Tmcs-cbe

Tmcs-cbe Tmcs cbe ni umoja wa wanafunzi wakatoliki kutoka chuo Cha Elimu ya Biashara CBE dar es salaam campus

Permanently closed.
28/04/2022

π—žπ—ͺπ—”π—‘π—œπ—‘π—œ 𝗑𝗔𝗣𝗔𝗦π—ͺ𝗔 π—žπ—¨π—¨π—‘π—šπ—”π— π—”?

πŸ› Naungama kwa sababu naogopa siku nikifa nitaenda motoni.

πŸ› Naungama kwa sababu kesho nataka kupokea Komunyo takatifu.

πŸ› Naungama kwa sababu najiandaa kusali vema novena ya Mtakatifu fulani niliyoichagua.

πŸ› Naungama kwa sababu nataka kubariki ndoa yangu, ili niepukane na uchumba sugu.

πŸ› Naungama kwa sababu nataka kufunga milango yote ya laana, ili mapepo yasinishambulie.

πŸ› Naungama kwa sababu Padre anione ili anipe pongezi na kunitolea mfano mzuri mbele ya Waamini.

πŸ› Naungama kwa sababu ni mazoea yangu niliyojiwekea tangu zamani ya kuungama angalau mara kwa wiki.

πŸ› Naungama kwa sababu wengine pia wanaungama, bila wao ukweli nisingeungama.

πŸ› Naungama kwa sababu nataka kujionyesha mbele za watu kuwa mimi ni Mtakatifu sana kuliko wao.

πŸ› Naungama kwa sababu mimi ni Mtumishi wa Altare na jumapili ni zamu yangu kutumikia.

πŸ› Naungama kwa sababu mimi ni Msimamizi wa Kipaimara nimeagizwa na Askofu niungame kila ninapopata nafasi.

πŸ› Naungama kwa sababu mimi ni Padre na nimeamuriwa kufanya hivyo ili niadhimishe Misa takatifu kikamilifu.

πŸ› Naungama kwa sababu mimi ni Mtawa pale Parokiani nisipoungama Waamini wengine watanifikiriaje.

πŸ› Naungama kwa sababu tu ya kutimiza sheria za Kanisa ambazo nilifundishwa tangu utotoni k**a Mkristo Mkatoliki.

πŸ‘‰ Mpendwa! K**a wewe ni miongoni mwa wale wanaoungama kwa sababu mbalimbali nilizozitaja hapo juu, basi tambu kitubio chako sio sahihi mbele za Mungu. Daima unapaswa kuungama kwa sababu tu umemkosea Mungu, na upo tayari kujenga upya urafiki wako na Mungu ulioharibiwa na dhambi zako za kila mara.

πŸ‘‰ Hivyo usiungame k**a hujadhamiria kuacha maovu yako, hata k**a kuungama ni haki yako. Kwani kuungama kwa mazoea ili kujionyesha kwa watu, haikusaidii kitu. Maana Kitubio cha kweli kinaanzia ndani ya moyo wako kwa njia ya toba na majuto ya dhati, halafu kinatimizwa kwa nje unapokwenda kwa Padre.

π—§π—¨π— π—¦π—œπ—™π—¨ π—¬π—˜π—¦π—¨ π—žπ—₯π—œπ—¦π—§π—’...

27/04/2022

*MAKANISA MATATU KATIKA KANISA KATOLIKI.*

1. KANISA LA WASAFIRI.

Hawa ni wale walioko duniani, bado wanapita katika milima na mabonde katika safari ya Imani, hawa ni mimi na wewe! Tunahimizwa kutenda mema na kuwa wavumilivu.

Mathayo 5:3-11

3 β€œHeri walio maskini rohoni, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
4. Heri walio na huzuni, maana watafarijiwa.
5. Heri walio wapole, maana watairithi nchi.
6. Heri wenye njaa na kiu ya kufanya atakavyo Mungu, maana watashibishwa.
7. Heri walio na huruma, maana watahurumiwa.
8. Heri wenye moyo safi, maana watamwona Mungu.
9. Heri wenye kuleta amani, maana wataitwa watoto wa Mungu.
10. Heri wanaoteswa kwa sababu ya kufanya atakavyo Mungu, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
11. Heri yenu ninyi watu wakiwatukana, wakiwadhulumu na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa ajili yangu."

2. KANISA LA WALIOKO TOHARANI, (PURGATORIO).

Hawa ni wale waliokufa wakiwa katika tumaini la wokovu, lakini hawakupata nafasi ya utakaso kamili katika ulimwengu, hii ni sehemu wanayopitia kwa ajili ya malipizi,

Nalo Kanisa la wasafiri wanao wajibu wa kuliombea kundi hili.

Zaburi 88,
4.Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni, nimekuwa k**a mtu asiye na msaada.
10. Wafu je! Utawafanyia miujiza?
Au waliofariki watasimama na kukuhimidi?
(Upatapo nafasi soma Zaburi yote)

2 Wamakabayo 12:38-46

43. Pia alichangisha fedha kutoka kwa watu wake fedha ipatayo drakma elfu mbili, akaipeleka Yerusalemu kwa ajili ya dhabihu ya kuondoa dhambi. Yuda alifanya tendo hilo jema kwa sababu aliamini juu ya ufufuo wa wafu.
44. K**a asingekuwa na imani kwamba; wafu watafufuliwa, ingekuwa ni upumbavu na kazi bure kuwaombea marehemu.
45. Lakini akiwa anatazamia tuzo nzuri waliowekewa waliokufa wakiwa waaminifu kwa Mungu, hilo lilikuwa wazo jema na takatifu. Kwa hiyo Yuda alitolea dhabihu ya upatanisho ili watu wapate kuondolewa dhambi zao.

3. KANISA LA WASHINDI.

Hawa ni wale ambao wapo mbinguni, walioshinda vita ya imani duniani!

Zaburi 16:10
"Maana hatakuachia kuzimu nafsi yangu, wala humwachi mtakatifu wako aone uharibifu"

Mathayo 27;53
"Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
Makaburi yakafunuka;
Ikainuka miili ya watakatifu waliolala;
Nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.

*NB:*
*Shamba, nyumba unayokaa ni ya marehemu pengine baba, ndugu au mama au ni matokeo ya jitihada ya mtu ambae ameshafariki. Elimu ulionayo ni jitihada za ndugu fulani ambaye pengine hayupo tena. Amani ulionayo ni matokeo ya watu waliopigana, saivi unakΓ a unachora nne, Dawa unazotumia ni watu walikaa chini wakatengeneza pengine hata hawakuzifaidi, saivi ukiumwa kidogo unaenda dukani/hospitali unapona mara moja. ALAFU MTU ANAKUJA ANAKUAMBIA-HAKUNA KUWAOMBEA MAREHEMU*.

27/04/2022

*MAISHA YA WATAKATIFU*

*MT. PETRO SHANEL,*
PADRE NA MFIADINI
( 28 APRILI)

Petro Shanel alizaliwa nchini Ufaransa mwaka 1803. Wazazi wake walikuwa Wakristo wema ambao walikuwa wakulima. Kabla hajaweza kutamka neno, mama yake alimfunza kufanya ishara ya msalaba, na alipoweza kutembea kidogo aliwasindikiza wazazi wake Kanisani kushiriki Misa.

Alipokua, Paroko alimpokea na kumfundisha. Masomo yake yalimtia hamu ya kwenda kuongoza watu waliokuwa bado katika upagani. Alipata Upadre, akaingia Shirika la Mapadre Maristi, akatumwa kuhudumia katika Misioni ya Australia. Alivuka bahari, na kisha safari ya siku nyingi alitua kisiwani Futuna. Alipofika, mara alimtolea Bikira Maria watu wa Futuna akitundika medali za Bikira Maria katika miti. Mtawala wa nchi hiyo alijifanya mwenyewe k**a mungu, hata hivyo alimpokea Petro kwake akamjengea nyumba ya kukaa.

Kadri siku zilivyoendelea watu walizidi kuja kwa mafundisho ya Katekismu, na mfalme alimwonea wivu Padre huyu akidhani kwamba raia zake watamwacha. Waganga wake wakamhimiza awakataze watu wasimwuzie Padre chakula.

Siku moja Bradha aliyekuwa naye alimwambia: "Nimesikia habari kwamba watu wanataka kukuua". Padre Shanel alimwambia: "Haidhuru, Bradha, heri yangu k**a ningejaliwa kufa kwa ajili ya Yesu Kristo". Mwana wa mfalme mwenyewe pamoja na wavulana wengine walibatizwa na Padre Shanel. Mfalme akawaka hasira. Akapeleka mnyampara wake akamwue Padre Petro, wakati Bradha alipokuwa safarini. Mnyampara alikwenda Misioni pamoja na watu wanne, wakaiteka nyumba yote. Wakampiga Padre kwa rungu mara mbili. Mfiadini Mtakatifu akaanguka chini, mnyampara mbaya huyo akammaliza kwa kumpasua kichwa, akazimia.

Mtakatifu Petro Shanel alikufa hivi mwaka 1841, miaka mitatu baada ya kuwasili kisiwani Futuna. Kifo chake kilikamilisha upesi kazi aliyokuwa ameianza, maana baada ya miezi michache kisiwa chote kikawa cha Kikristo. Mkatekumeni mmoja alisema: "Anatupenda. Anafanya mwenyewe alivyotufundisha. Anawasemehe maadui. Mafundisho yake ni mazuri." Papa alimtangaza kuwa Mtakatifu mwaka 1954.

*MT. PETRO SHINEL, UTUOMBEE*

*MASOMO YA MISA*

I. Mdo. 5:27-33

Zab. 34:1,8,15-19

INJILI. Yn. 3:31-36

27/04/2022

MASOMO YA MISA, APRIL 28, 2022

ALHAMISI, JUMA LA 2 LA PASAKA,

SOMO 1
Mdo 5:27-33

Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza, akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu. Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu. Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti. Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi. Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, pamoja na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wote wamtiio. Wao waliposikia wakachomwa mioyo yao; wakafanya shauri kuwaua.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab 34:1, 8, 15-19

(K)Maskini huyu aliita, Bwana akasikia.

Nitamhimidi Bwana kila wakati,
Sifa zake zi kinywani mwangu daima.
Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema;
Heri mtu yule anayemtumaini. (K)

Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki,
Na masikio yake hukielekea kilio chao.
Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya,
Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
Walilia, naye Bwana akasikia,
Akawaponya na taabu zao zote. (K)

Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo,
Na waliopondeka roho huwaokoa.
Mateso ya mwenye haki ni mengi,
Lakini Bwana humponya nayo yote. (K)

SHANGILIO
Yn. 20:29

Aleluya, aleluya,
Umesadiki, Toma, kwa kuwa umeniona, wa heri wale wasioona, wakasadiki.
Aleluya.

INJILI
Yn 3:31-36

Yeye ajaye kutoka juu, huyo yu juu ya yote. Yeye aliye wa dunia, asili yake ni ya dunia, naye anena mambo ya duniani. Yeye ajaye kutoka mbinguni yu juu ya yote. Yale aliyoyaona na kuyasikia ndiyo anayoyashuhudia, wala hakuna anayeukubali ushuhuda wake. Yeye aliyeukubali ushuhuda wake ametia muhuri ya kwamba Mungu ni kweli. Kwa kuwa yeye aliyetumwa na Mungu huyanena maneno ya Mungu; kwa sababu hamtoi Roho kwa kipimo. Baba ampenda Mwana, naye amempa vyote mkononi mwake. Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Neema isiyo na kikomo imetolewa ili roho iaminiyo iweze kuwekwa huru na dhambi; kwa maana mbingu zote, pamoja na rasilim...
26/04/2022

Neema isiyo na kikomo imetolewa ili roho iaminiyo iweze kuwekwa huru na dhambi; kwa maana mbingu zote, pamoja na rasilimali zake zisizo na kikomo, zimewekwa chini ya amri yetu. Tunapaswa kuchota kutoka kwenye kisima cha wokovu.

Kristo ndiye mwisho wa sheria ili kila aaminiye ahesabiwe haki. Ndani yetu sisi ni wenye dhambi; lakini katika Kristo sisi ni wenye haki.

Baada ya kutufanya kuwa wenye haki kwa njia ya haki ya Kristo, Mungu hututamka kuwa wenye haki, na hututendea k**a wenye haki. Anatutazama k**a watoto Wake wapendwa.

Kristo anafanya kazi dhidi ya nguvu ya dhambi, na pale dhambi ilipozidi, neema inaongezeka zaidi.

"Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo; ambaye kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo tunasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu." Warumi 5:1,2

~ AMANI IWE KWENU~

*SALA YA KUOMBEA MAKOSA YA KILA SIKU*Baba wa milele, ninakutolea Moyo Mtakatifu wa Yesu, na Upendo wake wote, na Mateso ...
21/04/2022

*SALA YA KUOMBEA MAKOSA YA KILA SIKU*

Baba wa milele, ninakutolea Moyo Mtakatifu wa Yesu, na Upendo wake wote, na Mateso yake yote, na Mastahili yake yote.
Kwanza.
Kulipia dhambi nilizozitenda leo na wakati wa maisha yangu yote. Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, k**a mwanzo na sasa na siku zote na milele, Amina.
Pili.
Kuyatakasa mema niliyoyafanya le na wakati wa maisha yangu yote. Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, k**a mwanzo na sasa na siku zote na milele, Amina.
Tatu.
Kutolea mazuri niliyopaswa kufanya na yale ambayo leo sikuyafanya na wakati wa maisha yangu yote. Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, k**a mwanzo na sasa na siku zote na milele, Amina.

"Mtawa wa Maklara aliyekuwa amekufa, alimtokea mkuu wake mara, aliyekuwa akimuombea, akamwambia "nilienda Mbinguni kwa sababu ya sala hii, kwa kusali kila siku nililipa madeni yangu

21/04/2022

MASOMO YA MISA, APRILI 21, 2022

OKTAVA YA PASAKA, ALHAMISI

SOMO 1
Mdo 3:11-26

Siku zile, kiwete yule aliyeponywa alipokuwa akiwashika Petro na Yohane, watu wote wakawakusanyikia mbio katika tao lile lililoitwa tao la Sulemani, wakishangaa sana. Hata Petro alipoyaona haya akawajibu wale watu, Enyi Waisraeli, mbona mnastaajabia haya, au mbona mnatukazia macho sisi, kana kwamba tumemfanya huyu aende kwa nguvu zetu sisi, au kwa utauwa wetu sisi? Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu, ambaye ninyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake afunguliwe. Bali ninyi mlimkana yule Mtakatifu, yule Mwenye haki, mkataka mpewe mwuaji; mkamwua yule Mkuu wa uzima, ambaye Mungu amemfufua katika wafu; na sisi tu mashahidi wake. Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote. Basi sasa, ndugu, najua ya kuwa mliyatenda haya kwa kutokujua kwenu, k**a na wakuu wenu walivyotenda. Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo. Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana; apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani; ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu. Kwa maana Musa kweli alisema ya kwamba, Bwana Mungu wenu atawainulieni nabii, katika ndugu zenu, k**a mimi; msikieni yeye katika mambo yote atakayonena nanyi. Na itakuwa ya kwamba kila mtu asiyemsikiliza nabii huyo ataangamizwa na kutengwa na watu wake. Naam, na manabii wote tangu Samweli na wale waliokuja baada yake, wote walionena, walihubiri habari za siku hizi. Ninyi mmekuwa watoto wa manabii na wa maagano yale, ambayo Mungu aliagana na baba zenu, akimwambia Ibrahimu, Katika uzao wako kabila zote za ulimwengu zitabarikiwa. Mungu, akiisha kumfufua mtumishi wake Yesu, alimtuma kwenu ninyi kwanza, ili kuwabarikia kwa kumwepusha kila mmoja wenu na maovu yake.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab 8:1, 4-8

(K)Ee, Mungu, Bwana wetu; jinsi lilivyo tukufu jna lako duniani mwote.

Wewe, Mungu, Bwana wetu
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;
Mtu ni kitu gani hata umkumbuke,
Na binadamu hata umwangalie? (K)

Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu;
Umemvika taji ya utukufu na heshima;
Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;
Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake. (K)

Kondoo, na ng'ombe wote pia;
Naam, na wanyama wa kondeni;
Ndege wa angani, na samaki wa baharini;
Na kila kipitacho njia za baharini. (K)

INJILI
Lk 24:35-48

Wanafunzi waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate.
Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu.
Wakash*tuka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho. Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu? Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa k**a mnavyoniona mimi kuwa nayo. Na baada ya kusema hayo aliwaonyesha mikono yake na miguu yake. Basi walipokuwa hawajaamini kwa furaha, huku wakistaajabu, aliwaambia, Mna chakula cho chote hapa? Wakampa kipande cha samaki wa kuokwa. Akakitwaa, akala mbele yao.
Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi. Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

Kumbukumbu la Torati 20:4kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda kuwapigania juu ya adui zenu, ili kuwaoko...
21/04/2022

Kumbukumbu la Torati 20:4

kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda kuwapigania juu ya adui zenu, ili kuwaokoa ninyi.

Ninakutakia Alhamisi njema yenye Baraka

Baadhi ya vijana wakatoliki waliohudhuria Easter conference
19/04/2022

Baadhi ya vijana wakatoliki waliohudhuria Easter conference

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tmcs-cbe posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Tmcs-cbe:

Share