Kasilo SDA Church

Kasilo SDA Church Kasilo

*Zingatia Kanuni sahihi za Kuoga, Kuepuka vifo vya gafla*Kwa nini nafasi za kiharusi ni nyingi katika bafuVIPIGO huwa vi...
17/11/2023

*Zingatia Kanuni sahihi za Kuoga, Kuepuka vifo vya gafla*

Kwa nini nafasi za kiharusi ni nyingi katika bafu

VIPIGO huwa vingi kwenye bafu kwa sababu tunapoanza kuoga, tunaloweka kichwa na nywele kwanza, ambayo ni njia mbaya.

Kwa njia hii, ikiwa unamwagilia kichwa mara ya kwanza, damu huinuka kwa kichwa haraka na mishipa inaweza kupasuka. Matokeo yake, kiharusi hutokea na kisha watu kujikuta wanaanguka chini.

Ripoti iliyochapishwa katika Journal of the Medical Association of Kanada inasema kwamba hatari ambazo hapo awali zilitabiriwa kusababisha kiharusi au kiharusi kidogo ni za kudumu na hatari zaidi.

Kulingana na tafiti nyingi duniani kote, visa vya vifo au kupooza kutokana na kiharusi wakati wa kuoga vinaongezeka siku baada ya siku. Kulingana na madaktari, mtu anapaswa kuoga wakati wa kufuata sheria fulani. Ikiwa hutaoga kwa kufuata sheria sahihi, unaweza kufa wakati wa kuoga. haipaswi kuloweka kichwa na nywele kwanza wakati wa kuoga kwa sababu mzunguko wa damu katika mwili wa binadamu ni katika joto fulani.

Joto la mwili wa binadamu huchukua muda kuzoea halijoto ya nje. Kulingana na madaktari, kumwaga maji juu ya kichwa kwanza huongeza kasi ya mzunguko wa damu, hatari ya kiharusi inaweza pia kuongezeka wakati huo.

Shinikizo la damu kupita kiasi linaweza kurarua mishipa ya ubongo. Njia sahihi ya kuoga

Pata kuloweka miguu kwanza, kisha loweka mwili juu taratibu. Mwishoni, unapaswa kumwagilia kichwa.

Njia hii lazima ifuatwe na wale walio na shinikizo la damu, cholesterol ya juu na migraine.

*Sambaza iwafikie wengi.*

11/11/2023

*TAFAKARI*

👇

*DINI YA NYUMBANI INAHITAJIKA SANA NA MANENO YETU NYUMBANI YANAPASWA YAWE MANENO SAHIHI, VINGINEVYO SHUHUDA ZETU KANISANI ZITAKUWA BURE. USIPOONESHA UNYENYEKEVU, UKARIMU, UPOLE NA NIA YA KUSOMA NA KUJIFUNZA NENO LA MUNGU UKIWA NYUMBANI. DINI YAKO ITAKUWA NI BURE, IKIWA KUNGEKUWA NA DINI YA KWELI NYUMBAN, BASI KUNGEKUWA NA NGUVU ZAIDI KANISANI*

*UZNZI NA UASHERATI👇🏿:✍🏿 *Mzinzi* huyu ni mme au mke wa mtu anayefanya tendo la ndoa na mke wa mtu au mme wa mtu mwingin...
03/07/2023

*UZNZI NA UASHERATI👇🏿:

✍🏿 *Mzinzi* huyu ni mme au mke wa mtu anayefanya tendo la ndoa na mke wa mtu au mme wa mtu mwingine nje ya ndoa yake.

*Mwasherati* huyu ni kijana wa k**e au kiume anayefanya tendo la ndoa *kabla* ya kuoa au kuolewa.

✍🏿 *Biblia* *inasema* nini kuhusu *UZINZI* na *UASHERATI* ? Soma *upone* *basi*

21 Nami *nimempa* muda ili *atubu* , wala *hataki* *kuutubia* *uzinzi* wake.
Ufunuo wa Yohana 2:21

22 Tazama, nitamtupa juu ya *kitanda* , na hao *wazinio* pamoja *naye* , wapate dhiki kubwa *wasipotubia* *matendo* yake;
Ufunuo wa Yohana 2:22

Lakini *uasherati* *usitajwe* kwenu *kamwe* , wala uchafu wo wote wa *kutamani* , k**a *iwastahilivyo* *watakatifu* ;
Waefeso 5:3

Wala *hawakuutubia* uuaji wao, wala uchawi wao, wala *uasherati* wao, wala *wivi* wao.
Ufunuo wa Yohana 9:21

26 Na yeye *ashindaye* , na *kuyatunza* matendo *yangu* hata mwisho, nitampa *mamlaka* juu ya *mataifa* ,
Ufunuo wa Yohana 2:26

25 *Umejenga* mahali pako *palipoinuka* penye kichwa cha kila njia, *ukaufanya* uzuri wako kuwa *chukizo* , *ukatanua* miguu yako kwa kila mtu *aliyepita* karibu, *ukaongeza* mambo *yako* ya *kikahaba* .
Ezekieli 16:25

28 Pia umefanya mambo ya *kikahaba* pamoja na *Waashuri* , kwa sababu ulikuwa *huwezi* *kushibishwa* ; naam, umefanya mambo ya *kikahaba* *pamoja* nao, wala *hujashiba* *bado* .
Ezekieli 16:28

33 Watu huwapa *makahaba* wote *zawadi* , bali wewe unawapa *wapenzi* wako *wote* zawadi *zako* , na kuwapa *rushwa* ili *waje* kwako *pande* zote, kwa ajili ya *mambo* yako ya *kikahaba* .
Ezekieli 16:33

36 Bwana *MUNGU* *asema* hivi; Kwa sababu *uchafu* wako *umemwagwa* , na uchi wako *umefunuliwa* , kwa njia ya *uzinzi* wako *pamoja* na *wapenzi* *wako* ; na kwa sababu ya *vinyago* vyote vya *machukizo* yako; na kwa *sababu* ya *damu* ya watoto wako, *uliyowapa* ;
Ezekieli 16:36

37 basi, tazama, *nitawakusanya* *wapenzi* wako wote ambao *umejifurahisha* *pamoja* *nao* , nao wote *uliowapenda* , *pamoja* na watu *wote* *uliowachukia* ; naam, *nitawakusanya* juu yako *pande* zote, na *kuwafunulia* uchi *wako* , wapate *kuuona* uchi wako *wote* .
Ezekieli 16:37

✍🏿 *Wapendwa* katika hayo yote *tushike* hili hapa

23 Kwa maana mshahara wa *dhambi* ni *mauti* ; bali *karama* ya *Mungu* ni *uzima* wa *milele* katika *Kristo* Yesu *Bwana* *wetu* .
Warumi 6:23

*Tafakuri* ya *siku* ☝🏿

24/06/2023

*SIO DAWA ZOTE ZIPO KWENYE MADUKA YA MADAWA!*🧏🏼🧏🏼‍♀️

*1 - Mazoezi ni dawa.*
*2 - Kufunga ni dawa.*
*3 - Chakula cha asili ni dawa.*
*4 - Kicheko ni dawa.*
*5 - Mboga na matunda ni dawa.*
*6 - Kupumzika na Usingizi wa kutosha ni dawa.*
*7 - Mwanga wa jua ni dawa.*
*8 - Kuwapenda wengine ni dawa*
*9 - Kujipenda ni dawa.*
*10 - Kuwa na moyo wa Shukrani ni dawa.*
*11 - Kuacha dhambi/kosa ni dawa.*
*12 - Kutafakari ni dawa.*
*13 - Kusoma na kujifunza Neno la Mungu ni dawa.*
*14 - Kula vizuri, kwa wakati na bila ziada ni dawa.*
*15 - Fikra sahihi ni dawa.*
*16 - Kumtegemea Mungu ni dawa*
*17 - Marafiki wazuri ni dawa.*
*18 - Kujisamehe na kusamehe wengine ni dawa.*
*19 - Kunywa maji mengi ni dawa.*
*20 - Moyo wenye amani ni dawa.*
*21- Kuvuta hewa safi ni dawa.*
*22 - Kuwa na kiasi katika kila jambo ni dawa*

*Ukinywa dawa hizi za kutosha , ni mara chache sana utahitaji zile za maduka ya dawa.*

*Fanya vizuri kwa kuwagawia wapendwa wako dawa hii ikiwa unawajali sana.*

26/08/2022

CHANGAMOTO HUTUPATIA KUKOMAA NA KUKUA AKILI
Changamoto ndo hutupa kukomaa na kukua kwa akili. Unapoweza kutatua changamoto na uwezo wako wa kukua kiakili unaongezeka.Unapopitia changamoto, usikate tamaa, pambana uvuke uende ngazi nyingine. Shuleni hakuna kuingia darasa jingine bila kufanya mtihani. Unavyopanda darasa ndivyo na mtihani unazidi ugumu kutokana na ngazi uliyopo. Na kwenye Maisha ndivyo hivyo hivyo!

Ukiona changamoto yako kubwa, fahamu upo ngazi ya juu .Pambana vuka. Unapoweza kutatua changamoto , inakupa ujasiri wa kushinda. Daudi alipoweza kupambana na Simba na Dubu MUNGU akamshindia,alimpa ujasri wa kupigana na goliati akijua MUNGU atamshindia. Acha kulia hovyo na kuona umeachwa, Mara kwanini wewe, Mara kukosa raha. Kuwa jasiriiiii! AMEN!

HAKUNA MAISHA YOYOTE YASIYO NA CHANGAMOTO. KUKOMAA NI KUTATUA CHANGAMOTO NA SIYO KUKIMBIA.

24/08/2022

HASIRA HUKAA KIFUANI MWA MPUMBAVU.
Leo naomba nigusie swala zima la Hasira.
Watu wengi wamejikuta kwenye matatizo makubwa kwa sababu ya hasira. Katikavitu unatakiwa kumwomba Mungu akuondolee katka Maisha yako ni kukuondolea roho chafu ya hasira.
Ndoa nyingi zimevunjika kwa sababu ya hasira. Watu wamejikuta wameua kwa sababu ya hasira, wameachishwa kazi sababu ya hasira,. Watu wamekosana na marafiki wazuri sana kisa hasira. Control hasira yako. Huwezi peke yako. Hasira ni roho ya kipepo kabisa inayotumwa kuleta uharibifu.
Usikubali hasira ikutawale. Kuna watu wamevunja ndoa zao nzuri sanaaaaa kwa sababu ya hasira na kukosa utulivu. Watu wameua Watoto wao wa kuwazaa kisa hasira tena kwa jambo dogo tu. Watu wamefungwa kifungo cha Maisha na ndoto zao zote kuisha sababu ya hasira.
Nikusaidie jambo leo, usifanye maamzi ukiwa na hasira. Maamzi ya hasira mara nyingi huongeza tatizo kuwa kubwa badala ya tatizo kuisha au kupungua makali. Ni kweli kosa limetokea,ni kweli umeudhiwa, ni kweli umefanyiwa vitendo vya unyama, ni kweli umedhulumiwa , ni kweli umesemwa uongo. Hebu pata utulivu kwanza. Tulia, pata hekima na maamuzi ambayo haitakugharimu wewe na kufanya tatizo kuwa kubwa sana.
Maamuzi wakati wa hasira yanaweza kukuletea aibu au fedheha. Maamzi wakati wa hasira yanaweza kukuondolea utu wako. . Maamzi wakati wa hasira yanaweza kuutoa uhai wako . Maamzi wakati wa hasira yanaweza kukunyima haki yakopia. Wengi wakati wa hasira hufanya maamzi bila hekima za kiMungu. Hutegemea akili zao , pesa zao, vyeo vyao, hisia zao, uzuri wao, taaluma zao nk. Hivi sio vitu vya kiMungu. Havitakupa jawabu la haki na hekima.
Omba utulivu sana unapopatwa na hasira. Omba Roho Mtakatifu akutulize na akusaidie ufanye maamzi ya Hekima za ki Mungu. Omba sana utulivu katika Maisha.
Tupitie maandiko yafuatayo kutoka katika Biblia takatifu ya neno la Mungu.
Kwanini hasira humwua mtu mpumbavu, nao wivu humwua mjinga AYUBU 5:2
Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga, na mtu mwenye hila mbaya huzirwa MITHALI 14:17
Mtu wa hasira huchochea ugomvi, bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano. MITHALI 15:18

22/08/2022

*TAFAKARI ZAIDI: WAKRISTO WA AWALI — WATII WA KWELI*

🌷 ```Wenye haki hutiwa katika tanuru la mateso ili wasafishwe, ili mfano wao uwafanye wengine waamini juu ya uhalisi wa imani na utauwa na kwamba, mwenendo wao usioyumba, uwahukumu wasio watauwa na wasio amini.```

🌷 *Mungu anawaruhusu waovu wasitawi na kuonesha uadui wao dhidi yake ili wote wapate kuona haki na rehema yake watakapoangamizwa. *

🌷 _Adhabu itatolewa kwa ajili ya kila tendo la ukatili linalofanywa dhidi ya waaminifu wa Mungu kana kwamba alifanyiwa Kristo mwenyewe._

```🌷 Tumaini Kuu
🌷 Ukurasa wa 34
🌷 Aya ya 2```

21/08/2022

JINSI YA KUEPUKA KUCHELEWA KANISANI_✍️

1. Piga pasi nguo zako zote kabla ya kulala.

2. Safisha na andaa viatu kabla ya kulala.

3. Tayarisha Biblia yako, Notebook, Kalamu, n.k mahali pamoja.

4. Tayarisha zaka na sadaka yako.(Kisha sema na Mungu unataka akufanyie nini kupitiahiyo sadaka)

5. Lala mapema.

6. Amka kwa wakati ikiwezekana tegesha alarm

7. Epuka kusema "Hata nikifika mapema, sitakutana na mtu yeyote"
Fika mapema na acha mtu aje akukute pia. Usisahau kwamba wewe pia ni mtu.

8.Iwapo itakuchukua dakika 15 kuendesha gari/kutembea hadikanisani, sikuzote toa muda wa ziada kwa kuwa lolote linaweza kutokea. Kwa mfano, ikiwa ibada itaanza
saa 1:00 asubuhi na inakuchukua dakika
10 kuendesha gari/kutembea hadi kanisani, ni bora kila mara kuondoka nyumbani saa 12:40 asubuhi.

9.Panga kufika kanisani angalau dakika30 kabla ya ibada kuanza.

10.Usitoe nafasi kwa marafiki na jamaa kukutembelea saa chache kabla ya Ibada. Ikiwa wanakuja wakati unajiandaa kwenda Kanisani, nenda Kanisani pamoja nao au wafanye wakungojee hadi urudi. Wao si muhimu zaidi kuliko Mungu.

🟩Kwenda kanisani mapemakunaleta baraka za Bwana juu ya maisha yako.

🟩Usiwe na mazoea ya kuchelewa kufika kanisani, ni aibu kwa Mungu wako.

🟩 Kuchelewa kanisani ni kukosa nidhamu kwa aliyekuumba(Mungu)

BADO NI MWAMINIFU WAKATI MUNGU HAONEKANIKufikiri kwamba hakuna mtu anayejali kuhusu kile kinachotutokea hakupendezi kabi...
19/08/2022

BADO NI MWAMINIFU WAKATI MUNGU HAONEKANI

Kufikiri kwamba hakuna mtu anayejali kuhusu kile kinachotutokea hakupendezi kabisa. Lakini kufikiri kwamba Mungu hajui au hatujali kunaweza kuhuzunisha zaidi.

🔹 Kwa Wayahudi waliokuwa uhamishoni Babeli, Mungu hakuonekana kujali sana hali yao. Bado walikuwa uhamishoni, bado walikuwa wanahisi kuachwa na Mungu kwa sababu ya dhambi yao. Lakini Isaya ananena maneno ya faraja kwao. Isaya 40 ni kifungu kizuri ambacho Isaya anazungumza kwa upole sana na watu kuhusu Mungu wao; “Atalilisha kundi lake k**a mchungaji, Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; Na kuwachukua kifuani mwake, Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole” *(Isa. 40:11).* Lakini baada ya muda mrefu sana, hawa walio uhamishoni walikuwa wakifikiri, Uko wapi, Ee Bwana? Hatuwezi kuona ushahidi wowote kwamba ungalipo—au kujali!

*Soma Isaya 40:27-31. Ni kwa njia zipi Isaya anamwelezea Mungu? Maelezo haya kuhusu Mungu yalikusudiwaje kujibu imani yao kwamba “ ‘njia yangu imefichwa, Bwana asiione; na hukumu yangu imempita Mungu wangu asiiangalie’ ” (Isa. 40:27)?*

🔹 Kundi lingine la watu ambao wanaweza kuwa wamefikiria kwamba njia yao ilikuwa imefichwa Mungu asiione linapatikana katika kitabu cha Esta. Katika kitabu hiki, Mungu hatajwi hata mara moja. Hata hivyo, kisa chote ni mfululizo wa matukio yanayojitokeza ya kuingilia kati kwa Mungu ili kuwaokoa watu wake kutokana na sheria isiyoweza kubatilishwa iliyotaka waangamizwe.

🔹 Kisa hiki hakielezei tu matukio ya zamani—kinawakilisha wakati katika siku zijazo watu wa Mungu watakapoteswa tena na sheria itatolewa tena kwa ajili ya kuangamizwa kwao *(Ufu. 13:15).* *Je, unaweza kuwazia jinsi ambavyo ingekuwa rahisi kuhitimisha kwamba ikiwa hali za kutisha namna hiyo zilikuwepo. kwa hakika Mungu ni lazima aliwaacha watu wake?* Lakini hatupaswi kuogopa. Mungu yule yule aliyewaokoa wateule wake katika kisa cha Esta atawaokoa tena katika pambano la mwisho.

🔹 *Tumesoma jinsi Isaya alivyomwelezea Mungu kwa watu waliokuwa uhamishoni. Ungeweza kumwelezeaje Mungu kwa watu waliohisi kwamba Mungu alikuwa ametoweka na alikuwa amewaacha? Unawezaje kuwafundisha kuona kwa macho ya imani kutotegemea kile wanachokiona kuwazunguka kwa macho yao ya kibinadamu?*

*NAKUTAKIA TAFAKARI NJEMA*

☘️☘️☘️☘️☘️☘️☘️☘️☘️☘️

*Misingi ya kuishi Pamoja!*1. Ukifika Sehemu... *Salimia*2. Ukiondoka Sehemu..... *Aga*3. Ukisaidiwa....... *Shukuru*4. ...
18/08/2022

*Misingi ya kuishi Pamoja!*
1. Ukifika Sehemu... *Salimia*
2. Ukiondoka Sehemu..... *Aga*
3. Ukisaidiwa....... *Shukuru*
4. Ukiahidi...... *Tekeleza*
5. Ukikosea.... *Omba Msamaha*
6. K**a Hujaelewa..... *Uliza*
7. Unacho... *Gawa Kwa Wengine*
8. Huna.... *Usione Donge*
9. Ukivunja.... *Lipa*
10. K**a Hupendi...... *Heshimu*
11. Ukipendwa... *Onesha Upendo*
12. Huwezi Kusaidia... *Usisumbue*
13. Ukiharibu... *Rekebisha*
14. Ukikopa.... *Lipa*
15. Wakikuuliza .... *Jibu*
16. Ukiwasha....... *Zima*
17. Ukifungua...... *Funga*
18. Ukinunua.... *Lipa*
19. Ukichafua.. *Safisha*
20. Ukipungiwa..... *Punga*
21. Ukipewa.... *Shukuru*
22. Ukiazima... *Rudisha*

*''Ukizifuata kanuni Hizi, Utaona Jinsi Utakavyoishi Na Watu Vizuri Hata K**a Huna Hela, Hii Ni kwa Binadamu Wote Hata K**a Ni Kiongozi'''*

28/07/2022

TABIA NA JAMII

Umewahi kuskia mtu amekosea, halafu akaambiwa "hapa umekosea, tena umemkosea MUNGU", lakini majibu yake yakawa ni haya, "vyema, mahusiano yangu na MUNGU, ni suala binafsi! Sitaki ulizungumzie". Umewahi kuona mtu anafanya kitu katika namna isiyo sahihi lakini akakataa kurekebishwa?! Nina imani umewahi.

Nataka kusema nini?! Nataka kusema hivi, kwamba; Ni kweli yawezekana unaweza kufanya mambo peke yako! Ni kweli mahusiano yako na MUNGU, ni suala binafsi! Lakini, nataka nikwambie hivi, pamoja na hayo yote, "Jamii (yoyote ile), ina mchango mkubwa katika kufanya kwako mambo! Jamii, ina nafasi katika kuyajenga mahusiano yako na MUNGU! Jamii, ina nafasi katika kurejesha sura (tabia) ya MUNGU ndani yako". Yaani, kwa Lugha nyingine ni kwamba, "ukamilifu unafikiwa kwa kukusanyika, sio kwa kujitenga na watu''.

KWA NINI NI HIVYO?!

- Paulo anatuweka wazi kabisa katika somo la leo kwamba, MUNGU ameweka katika jamii zawadi mbalimbali, karama mbalimbali, na maarifa mbalimbali ya kutufanya tufikie ukamilifu. Yaani, ili tufikie ukamilifu katika mambo yote, ili tufikie ukamilifu wa kikristo, ili kazi ya huduma ikamilike, ili mwili wa Kristo ujengwe, ili sura nzuri ya MUNGU irejee ndani yetu, MUNGU ametoa vipawa mbalimbali katika jamii (Waefeso 4:11), vipawa ambavyo tukiviunganisha, tukasikilizana na kwenda kwa pamoja , tunafikia ukamilifu! Si wa kikristo pekee (Waefeso 4:12), bali ukamilifu katika mambo yote pia.

Je, haiwezekani kwa mtu kuufikia ukamilifu wa Kikristo peke yake pasipo jamii?!

- Kwa hakika inawezekana kuwa Mkristo peke yako kabisa! Inawezekana kuufikia ukamilifu peke yako kabisa. Wanaume na wanawake hawafungwi chini ya shinikizo linalowazunguka! Kwamba, "ni lazima kutegemeana" ili kushinda, hapana. Wanaume na wanawake wanaweza kusimama peke yao k**a wakristo! Wanaume na wanawake wanaweza kusimama peke yao na kuufikia ukamilifu pasipo msaada wa jamii!!! Tumelishuhudia hili mara nyingi, karne nyingi wakristo wengi wamekuwa wakisimama peke yao na kushinda pasipo jamii.

Anachojaribu kutwambia Paulo katika somo la leo ni kwamba, "Ukamilifu unaweza kufikiwa zaidi kwa haraka na kwa uzuri, pasipo mateso wala maumivu, k**a tutafanya kazi kwa pamoja katika ushirika na kila mmoja" (Waefeso 4:12). "Kazi ya injili inaweza kufika kwa watu wengi zaidi ikiwa tutakaa katika jamii (Waefeso 4:12), Lakini pia, falme na mamlaka za uovu zitaangushwa, ikiwa tutashirikiana k**a jamii ya Kikristo na kila mmoja akifanya sehemu yake! Tazama waefeso 3:10.

Ni kweli injili itaenea hata kwa kusimama peke yako, lakini kwa vikwazo vingi, na si kwa wengi k**a ambavyo tungesimama k**a jamii. Ni kweli kusimama peke yako, kutatikisa na kuangusha falme na mamlaka za uovu, lakini si k**a ambavyo ingekuwa k**a tungesimama pamoja. Ni kweli ukisimama peke yako utafika katika safari yako ya ukamilifu, lakini kwa mateso mengi, k**a ambavyo tumeshuhudia wenzetu waliokuwepo kabla, kina Danieli, Ayubu, Yusufu, Ibrahimu, Mitume, walivyoteseka mpaka kuufikia ukamilifu. Lakini sasa, tutafanyaje ikiwa jamii yenyewe inaenda mbali zaidi na BWANA?! Tutafanyaje ikiwa jamii yenyewe inamkataa BWANA?! Hapa ndipo linapokuja swala la kusimama peke yako na kuvumilia mateso mpaka kuufikia ukamilifu.

Nipende tu kusema hivi, shetani anajua nguvu iliyopo katika ushirika, anatambua kwamba, k**a tutashirikiana kwa pamoja na kila mmoja akafanya sehemu yake, mara moja, injili itaenea, ufalme wake utaangushwa na tutaweza kuufikia ukamilifu wa Kikristo mara moja- Hii ndio sababu anafanya kila liwezekanalo kuvuruga ushirika! Kuvuruga jamii.

K**a jumuiya ya Kanisa, k**a jamii ya Kikristo, nashauri, tungekaa na kuliangalia swala hili na kutafuta ni kwa namna gani tunaweza kudumu katika ushirika. Kwa nini?! Kwa sababu muda umeenda sana, injili inatakiwa iende na tunatakiwa kuufikia ukamilifu ambao hatutaweza kumwona BWANA pasipokuwa nao (Waebrania 12:14). Ikiwa tunahitaji kuokolewa sisi sote pamoja na familia zetu, tafadhali tushughulikie ili somo la leo.

Nimalizie kwa kusema hivi, "Utakaso na Ukomavu" havifikiwi na watu kwa kujitenga. "Utakaso na Ukomavu", vinafikiwa na watu katika jamii". Yaani ni kwamba; Tunapokaa katika ushirika na kuzitumia karama tulizopewa vizuri ( wengine wakihubiri, wengine wakifundisha, wengine wakiimba, wengine wakionya) tunatakasana sisi kwa sisi! Lakini pia, tunapopitia changamoto kwa pamoja k**a jamii na kuzitatua pamoja kwa namna mbalimbali kutoka kwa wenzetu- hii hutusaidia kukomaa kiroho. Mwisho, neno Jamii lina maana ya "Mkusanyiko wa watu wanaoishi kwa pamoja katika eneo moja la kijiografia wakiunganishwa na vitu fulani vinavyofanana".

TAFAKARI NJEMA SANA...

Address

Kasilo
Biharamulo

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255687631960

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kasilo SDA Church posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Kasilo SDA Church:

Share