29/06/2025
MTUMISHI:PRECIOUS IBRAHIMU
SOMO:UKIRI
Ukiri ni nini? Ni kules kusema jambo,ambalo umeambiwa uliseme ukiwa na uhakika nalo.
Mfano; neno moja katika kanisa la wana Efatha tunalitumia lakini lina maana kubwa. Sana na unapolitamka linafanya mambo makubwa sana ni neno Efatha maana yake FUNGUKA linapatikana kwenye kitabu cha Marko 7:30.
Neno hili unapolisema wakati unaombea wagonjwa au waliofungwa na vifungo mbalimbali k**a mapepo na magonjwa alafu ukisema neno Efatha yaani FUNGUKA katika jina la Yesu na ukiamini wanafunguliwa na kuponywa .unachotakiwa kuamini na kukiri wakati huo huo unapokea. Nguvu ya Mungu inayozidi ili kumfungua au kumponya.
Unapotumia neno la ukiri litakupa ushindi inategemea na wewe umeamini nini.
Mathayo 15:21-28. "Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako k**a utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile"
Tunaona imani ya huhu mwanamke mkananayo,akingangana mpaka akapata alicbokiwa anakipigania na hiyo yote au kilichomuwezesha kupata akitakacho ni imani yake kwa Bwana Yesu.