07/12/2022
ASKOFU wa KKKT, Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dkt. Alex Malasusa, amegusia suala la Kanisa hilo kuwa na Katiba moja ambayo itatumiwa na Dayosisi zote pale mchakato wake utakapokamilika.
Askofu Dkt. Malasusa aliyazungumza hayo wakati wa Mkutano Mkuu wa 36 wa Dayosisi hiyo, ulofanyika Usharika wa Mbezi Beach Dar es Salaam wiki iliyopita. Aliwajulisha wajumbe hao kuwa kikosi kazi tayari kimeundwa kwa ajili ya kushughulikia mchakato huo na kueleza kuwa kwa sababu DMP ni sehemu ya KKKT haina budi kujua juu ya jambo hilo.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba, Dkt. Rogate Mshana anasema bado wanaendelea na mchakato kukusanya maoni juu ya Katiba pendekezwa kutoka kwa watu na vyombo vya Kanisa. Kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba, Dkt. Rogathe Mshana ambaye alizungumza na Upendo Media hivi karibuni, alisema mchakato huo utakamilika mwaka 2025.
Dkt. Mshana alisema ni lazima mchakato upite kwenye Dayosisiย na makundi mbalimbali ili kukusanya maoni na itakapofika mwaka 2025, Mkutano Mkuu wa Kanisa ndiyo utakaoidhinisha Katiba moja ya Kanisa.
Mchakato wa KKKT kuwa na Katiba moja ulitajwa kwa mara ya kwanza kwenye Halmashauri Kuu ya Kanisa, iliyofanyika mwezi Mei mwaka huu wa 2022 jijini Arusha, kisha ikaundwa Kamati ambayo itashughulika suala hilo.
Kamati hiyo ya Katiba inaaongozwa na Mwenyekiti, Ask. Dkt. Msafiri Mbilu wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini Mashariki (Lushoto โ Tanga) na tangu ilipoundwa imeyafikia makundi makubwa ndani ya Kanisa ambayo kwa mujibu wa Dkt. Mshana yaliunga mkono wazo la Kanisa kuwa na Katiba moja.