Madhabahu Ya YANAK

Madhabahu Ya YANAK Madhabahu ya YANAK ni madhabahu TAKATIFU YA MUNGU Yenye Ishara, Maajabu na Miujiza. MUNGU anaponya watu na kuwafungua kutoka kwenye vifungo mbalimbali.

01/03/2020

SHERIA MPYA YA KWENYE MADHABAHU YA YANAK

Siku ya Jumapili Ikifika saa 4:00 asubuhi mtu hajaingia ndani ya MADHABAHU, Haruhusiwi kuingia tena. Hivyo ni lazima mtu ahakikishe kuwa Saa 4:00 juu ya alama inamkuta akiwa ndani ya MADHABAHU. MUNGU Hapendi usumbufu kwenye UTUKUFU wake, na anachukia UTOVU WA NIDHAMU. Watu kazini wanawahi saa 1 au saa 2 asubuhi wameshafika kazini wanaogopa kufukuzwa kazi, lkn kwa MUNGU wanachelewa, wanamchukulia MUNGU mshkaji, wanamchukulia poa, yaani Sijui wanamwonaje wao! Makanisa yanafanywa k**a Kumbi za disco, mtu anaingia muda anaotaka. Anamkuta mhubiri mbele anahubiri, wala roho haimhukumu anaona Sawa. Hawa ni wafu! Huu ni UFU! Una jina la kuwa hai lkn umekufa wewe! Mchungaji wako anahubiri, wewe ndo unaingia! Wewe ni bosi au ndo MUNGU mwenyewe? Kumbuka kwa MUNGU hakuna bosi. Wote sisi ni wafuasi wa YESU, Wote tunatakiwa tumtii MFALME WA WAFALME.

01/03/2020

UTUKUFU WA MUNGU WAWA MKUU KWENYE MADHABAHU YA YANAK

IBADA ya leo 1/3/2020 UTUKUFU WA MUNGU WAWA MKUU, MUNGU WA UTUKUFU Ameshuka kwa Nguvu zake na kusema na watu. Cha AJABU ni kuwa mama mzazi mwenyewe wa NABII WA BWANA MUNGU WA UTUKUFU, ameshukiwa live na MUNGU na kumuonya kwamba aweke umama pembeni mbele ya NABII WA BWANA, Ili apate Kufanikiwa na Kubarikiwa, aweke umama pembeni, amchukulie mwanae k**a NABII WA BWANA kwa kuwa MBINGU IMEMCHAGUA.

MSHUMAA WATENGENEZA PAKAUpande wa Kulia wa Mshumaa unaona umbile la Paka, Kichwa chake, masikio, mgongo, miguu na mkia. ...
12/02/2020

MSHUMAA WATENGENEZA PAKA

Upande wa Kulia wa Mshumaa unaona umbile la Paka, Kichwa chake, masikio, mgongo, miguu na mkia. Paka anasimama kwa niaba ya wachawi na nguvu za giza. MUNGU WA UTUKUFU alikuwa akimaanisha kuwa hakuna uchawi wowote wala nguvu za giza zozote wala ufalme wowote unaoweza kunidhuru, wala kudhuru huduma au kuharibu Huduma. Hakuna uchawi wala uganga juu ya Israeli na kwa Yakobo, yaani kwa watoto wa MUNGU WA UTUKUFU wanaomtumaini. Watu wa MUNGU ni hodari na jasiri na ni Washindi, maana wanalindwa na NGUVU ZA MUNGU BABA WA UTUKUFU.

25/01/2020

ATOLEWA KWENYE BAHARI YA DAMU
MUNGU WA UTUKUFU amkomboa Kijana mmoja na kumtoa kwenye bahari ya damu alipokuwa amewekwa huku akitumikishwa k**a mbwa kwa ajili ya kuingizia watu pesa. Kijana huyo kibinadamu ana Nyota Kubwa ya Pesa, lakini maisha yake yalikuwa yameharibiwa kabisa na kufanywa msukule. Hapo awali alikuwa na maisha yake mazuri ya Kisasa lkn vyote vilikwenda, pesa na mali akabaki hana hata mia. Na kumbe vilichukuliwa na kubakishwa mtupu, yaani alifungwa Kweli kweli na alikuwa akiishi k**a msukule, na ndiyo maana akawa haoni mbele wala haoni mstakabali wa maisha yake, mtu aliyejifia na kujikatia tamaa, alikuwa k**a MFU. ATUKUZWE MUNGU WA UTUKUFU aliyemkomboa na kumrejesha upya na kumfungua. Hii ilitokea kwenye Ibada ya Jumapili ya trh 12/1/2020 ambapo niliwasha Mshumaa kwa ajili ya Ibada lkn ukazimika wakati haijawahi kutokea Mshumaa ukazimika hata uwashe feni uweke upepo mkali uisogeze karibu, Mshumaa wa Kwenye Madhabahu huwa hauzimiki. Ukawashwa tena kwa mara ya pili ukazimika, hivyo ikabaki kuwashwa kwa mara ya Mwisho, maana MUNGU anaongea mwisho mara 3 kuthibitisha jambo. Ndipo akaingia Mwana-Yanak mmoja ambaye alikurupushwa na MUNGU aje kwenye madhabahu, alipoingia akaambiwa na MUNGU BABA WA UTUKUFU kwamba awashe huo Mshumaa na atangaze kwamba, "Huu Mshumaa ukizimika, HUDUMA YA YANAK imekufa! Lakini Huu mshumaa ukiwaka k**a kawaida mpk mwisho, HUDUMA YA YANAK YA KINABII inaanza rasmi kutenda kazi. Kibinadamu aliogopa kutamka yale maneno, akasema km uliwashwa mara 2 zote ukazimika itakuwaje? Je nikitamka hivyo mshumaa ukazimika itakuwaje? Lakini Sauti ikamwambia Sema hayo maneno wala usiogope! Yeye akawa akiogopa akihofia huduma isife. Sauti ikamwambia kwa mara tatu Sema wala usiogope. Ndipo akajikaza na kutamka kwa Ujasiri akasema, "Nimeuwasha huu mshumaa, ukizimika, HUDUMA YA YANAK IMEKUFA! LAKINI UKIWAKA K**A KAWAIDA UNAVYOWAKAGA SIKU ZOTE MPAKA MWISHO, BASI HUDUMA YA YANAK YA KINABII INAANZA RASMI!". Basi huo Mshumaa ukawaka k**a kawaida mpaka mwisho. Na ule Mshumaa kule kuzimika kwa mara ya kwanza vilikuwa ni vita ambavyo vilikuwa vikiisak**a huduma ifungwe, huduma ife, madhabahu ifungwe! Maana vitu vizuri vina upinzani MKUBWA sana. Lakini ashukuliwe MUNGU BABA WA UTUKUFU Atupaye kushinda. Maana amesema vita si vyetu, ni vyake yeye. Na kwamba mtu yeyote anayemchokoza mwana wake, achokoza MBONI YA JICHO LA MUNGU. Sasa huyo anayechokoza Mboni ya jicho la MUNGU Je ataachwa SALAMA? Basi yule Mtumishi wa MUNGU aliyeambiwa awashe Mshumaa, MUNGU WA UTUKUFU akamwambia kuwa atoe SADAKA ainenee na kwamba kuna jambo kubwa atakalotenda MUNGU ndani ya Siku 7. Basi kwa mawazo ya kibinadamu kila mtu akaanza kuwaza la kwake, huyu anawaza hivi, huyu anawaza hivi, kila mtu anafikiria jambo atakalolitenda MUNGU. Kumbe kila mtu na mawazo yake na hakuna aliyepata. Kumbe jambo KUBWA MNO alilolitenda MUNGU WA UTUKUFU ni kumkomboa huyo kijana, na alikombolewa Siku ya mwisho yaani ya Saba yenyewe jumamosi. Unajua kibinadamu unaweza kuwaza kupata fedha mali utajiri, lkn MUNGU anachokitaka kwamba watu wakombolewe, wafunguliwe, wawekwe huru, wapate WOKOVU, hayo mengine yafuate. Imeandikwa kwenye biblia kuwa kuna furaha Mbinguni mwenye dhambi mmoja akitubu, mtu aliyepotea akionekana ni Furaha KUBWA, lkn haijaandikwa kwamba mtu mmoja akipata nyumba au gari au Pesa kuna Furaha KUBWA MBINGUNI. Hiyo ni furaha yako wewe Siyo ya Mbingu, Mbingu Furaha yake watu waokolewe kutoka kwenye vifungo na minyororo ya mwovu Shetani, Mbingu Furaha yake watu waokoke, wapate WOKOVU halisi usiochakachuliwa. Mbingu Furaha yake watu wawe WATAKATIFU.
Hayo ndiyo aliyoyatenda MUNGU.

31/08/2019

"WIMBO KUTOKA MBINGUNI"
Ulikuwa ni wimbo wa aina yake ambao mtumishi wa MUNGU kutoka kwenye MADHABAHU YA YANAK alipewa kwenye Ndoto, ambapo ktk ndoto hiyo walionekana wakiimba, "Niongoze, Niongoze, Kiongozi" Ni maneno machache yenye nguvu na uwezo usiokuwa wa Kawaida. Ambapo Wimbo huo una UPAKO na UWEZA wa Kiungu. K**a ilivyokuwa kwenye ndoto ndivyo ilivyokuwa kwenye MADHABAHU nguvu na uwezo wa huo Wimbo haukuwa wa kawaida. Kwa nini MUNGU alitoa maneno hayo? Maana anajua kuwa kuna watu wanashikiliwa na Akili za watu. Mtu mwingine imani yake anaiweka kwa ndugu jamaa na marafiki. Imani ya mtu haishikiliwi na mtu. MUNGU huongea na mtu mmoja na humwongoza Kivyake tofauti na wengine, hivyo haitakiwi mtu aongozwe na watu au mtu. Mtu huongozwa na MUNGU MWENYEWE. Maana ukiongozwa na mtu unaweza kupotezwa na kutumbukia Shimoni. Usikubali huduma yako iongozwe na mtu mwingine na kutawaliwa na mtu mwingine. Usikubali ndoa yako familia yako, nyumba yako kutawaliwa na kuongozwa na mtu mwingine. MUNGU Ndiye KIONGOZI. Simama Imara na MUNGU, Utauona mkono wake. Kwani ukimtumainia mtu au watu, Shetani atawatumia hao watu Kinyume, mwisho utajikuta umepoteza ama kupatwa na mabaya. God's First.

27/05/2019

ARUDISHIWA DAMU YAKE ILIYOKUWA IMEHIFADHIWA KWENYE MBUZI
Mama mmoja arudishiwa damu yake iliyokuwa imehifadhiwa kwenye Mbuzi, ni kuwa mama huyo adui yake alikuwa ametuma mbuzi akanyonya damu yake yote kupitia kwenye mguu wa Kulia, hivyo kwa macho ya rohoni mguu huo ni mwembamba km kidole lkn kwa macho ya nyama watu wanaona uko kawaida. Mbuzi huyo alikuwa akimpelekea bosi wake hiyo damu, na km angeifikisha mama huyo alikuwa anakata roho, lkn nguvu za MUNGU zilimsimamisha huyo mbuzi na kumgandisha hata akashindwa kwenda kwa bosi wake kupeleka hiyo damu, MUNGU akamwambia mtumishi wake amrudishie huyo mama damu yake, Mtumishi wa MUNGU akamrudishia huyo mama damu, damu yake ilikuwa imeonekana kwenye tumbo la mbuzi huyo, hivyo ikahamishwa na kurudishwa kwa mwenye nayo.

12/04/2019

AFUFULIWA AKIWA HAI
Hii ni Ajabu na Kweli, mwanamke mmoja afufuliwa akiwa hai, alikuja kwenye madhabahu ya Yanak akiwa hatazamiki mara mbili, ni kuwa ktk ulimwengu wa roho walishamuua siku nyingi sana na kumzika mpaka akaoza, maana maiti ikizikwa huwa inaoza na mwili unameguka meguka viungo vinatoka. Huyu tayari alishaanza kumeguka maana kucha zilishaanza kutoka na mwili wote kuoza, maana alijaa vidonda na kila akiwashwa akijikuna vinatoka vidonda, mguu ulioza kabisa akijikuna yanatoka maji, ngozi ilikuwa imetoka kwenye vidole vya miguuni na mikononi unaona nyama tu, Kichwa chote hakifai mpk hakina nywele, jicho linataka kuchomoka, ngozi yote imeathirika na nyayo za miguu ni km magamba, sauti imekauka haitoki, na ukimwona unaweza kushtuka au kumwota usiku, na kibinadamu hakuna mtu wa kumfanyia maombi kwa karibu, labda maombi ya mbali au ya kwenye simu, na unaweza usile chakula hata kumhudumia inataka moyo. Ukikaa naye Kichwa kinakuwa km kinataka kudondoka muda wote, kumbe anakaa anakabwa, alivyokuja ilikuwa ni siku ya 3 hajala, kila akitaka kula kitu kinamkaba hivyo akawa hali kitu chochote ndo kuja kwenye madhabahu. Mtumishi akamwambia ulishakufa siku nyingi sana ukazikwa na kuoza, naye akasema kuwa kila akilala ndoto zake huota watu waliokufa, na nyumbani kwake hupishana na watu asiowaona, yaani anaona km watu wanapita anapishana nao ila hawaonekani kwa macho. Basi mtumishi akamwombea maombi ya kumfufua kisha akamvua Sanda, alafu akamtoa hicho kitu kinachomkaba maana hata alipopewa kunywa Damu ya YESU ilikuwa haipiti kooni koo lilikuwa linakwaruza kwa nguvu. Koo likakaa sawa, akatolewa JINI MAITI, Jini Sharifu, Jini mahaba na Nyoka, naye akaona majoka mawili makubwa moja linamtishia na kumtolea ulimi. Maombi yake ya ukombozi yalikuwa ya Siku 7. Siku ya tatu mtumishi alimtapisha, alitapika uvundo mtupu, mtu aliyeoza lazima atapike vilivyooza, yalikuwa manyamanyama yaliyooza uvundo mtupu. Mtumishi alimuuliza km alishawahi kuombewa kwa ukaribu mahala kokote, akasema kuwa amezunguka sehemu nyingi, hakuna aliyewahi kumwombea maombi ya mtu mmoja mmoja. Pia ametafuta tiba mpk amechoka hamna kitu, katumia dawa nyingi za hospitalini na za asili lkn wapi! Ni kuwa asingeweza kupona kwa kuwa mwili wake haukuwepo alikuwa ameshazikwa, hivyo alikuwa anapoteza hela za kujitibia maana alikuwa hapaki mwili wake. Ukiona mambo hayaendi inabidi ukutane na watu wenye macho ya rohoni ndo wanajua chanzo nini wanakuombea ndipo mambo yanakaa SAWA. Na unaweza kukutana na mtu mwenye macho ya rohoni ila asiweze kukufungua maana wengine wamepewa kuona ila hawajapewa nguvu ya Kufungua watu na kuwakomboa, ila wengine wamepewa vyote macho ya rohoni na uwezo wa kuwafungua watu na kuwakomboa. Basi huyo mwanamke Alipokuwa akiingia kwenye madhabahu yaani harufu kote inatanda, harufu ya maiti ilikuwa inatanda, baada ya harufu za maiti ikawa harufu za vidonda mpaka mtumishi anashindwa Kupumua, angekuwa ni mtu mwingine kiukweli asingeweza kumwombea, angemkwepa. Na kumbe huyo mtu km asingekuja kuombewa baada ya siku mbili alikuwa anachukuliwa kijumla. Alianza kuombewa trh 1 march, angekufa kabisa trh 3. Sasa anaendelea vzr, kilichokuwa kinamkaba hakimkabi tena, Kula anakula vizuri, Vidonda vimekauka, Sauti inatoka vizuri, na Anapendeza. Na haya yote ni mambo ya nguvu za giza, aliyemroga huyu nasema ni mchawi mwenye roho mbaya kuliko wote duniani. Na Kilichokuwa kinafuatia mwili wake wote ungemegukameguka. Ashukuriwe MUNGU WA UTUKUFU aliyemponya.
Hayo ndiyo aliyoyatenda MUNGU.

28/03/2019

ATOLEWA YAI LA MBUNI TUMBONI
Mama mmoja akombolewa kwa kufanyiwa maombi ya ukombozi ya Siku 7. Atolewa hirizi kila mguu, Atolewa ute bandia mguuni, atolewa magoti ya miti, nyoka 7 waliokufa, mkufu wa kichawi, Pete, mkono wa nyoka, (Yaani mkono wake wa kushoto ulikuwa ni Nyoka) mkono huu ulikuwa ukimuuma sana ulikuwa km unataka kunyofoka, atolewa hirizi kwenye kizazi, Yai la mbuni tumboni lenye mwewe ndani mwenye macho ya rangi mbili tofauti, groves nyeusi mikononi, nafsi bandia, giza mwilini, vazi jeusi nk. Alikuwa na vifungo siyo vya nchi hii. Kwa kuanza mama huyo alitolewa magoti ya miti, kisha Mtumishi alianza kumtoa hirizi miguuni, mguu mmoja kulikuwa na hirizi nyeusi, mguu mwingine kulikuwa na hirizi nyekundu, hirizi ya kwenye mguu wa Kulia ilitoka haraka, lkn ya kwenye mguu wa kushoto ilikuwa iking'ang'ania, ilikuwa ikihamahama mara ipande juu mara ishuke chini. Lkn mwisho ikatoka. Siku ya pili alitolewa umauti na kurudishiwa Sura yake, kwa sababu alikuwa ameshavishwa umauti maana adui alimtegea mtego akaanguka chini kwa kishindo kutaka kuitoa roho yake, aliponyanyuka akawa hatembei, lkn MUNGU alimnusuru asife, hivyo alipotolewa magoti ya miti alianza kutembea pale pale japo alikuwa akichechemea kidogo sana, hata alipotolewa hirizi miguuni bado aliendelea kuchechemea kidogo. Maombi yaliyofuata alivuliwa mkufu wenye vidungulidunguli vya rangi nyekundu, nyeusi na nyeupe kisha akatolewa ute mweusi waliokuwa wamemwekea kwenye mguu wa kushoto na kurudishiwa ute wake. Huo ute mweusi ndio uliokuwa ukimfanya atembee kwa kuchechemea. Maana alipokuwa ameenda hospitali kupima aliambiwa hana ute na mifupa ya kwenye magoti inasagika kwa kuwa hakuna ute, kumbe washenzi walikuwa wamemwekea joints za miti na ute mweusi na kusababisha miguu kuuma sana. Wakati mwingine unaweza kwenda hospitali ukaambiwa una tatizo fulani kumbe ni hayo mashetani yamesababisha uonekane unaumwa huo ugonjwa, siyo kila ugonjwa ni wa kweli. Baada ya kumtoa huo ute mweusi mguuni na kumrudishia ute wake, alitembea vizuri sana bila kuchechemea. Maombi yaliyofuata ni kumtoa kwenye bahari ya damu, ktk ulimwengu wa roho alionekana yuko kwenye bahari ya damu akitapatapa na kuomba Msaada, kisha alifanyiwa maombi ya Yai la maadui, kisha alifanyiwa maombi ya kuondoa weusi kwenye mikono yake, huo weusi ulikaa km groves, utafikiri mtu kavaa groves, mikono myeusi ni ili mtu asik**ate pesa na kila akifanyacho kiwe ziro. Kisha yakafuata maombi ya kukikomboa kizazi chake, yalikuwa ya nguvu sana, maana kizazi chake kilikuwa kimefungwa kisibarikiwe, watoto wake wahangaike, wasifanikiwe na wasipate ndoa, wakati wa kukikomboa kizazi chake likatolewa yai la mbuni lenye mwewe ndani yake mwenye macho mawili yenye rangi tofauti, jicho moja lina rangi nyekundu, lingine lina rangi blue, hili yai lilitoka tumboni, pia ikatolewa hirizi nyeusi kwenye kizazi chake. Kisha yakafanyika maombi ya kutoa hizo nyoka 7 nyeusi waliokufa, walikuwa wamejivingirisha ndani ya mwili wake katikati. Yakafanyika maombi ya kuvua pete iliyokuwa kwenye kidole cha kati cha mkono wa kulia, pete ilihamia kwenye kidole cha kati cha mkono wa kushoto, kazi yake ni kufunga baraka zake na za watoto wake, pete ilivuka kwa NGUVU ZA MUNGU. Ikatolewa nafsi iliyo ndani yake na akarudishiwa nafsi yake, likatolewa giza kwenye mwili wake, akavuliwa vazi jeusi alilovikwa na akaona vibwengo vinne, vibwengo hivyo vilitoka kwenye hilo vazi. Akaingizwa kwenye BESENI LA UPAKO LA DAMU YA YESU. Ni beseni lenye nguvu sana, ili MUNGU WA UTUKUFU amshughulikie mwenyewe kwa ajili ya vifungo vingi alivyonavyo. Kweli alishughulikiwa KIKAMILIFU. Akatakaswa kwa damu ya YESU mwili mzima, kisha akashushiwa nguvu za MUNGU na kupewa MOTO wa MUNGU ili awe na MOTO wa MUNGU ndani yake. Kweli akapokea moto wa MUNGU, maana hapo kwanza hakuwahi kuusikia moto wa MUNGU ni kutokana na vifungo vingi alivyokuwa navyo, baada ya kufunguliwa ndio anausikia MOTO wa MUNGU.
ONYO:
Enyi wachawi acheni kuroga watu, huo ni ujinga na kutokuwa na akili, watu wanatafuta maendeleo nyie mnawarudisha nyuma, watu wanatafuta afya nyie mnawapa magonjwa, mnapata faida gani kwa hizo roho mbaya zenu? Washenzi ninyi, uchawi hauna nguvu mbele za MUNGU.

26/02/2019

AOKOKA NA KIFO, NDO ALIKUWA AKIKATA ROHO
Mtumishi amwombea dada mmoja ambaye ni mama mjamzito wa miezi 8. Dada huyo alisema kuwa Sikio linamuuma sana ana maumivu makali tangu saa 4 asubuhi mpk muda huo mchana. Chanzo cha maumivu ni kuwa alikuwa akila chakula, baada ya kumaliza kula alicheua chakula kikaingia puani, kisha kikaenda kwenye Sikio kikatua hapo, hivyo anasikia kitu kinamchoma sana kwenye Sikio maumivu ni makali mno. Mtumishi akamwombea dada huyo, akamwombea uponyaji ikashindikana, ndo kwanza maumivu yakawa yakizidi kiasi kwamba mpk huyo dada analia machozi, hivyo mtumishi akateketeza nguvu za giza, akakemea lkn wapi! Ndo kwanza maumivu yanachachamaa mpk mama mjamzito anajinyonganyonga, mwisho akawa hawezi tena kutoa sauti ila akanyosha kidole kuonyeshea watu kana kwamba kuna watu anawaona. Mtumishi akatumia Damu ya YESU lkn wapi! Maumivu yanazidi. Mwisho akakaa na kutafakari ni nini anatakiwa aombe, huku akimuuliza MUNGU, ndipo akajua kuwa ni roho ya MAUTI imetumwa kumchukua. Mtumishi alipokemea roho ya mauti ndipo mauti ikachachamaa kweli kweli, mama wa watu akajinyonganyonga na mwisho akawa akinyoosha miguu kukata roho, yaani roho ndo ilikuwa inachomoka. Mtumishi akajisemea moyoni kuwa huyu mtu hawezi kufa mbele yangu, maana MUNGU amenipa mamlaka ya kukemea roho za mauti. Kisha Mtumishi akaiambia roho ya MAUTI, "Wewe Roho ya MAUTI sikiliza, MUNGU amenipa MAMLAKA ya kukutoa, hivyo haraka sana ondoka umwachie mtu huyu". Kisha akaikemea na kuiteketeza, Roho ya MAUTI ikamwachia na kuondoka zake. Hapo hapo akawa mzima, akanyanyuka akaanza kuongea na kucheka utafikiri siyo yeye aliyekuwa akijinyonganyonga kwa maumivu. Akasema hakuna tena maumivu kwenye Sikio, wala kitu kilichokuwa kinamchoma Sikioni hakipo tena. Akasema kuwa muda ule alipokuwa akionyesha kwa kidole, alikuwa akiona misukule inamwita na baba yake mzazi aliyefariki kwa kuchukuliwa msukule akawa akimwita huku nyuma yake alikuwa akimwona mbaya wake aliyekuwa akitaka kumtoa roho. Na huyo mtu alikuwa amemtokea siku mbili zilizopita akimtambishia kuwa baada ya kumchukua baba yake mzazi, atafuatia yeye. Na mtu huyo ni mtu wa karibu.
Hivi sasa huyo dada ni mtumishi wa YANAK,
Hayo ndiyo aliyoyatenda MUNGU.

26/02/2019

MTOTO AREJESHWA BAADA YA MIAKA 8
Mtoto wa kiume arejeshwa baada ya miaka 8, tangu azaliwe alikuwa akiishi ndani ya Shimo huku akitumika kiuchawi. Ni kuwa alianza kuonyesha vituko tangu mtoto mdogo kabisa. Kuna siku mama yake alipika chakula cha usiku kwa ajili ya mgeni, Wali Samaki. Usiku huo walipokuwa wakijiandaa kupakua, alimwaga Sufuria la wali kwenye kochi alafu akausambaza, Samaki akaitia maji Sufuria mpaka juu. Kuna Siku waliandaa Chips Kuku kwenye Sinia, baada ya kunawa mikono ili wale, hapo hapo akatapika kwenye Sinia, Chips kuku zikajaa matapishi. Ukitaka kuangalia Tv hasa vipindi vizuri unavyopenda, hugeuza tv, hata umkataze vipi hakataziki! Hata umchape vipi hasikii! Hata uongee naye maneno matamu hasikii. Huwezi kukaa sebuleni kuangalia tv maana muda wote anaigeuzia upande ili watu wasiangalie. Ukiwasha friji anaizima. Kila unapoiwasha anaizima. Kuna siku alivua nguo zote akawa uchi kabisa akaenda kukaa katikati ya barabara ya lami huku magari yanapita. Alikuwa anajibu vibaya anasemesha, anakula sana, anawachokoza wadogo zake sana mpk anakera. Ukimshika huwezi ana nguvu zisizo za kawaida, ana uwezo wa kumbeba mtu mzima. Mama yake alikuwa akijifungia chumbani analia kwa sababu ya mtoto kumsemesha. Basi alipokuja kwenye maombi tuliona mtoto huyo hayupo, alikuwa akiishi ndani ya shimo refu huku akitumikishwa kiuchawi sana. Mtumishi aliita nafsi yake kuirejesha, nafsi ililetwa ikiwa ndani ya chungu. Lkn kila alipokuwa akiirejesha ndani ya mwili wa mtoto ikawa inagoma kuingia, aliyekuwa akimtumikisha alikuwa ameishikilia anaivuta huku akimuita huyo mtoto mara tatu na kumwambia kuwa kweli unataka kuniacha? Mtumishi alimrushia bahari ya moto huyo mtu hata akaiachia nafsi ikaingia ndani ya mtoto na kile chungu akakivunja. Baada ya Nafsi kurudi mizimu ikawa imemshikilia, alikuwa kwenye maagano alikuwa amewekwa na baba yake, tukavunja maagano ya kimizimu, kisha mtoto alienda anajivuta kwa kutembelea Tumbo mpk mahali alipokaa mama yake, wakati huo mama yake alikuwa ameshikwa na uchungu km wa kujifungua. Mtoto alipomfikia mama yake akachungulia mahali alikotoka, yaani sehemu za siri, maana yake anazaliwa upya. Kisha madude yote yakamtoka akawa safi mpya, akawa amezaliwa upya na hapo uchungu wote ukamtoka mama yake, tumbo likawa sawa. Kutoka hapo mtoto akawa mpole sana. Walipofika nyumbani mtoto akawa analalamika sana kuwa Tumbo linamuuma sana, mpk hakula kitu chochote, mtumishi akasema ni kwa sababu nafsi imerudishwa lkn bado mtoto hajafunguliwa vifungo, maana unapokuwa unatumika unalishwa vitu vingi. Hivyo kesho yake jumatatu mtoto akaja kwenye MAOMBI, akatapishwa uchafu wote, akatolewa hirizi kubwa tumboni, maana hiyo ndiyo iliyokuwa ikimfanya mtoto aumwe tumbo, hirizi hiyo ilikuwa kubwa ilijikusanya ikaunda umbo km la tufe, tumbo likawa gumu km jiwe, alafu ikatolewa. Akavuliwa pete alizokuwa amevishwa, akaombewa kurudishiwa NYOTA zake, mtumishi aliziita nyota zake zikaja lkn zikawa zinagoma kumpa huyo mtoto, adui alizishikilia, mkono wa mtumishi msaidizi ukawa mzito mno, maana yeye ndiye aliyekuwa amezibeba hizo nyota. Mtumishi kiongozi akawamwagia adui bahari ya moto, wakaziachia nyota, mtumishi msaidizi alipotaka kumkabidhi huyo mtoto nyota zake, miguu yake ikafungwa na kubanwa akawa hawezi kuamka wala kujisogeza, ikabidi mtumishi awateketeze hao waliomshikilia miguu yake ili waiachilie. Wakaiachilia na mtoto akapewa NYOTA zake zote 3. Walipokuwa wakirudi nyumbani kwao mtoto na mama yake, walikaa siti tofauti kwenye gari la abiria. Mtoto alikaa na baba mmoja na wala hawafahamiani wala hawajawahi kuonana. Baba huyo akamuuliza mtoto jina lake, mahali anakoishi na shule anayosoma, kisha akamwambia kuwa naona umetoka kwenye maombi, MUNGU amekufungua, na mizimu inayokufuatilia imeshindwa, na MUNGU amekurudishia Nyota zako, wewe ni mtu mkubwa, nyota yako ni kali sana, utakuwa Profesa, utazaa watoto wanne, wa kiume 3, wa k**e 1. Ole wako atakayekufuatilia tena akurudishe kwenye mizimu, hata km ni baba yako! Au nani! Nakwambia atakufa.

15/02/2019

ATOLEWA NDANI YA SHIMO NA KURUDISHIWA VIUNGO VYA MWILI WAKE
Dada mmoja alichukuliwa na mchawi na kuwekwa ndani ya shimo refu na viungo vya mwili wake vyote viligawiwa watu wengine, yeye akabaki km fuvu au skrepa, macho yake alipewa kijana mmoja ayatumie, masikio yake nayo alipewa huyo kijana na macho na masikio ya huyo kijana alipewa huyo dada, na viungo vingine vya huyo dada walipewa watu wengine wavitumie kiuchawi. Hivyo yeye aliyekuwa akiishi siyo halisi, halisi ni yule aliyekuwa ndani ya shimo akipata mateso makali. Tulimwita na kumrudushisha pia tukavirudisha viungo vyake japo macho yalikuwa yamegoma kabisa kurudi, tulitumia nguvu nyingi sana mpk kuyarudisha maana shetani alikuwa ameyang'ang'ania. Baada ya macho kurudi Niliyajaza Nguvu za MUNGU na moto na uponyaji na ukombozi, yaani macho yake yafungue na kukomboa watu na kuponya. Na muda huo huo MUNGU akamtumia kuponya mtu kwa kumtazama tu kwa macho. Alikuwepo mama mmoja akiumwa sana mguu na mkono kwa muda mrefu, aliponywa hapo hapo. Huyo dada aliporudi nyumbani alikutana Kimwili na mume wake, aliumia sana na kusikia maumivu makali kiasi cha kupiga Kelele alikuwa km ndo anabikiriwa wakati siku zote yuko na mume wake. Ni kwa sababu hakuwa na viungo vyake, hivyo hata sehemu za siri hazikuwa zake, hivyo aliporudishiwa viungo na sehemu zake za siri zilirudi, ina maana yeye sehemu zake za siri zilikuwa hazifanyi kitu chochote. Sehemu alizokuwa nazo si zake. Pia siku zote alipokuwa akifanya tendo la ndoa na mumewe, mchawi wake alikuwa akimtoa na kumweka pembeni bila yeye kujijua na huyo mchawi yeye ndo akawa anashiriki tendo la ndoa na mume wa huyo dada. Na ndio maana siku zote huyo dada alikuwa akilalamika kuwa kila akilala na mumewe hasikii chochote mpk akawa hapendi kulala na mumewe, anaona ni mzigo au ni utumwa. Duniani kuna mambo, lkn ashukuriwe MUNGU wa UTUKUFU aliyemfungua na kumkomboa.
Hayo ndiyo aliyoyatenda MUNGU.

Address

Kitunda
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Madhabahu Ya YANAK posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share