NABII Herieth

NABII Herieth HARRIET MBINGUNI ni MTUMISHI WA MUNGU WA UTUKUFU ALIYETUKUKA.

08/09/2021

KUTOKA KWENYE KIWANGO CHA KUOMBA KWENDA KWENYE KIWANGO CHA KUAGIZA

Kila mtu huomba, huomba sana tena huomba, huomba Kila Siku, Kila Siku ni maombi. Huomba kwa uchungu pale mtu anapokuwa na matatizo au tatizo zito. Huomba kwa kuugua. Pia kuna maombi mepesi ambayo siyo ya kuumia wala kuugua, mtu anaomba kwa kulilux. Neno linasema ombeni bila kukoma, bila kukoma ni mpaka pale mtu atakapopata kile kitu anachokitaka. Lakini mtu anatakiwa apige hatua kutoka kwenye Kiwango cha kuomba kwenda kwenye Kiwango cha kuagiza. Kuomba ni kubembeleza, kurudia-rudia maneno, yaani asubuhi umeomba hilo, mchana, usiku, kesho hilohilo, keshokutwa hilohilo yaani unarudia-rudia kutokana na uhitaji wako. Kuomba mtu anaomba hadi analia machozi, anaumia, anaugua maumivu makali. Nk. Kuna wakati mtu anatakiwa avuke kiwango hicho cha kuomba na kwenda kwenye kiwango cha kuagiza. Kumb 12:20 "Ukisema nataka kula nyama, waweza Kula nyama kwa kufuata yote inayotamani roho yako". Mtu anayeagiza anasema nataka, Nipe au Niletee kitu fulani. Kuna kipindi mtu anamwambia MUNGU, BWANA nataka unifanyie hiki kitu, BWANA nipe kitu fulani. Na MUNGU anafanya bila AJIZI. Ukifikia hiyo hatua ni raha sana.

03/09/2021

Pendelea kuongelea kuhusu ukuu wa MUNGU na matendo yake, ongelea mambo mazuri, Siyo kuongelea mambo mabaya. Ukiongea kuhusu mazuri, mazuri yanakujilia, ukiongelea kuhusu mabaya, mabaya hayaishi au unayakaribisha.

30/08/2021

HATUA TATU ZA KUBARIKIWA

1. KULISHWA NA KUNGURU 1fal 17:1-6
2. KULISHWA NA MJANE 1fal 17:7-12
3. KULISHWA NA MALAIKA 1fal 19:4-8

+255625187824 / +255713174677 / +255683807775

30/08/2021

KULISHWA NA KUNGURU

MUNGU WA UTUKUFU aliwaamuru Kunguru wamlishe Eliya. 1Falme 17:1-6
Ni kweli Kunguru walimlisha Eliya Nabii, je ni kweli Eliya alifurahia kulishwa na kunguru? Je! Na wewe waweza kufurahia kulishwa na Kunguru? Kwanza Kunguru ni mchafu, na Chakula anabebea mdomoni, tena hutoka udenda, hula uchafu hata kuokoteleza jalalani, alafu mdomo huo huo abebee chakula akupe ule. K**a tujuavyo njaa inauma, mbele ya njaa waweza kula chochote kitu iwapo hakuna chakula cha maana. Kuna watu wanaiba kwa sababu ya njaa, njaa ni kitu kisichovumilika waweza kula vya jalalani. Sasa iwapo hakuna chakula kiwacho chote ni wazi kuwa chakula kilichobebwa na Kunguru kwa mdomo wake kitaliwa tu! Utake usitake! Nabii Eliya ilimlazimu kula chakula Kilicholetwa na Kunguru kwa Sababu alikuwa hana jinsi, na MUNGU ndiye aliyemwamuru Kunguru amlishe Eliya. Kila mwanadamu huwa kuna mazingira anayoyapitia ambayo pengine haendani nayo hata kidogo kutokana na hadhi yake, lakini inamlazimu kuyapitia kwa kuwa MUNGU ndiye aliyepanga, huko ndiko kulishwa na Kunguru. K**a kuna kazi unafanya haiendani na wewe huko ni kulishwa na Kunguru! K**a unafanya biashara isiyo hadhi yako huko ni Kulishwa na Kunguru! K**a umeoa au kuolewa na mtu ambaye hukutarajia au ambaye hukumtaka, huko ni kulishwa na Kunguru! K**a unaishi kwa mtu, mjomba, kaka, dada, shangazi, mama mdogo, rafiki na umefikia umri wa kujitegemea huko ni kulishwa na kunguru! K**a unakula Chakula ilimradi usife huko ni kulishwa na Kunguru! K**a unavaa mavazi yaliyopitwa na wakati, machakavu huko ni kulishwa na Kunguru! K**a unaishi kwenye nyumba Chakavu au isiyo hadhi yako, huko ni Kulishwa na Kunguru! Unamkuta mtu Nywele ni Kikunguru-kunguru! Mavazi Kikunguru-kunguru! Chakula Kikunguru-kunguru! Kitanda Kikunguru-kunguru! Mashuka Kikunguru-kunguru! Makazi Kikunguru-kunguru! Ngozi Kikunguru-kunguru! Mafuta Kikunguru-kunguru! Vyombo Kikunguru-kunguru! Fenicha Kikunguru-kunguru! Huduma Kikunguru-kunguru! Usafiri Kikunguru-kunguru! Mwombe MUNGU kuwa nimechoka maisha ya Kikunguru-kunguru, Maisha ya Kikunguru-kunguru hayana raha yoyote. Hata kiroho ni Kikunguru-kunguru! Mtu mahali alipo kiroho sipo anapotakiwa kuwa. Kataa maisha ya Kikunguru-Kunguru. K**a nilivyosema kuwa kulishwa na Kunguru ni kupitia mazingira ambayo yanakulazimu kwa kuwa unakuwa huna jinsi, ila wewe nafsi yako unakuwa haupendi kabisa. Mwambie MUNGU yatosha kwa muda niliolishwa na Kunguru

Mawasiliano
+255625187824/+255713174677/+255683807775
Nabii herieth

19/08/2021

NGOME (8)

Wenzetu waliotangulia walikuwa wakipigana Kimwili, Yonathani aliipiga Ngome ya Wafilisti, Sauli Daudi na wengineo, kwa Sababu walikuwa ni maadui zao. Sisi tunapigana Vita Katika Ulimwengu wa Roho, Siyo katika ulimwengu wa mwili. Hivyo Sisi tunapambana na Shetani na Mawakala wake, tunavunja Ngome zote za Shetani. Na MUNGU wetu aliyetukuka yeye ndiye NGOME juu ya Ngome zote.
Huwa hatukosi kuzijua hila za Shetani mapema;.
2 Falme 8:7-15 Hapa tunaona kuwa Ben-Hadadi Mfalme wa Shamu alikuwa anaumwa, aliposikia Elisha amekuja akamtuma Hazaeli mtumishi wake akamuulize k**a atapona. Hazaeli akaenda kumuuliza Elisha, Elisha akasema Ben-Hadadi atakufa, kisha Elisha akalia machozi. Hazaeli akamwuliza unalilia nini, Elisha akajibu kwa Sababu nayajua mabaya utakayowatenda wana israeli, utazichoma moto NGOME zao, utawaua vijana wao kwa upanga, utawaseta-seta watoto wao wachanga na wanawake wao wenye mimba utawapasua. Hazaeli akasema, Lakini mimi mtumwa wako ni nani mimi niliye mbwa tu hata nifanye jambo hili kubwa?. Elisha akajibu, Bwana amenionyesha ya kwamba wewe utakuwa Mfame juu ya Shamu.
Watu wa MUNGU hawakosi kuzijua hila za Shetani mapema. Hazaeli alikuwa ni Kiongozi asiye na Sifa, Elisha alilijua hilo lakini hakuwa na uwezo wa kumzuia asiwe kiongozi maana k**a angewaambia watu kuwa Hazaeli hafai wasingemuelewa maana watu walimwona jinsi alivyo kwamba anaonekana mchapakazi, mpole mwenye kujali, kumbe watu wanakuwa wapole na wanyenyekevu wakiwa hawajapata NGUVU, mtu kabla hajapata madaraka anakuwa mpole anakuwa karibu na wananchi kwa Sababu kuna kitu anakitafuta, lakini akishakipata akawa na NGUVU na Mamlaka wala haonekani tena, wala hawajali watu. Anatenda k**a atakavyo yeye, wala hasikilizi ushauri wa watu. Linahitajika jicho la tatu kumjua Kiongozi mzuri mwenye moyo na wananchi, mwenye huruma na watu, mpenda maendeleo, Mzalendo wa Nchi yake. Na kweli Ben-Hadadi alipokufa Hazaeli akawa Mfalme mahala pake. Ebu angalia kiongozi wa nchi anapokufa anayechukua nafasi yake yukoje? Ben-Hadadi alikuwa mzuri, lakini Hazaeli aliharibu kabisa, na si kuharibu, bali alikuwa hafai! Yaani mtu anatawala huku wananchi wanalia wanamwombea Kifo na laana, kutawala hakuhitaji Nguvu za mwili, kunahitaji Hekima.
Zaburi 9:9 "BWANA atakuwa NGOME kwake aliyeonewa, Naam, Ngome kwa Nyakati za Shida".
Zaburi 27:1-3 "BWANA ni nuru ya WOKOVU wangu, nimwogope nani? BWANA ni NGOME ya Uzima wangu, nimhofu nani?".

16/08/2021

NGOME (7)

VUNJA NGOME ZA SHETANI

1. NGOME ZA MAGONJWA
2. NGOME ZA UMASKINI
3. NGOME ZA MAUTI
4. NGOME ZA KUVUNJA NDOA NA CHUMBA ZA WATU
5. NGOME ZA KUTOKUOA NA KUOLEWA
6. NGOME ZA AIBU NA FEDHEHA
7. NGOME ZA UTAABISHAJI NA MAHANGAIKO
8. NGOME ZA UOVU NA UASI
9. NGOME ZA USAGAJI NA USHOGA
10. NGOME ZA UONEVU

11. NGOME ZA MAPEPO
12. NGOME ZA MASHETANI
13. NGOME ZA MIZIMU
14. NGOME ZA WACHAWI NA KILA AINA YA NGUVU ZA GIZA

Kila Ngome inavunjwa kwa NGUVU KUTUMIA NGUVU ZA MUNGU, Nguvu za MUNGU zinaachiliwa kutokana na ukubwa wa Ngome au uzito wa ngome. Ngome nzito NGUVU nyingi, na hii yote inatendeka kwa JINA LA YESU, JINA LA YESU ndilo liwezalo.

Mhubiri 9:14 "Palikuwa na mji mdogo, na watu ndani yake walikuwa wachache, akaja mfalme mkuu juu yake, akauhusuru, akajenga ngome kubwa ili kuupiga". Ebu fikiria kuwa mji mdogo wenye watu wachache, mfalme mkuu pamoja na ukuu wake anajenga ngome kubwa ili kuupiga!. Unafikiria kwa nini mfalme alifanya vile? Je hana akili au ni mwoga? La hasha! Bali alikuwa anajihami, watu wachache huwa hawadharauliwi, watu wanaweza kuwa wawili watatu ila wana nguvu sana wakaweza kuwaangamiza watu wengi, hivyo mfalme alikuwa Sahihi. Lakini sisi tuna MUNGU anayeweza, iwe kwa wengi au wachache! MUNGU anaweza hata kumwangalia mtu mmoja tu, kinachotakiwa ni IMANI, Ukimwamini MUNGU bila woga wala wasiwasi, MUNGU anatenda.

16/08/2021

NGOME (6)

Shetani hupambana na mtu ambaye ni NGOME, hupenda kumfuatilia mtu huyo, maana anajua kuwa akimpata huyo habari imeisha. Ngome ndani ya Familia, Ngome kwenye ukoo, Ngome ndani ya Kanisa, Ngome kwenye Taifa. Ngome ndani ya Familia anaweza kuwa mtoto anayetegemewa, au baba au mama, ndugu nk. Ngome ndani ya Taifa ni wale wanaoliingizia Taifa Kipato kingi au wanaolitangaza Taifa, watu wanaoajiri wafanyakazi wengi, au mtu daktari bingwa au mtu mahili wa kitu fulani. Ni kuwaombea hawa watu. Cha ajabu zaidi kuna baadhi ya watu nao wanapenda kupambana na mtu ambaye ni NGOME, Wanapenda kumsimanga na kumnenea visivyo hata kumpangia njama, wanachotaka ni kummaliza badala ya kumshukuru MUNGU kwa ajili yake na kumuunga mkono ili maisha ya watu yainuliwe. Mtu ambaye ni NGOME akifilisika au kufa watu wengine wanafurahi, kuna watu wa ajabu ambao wanafurahia kuanguka kwa wenzao, huu ni ushetani uliokithiri. Wengine hawataki kukuona ukiinuka, wanataka kuona ukitaabika na kubaki palepale. Watu k**a hawa maisha yao ni mabaya. Hawawezi kuinuliwa zaidi, watabaki palepale na k**a wako vizuri mbeleni kuna Anguko maana wanakosa baraka za MUNGU. Pia kuna watu wana VIPAJI vizuri sana vya kuweza kuingizia Taifa Kipato au kuinua watu, lakini asilimia kubwa ya watu wenye Vipaji hawana Uwezo wa kifedha, wanashindwa watoke vipi, inatakiwa Serikali iangalie namna ya kuwasaidia, maana wanapotoka Uchumi wa Nchi unaongezeka, watu wanapata ajira na miradi mingi kufunguliwa, hakuna kitu kizuri k**a Sanaa na Usanii ni vitu vyenye mvuto na ushawishi mkubwa. Mtu mmoja anapoinuka huinuka na wengi. Kuna watu wanapenda kuwa wajasiriamali vitega uchumi hawana, hawa wanatakiwa wasaidiwe ni NGOME. Kuna watu wana VIPAWA na KARAMA makanisani ila hawapati Saport yoyote, tena wengine wapo chini ya Watumishi wa MUNGU wenye UWEZO wa kuwasaidia lakini hawapati Msaada wowote, Kanisa likishainuliwa lina wajibu wa kusaidia watu na kusaport Vipawa. Haipendezi kuona vifaranga vya kuku vinahangaika wakati vina mama yao, mwisho vinaliwa na Kunguru. Mtu mmoja anapoinuliwa inatakiwa kumuunga mkono ili mpate baraka zake, siyo kumtenga na kumteta. Iwapo mtu ni mfanyabiashara, au mkulima, au mfanyakazi, Mwimbaji, Mwinjilisti/Mwalimu/Mchungaji/Mtume/Nabii au mbunifu, mtu wa Sanaa, mwanasiasa nk. Inatakiwa kupeana Saport na kuombeana NGOME zinapokuwa nyingi ndipo maendeleo huja kwa wingi. Tukizikandamiza NGOME maendeleo yatakujaje? Nchi hujengwa na wananchi. UMOJA NI NGUVU.

16/08/2021

NGOME (5)

K**a nilivyosema awali, kuwa pia Ngome ni makazi ya maroho na pepo wachafu ndani ya mtu au kwenye mji yaliyokaa kwa muda mrefu kwa ajili ya Kuleta uharibifu.
Ufunuo 18:2 "Akalia kwa Sauti kuu akisema, Umeanguka Umeanguka, Babeli ule mkuu, umekuwa maskani ya mashetani na Ngome ya Kila roho mchafu, na Ngome ya kila Ndege mchafu mwenye Kuchukiza.
Ngome ya Shetani inaweza kuwa ndani ya mtu pia, ni yale maroho yaliyokaa muda mrefu ndani ya mtu na kumtesa. Kuna mtu anakuwa na roho ya uzinzi mpaka unashangaa, kutokana na Uzinzi alionao mtu inakuwa ni Ngome! Kuna mtu ana roho ya Ulevi imekithiri, ila ni Ngome. Kuna mtu amefungwa kweli ana vifungo Kibao, hiyo ni Ngome. Na watu wengi wakishaokoka wakampokea YESU wanafikiri Kila kitu kimeisha hawana haja ya maombi ya UKOMBOZI, na ndiyo maana wengi wao maisha yanakuwa ya duni au ya Chini, k**a mtu hana Kifungo chochote hapo sawa. Ila k**a ana Vifungo usiombe maombi ya Ukombozi inakuwa Shida, ndo wale wameokoka lakini maisha yao yanakuwa hayaeleweki, kuna watu wako makanisani wana vifungo k**a vyote, na mtu anaomba na kunena kwa Lugha. K**a mtu ana Vifungo anakombolewa vipi eti kwa kuongozwa tu Sala ya Toba na kuanza kusali?
Maroho na Pepo wachafu ndani ya mji hufanya mji usiendelee, ndiyo maana neno linasema umekuwa maskani ya mashetani na ngome ya kila roho chafu. Kuna mitaa unakuta haiendelei, kuna mikoa haiendelei, kunakuwa na Ngome za shetani na vizuizi, mtaa mji kukombolewa inahitaji maombi, kuzivunja Ngome za Shetani.

Tuangalie maana nyingine ya NGOME kwa upande mwingine

1. Ngome ni kitu cha kutegemewa, Kitu ambacho mtu anakitegemea ndiyo huitwa Ngome. Au ngome inaweza kuwa ni mtu ambaye anategemewa. Hivyo katika michezo Ngome ni mchezaji anayekaa nyuma kwa ajili ya kuzuia mashambulizi, na katika mchezo wowote ngome ni mchezaji anayetegemewa

2. Ngome ni Jengo lililojengwa kwa ajili ya kujihami na maadui au mashambulizi.

Katika Familia pia huwa kuna mtu ambaye anategemewa, anaweza kuwa mtoto/ndugu au mzazi kwamba akifa huyo basi. Katika Nchi pia huwa kuna vitu ambavyo vinategemewa. Kwenye Vita maadui hulenga vile vitu vinavyotegemewa, hushambulia wanajeshi au askari wanaotegemewa kwamba tukimuua yeye basi tumemaliza mchezo. Mahali popote hushambuliwa sana mtu anayetegemewa ambaye ndiye NGUZO au NGOME. Na katika michezo mara nyingi mshambuliaji hatari au mchezaji mzuri anayetegemewa na Timu huweza kushambuliwa ili kumvunja nguvu ashindwe kucheza ili asije akaipatia TIMU ushindi.

16/08/2021

NGOME (4)

NINI MAANA YA NGOME?

1. Ngome ni Kituo ambacho watu hukutana kwa ajili ya kupanga mashambulizi, kwamba wavamie wapi, wamlenge nani nk.

2. Ngome ni mahali ambapo shetani ameweka kituo chake kwa ajili ya kufanya mashambulizi.

3. Ngome ni makazi ya maroho na pepo wachafu waliokaa muda mrefu ndani ya mtu au mji kwa ajili ya kuleta uharibifu. Pia inaweza kuwa katika mji au mtaa kwenye makazi ya watu. Ufunuo 18:2

Shetani anapopanga mipango yake hutumia mawakala wake katika utendaji wa kazi, ni sawa na jinsi MUNGU WA UTUKUFU anavyowatumia watumishi wake. Shetani hutumia wachawi, waganga wa kienyeji, pepo wachafu, majini na mashetani na roho za mizimu. Ngome za shetani ni uharibifu tu.
K**a nilivyosema kuwa Ngome ni Kituo ambacho Shetani hukutana na mawakala wake kwa ajili ya kupanga mashambulizi, wavamie wapi, wamshambulie nani, au ngome ni makazi ambayo shetani ameweka mashambulizi yake, ni sawa na majambazi wanakuwa na mahali pa kukutania ili wapange mipango yao ya uvamizi, wanapanga wamvamie nani na wamvamie kwa jinsi gani, uvamizi huwa haufanani. Hivyo Shetani naye ana uwezo wa kupanga hatima ya mtu iweje, k**a iishie kwenye kilio au mtu aishie kujinyonga, au mtu asizae, au mtu asiolewe au asioe, au mtu apoteze vyote, au mtu we wa kuzalishwa na kuachwa, au mtu afanye vizuri aishie pabaya, au mtu ahangaike katika maisha yake yote, ana uwezo mpaka wa kuutoa uhai wa mtu. Hivyo Ngome ni maskani za shetani za kuleta uharibifu, kuna maskani za majambazi, kuna maskani za wavuta bangi, kuna maskani za makahaba, nk. MUNGU anaposema VUNJA ngome zote za Shetani inatakiwa kuvunja kweli kweli kwa kuwa shetani muda wote ana mipango mibaya. Ana mipango mibaya juu ya mtu, ana mipango mibaya juu ya Taifa hili kuliangamiza na kutuletea mambo ya ajabu, Kuharibu kizazi chetu nk. lakini MUNGU yupo muweza wa yote. Askari polisi wanapoamua kutembeza Msako kusaka maskani za majambazi na kuwak**ata na kuteketeza maskani zao, basi ujambazi huisha wote. Na wakifanya Msako kuvamia maskani za wavuta bangi, basi wavuta bangi hawataonekana tena wakivuta bangi, wakifanya msako kwenye maskani za makahaba, makahaba hawataonekana tena kwenye maskani zao na ukahaba utaisha. Hivyo na watumishi wa MUNGU wakiamua kuvunja NGOME za shetani, NGOME zitaanguka. Maana ndio askari wa MUNGU.
Siyo mpango wa MUNGU kwamba watu waanze vizuri waishie Pabaya!
Siyo mpango wa MUNGU migongano na malumbano, MUNGU anapenda AMANI, UTULIVU na USIKIVU.

15/08/2021

NGOME (3)

Je! Ni mpango wa MUNGU kwamba mtu awe na mtoto tumboni mpk miezi 9 mtoto anafariki siku ya kutoka tumboni? Je! Ni mpango wa MUNGU kuwa mzazi anasomesha mtoto wake, anapomaliza masomo yake ndo anafariki? Au anapoanza kazi kwa mara ya kwanza anakufa? Je! Ni mpango wa MUNGU kwamba mtu anahangaika siku zote apate kitu fulani, pengine mradi, anapopata ndo anafariki bila kutendea kazi au bila kufaidi? Je! Ni mpango wa MUNGU kwamba mtu analilia ndoa, anapoipata anafariki siku ya ndoa au ndoa inapokaribia, au siku chache baada ya Ndoa? Je! Ni mpango wa MUNGU kwamba watu wana VIPAJI, KARAMA, UJUZI, lakini wanashindwa kupata mpenyo namna ya kutoka mpaka wanakufa na Vipaji vyao? La Hasha! Huo Siyo mpango wa MUNGU. Hapa kwenye ROHO ZA MAUTI kuna watu wengine wanatembea lakini walishakufa, wanaishi majumbani lakini walishakufa, wanasubili siku ifike ya kuondoka kimwili moja kwa moja. Hawa nao ni wafu wanahitaji Kufufuliwa. Mtu aliyekufa ukiwa na macho ya rohoni unamuona.

5. ROHO ZA AIBU NA FEDHEHA
Huu ni mpango Kabambe ambao Shetani huupanga kwa ajili ya kuwatia watu aibu na Fedheha, kuaibishwa. Mtu anaweza kuaibishwa au kuaibika. Mpaka mtu mwenyewe anaona kuwa kweli ameaibika, kuna kuaibika mtu mmoja, kuna kuaibika kundi la watu k**a vile familia, ukoo, kuna kuaibika Mtaa au Kijiji fulani, kuna kuaibika Wilaya au Mkoa fulani, kuna kuaibika Taifa zima. Kuna Tukio linaweza kutokea Taifa Zima likatiwa aibu tena na mtu mmoja tu. Familia kutiwa aibu, kuna mtoto kuitia aibu Familia, au kuna mzazi kuitia aibu Familia, yote hayo yapo. Mfano baba mwenye nyumba kutembea na mfanyakazi wa ndani wakati una mke wako, au kutembea na binti yako au na jirani yako au na ndugu ya mke wako! Au kufunua utupu wowote wa karibu, tayari ni aibu kwa Familia, wewe utaona ni Sawa hakuna Shida yoyote, lakini wale unaoishi nao na watu wanaokuzunguka wanaona ni aibu na fedheha, halikadhalika mke naye akifanya vitendo viovu, ni aibu na Fedheha kwa mume wake na watoto.

6. ROHO ZA USUMBUFU NA UTAABISHAJI
Roho hizi huwa ni kero, lengo ni kumsumbua mtu, kumtaabisha, unaweza kuona siku yako umesumbuka sana, umehangaika, umetaabika kweli. Kidogo mtu amekaa mara mdudu kaingia jichoni! Mtu kaenda chooni haja kubwa haitoki! Anasubili hata nusu saa ili mradi akomolewe, unapika mara unaungua, kidogo mara umemwaga maji, mara vitu vinakuponyoka mkononi, ukishika hiki kinadondoka! Mara umejikwaa! Unatafuta kitu hukioni wakati kiko peupe! Unapika chakula kwa Ustadi kuja kula kibichi.

15/08/2021

NGOME (2)

3. KULETA MAGONJWA
Huu ni mpango wa shetani japo haimaanishi kuwa magonjwa yote ni ya shetani, hapana! Kuna magonjwa ambayo yapo watu wanaumwa hata mtu wa MUNGU anaweza kuumwa, lkn magonjwa mengi ni ya Kipepo yanatengenezwa kuzimu na kisha watu wanaletewa duniani. Visukari Presha Kansa nk. MUNGU hawezi kuleta magonjwa kiasi hicho na kuwatesa watu kiasi hicho, yaani unaishi duniani k**a adhabu, kila siku madawa na vidonge ndo uishi. Magonjwa haya yote hayakuwepo tangu enzi, Soma kwenye biblia utaona magonjwa yaliyoandikwa ni mengi ila ni yale ya kawaida, kuumwa kichwa, homa, Malaria, tumbo, kuharisha, nk. Lkn magonjwa ya ajabu makubwa ya kutesa watu hayakuwepo. Shetani hukaa na kupanga alete ugonjwa gani, akishapanga anauleta. Akishauleta watu wanaupokea na kuuchukulia ni ugonjwa wa kawaida. Baada ya muda wa miaka kadhaa anapanga ugonjwa mwingine na kuuleta. Hata magonjwa yanayotengenezwa na watu ni kuwa shetani anawaingia watengeneze, anawapa ubunifu wa kutengeneza ugonjwa fulani, na jina la ugonjwa linaandaliwa ili mradi kuwatesa watu wakipate cha moto duniani. Hata watu wake mwenyewe anawatesa, huwa hana urafiki, ndiyo maana anaitwa mwovu, mwovu ni mwovu. Anachotaka watu wateseke, hata wenye Pesa wanateseka na magonjwa makubwa MAZITO, kwa ujumla kwa shetani hakuna raha. Kuna magonjwa ya Msimu na magonjwa ya KUDUMU, kazi za shetani. Magonjwa haya yanaingia mpaka makanisani haitakiwi watu wayapokee Siyo mpango wa MUNGU. Kuna familia au ukoo unatawaliwa na magonjwa fulani au ugonjwa fulani, Siyo mpango wa MUNGU eti magonjwa ya kurithi, VUNJA NGOME ZA MAGONJWA.
Sasa imeandaliwa corona, baada ya miaka michache unaletwa ugonjwa mwingine.

4. ROHO ZA MAUTI
roho za mauti ni adui mkubwa, siyo kila mtu anayekufa ni mpango wa MUNGU, hapana! Kuna watu hawana ulinzi wa MUNGU, na shetani huwaondoa duniani. Watu huchukuliwa kwa njia mbalimbali, kwa njia ya magonjwa, ajali za vyombo vya usafiri, moto, usingizi, nk. Siyo kila anayekufa usingizini ameenda mbinguni eti kwa kuwa amekufa usingizini, hapana. Kuna watu huchomwa VISU usingizini wakafa, usione jeraha wala damu, vinatendeka katika ulimwengu wa roho. Alafu unasema kafa kifo chema akiwa usingizini, kumbe kafa akipambana akitaabika kwa maumivu na majeraha. Wengine huchukuliwa tangu wakiwa tumboni yaani kabla hawajazaliwa hufa, Siyo wajawazito wote mimba zinazotoka ni bahata mbaya. Kuna watu ambao huonekana ni msaada mkubwa, shetani akawaondoa.

15/08/2021

NGOME (1)

Ujumbe wa leo trh 16/8/2021 Siku ya Jumapili, BWANA anasema, "Vunja Ngome zote za mwovu shetani".
Ni muhimu kuvunja ngome zote za mwovu shetani. Na kwa nini MUNGU hajamwita shetani, kamwita mwovu shetani? Mtu mbaya na mwovu ni vitu viwili tofauti, bora mbaya kuliko mwovu. Mwovu ni mtu aliyekithiri katika uharibifu yaani matendo yake hayafai. Nini maana ya Ngome? Lazima ujue Ngome maana yake nini ili uweze kuzivunja vizuri na kuziangamiza zote na kuziteketeza. Ngome. Ngome ni Vituo vya Shetani ambavyo hutumika kwa ajili ya kupanga mashambulizi, ni chimbuko la kuleta uharibifu. Ni makazi ya uharibifu, kwenye ngome kuna zana zote zinazotumika kwa ajili ya kuleta uharibifu. Kuleta uharibifu kwa mtu mmoja aliyekusudiwa, kuleta uharibifu kwa familia nzima, kuleta uharibifu kwa Taifa zima nk. Kuna ngome za mapepo, ngome za maroho kutoka kuzimu, ngome za majini na mashetani, ngome za mizimu, ngome za wachawi na kila aina ya mawakala wa Shetani wanaotumika kuleta uharibifu. Ngome za shetani zimekuwa nyingi na anapanga uharibifu mwingi.

1. KUHARIBU NDOA
Hili ni Shambulizi kutoka kwa shetani, mtoto hata kabla hajazaliwa shetani humpigia mahesabu, humwandalia mpango kabambe na njia yake mwenyewe. Humwandalia na mtu wa kukutana naye kwa mipango yake maalamu kwa ajili ya kutimiza adhma yake, siyo kila Ndoa ni mpango wa MUNGU. Wengine shetani huwaandalia Ndoa ili awape machozi.
Pia Shambulizi katika Ndoa ni kuwa kuna Ndoa nzuri zilizopangwa na MUNGU lkn Shetani pia hujaribu kuleta mashambulizi, ila kwa kuwa wanandoa ni wacha MUNGU na waombaji basi shetani hushindwa. Pia unaweza kuwa umeokoka unamcha MUNGU lkn shetani akawa na mpango wa kukukutanisha na mtu ambaye siyo sahihi, lengo ili aharibu kile kitu kilicho ndani yako. Na shetani anaweza kumfanya huyo mwanaume au mwanamke aonekana kana kwamba ni mtu bora kuliko wote ili uingie mkenge, lkn ukisali sana hukosi kuzijua hila za ibilisi k**a yasemavyo maandiko. Wengine wanasukwa hakuna kuoa hakuna kuolewa kwa vyovyote vile hata iweje! Labda kuzalishwa na kuachwa.

2. KULETA UMASKINI

huu ni mpango wa shetani ambapo kwa kutumia mawakala wake huwapiga watu umaskini. Hata k**a mtu ana Hela unakuta mbeleni zinaisha zote utafikiri Siyo yeye aliyekuwa na pesa, kuna watu huwa hawaambulii kitu, kila wanachokifanya hakiendi, kila anachogusa hakiendi mpaka mwisho wa uhai wake. Pengine watoto wote hupigwa umaskini au familia nzima au ukoo ukawa ni wa kimaskini. Hapa kuna roho za utaabishaji na mahangaiko.

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255625187824

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when NABII Herieth posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share