Sheikh Hamza Rajab Abuu Seif

Sheikh Hamza Rajab Abuu Seif karibu katika Mawaidha na Darsa mbalimbali

29/09/2021

Assalaam alaykum warahmatullaah wabarakaatuh

MAADAM UNALALA MUSTAREHE BILA YA KUAMSHWA NA MAUMIVU YOYOTE....NA UNAGEUKA HUKU NA HUKO UNAVYOTAKA.....NA UNAKWENDA UNAP...
10/06/2020

MAADAM UNALALA MUSTAREHE BILA YA KUAMSHWA NA MAUMIVU YOYOTE....

NA UNAGEUKA HUKU NA HUKO UNAVYOTAKA.....

NA UNAKWENDA UNAPOPATAKA .....

NA UNATAMKA UNAVYOTAKA......

NA UNAKULA UNACHOTAKA .....

BASI SEMA KWA HISIA SANA MANENO HAYA: ALHAMDULILLAAH MUDA WOTE.

*KILA SIFA NJEMA ANASTAHIKI ALLAH MTUKUFU DAIMA MILELE

Unajua yanayotakikana kufanywa zaidi siku ya ijumaa??? Ni mengi lakini anza na hili: Amesema Mtume wa Allah Rehma na Ama...
05/06/2020

Unajua yanayotakikana kufanywa zaidi siku ya ijumaa???
Ni mengi lakini anza na hili:

Amesema Mtume wa Allah Rehma na Amani Ziwe Juu yake:

Niswalieni sana siku ya ijumaa, na usiku wa ijumaa.

Atakayeniswalia mara moja, Allah atamswalia mara kumi.

Tusipitwe na fadhila hii ya siku ya ijumaa, bali kila siku na kila wakati mswalie Mtume wako Rehma na Amani Ziwe Juu yake.

اللهم صل وسلم وبارك على سيدنا ونبينا محمد وعلى آله وصحبه أجمعين

ASSALAAM ALAYKUM WARAHMATULLAAH WABARAKAATUH MNAMJUA BAKHILI???? AMESEMA MTUME WA ALLAH REHMA NA AMANI ZIWE JUU: *BAKHIL...
05/06/2020

ASSALAAM ALAYKUM WARAHMATULLAAH WABARAKAATUH

MNAMJUA BAKHILI????
AMESEMA MTUME WA ALLAH REHMA NA AMANI ZIWE JUU:

*BAKHILI NI YULE AMBAYE NIKITAJWA MBELE YAKE HANISWALII*

ALLAAHUMMA SWALLI ALAA MUHAMMAD WA AALIY MUHAMMAD

05/06/2020

🌅 *Nyiradi Za Asubuhi (Hisnul Muumin)* 🌅


سُبْحـانَ اللهِ وَبِحَمْـدِهِ

“Ametakasika Allaah na sifa njema zote ni zake”
(mara mia moja)h


اللّهـمَّ أَنْتَ رَبِّـي لا إلهَ إلاّ أَنْتَ، خَلَقْتَنـي وَأَنا عَبْـدُك، وَأَنا عَلـى عَهْـدِكَ وَوَعْـدِكَ ما اسْتَـطَعْـت، أَعـوذُبِكَ مِنْ شَـرِّ ما صَنَـعْت، أَبـوءُ لَـكَ بِنِعْـمَتِـكَ عَلَـيَّ وَأَبـوءُ بِذَنْـبي فَاغْفـِرْ لي فَإِنَّـهُ لا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إِلاّ أَنْتَ.

“Ee Allaah Wewe ni Rabb wangu, hapana muabudiwa wa haki ila Wewe, umeniumba mimi na mimi ni mja wako, nami niko juu ya ahadi yako, na agano lako, kiasi cha uwezo wangu, najilinda kwako kutokana na shari ya nilicho kifanya, nakiri kwako kwa kunineemesha, na nakiri kwa madhambi yangu, basi nakuomba unisamehe kwani hasamehe madhambi ila Wewe”


أَصْـبَحْنا وَأَصْـبَحَ المـلكُ لله وَالحَمدُ لله، لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحدَهُ لا شَريكَ لهُ، لهُ المُـلكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كلّ شَيءٍ قدير، رَبِّ أسْـأَلُـكَ خَـيرَ ما في هَذا الْيَوْمِ وَخَـيرَ ما بَعْـدَهُ، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّ هَذا الْيَوْمِ وَشَرِّ ما بَعْـدَهُ، رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنَ الْكَسَـلِ وَسـوءِ الْكِـبَر، رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنْ عَـذابٍ في النّـارِ وَعَـذابٍ في القَـبْر

“Tumeingia wakati wa asubuhi na umekuwa Ufalme ni wa Allaah , na sifa njema ni zake Allaah , hapana muabudiwa wa haki, ila Allaah , hali yakuwa peke yake, hana mshirika. Niwake Ufalme, na nizake sifa njema, na yeye juu ya kila kitu ni muweza, Ee Mola, nakuomba kheri ya siku ya leo, na kheri ya baada ya siku hii, na ninajilinda Kwako kutokana na shari ya siku ya leo na shari ya baada ya siku hii. Ee Mola, najilinda Kwako, kutokana na uvivu, na ubaya wa uzee (uzee mbaya) Ee Mola najilinda Kwako kutokana na adhabu ya moto na adhabu ya kaburi”


اللّهُـمَّ بِكَ أَصْـبَحْنا وَبِكَ أَمْسَـينا، وَبِكَ نَحْـيا وَبِكَ نَمـوتُ وَإِلَـيْكَ النِّـشور.

“Ee Allaah kwa sababu yako tumeingia katika asubuhi, na kwa ajili yako tumeingia jioni, na kwa ajili yako ndio tumekuwa hai, na kwa ajili yako tutakufa, na kwako tutafuliwa”


اللَّهمَّ! فَاطِرَ السَّمَوَاتِ وَالْأَرْضِ، عَالِمَ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ، رَبَّ كُلِّ شَيْءٍ وَمَلِيكَهُ، أَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ نَفْسِي، وَشَرِّ الشَّيْطَانِ وَشِرْكِهِ.

“Ee Allaah! Muumba wa mbingu na ardhi, mola wa kila kitu na Mfalme wake, nakiri kwamba hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Wewe, najilinda kwako na shari ya nafsi yangu na shari ya shaytwaan na shirki yake”


بِسـمِ اللهِ الذي لا يَضُـرُّ مَعَ اسمِـهِ شَيءٌ في الأرْضِ وَلا في السّمـاءِ وَهـوَ السّمـيعُ العَلـيم (ثلاثاً)

“Kwa jina la Allaah ambae hakidhuru kwa jina lake kitu chochote kile kilicho ardhini, wala mbinguni, nae ni Msikivu na ni Mjuzi"
(mara tatu)


اللهُمَّ! إِنِّي أَسْأَلُكَ الْعَافِيَةَ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ، اللّهُـمَّ إِنِّـي أسْـأَلُـكَ العَـفْوَ وَالعـافِـيةَ في ديني وَدُنْـيايَ وَأهْـلي وَمالـي، اللّهُـمَّ اسْتُـرْ عـوْراتي وَآمِـنْ رَوْعاتـي، اللّهُـمَّ احْفَظْـني مِن بَـينِ يَدَيَّ وَمِن خَلْفـي وَعَن يَمـيني وَعَن شِمـالي، وَمِن فَوْقـي، وَأَعـوذُ بِعَظَمَـتِكَ أَن أُغْـتالَ مِن تَحْتـي

“Ee Allaah! Ninakuomba afya katika dunia na Aakhirah, Ee Allaah! ninakuomba msamaha na afya duniani na akhera. Ee Allaah hakika mimi nakuomba msamaha na afya katika dini yangu na dunia yangu na jamaa zangu, na mali yangu, Ee Allaah nisitiri uchi wangu, na unitulize khofu yangu, Ee Allaah nihifadhi mbele yangu, na nyuma yangu, na kulia kwangu, na kushoto kwangu, najuu yangu, na najilinda kwa utukufu wako kwa kutekwa chini yangu”


أَصْـبَحْنا علـى فِطْـرَةِ الإسْلام، وَعَلـى كَلِـمَةِ الإخْـلاص، وَعلـى دينِ نَبِـيِّنا مُحَـمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم وعَاـى مِلَّـةِ أبينـا إِبْـراهيـمَ حَنيـفاً مُسْلِـماً وَمـا كـانَ مِنَ المُشـرِكيـن.

“Tumeingia asubuhi na maumbile ya Kiislamu na neno la ikhlaasw na dini ya Rasuli wetu Muhammad صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم na mila (dini) ya baba yetu Ibraahiym iliyo sawa hali yakuwa Musilamu wala hakuwa ni mwenye kumshirikisha Allaah"

أَصْبَحْتُ أُثْنِي عَلَيْكَ حَمْدًا، وَأَشْهَدُ أَنْ لا إِلَهَ إِلا الله (ثَلاثًا)

Nakupa sifa zote za himidi na ninashuhudia hapana muabudiwa waY haki ila Allaah. (mara tatu)


لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شَـريكَ لهُ، لهُ المُـلْكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كُلّ شَيءٍ قَدير

“Hapana muabudiwa wa haki ila ni Allaah peke yake hana mshirika wake, niwake Ufalme na nizake sifa njema zote, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza” (mara mia)


سُبْحَانَ اللهِ عَدَدَ خَلْقِهِ، سبْحَانَ اللهِ رِضَا نَفْسِهِ، سُبْحَانَ اللهِ زِنَةَ عَرْشِهِ، سُبْحَانَ اللهِ مِدَادَ كَلِمَاتِهِ.
(ثَلاثَ مَرَّات في الصباح)

“Ametakasika Allaah kwa sifa njema zote ni zake, Ametakasika Allaah kwa hisabu ya viumbe vyake, Ametakasika Allaah kwa radhi yake, Ametakasika Allaah kwa uzito wa arshi yake, Ametakasika Allaah kwa wino wa maneno yake “
(mara tatu kila asubuhi)

➡ Amesema Rasuli صلى الله عليه وسلم “Mwenye kusema inapoingia asubuhi

سُبْحـانَ اللهِ وَبِحَمْـدِهِ عَدَدَ خَلْـقِه،Y وَرِضـا نَفْسِـه، وَزِنَـةَ عَـرْشِـه، وَمِـدادَ كَلِمـاتِـه

“Ametakasika Allaah na sifa njema zote ni zake, kwa hisabu ya viumbe vyake, na radhi yake, na uzito wa arshi yake, na wino wa maneno yake “
(mara tatu kila asubuhi)

*️⃣*️⃣*️⃣*️⃣*️⃣
*️⃣*️⃣*️⃣*️⃣*️⃣

03/06/2020

ASSALAAM ALAYKUM WARAHMATULLAAH WABARAKAATUH

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sheikh Hamza Rajab Abuu Seif posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share