Shujaa wa Imakulata Tanzania

Shujaa wa Imakulata Tanzania Karibu katika ukurasa wa Shujaa Immakulata Tanzania. Karibu tuungane pamoja katika kulieneza na kulitukiza jina la Mama Bikira Maria.

Karibu tuungane pamoja katika kulieneza na kulitukiza jina la Mama Bikira Maria katika Nyayo za Mtakatifu Maximilian Maria Kolbe

25/03/2022

Heri ya sherehe ya kupashwa habari Mama yetu Bikira Maria

Utuombee Mama wa MUNGU
23/03/2022

Utuombee Mama wa MUNGU

Umekuwa kimbilio letu nyakati zote.
10/03/2022

Umekuwa kimbilio letu nyakati zote.

Tunawatakia siku njema na yenye Baraka
03/03/2022

Tunawatakia siku njema na yenye Baraka

Mama wa Mungu UTUOMBEE.
12/02/2022

Mama wa Mungu UTUOMBEE.

"Duniani tunaona watu wengi wasio na furaha, waliopotoka ambao hawajui hata kusudi la maisha yao, wanaopenda vitu vingi ...
08/02/2022

"Duniani tunaona watu wengi wasio na furaha, waliopotoka ambao hawajui hata kusudi la maisha yao, wanaopenda vitu vingi vya muda mfupi badala ya mema ya Mungu. Wengi wao hawajali upendo wa hali ya juu. Tunataka kuutambulisha na kuuzidisha utukufu wa Imakulata katika nafsi hizi na tunamsihi atufanye nyenzo muhimu katika mikono yake safi na yenye rehema, tusimzuie; atuendeshe hata kwa nguvu k**a tukikataa kumtii."
"Roho ya uovu inadhoofisha kwa namna ya pekee wale waliowekwa wakfu kwa Imakulata, kwa sababu roho muovu anataka kumchukiza angalau kwa njia yao. Hata hivyo, majaribio yake dhidi ya nafsi zilizowekwa wakfu kwa uaminifu daima huishia katika kushindwa kwa aibu zaidi.” aliandika Mtakatifu Maximilian Juu ya Utume wa Shujaa wa Imakulata.

KUSUDI AU LENGO LA UTUME WA SHUJAA WA IMAKULATA.Maximilian alieleza kuwa kusudi la Jeshi la Maria  ni kurudisha roho kwe...
06/02/2022

KUSUDI AU LENGO LA UTUME WA SHUJAA WA IMAKULATA.
Maximilian alieleza kuwa kusudi la Jeshi la Maria ni kurudisha roho kwenye maarifa na umuhimu wa Mimba Safi ya Bikira Maria Mbarikiwa, na jinsi kila roho inavyoweza kuingia kwa urahisi katika fumbo hili la kufariji kupitia Tendo lao la kibinafsi la kuwekwa wakfu kwa Imakulata. Pia aliongeza kuwa malengo ya Shujaa wa Imakulata ni utakaso wa kibinafsi, wongofu wa ulimwengu na hatimaye utawala wa ulimwengu wote wa Moyo Mtakatifu wa Yesu.
Kwa mujibu wa Mtakatifu Mximilian, kujiunga na Utume wa Shujaa wa kunahusisha kufanya tendo la kibinafsi la kuwekwa wakfu kwa Bikira Maria. Wanachama huvaa Medali ya Miujiza k**a ishara ya nje ya kujitolea kwao. Madhumuni ya mashujaa yamo katika maneno haya: kufanya yote uwezayo kwa ajili ya uongofu wa wakosefu, uongofu wa wazushi wa ukweli unaotokana na mafundisho ya Kanisa Katoliki, juu ya Freemasons wote, na kwa ajili ya utakaso wa watu wote chini ya ufadhili wa Bikira Maria. Uwekwaji wakfu kwa Maria katika Shujaa wa Imakulata ni tendo rasmi la kujitoa ambalo haliishii kwa Bikira Maria bali linaongozwa na Kristo. Kauli mbiu ya Shujaa wa Imakulata ni "Kuongoza kila mtu kupitia Bikira Maria hadi kwa Moyo Mtakatifu zaidi wa Yesu.
Wanchama ndani ya utume huu wanashiriki katika kujitolea kwa kazi ya kuwaongoa wote kwa pamoja na kila mmoja mmoja kwa wale wanaohitaji uongofu, na katika kazi ya utakaso wa kila nafsi ambayo kwa sasa inaishi na itaishi katika siku zijazo bila ubaguzi. Shujaa wa makulata inakuza shughuli zake chini ya ulinzi wa Mama Bikira Maria na kupitia upatanishi wa Moyo mtakatifu wa Yesu.
Kwa kujiunga na Shujaa wa Imakulata , washiriki wanakuwa vyombo vya kujitolea vya Mama Yetu, mjakazi wa Bwana na chombo safi cha Mungu. Wanakuwa wanachama wa vuguvugu la kimataifa linaloshiriki katika utume wa kimama wa Maria wa wongofu na utakaso wa roho zote. Mtakatifu Maximilian alitamani kupitia Shujaa wa Imakulata ulimwengu wote uwe chini ya ulinzi wa Mama Bikira Maria, na kupitia kwake ulimwengu wote upatanishwe kwa Moyo Mtakatifu wa Yesu.

Ulimwengu wote ukitambua thamani aliyonayo mama Bikira Maria, basi wote tungekuwa na uhakika wa kukombolewa maana Mama B...
05/02/2022

Ulimwengu wote ukitambua thamani aliyonayo mama Bikira Maria, basi wote tungekuwa na uhakika wa kukombolewa maana Mama Bikira ni njia fupi na ya hakika ya kumfikia mwanaye bwana wetu Yesu Kristo. Mama Maria ni mfano tosha wa ufuasi kwa bwana wetu Yesu Kristo. Alikuwa na Yesu wakati wote, wa furaha na mateso. Licha ya uchungu mkubwa aliouhisi k**a Mama kutokana na mateso ya Mwanaye, hakukata tamaa, alikuwa naye mpaka wakati wa mwisho pale msalabani. MIMI NA WEWE TUNAITWA TUNA JUKUMU LA KUHAKIKISHA JINA LA MAMA MARIA LINAWAFIKIA WATU WOTE ULIMWENGUNI KWA KUTUMIA NJIA MBALIMBALI. NA MOJAWAPO YA NJIA NI HUU UTUME WETU WA SHUJAA IMAKULATA AMBAPO MWANZILISHI WAKE MTAKATIFU MAXIMILIAN KOLBE ALITAMANI KUPITIA MIKONO SAFI YA MAMA, ROHO ZOTE ZIKOMBOLEWE NA KUELEKEZWA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU KRISTO.

NINI KILICHOMFANYA MTAKATIFU MAXIMILIAN KOLBE AANZISHE UTUME WA SHUJAA WA IMAKULATA.Wakati akiwa masmoni , Roma nchini I...
04/02/2022

NINI KILICHOMFANYA MTAKATIFU MAXIMILIAN KOLBE AANZISHE UTUME WA SHUJAA WA IMAKULATA.
Wakati akiwa masmoni , Roma nchini Italia, K**a tulivyoona katika sehemu ya kwanza Mtakatifu Maximiliani alishuhudia maandamano makali dhidi ya Papa Pius wa X (10) na Benedict wa XV (15) huko Roma wakati wa sherehe ya ukumbusho wa Freemasons. Freemasons Waliweka maneno ya kumkashifu Papa chini ya madirisha ya Vatikani. Pia katika maandamano hayo Malaika mkuu, Mikaeli, alionyeshwa akiwa amelala chini ya miguu ya Lusifa. Wakati huo huo, vipeperushi vingi vilisambazwa kwa watu ambamo Baba Mtakatifu (yaani, Papa) alishambuliwa kwa aibu.
Baada ya kushuhudia vitendo hvivyo vya freemasons ambavyo vilikuwa ni shambulio na dhikaka kwa Kanisa, Muda mfupi baadaye, mnamo tarehe 16 Oktoba 1917, akishirikiana na wanafunzi wenzake Maximilian Maria Kolbe alipanga kuanzisha Jeshi la Maria ,maarufu k**a Jeshi la Yule Asiye na Dhambi ili kufanya kazi ya kuwaongoa wenye dhambi na maadui wa Kanisa Katoliki, hasa Freemasons, kupitia maombezi ya Bikira Maria. Kolbe aliuthamini sana utume huo jambo lilomfanya aongeze sala ya utume huu katika medali ya kimiuijiza. Sala hiyo amabyo aliiweka katika medali ya miujiza ilisomeka ‘’Ewe Bikira Maria uliyepewa mimba bila dhambi, utuombee sisi tunaokimbilia kwako na wale wote wasiokukimbilia hasa maadui wa Kanisa Takatifu na wale wote waliopendekezwa kwako”

Address

Segerea
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shujaa wa Imakulata Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Shujaa wa Imakulata Tanzania:

Share