SOMO:-"Sadaka Inapotumika Kutengeneza Maisha ya Familia Yaliyofungwa na Sadaka"Unaweza kutumia njia zifuatazo kutuma sadaka yako kwetu:- M-PESA ...