Habari Njema Ministry

Habari Njema Ministry Maalum kwa Ujumbe wa neno la Mungu, Injili ya Yesu Kristo na tumaini la Wokovu wetu.

19/02/2022

Lakini sasa, njia ya Mungu ya kuwakubali watu kuwa waadilifu imekwisha dhihirishwa, tena bila kutegemea sheria. Sheria na manabii hushuhudia jambo hili.
Mungu huwakubali watu kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao kwa Yesu Kristo; Mungu hufanya hivyo kwa wote wanaoamini; hakuna ubaguzi wowote.
Warumi 3:21- 22 BHNTLK

UPENDO WA MUNGU❤️Upendo wa Mungu ni zaidi ya vitu, ni zaidi ya baraka za mwilini yaani  zaidi ya pesa, mali, kazi, vyeo,...
19/02/2022

UPENDO WA MUNGU❤️
Upendo wa Mungu ni zaidi ya vitu, ni zaidi ya baraka za mwilini yaani zaidi ya pesa, mali, kazi, vyeo, nyumba, mke/mume mzuri. HUU NDIO UPENDO KAMILI WA MUNGU; SOMA ZOTE👇🏾

08/06/2020

HII NI ZAIDI YA OFA

Utafanyaje?
Kwa mfano unaingia kwenye duka kubwa la jumla na rejareja kununua kiberiti cha mia afu kabla hujamwambia muuzaji nataka kibiriti anakwambia chukua kitu kimoja tu unachohitaji katika hili duka BURE?

Je utachukua kiberiti ulichokuwa unatahitaji wakati huo?

Mtu asiyefikiri atachukua kiberiti na kurudi nyumbani amefurahi na kuwasimulia wenzie nimeenda dukani kununua kiberiti nikapewa bure sijalipa.

lakini mwenye akili atasahau kabisa k**a kilichompeleka dukani ni kiberiti, atachagua kitu chenye thamani kuliko vyote katika lile duka ili ajipatie faida mara dufu.

Ofa hii unayo wewe unaehangaika na shida mbali mbali za dunia, yupo aliye na thamani kuliko majibu ya shida na uhitaji wako, huyu unampata bure.

Najua unavitu unavihitaji sasa kuliko huyu, ndio sababu umesikia sana habari zake lakini huamini maana unafikiri hana msaada kwako, naomba leo ufikiri tofauti hivyo unavyohitaji ni k**a kiberiti cha mia tu huyu ndio wa thamani kuliko vyote unavyohitaji na unampata bure hutoi hata mia.

Ni kweli unachohitaji wewe ni uponyaji tu, unahitaji utajiri tu, unahitaji muujiza tu, unahitaji mtoto tu, unahitaji kupandishwa cheo tu, unahitaji ajira tu, unahitaji mke tu au mume tu na chochote unachohitaji.

Napenda kukwambia huyu anathamani kuliko vyote vilivyo na thamani, huyu ni vyote katika vyote, ukimpata yeye umepata vyote.

Huyu ninayemzungumzia ni YESU. Najua hili jina umelisikia sana habari zake na unalichukulia poa tu, najua umewahi kulitumia mara kibao hajaona likikusaidia, lakini siku ya leo ni ya kipekee sana kwako narudia kwa herufi kubwa kwa Jina la YESU, LEO NI SIKU YA KIPEKEE SANA KWAKO.

Utarudi kunishuhudia, Wewe fanya tu k**a ninavyokuambia.

Najua umewahi kusikia habari zake angalau mara moja, k**a hujawahi kabisa kumsikia huyu Yesu ni mwana wa Mungu alieshuka duniani kuukomboa ulimwengu.

Kwa ajili yetu aliteswa msalabani akafa siku ya tatu akafufuka, hii yote ni kwa ajili yetu wanadamu ili tusamehewe dhambi zote, na tuwe huru mbali na laana, shida, mateso yaletwayo na dhambi.

Sio dhambi zetu tu bali dhambi tangu vizazi hadi vizazi tangu enzi za Adam mpaka, ukoo wako mpaka baba na mama yako.

Sasa unachotakiwa kufanya hakihitaji nguvu, ni rahisi tena BURE hutoi hata mia, Mungu ametupa ofa ambayo haijawahi kutokea.

Muamini Yesu tu, yaani amini kwamba Yesu ni Bwana na mwokozi wa maisha yako hapa ulimwengu na ya kuwa yeye ni njia, kweli na uzima.

Amini kwamba hakuna jina lingine mbinguni, duniani wala kuzimu liwezalo kuokoa isipokuwa jina la Yesu.

Amini kwamba Yesu ni mwana pekee wa Mungu alietumwa kuukomboa ulimwengu. MUAMINI TU.

Yesu ni wa rehema hata k**a umefanya dhambi kubwa kiasi gani ukimwamini anakupokea uwe wake usiwe na wasi wasi MUAMINI TU!

Ukiamini chukua hatua ya kunipigia simu kwa hatua zaidi au mtafute mtumishi wa Mungu moja kwa moja huko uliko ili ukiri kwa sala ulichoamini na kubatizwa utakuwa umempokea Yesu. Hofa hii ni ya Leo hakuna ajuae kesho, fanya uamuzi leo amini leo umpokee Yesu.

K**a umempokea Yesu hongera sana, usiache kusambaza habari hii njema kwa wengine. Ubarikiwe Yesu anakupenda sana.

Mwl Mbwaga Joshua
+255763821004
+255621148970

27/05/2020

Mungu mwenyewe amesema: "Sitakuacha kamwe wala sitakutupa".
Ebr 13:5b BHN

MASKINI GARI YANGU!Mzee mmoja alikuwa anamiliki kampuni ya mabasi ya safari za mbali.Siku moja Mzee huyo alipita maeneo ...
26/05/2020

MASKINI GARI YANGU!

Mzee mmoja alikuwa anamiliki kampuni ya mabasi ya safari za mbali.

Siku moja Mzee huyo alipita maeneo ya gereji yake akamkuta fundi anataka kulifungua moja ya basi aliyokuwa akilipenda na kuliamini kati ya mabasi yake makubwa.

Ni basi alilonunua kwa bei ghali kuliko mabasi mengine yote kwa sababu ya uimara wake na pia ni basi la kisasa.

Akashangaa, " hili si basi langu limefuata nini hapa gereji!"

Mzee akamkatisha Yule fundi kuendelea kuifungua ile gari. Kwa sauti ya ukali akamkemea; Mazungumzo yao yalikuwa hivi;

Mzee: ehee! Embu iache gari yangu na unieleze ni nani amekwambia uifungue hii gari na imefikaje huku gereji.

Fundi: Samahani mzee ni dereva amelileta.

Mzee(akamgeukia dereva kwa ukali): We dereva imekuwaje umeharibu hii gari? Hata mwaka bado haijamaliza.

Dereva: Hili basi halijaharibika Bosi nimekuja kulifanyia service.

Mzee : Service! Kwani limekusumbua?

Dereva: Hapana Bosi ni kawaida kila baada ya muda Fulani tunayafanyia mabasi service nimeona basi langu sijalifanyia service kwa muda mrefu.

Mzee: We una wazimu nini! Hivi unalifananisha hili basi na hayo mabasi mengine hivi unajua basi hili nimenunua kwa bei gani? Hivi umeona kampuni yoyote ina basi la kisasa k**a hili? Hili ni basi pekee katika nchi hii. Ni imara na haliaharibiki ovyo. Mnataka kuanza kulifungua fungua mlete ubovu?

Dereva: Sawa Bossi nimekuelewa nisamehe sitalileta tena gereji.

Fundi: lakini mzee ni muhimu gari yoyote ifanyiwe service.

Mzee: We bwege nini! Si kwa gari hii. Hivi umewahi kufungua gari k**a hii lini?

Fundi: Ni kweli sijawahi kufungua lakini sitegemei k**a system yake itakuwa tofauti na magari mengine.

Mzee: Kwenda huko! sitaki ufungue hili gari magari yangu yote gusa ila sio hili basi.

Fundi: Sawa Mzee lakini gari ni gari tu.

Mzee alikataa kabisa ile basi yake kufanyiwa service.

Siku iliyofuata k**a ilivyokuwa kawaida yake gari lilipakia abiria na kuanza kuondoka lilipokaribia mahali lilipokua linaenda kufika ghafla likiwa kwenye mteremko na spidi kali breki zote zikakataa kushikika.

Dereva alihangaika sana lakini kutokana na kuchanganyikiwa hasa alipogundua breki hazina kazi alihama njia likapinduka.
Dereva na watu wachache walipoteza maisha pale pale. Na wengine wengi walijeruhiwa.

Yule mzee alipopata ile habari alichanganyikiwa, aliumia sana. Alimpoteza dereva wake na roho za watu wasio na hatia katika gari yake , aliingia hasara kwa gari yake kuharibika vibaya mno na kuingia gharama nyingine za fedha nyingi kutokana na kesi ya ajali iliyomkabili.

Baada ya mwezi mmoja Mzee alikutana na Yule fundi mazungumzo yao yalikuwa hivi;

Fundi: pole sana mzee kwa majanga yaliyokupata.

Mzee: Ahsante yani nimepata hasara kubwa sana sikutegemea.

Fundi: Pole sana, ni kawaida katika biashara vitu hivi vipo kilichobaki ni kukubali matokeo na kuangalia mbele.

Mzee: Yani basi lile sina hamu nalo, kumbe ni mbovu kiasi kile aisee siwezi kununua tena gari k**a ile naapa.

Fundi: Ile gari ni imara sana mzee, zile gari ni gari bora zinazoaminika kwa sasa usikate tamaa.

Mzee: We unaongea nini? acha upumbavu kwa kile kilichonipata bado unanishawishi niendelee kuziamini tena zile gari.

Fundi: Kumbuka neno nililokwambia gari ni gari. Tatizo sio gari lile tatizo ni wewe hukutaka kuelewa. Tungelifanyia lile gari service siku ile kisingetokea tunachokiongelea leo. Huwezi jua kinachoendelea ndani ya gari mpaka ulifungue haijalishi linaonekaneje au lina jina kubwa kiasi gani gari ni gari tu.

>> Kuliamini gari kulimgharimu mzee, kwa jinsi alivyolifahamu gari na uzoefu aliokuwa nao aliona hakuna sababu ya kulifanyia service.

Hii inatokea pia katika kanisa; Wakristo wengi hawana mzigo wa kuwaombea watu waliosimama, wale wanaowakubali na kubarikiwa nao, wale walio waweka mioyoni na kuwaona ni bora kuliko wengine badala yake huishia kuwasifu na kujivuna nao. Utasikia;

Huyu mtumishi kwa kweli ananibariki yani ni tofauti kabisa na watumishi wengine. Yani hana makuu kabisa. Kwanza anahekima, hapendi kujiinua ni mnyenyekevu hapendi pesa k**a watumishi wengine. Pia anaupako balaa kwa kweli huyu baba basi tu.

Ni kweli hivyo ndivyo umuonavyo lakini kumbuka huyo ni mwanadamu. Mchungaji mmoja alisema “the best of man is still a man”. Yaani mwanadamu hata awe bora vipi atabaki tu kuwa mwanadamu hawi malaika”.

Ukimwona mtumishi amesimama, akimuona mtumishi amekamilika usiahirishe kumuombea huyo ni mwanadamu. Kumsifia mtu aliesimama hakumfanyi mtu aendelea kusimama zaidi unamuongezea vita ya shetani kumwangusha.

Sisemi tusibarikiwe na kuwabariki kwa ukamilifu wao bali tusiishie kubarikiwa na kuwabariki na kuwasifu tuwaombee kwa Mungu aonae sirini. Maana yeye ndiye anaejua udhaifu wao. Nani ajuae maisha yao kwa undani?

Wapo waliovunjika mioyo na kupoteza imani kabisa na watumishi wote. Wanasema hakuna mtumishi wa kweli kwa sababu Yule mtumishi waliemuamini sana ameanguka.

Muombee mtumishi unaemwamini sana ili isije ikatokea na kwako huyo ni mwanadamu tu si malaika. Muimbaji mmoja aliimba akasema mtu akiokoka hageuki kuwa malaika.

Ukiona wanandoa wanaishi kwa amani usiishie kubarikiwa tuwaombee.
Wapo waliokata tamaa ya kuoa na kuolewa kwa sababu waliwaona wanapendana wameachana. Wale waliosema sijawai ona watu wanaopendana k**a hawa aliposikia wametengana akasema akilini mwake hakuna upendo wa kweli. tuwaombee.

Wapo waliokata tamaa ya kuoa na kuolewa kwa sababu waliwaona wanapendana wameachana. Wale waliosema sijawai ona watu wanaopendana k**a hawa aliposikia wametengana akasema akilini mwake hakuna upendo wa kweli.

>>YULE MZEE BAADA YA GARI ALILOKUWA ANALIAMINI KUANGUKA ALIKATA TAMAA NA KULICHUKIA LILE GARI. WAOMBEE WATUMISHI UNAOWAAMINI ILI WASIMAMA WASIJE WAKAANGUKA MAANA WAKIANGUKA UTAWACHUKIA NA KUJITENGA NAO.

Tunaona makanisa yanavunjika kwa sababu tu mtumishi kaanguka. Hii ni mbinu ya shetani imeandikwa Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika 26:31
1 Thes 5: 3 WAKATI WASEMAPO KUNA AMANI NA SALAMA, NDIPO UHARIBIFU UWAJIAPO KWA GHAFLA K**A UTUNGU UMJIAVYO MWENYE MIMBA, WALA HAKIKA HAWATAOKOLEWA.

Mwl Mbwaga Joshua
+255763821004

MAMBO MATATU YALIYO AJABU KWANGU, NAAM MANNE JUU YA UHUSIANO WA MTU NA MUNGU.Na Daima Kashililika  Kuna mambo matatu yal...
21/05/2019

MAMBO MATATU YALIYO AJABU KWANGU, NAAM MANNE JUU YA UHUSIANO WA MTU NA MUNGU.
Na Daima Kashililika

Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne yanayostaabusha juu ya uhusiano wa mtu na Mungu.

1. MAZINGIRA
Uhusiano wako na Mungu hutegemea sana mazingira uliyopo, hali ya kiroho ya eneo ulipo, upo uhusiano wa moja kwa moja kati ya Mazingira(Ardhi) na Imani ya mtu au Jamii,

Mazingira ni moja kati ya mambo ya ajabu kutufanya sisi kusitawi katika kumjua Mungu au kudumaa***(kati ya Ajali mbaya duniani).

Inategemea sana mbegu imepandwa katika udongo wa aina gani ili kukua na kuzaa matunda, Udongo naouzungumzia hapa ni Mazingira,

2. WATU
Umezungukwa na watu wa aina gani, Umezungukwa na watu wenye mitazamo gani, Wenye misimamo ipi katika Imani, Wana nguvu gani katika Kumtafuta Mungu, Ni watu(Marafiki, Familia, Ndugu na Jamaa).

Huwa haitegemei sana Viwango vyao vya kiroho na Mahusiano yao na Mungu kukufanya wewe ukue, Ila ni kichocheo kikubwa cha kukua kwako,

Akili zetu wanadamu zimeundwa katika namna ya kuchangamana na watu na mazingira ndipo kutuumba kuwa katika namna Jamii Inayotuzunguka na Mungu hutuona, Hakikisha upo katika jamii ya watu sahihi ili ndani yako pia uumbike sawa na Mungu anavokutazama.

3. HALI
Ni Hali ya Uchumi, Afya, hali ya inayoruhusu hali isiyoruhusu, Vyote huwa ni mambo ya msingi kuzingatia juu ya mahusiano yako na Mungu,

Kuna wengine pamoja na mali nyingi walizonazo lakini mahusiano yao na Mungu si tajiri, wengine ni masikini wa mali hata rohoni, wengine wakati wote tunawaza hatuwezi, wakati mwingine magonjwa tuliyonayo, Hali ya afya, husababisha watu kukata tamaa na maisha, na kuona kuwa Mungu labda hawezi tena,

Kumbuka hali uliyonayo iwe nzuri au isiwe nzuri hata siku moja isiwe ni sababu ya kutoka katika Imani (Kuharibu mahusiano yako na Mungu)

4. MAJIRA NA NYAKATI
Hapa nazungumzia Muda, Kati ya vitu Mungu amempa mwanadamu ni muda*** Na ukifika wakati hukutumia muda sawasawa na Mungu anavyosema uwe na uhakika, utaishi maisha yako yote na udhihirisho wa Mungu katika ujumla wakati hutouona lakini Mbinguni utakwenda, Hutoyafaidi Maisha Ambayo Mungu aweyaweka kwa ajili yako hapa duniani. Tumia muda Vizuri.

K**a mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi; Isaya 1:19
Yaani k**a mkikubali na kutii haya hakika yake ni kula mema (Yameandaliwa yatari na kuwekwa kwa ajili ya mimi na wewe) juu ya uso wa Ulimwengu huu.

Yesu anakupenda.
Utukufu Heshima Enzi na Adhama zina Mungu aliyeziumba Mbingu na Nchi.



.
Daima Kashililika
0757357871
Habari Njema Ministry 2019

Address

Email:hnministriestz@gmail. Com
Dar Es Salaam

Telephone

+255763821004

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari Njema Ministry posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Habari Njema Ministry:

Share