06/06/2026
RHAPSODI YA UHAKIKA
Jumamosi, June 6, 2026
Mchungaji Chris

UKWELI KUHUSU ADUI YETU
Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa msh*taki wenu Ibilisi, k**a simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze (1 Petro 5:8).
Kuna mitazamo na dhana nyingi kuhusu Shetani, adui yetu, lakini ni Neno la Mungu pekee ndio hufunua utambulisho wake halisi. Biblia ndio kitabu chenye mamlaka zaidi ya vyote kuhusiana na kweli za kiroho, kwa kupitia Biblia, Mungu anafunua alikoanzia ibilisi, jinsi alivyo, na utendaji kazi wake. Pasipo kuwa na maarifa haya, watu hutembea katika ujinga; lakini ukiwa na maarifa haya, unatembea katika nuru , ufahamu, na utawala.
K**a unaamini katika Mungu, ni lazima pia uamini kile Alichosema. Mungu uyu huyu aliyejifunua kwetu katika Maandiko pia anatuambia waziwazi kwamba ibilisi yupo. Hivyo basi, kukataa kuwa Shetani yupo, ni kukataa ushuhuda wake Mungu mwenyewe. Maandiko hayamsemi ibilisi kuwa ni wazo la kufikirika; maandiko yanamuonyesha kuwa ni kiumbe wa kiroho mwenye nafsi halisi.
Tena Biblia pia inatuambia kuhusiana na mwanzo wake. Aliwahi kuwa malaika aliyekuja kumuasi Mungu na kuwa adui. Mtu anapopuuzia uwepo wa Shetani, mara nyingi hujikuta akishindwa kubaini tabia na njama zake za uovu za kujaribu kushawishi, kudanganya, kuua, na kuharibu.
Lakini maarifa ya Neno yanakupa ufahamu (utambuzi), ujasiri, na faida ya kuenenda kwa hekima na kiroho maishani. Inakuwezesha kuwa na maarifa na imani unayohitaji ili kutembea katika utawala endelevu juu ya Shetani na wajumbe wake wa giza.
Alisema, “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru” (Luka 10:19). Haleluya! Ndiyo, unaye adui, ibilisi; lakini ni adui aliyeshindwa. Yuko chini ya miguu yako. Hauko katika huruma yake; ametiishwa kwenye mamlaka yako katika Kristo. Wewe ni mkuu kwake, kwa maana unazo nguvu [na uweza] wa kumtoa (Mathayo 10:8, Marko 16:17). Tembea katika maarifa haya na utumie mamlaka yako katika Jina la Yesu.
SALA
Mpendwa Baba, ninashukuru kwa nuru ya Neno lako yenye kunipa ufahamu juu ya kweli za kiroho. Ufahamu wangu umeangaziwa kupitia Maandiko, na ninatembea katika hekima, utambuzi, na ushindi. Nina usikivu, nina mizizi katika kweli yako, nikidhihirisha mamlaka na utawala nilio nao ndani ya Kristo juu ya Shetani na ufalme wa giza, katika Jina la Yesu. Amina.
MASOMO ZAIDI:
1 Petro 5:8 AMPC; Yakobo 4:7; Luka 10:18-19
MPANGO WA KUSOMA BIBLIA KWA MWAKA 1:
Yohana 20:1-18 & 1 Mambo ya Nyakati 20-22
MPANGO WA KUSOMA BIBLIA KWA MIAKA 2:
1 Wakorintho 15:50-58 & Muhubiri 3-4
Sala Ya Wokovu
“Ee Bwana Mungu, ninamwamini kwa moyo wangu wote Yesu Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Ninaamini kuwa alikufa kwa ajili yangu na kuwa Mungu alimfufua kutoka kwa wafu. Ninaamini kuwa yu hai leo hii. Ninakiri kwa kinywa changu kuwa Yesu Kristo ni Bwana wa maisha yangu kuanzia leo. Kupitia Yeye na katika Jina Lake, nina uzima wa milele; nimezaliwa upya. Ahsante Bwana, kwa kuiokoa nafsi yangu! Sasa, mimi ni mwana wa Mungu. Haleluya!”
Imetolewa kutoka: Rhapsody of Realities Daily Devotional
Weka maoni kuhusu Rhapsodi ya leo kwenye https://www.rhapsodyofrealities.org