28/03/2019
ATOLEWA YAI LA MBUNI TUMBONI
Mama mmoja akombolewa kwa kufanyiwa maombi ya ukombozi ya Siku 7. Atolewa hirizi kila mguu, Atolewa ute bandia mguuni, atolewa magoti ya miti, nyoka 7 waliokufa, mkufu wa kichawi, Pete, mkono wa nyoka, (Yaani mkono wake wa kushoto ulikuwa ni Nyoka) mkono huu ulikuwa ukimuuma sana ulikuwa km unataka kunyofoka, atolewa hirizi kwenye kizazi, Yai la mbuni tumboni lenye mwewe ndani mwenye macho ya rangi mbili tofauti, groves nyeusi mikononi, nafsi bandia, giza mwilini, vazi jeusi nk. Alikuwa na vifungo siyo vya nchi hii. Kwa kuanza mama huyo alitolewa magoti ya miti, kisha Mtumishi alianza kumtoa hirizi miguuni, mguu mmoja kulikuwa na hirizi nyeusi, mguu mwingine kulikuwa na hirizi nyekundu, hirizi ya kwenye mguu wa Kulia ilitoka haraka, lkn ya kwenye mguu wa kushoto ilikuwa iking'ang'ania, ilikuwa ikihamahama mara ipande juu mara ishuke chini. Lkn mwisho ikatoka. Siku ya pili alitolewa umauti na kurudishiwa Sura yake, kwa sababu alikuwa ameshavishwa umauti maana adui alimtegea mtego akaanguka chini kwa kishindo kutaka kuitoa roho yake, aliponyanyuka akawa hatembei, lkn MUNGU alimnusuru asife, hivyo alipotolewa magoti ya miti alianza kutembea pale pale japo alikuwa akichechemea kidogo sana, hata alipotolewa hirizi miguuni bado aliendelea kuchechemea kidogo. Maombi yaliyofuata alivuliwa mkufu wenye vidungulidunguli vya rangi nyekundu, nyeusi na nyeupe kisha akatolewa ute mweusi waliokuwa wamemwekea kwenye mguu wa kushoto na kurudishiwa ute wake. Huo ute mweusi ndio uliokuwa ukimfanya atembee kwa kuchechemea. Maana alipokuwa ameenda hospitali kupima aliambiwa hana ute na mifupa ya kwenye magoti inasagika kwa kuwa hakuna ute, kumbe washenzi walikuwa wamemwekea joints za miti na ute mweusi na kusababisha miguu kuuma sana. Wakati mwingine unaweza kwenda hospitali ukaambiwa una tatizo fulani kumbe ni hayo mashetani yamesababisha uonekane unaumwa huo ugonjwa, siyo kila ugonjwa ni wa kweli. Baada ya kumtoa huo ute mweusi mguuni na kumrudishia ute wake, alitembea vizuri sana bila kuchechemea. Maombi yaliyofuata ni kumtoa kwenye bahari ya damu, ktk ulimwengu wa roho alionekana yuko kwenye bahari ya damu akitapatapa na kuomba Msaada, kisha alifanyiwa maombi ya Yai la maadui, kisha alifanyiwa maombi ya kuondoa weusi kwenye mikono yake, huo weusi ulikaa km groves, utafikiri mtu kavaa groves, mikono myeusi ni ili mtu asik**ate pesa na kila akifanyacho kiwe ziro. Kisha yakafuata maombi ya kukikomboa kizazi chake, yalikuwa ya nguvu sana, maana kizazi chake kilikuwa kimefungwa kisibarikiwe, watoto wake wahangaike, wasifanikiwe na wasipate ndoa, wakati wa kukikomboa kizazi chake likatolewa yai la mbuni lenye mwewe ndani yake mwenye macho mawili yenye rangi tofauti, jicho moja lina rangi nyekundu, lingine lina rangi blue, hili yai lilitoka tumboni, pia ikatolewa hirizi nyeusi kwenye kizazi chake. Kisha yakafanyika maombi ya kutoa hizo nyoka 7 nyeusi waliokufa, walikuwa wamejivingirisha ndani ya mwili wake katikati. Yakafanyika maombi ya kuvua pete iliyokuwa kwenye kidole cha kati cha mkono wa kulia, pete ilihamia kwenye kidole cha kati cha mkono wa kushoto, kazi yake ni kufunga baraka zake na za watoto wake, pete ilivuka kwa NGUVU ZA MUNGU. Ikatolewa nafsi iliyo ndani yake na akarudishiwa nafsi yake, likatolewa giza kwenye mwili wake, akavuliwa vazi jeusi alilovikwa na akaona vibwengo vinne, vibwengo hivyo vilitoka kwenye hilo vazi. Akaingizwa kwenye BESENI LA UPAKO LA DAMU YA YESU. Ni beseni lenye nguvu sana, ili MUNGU WA UTUKUFU amshughulikie mwenyewe kwa ajili ya vifungo vingi alivyonavyo. Kweli alishughulikiwa KIKAMILIFU. Akatakaswa kwa damu ya YESU mwili mzima, kisha akashushiwa nguvu za MUNGU na kupewa MOTO wa MUNGU ili awe na MOTO wa MUNGU ndani yake. Kweli akapokea moto wa MUNGU, maana hapo kwanza hakuwahi kuusikia moto wa MUNGU ni kutokana na vifungo vingi alivyokuwa navyo, baada ya kufunguliwa ndio anausikia MOTO wa MUNGU.
ONYO:
Enyi wachawi acheni kuroga watu, huo ni ujinga na kutokuwa na akili, watu wanatafuta maendeleo nyie mnawarudisha nyuma, watu wanatafuta afya nyie mnawapa magonjwa, mnapata faida gani kwa hizo roho mbaya zenu? Washenzi ninyi, uchawi hauna nguvu mbele za MUNGU.