20/06/2022
Online Seminar
With: Minister PANDISHA
"For All The Promises Of God In Jesus Christ Are YES And AMEN." { 2 CORINTHIANS 1:20 }
Somo: Uponyaji Wa Mungu Kwa Kuwekewa Mikono.
NUKUU
"Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; Kwa Jina Langu watatoa pepo, watasema kwa lugha mpya, watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha hakita wadhuru kabisa; WATAWEKA MIKONO YAO JUU YA WAGONJWA, NAO WATAPATA AFYA." { Marko 16:17-18 }
"Wala hakuweza kufanya muujiza wowote huko, isipokuwa ALIWEKA MIKONO YAKE JUU YA WAGONJWA WACHACHE, AKAWAPONYA." { Marko 6:5 }
"Mungu akafanya KWA MIKONO YA PAULO miujiza ya kupita kawaida." { Matendo 19:11 }
Katika mikono ya mwanadamu kuna nguvu na siri nyingi sana katika mambo ya kiroho. Huduma ya kuwekea mikono ina mapana sana. Ila katika somo hili, tutaangazia nguvu ya UPONYAJI WA MAGONJWA NA MADHAIFU kwa kuwekea mikono.
✓Katika maisha yako Muamini ni lazima kujua ni kwa jinsi gani TUNAMUAMINI MUNGU. Kwa JINSI GANI TUNATAKIWA KUMUAMINI YESU KRISTO. Jibu ni kwamba TUNAMUAMINI MUNGU KWA KULIAMINI NENO LAKE. KILE ALICHOKISEMA, KILE ALICHOKIAHIDI KATIKA NENO LAKE.
"Naye Yesu akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hatoishi kwa mkate ( chakula ) tuu, bali ( Ataishi ) KWA KILA NENO LITOKALO KINYWANI MWA MUNGU" { Mathayo 4:4,Luka 4:4 }
Kumbe Imani halisi ni KUMUAMINI MUNGU KUPITIA KULIAMINI NENO LAKE. Kumbe, jinsi ulivyolisoma Neno La Mungu katika Biblia yako, ndivyo hivyohivyo litakavyofanya k**a utaliamini na kulikubali. Neno La Mungu limekuja kwetu ili LITIMIZE MAPENZI YA MUNGU KWETU.
"Maana ahadi zote za Mungu zilizopo ndani ya Yesu Kristo ni NDIYO Tena AMEN" { 2 Korintho 1:20 } [ Amen maana yake ni HAKIKA au Kweli hasa nisemavyo ]
Unatakiwa kuwa na Uhakika na Neno Lake. Mungu hawezi kusema Uongo wala hana sababu ya kusema Uongo.
"Mungu si mwanadamu hata aseme uongo....iwapo amelisema hatalitenda.? Iwapo amenena hatalitimiliza.? { Hesabu 23:19 }
✓Unachopaswa kufanya ni jambo hili
"Amini kuamini kwako na Tilia mashaka Mashaka yako" Ukiona unakuwa na mashaka na Neno la MUNGU kwamba
"Hii haipo hivi"
"Hii si ya nyakati hizi"
Au
"Hili linawezekana kwa watu maalumu au watumishi wa MUNGU peke yao"; Ukiwaza kwa mashaka hayo ujue wewe siyo MUAMINI na hakuna kitakachofanyika hata k**a Neno limesema hivyo. Ukiliamini Neno la MUNGU kwamba hivi lilivyo ndivyo; Utakuwa muamini kwelikweli na utaanza kumpendeza MUNGU.
"Pasipo imani haiwezekani kumpendeza (MUNGU)".{Waebrania 11:6}
✓Sasa Neno la MUNGU linatuagiza KUWAWEKEA WAGONJWA MIKONO YETU ili wawe wazima. Na nilazima ujue kwamba halisemi wachungaji au walimu wawekee wagonjwa mikono, hapana, linasema WAAMINI. Hii inamaana kwamba hata k**a UMEOKOKA dakika iliyopita, ukiweka mikono yako juu ya mgonjwa atakuwa mzima. Na ukumbuke Neno la MUNGU halisemi weka mikono juu ya mgonjwa wa malaria na kichomi tu, hapana , ni kwa mgonjwa wa ugonjwa wowote ule, ulio na jina na hata usio na jina.
Shida ya hili Neno kutokukubalika kirahisi mioyoni mwa waamini ni mbili:-
1. Waamini hatufundishwi juu ya maisha ya imani ya kumuamini MUNGU na NENO lake na hivyo tunaendelea kuishi na wagonjwa majumbani na hospitali tukiona ni sawasawa wao kuumwa.
2. Shetani amepofusha fikra/akili zetu ili tusimuamini MUNGU na NENO lake.
"Ndipo (YESU) akawafunulia akili zao, wapate kuyaelewa na maandiko".{Luka 24:45}.
"mungu wa dunia hii amepofusha fikra(akili) zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake KRISTO aliye sura yake MUNGU" { 2 Korintho 4:4 }.
✓ Huduma ya KUWAWEKEA MIKONO WAGONJWA ili wawe wazima ni AHADI YA YESU KRISTO MWENYEWE k**a tulivyoona katika Neno lake {Marko 16:17-18} na hii imedhihirika kwanza katika huduma yake Yesu Mwenyewe na hata kwa waliotii neno hili. Hapa nakuonesha kwa uchache tu walioweza kuwasaidia wagonjwa kwa kuwawekea mikono na wakawa wazima.
"Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona akaanguka miguuni pake, akimsihi sana, akisema, Binti yangu mdogo yu katika kufa; nakuomba uje, UWEKE MKONO WAKO JUU YAKE, apate kupona na kuishi". { Marko 5:22-23 }
"Wakafika Bethsaida, wakamleta kipofu, WAKAMSIHI AMGUSE. Ndipo AKAWEKA TENA MIKONO YAKE JUU YA MACHO YAKE, naye akatazama sana; akawa mzima, akaona vyote waziwazi". { Marko 8:22,25 }
"Wakamletea kiziwi, naye ni mwenye utasi (kiguvumizi) wakamsihi AMWEKEE MIKONO"{Marko 7:32}
" WATAWEKA MIKONO YAO juu ya wagonjwa nao watapata afya. { Marko 16:18 }
" Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo la udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyooka kabisa. YESU alipomwona alimuita, akamwambia mama, umefunguliwa katika udhaifu wako. AKAWEKA MIKONO YAKE juu yake (yule mama), naye akanyooka mara hiyo, akamtukuza MUNGU" { LUKA 13:11-13 }
"Na jua lilipokuwa likichwa, wote waliokuwa wagonjwa wenye maradhi mbalimbali waliwaleta kwake, AKAWEKA MIKONO YAKE JUU YA KILA MMOJA AKAWAPONYA". { Luka 4:40 }
"Ikawa baba yake Publio alikuwa hawezi homa na kuhara damu. Paulo akaingia kwake, AKAWEKA MIKONO YAKE JUU YAKE na kumpoza". { Matendo 28:8 }
"(YESU) ALIWEKA MIKONO YAKE juu ya wagonjwa wachache, AKAWAPONYA".{ Marko 6:5 }
"YESU akajibu akasema, muwe radhi kwa hili. Akamgusa sikio, akamponya".{ Luka 22:50-51 }
UKIAMINI, HAKUNA LINALOSHINDIKANA KWA MUNGU. MUAMINI MUNGU KWA NENO LAKE NA UWEKE MIKONO YAKO JUU YA WAGONJWA; OMBA KWA IMANI; WATAPATA AFYA. AMINI NAKUAMBIA. MIMI NILIAMINI HIVYO IKAWA HIVYO.
STAY IN CHRIST JESUS IN THE NAME OF JESUS, Amen.