BAKIIF Islamic

BAKIIF Islamic Taasisi inaendeleza sababu ya ufahamu bora wa Uislamu wa kweli. Kukuza ujenzi wa amani na haki kupitia mazungumzo baina ya dini mbalimbali.

Taasisi ya Dini "sauti ya pamoja ya ulimwengu wa Kiislamu" inayojitahidi kupata masuluhisho ya Kiislamu kwa maswali yanayohusiana na matatizo ya kijamii, kiuchumi na kimaadili ya siku hizi. Kuimarisha udugu wa Kiislamu na kukuza maelewano bora na watu wa imani nyingine za kidini.

Tuna kukaribisha katika Swala ya Eid al-FitrSiku ya Eid itakuwa Jioni ya Alhamisi, Apr 20, 2023  au Jioni ya Ijumaa, Apr...
18/04/2023

Tuna kukaribisha katika Swala ya Eid al-Fitr

Siku ya Eid itakuwa
Jioni ya Alhamisi, Apr 20, 2023 au Jioni ya Ijumaa, Aprili 21, 2023.
Waislamu wote wa Dar es salaam hususwa wakazi wa Kimara Baruti, Kimara Korogwe na Kimara Mwisho, Swala ya Eid itaswaliwa viwanja vya Msikiti wa 'Baabul-Ilmi' uliopo karibu na chuo cha Afya ya KAM College, maarufu k**a BAKIIF Islamic.
Tunakuomba kuhudhuria katika Swala hii hapa Msikitini, ukiwa wewe pamoja na familia yako, pia ''Zakatil Fitir'' itafanyika kuwapa wahitaji hapa Msikitini.

BAKIIF Islamic
0755 351 262

السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللهِ وَبَرَكَاتُهُ​K**a mjuavyo uislamu sio dini ngumu, thamani ya Biriani, Pilau na U...
19/11/2022

السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللهِ وَبَرَكَاتُهُ​

K**a mjuavyo uislamu sio dini ngumu, thamani ya Biriani, Pilau na Ubwabwa, viliwe katika mjumuiko wa kheri ambao MUNGU anauridhia, hivyo tunachukua fursa hii kuwatangazia waislamu wote wa maeneo ya Kimara kwamba Tare 12/12/2022 siku ya Jumamosi saa mbili kamili usiku tutakuwa na Mawlid ya kumuadhimisha mtukufu wa Umma, Nabii Muhammad S.a.w hapa BAKIIF ISLAMIC, Kimara-Korogwe Dar es salaam, Tanzania.

Nachukua fursa hii kukukaribisha ufike bila kukosa, tusherehekee kwa pamoja khafla hii ya Mazazi ya Mtume Muhammad s.a.w, na pia unaweza kuchangia kufanikisha shughuli hii adhwim kwa kuwakilisha mchango wako au swadaka yako hapa BAKIIF ISLAMIC. Katika siku hiyo tutapata wasaa wa kuwarehemu ndugu zetu walio tangulia mbele za haki. Hivyo usikose kujumuika nasi katika viwanja vya BAKIIF.

Wabillahi taufiq walhidayah"

BAKIIF ISLAMIC
P.O.BOX 55185
Kimara Korogwe,
KAM College Road, Kivulini Street
House no 36
Phone +255 755 351 262

Swalah ya Ijumaa ni wajibu kwa kila Muislamu aliyebalegheEnyi mlioamini! Kukinadiwa Swala kwa siku ya Ijumaa, endeni kwa...
13/10/2022

Swalah ya Ijumaa ni wajibu kwa kila Muislamu aliyebaleghe

Enyi mlioamini! Kukinadiwa Swala kwa siku ya Ijumaa, endeni kwa haraka kwenye utajo wa Mwenyezi Mungu, na muache kufanya biashara.

Hawatoacha watu kuhudhuria Ijumaa, au Mwenyezi Mungu Atapiga mihuri juu ya nyoyo zao, kisha wawe ni miongoni mwa walioghafilika.

BAKIIF-ISLAMIC
+255755351262

KWENYE DINI YA KIISLAMU HAKUNA KITU KINAITWA "KUOKOKA"Sababu kubwa ni kwamba uislamu haukatazi kufanya madhambi bali uis...
19/07/2022

KWENYE DINI YA KIISLAMU HAKUNA KITU KINAITWA "KUOKOKA"

Sababu kubwa ni kwamba uislamu haukatazi kufanya madhambi bali uislamu unakataza kufikiria kufanya dhambi.

Yaani uislamu unashinikiza fikra zako zisijikite wala kupata nafasi kufikiria kunako kufanya dhambi. Mfumo mzima wa maisha ya mwislamu kwake ni ibada. Kila jambo alifanyalo muislamu kwa nia nzuri kwake ni ibada.

Fikra ni sawa sawa na Nia. Hivyo uwislamu unaipigania fikra yako nasio matendo yako, kwasababu fikra ndio Nia na ndio mzizi mkuu wa wewe kufanya madhambi na mema.

Hakuna tendo lolote litafanywa bila kulifikiria kwanza (kuliwekea nia) liwe baya au zuri ni lazima ufikirie kwanza yaani uwe na nia nalo. Sasa Uislamu unaipigania nia yako yaani ile fikra yako nasio matendo yako.
Tendo linaweza kuwa baya lakini nia yake ilikuwa ni zuri. Kwa mfano: Askari wa nchi kujiunga na kundi la ujambazi ili kuwafahamu hao majambazi na kubaini mipango yao na njia zao kwa kuwa nao pamoja ili baadae kuweza kuwadhibiti: Hapo utakuta tendo hilo kimtazamo ni baya kabisa na halifai lakini nia yake ni nzuri kwasababu inakuja kuilinda jamii hapo baadae isiweze kudhurika.

Pia tendo linaweza kuwa zuri lakini nia yake ilikuwa ni mbaya: Mfano; ibada za ria (kufanya ibada ili watu wakuone) hii ibada haitapokelewa na MUNGU kwasababu nia yako wewe ni watu wakuone, wakusifie na kukutukuza lakini kiuhalisia hukufanya kwa ajili ya MUNGU. Kwa hiyo unakuta hapo tendo ni zuri kimtazamo lakini nia ya muhusika ni mbovu na wala haifai.

HIVYO BASI, KWENYE UISLAMU HAKUNA "KUOKOKA" Kwasababu uislamu haupambani na matendo yako bali uislamu unapambana na nia yako. Kwani hata huko kuokoka bado kunaweza kukawa na nia mbaya. Pia ili uwokoke lazima ufikirie kunako kuokoka yaani lazima kuwe na nia hiyo. Sasa nia ni jambo kuu ambalo uislamu hulitazama, yaani ile fikra yako kunako kufanya jambo fulani.

Kwanini uislamu unakataza fikra mbovu.? Hii ni kwasababu kadiri fikra mbovu unapoipa nafasi kichwani kwako ndivyo inaelekea kutekelezeka kimatendo. Hivyo uislamu unakataza kabisa kufikiria kunako kufanya dhambi.

YESU Alisema kuwaambia watu wake "Hakika Musa aliwakataza msizini, lakini mimi ninawakataza msifikirie kunako zinaa"

Address

P. O. BOX 55185 Kam College Road, Kivulini Street, House No: 36, Ubungo District, Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BAKIIF Islamic posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to BAKIIF Islamic:

Share