MWL Kabyemela

MWL Kabyemela Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MWL Kabyemela, Religious Center, Chalinze.

26/11/2018

Shalom. Namtukuza Mungu sana kwa ajili yenu rafiki zangu. Leo tuangalie kidogo kuhusu NGUVU YA KIAPO. watu wengi mnaelewa kuhusu neno kiapo, ni neno la kawaida katika ulimwengu wa ceiling. Watu wanaapa wakiwa mahak**ani, kwenye chaguzi mbalimbali nk. Lakini kwenye ulimwengu wa roho kiapo ni hatari kinaambatana na kutoa uhai. Waebrania 6:16-17 imeandikwa mwanadamu huapa kwa aliye mkuu kuliko wao,na ukomo wa mashindano yote ni kiapo. Kumbe mtu anaapa kwa aliye mkuu ni ama Mungu aliye hai, mzimu, Bibi, babu nk. Huwezi kuapa kwa mdogo. Yoshua 6:26 baada ya kutumia nguvu nyingi kuiangusha Yeriko Yoshua aliwaapisha wana wa Israel kuwa mtu yeyote atakayeinuka kuujenga Yeriko akianza Kuchimba msingi tu atafiwa na mtoto wake wa kwanza, akianza kuinua kuta atafiwa na mwanae mdogo wa kiume. Baada ya miaka mingi sana kupita na Yoshua hayupo tena akainuka mfalme Hiel akataka kuujenga Yeriko kuanza tu Mtoto wake wa kwanza akafa, bado akokomaa alivyoinua kuta mwanae mdogo wa kiume akafa sawa na neno (kiapo) alilonena Yoshua mtumishi wa Mungu. 1wafalme 16:34.Ndugu zangu kuna mtu anaweza kuapa na kutoa kafara kwa waganga wa kienyeji wachawi kuwa hautoolewa, hautozaa, hautofanikiwa, utafilisika, utakufa ,utafukuzwa Kazinja, lazima uachike lakini yuko Mungu aliye hai na mimi k**a kuani wa Mungu natamka yeyote aliye apa kichawi juu yako basi uovu ule umpate yeye ktk jina la Yesu.

07/11/2018

Maisha ya mwanadamu yamejaa Vita. Ama unajua au haijui kila siku maisha yetu yamejaa vita. 1wakorinto 10:3-4’’ Maana ingawa tunaenenda katika mwili hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili(Maana siraha za vita vyetu si za kimwili bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome”)
Maandiko haya yanatuonesha kuwa tuna vita ingawa vita yenyewe siyo ya mwilini. Waefeso 6:10-13……………..”12 kwa maana kushindwa kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka , juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wa baya katika ulimwengu waroho 13 kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu na mkiisha kuyatimiza yote kusimama’’
Tunayo vita k**a ulikuwa haujui basi nataka ufahamu kuwa tunayo vita, Vita kwenye uchumi, ndoa,mahusiano, biashara, masomo,huduma na katika kila nyanja ya maisha yetu vita hii haipo mwilini bali ipo rohoni.
Kumbukumbu 2:24’’Ondokeni mshike safari yenu mvuke bonde la Arnoni, tazama ninamtia Sihoni Mwamori mfalme wa Heshboni mkononi mwako na nchi yake, anzeni kuimiliki mshindane naye katika mapigano”.
Hata k**a Mungu amesema kukubariki,baraka hizo utazipata kwa kupigana, hakuna namna ya kuzipata bila kupigana. Watu wengi wameomba,wametoa sadaka, wamefunga wametamkiwa maneno mengi ya baraka lakini wanashangaa hawazipati hizo baraka shida siyo Mungu bali ni kutokujua kuwa lazima kushindana, kupigana ili kuzipata baraka hizo.

05/11/2018

Uumbaji wa Mungu.Maisha ya mwanadamu yamejaa Vita. Ama unajua au haijui kila siku maisha yetu yamejaa vita. 1wakorinto 10:3-4’’ Maana ingawa tunaenenda katika mwili hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili(Maana siraha za vita vyetu si za kimwili bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome”)
Maandiko haya yanatuonesha kuwa tuna vita ingawa vita yenyewe siyo ya mwilini. Waefeso 6:10-13……………..”12 kwa maana kushindwa kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka , juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wa baya katika ulimwengu waroho 13 kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu na mkiisha kuyatimiza yote kusimama’’
Tunayo vita k**a ulikuwa haujui basi nataka ufahamu kuwa tunayo vita, Vita kwenye uchumi, ndoa,mahusiano, biashara, masomo,huduma na katika kila nyanja ya maisha yetu vita hii haipo mwilini bali ipo rohoni.
Kumbukumbu 2:24’’Ondokeni mshike safari yenu mvuke bonde la Arnoni, tazama ninamtia Sihoni Mwamori mfalme wa Heshboni mkononi mwako na nchi yake, anzeni kuimiliki mshindane naye katika mapigano”.
Hata k**a Mungu amesema kukubariki,baraka hizo utazipata kwa kupigana, hakuna namna ya kuzipata bila kupigana. Watu wengi wameomba,wametoa sadaka, wamefunga wametamkiwa maneno mengi ya baraka lakini wanashangaa hawazipati hizo baraka shida siyo Mungu bali ni kutokujua kuwa lazima kushindana, kupigana ili kuzipata baraka hizo.
Ninamshukuru sana Mungu aliyenipa kibari na nguvu ya kumtumikia nikiwa pia askari. Jambo hili linanisaidia sana kujua mambo ya vita ya rohoni
Kimsingi ni ngumu sana kupigana vita na adui usiyemjua .Askari huwa hatuendi kupigana vita au kumk**ata adui bila kumchunguza/kumpeleleza kwanza ili kujua yuko wapi anambinu gani, anatumia siraha gani amejificha wapi ndipo uingie vitani. Hauwezi kupigana vita na adui usiye mjua. Wengi tunamjua Mungu na tunajua adui yeu mkubwa na wakati wote ni shetani ila hatumjui vizuri shetani ndiyo maana tunapigika tuna henya na tunataabika.
Kitabu hiki cha UJUE UUMBAJI WA MUNGU kitakusaidia kujua namna ya kushughulikia mambo yako yote katika ulimwengu wa roho, lakini pia kitakusaidia kumjua vizuri adui yako na namna sahihi ya kupambana naye.
Mungu akuwezeshe kuyajua hayo yote kupitia kitabu hiki katika jina la Yesu AMINA.
KITABU HIKI KIPO TAYARI SOKON.UNAWEZA KUKIPATA TUWASILIANE KWA NO 0783 484341 &0712 264081

05/11/2018

Karibuni rafiki zangu wote katika page yangu mpya ya facebook.Page hii ni maalumu kwa ajili ya kulitangaza neno la Mungu.Mungu awabariki sana kwa kuambatana nami.

Address

Chalinze

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MWL Kabyemela posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share