Mwl. Daniel Piniel

Mwl. Daniel Piniel Mimi ni Nuru ya ulimwengu ikiwa Nuru ya Kristo imo ndani yangu. Hekima hunena!!

NI NANI WA KUTUHUKUMU IKIWA YESU KRISTO TUNAYE MWAMINI NDIYE MWENYE KUTUHESABIA HAKI??? BASI HAKUNA HUKUMU JUU YETU SISI...
15/05/2026

NI NANI WA KUTUHUKUMU IKIWA YESU KRISTO TUNAYE MWAMINI NDIYE MWENYE KUTUHESABIA HAKI???

BASI HAKUNA HUKUMU JUU YETU SISI TULIO KATIKA KRISTO!!

💪Daniel Ole Piniel 😀.

15/05/2026

Celebrating my 7th year on Facebook. Thank you for your continuing support. I could never have made it without you. 🙏🤗🎉

NI NANI MWENYE AKILI KATI YA WANADAMU?Ni yule afanyae bidii katika kumtafuta Mungu hasa katika nyakati hizi. “Toka mbing...
04/03/2026

NI NANI MWENYE AKILI KATI YA WANADAMU?

Ni yule afanyae bidii katika kumtafuta Mungu hasa katika nyakati hizi.

“Toka mbinguni BWANA aliwachungulia wanadamu, Aone k**a yuko mtu mwenye akili, Amtafutaye Mungu.” Zab. 14:2.

Basi tumtafute BWANA, kwa kuwa ni jambo jema lenye tumaini la waokovu wetu.

“Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu;..” Isaya 55:6.

Kumtafuta BWANA ni agizo lenye kuhitaji utii, kwani lina thawabu kwao wamtafutao BWANA.

“Mtafuteni BWANA, enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya BWANA.” Sefania 2:3.

“SIKU YA HASIRA YA BWANA INAKUJA”

Tumtafute BWANA ili tupate kuokolewa. Mwenye kufahamu Neno la Mungu na afahamu.

24/01/2024
31/12/2023

HAPPY NEW YEAR 2024

SADAKA ILIYO KUU NI KUWAJALI WAHITAJIHata fungu la Kumi kwa Kanisa haizidi sadaka ya kutoa kwa wenye uhitaji walio ndugu...
11/12/2023

SADAKA ILIYO KUU NI KUWAJALI WAHITAJI

Hata fungu la Kumi kwa Kanisa haizidi sadaka ya kutoa kwa wenye uhitaji walio ndugu.

Nasema si kwa sheria bali kwa Imani ya Kristo Yesu aliye Kuhani Mkuu mwenye kustahili Sadaka za Kikuhani ikwepo Fungu la Kumi.

“Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.” Yakobo 1:27

Ndugu zangu, imetupasa kuufikia kimo cha ukamilifu ambao ni UPENDANO WA KINDUGU katika Kristo Yesu. Ndiyo maana nasema nawe kuhusu utoaji wako katika kumtolea Mungu sadaka.

Sadaka tuzitoazo katika Madhehebu yetu, Je hutusaidia kufikia kimo cha Ukamilifu ambao ni UPENDANO WA KINDUGU?

Mfano, Katika sadaka za fungu la Kumi ambayo ni sheria kutoa kwa kuhani asiye na asili ya kufa au kutoa kwa yeye aliyekusudiwa k**a maandiko yasemavyo. Na kuhani asiye na asili ya Kufa ni MELKIZEDEKI Mfalme wa Salemu ambaye kwa Ufunuo ni YESU KRISTO aliye Hai hata Milele naye ni Kuhani wetu Mbinguni.

“Tena hayo tusemayo ni dhahiri sana zaidi, ikiwa ametokea kuhani mwingine (Yesu Kristo) mithili ya Melkizedeki; 16 asiyekuwa kuhani kwa sheria ya amri iliyo ya jinsi ya mwili, bali kwa nguvu za uzima usio na ukomo;17 maana ameshuhudiwa kwamba, Wewe u kuhani milele Kwa mfano wa Melkizedeki. Ebr 7:15”

Kwa asili Ibrahimu alistahili kupokea sehemu ya Kumi kutoka kwa Israel kwa maana hapakua na aliye mkuu kuliko yeye, na kwa Sheria kabila la Lawi naye alipokea.

Lakini Je, kwa Sheria ya Roho, yuko wapi Kuhani mwenye kustahili sadaka za FUNGU LA KUMI? Au kwa sheria ya Roho, Kristo Yesu aliye kuhani husema nini kuhusu Kumtolea? Kwa maana imekwisha kunenwa kuwa “Basi, ile amri ya zamani inawekwa kando kwa sababu ni dhaifu na haifai.Kwa maana Sheria haikufanya kitu chochote kiwe kikamilifu, lakini kuletwa kwa tumaini bora kulifanya hivyo, na kupitia tumaini hilo tunamkaribia Mungu”

Kinachofanya Sheria ya zamani kuwa dhaifu ni kuwepo kwa sheria mpya ya Roho kwa Kristo Yesu aliye Kuhani Mkuu sana.

“Yule mwandishi akamwambia, Hakika, Mwalimu (Yesu), umesema vema ya kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye; 33 na kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani k**a nafsi yako, KWAFAA KULIKO SADAKA nzima za kuteketezwa na DHABIHU ZOTE pia.”
Marko 12:32

UTIMILIFU wa Sheria yote upo katika UPENDO. Ndiyo maana imetupasa kupenda Rehema kuliko Sadaka.

Kutoa sadaka za fungu la Kumi na Zaka Madhabahuni kwa mapokea ya Kanisa imepaswa kuwa kwa Sheria ya Roho ambayo ni kwaajili ya UPENDO na wala si kwa Sheria ya zamani iliyo dhaifu. Kwa maana kumtolea Mungu kwa njia ya Upendo kunafanya kumkaribia Mungu zaidi kuliko kutoa kwa Sheria. Hata sasa hakuna Wakristo wengi wanaotoa kwa Sheria bali kwa UPENDO.

Wala tusidhani kuwa UTII wetu upo katika kutoa Sadaka za Mapokeo katika Madhehebu yetu, bali UTII wetu upo katika Amri iliyo Kuu iliyotoka kwa Bwana mwenyewe Akisema “Amri mpya nawapa, Mpendane. K**a vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.” “Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.” Hapa ndipo kipimo cha UTII wala si katika sadaka za Mapokeo.

BASI SASA, Tumtolee Kuhani wetu YESU KRISTO k**a anavyotaka yeye wala si kwa Mapokeo na Sheria iliyo dhaifu. Na kumtolea yeye ni njia ya Amri yake kwamba Mpende jirani yako ambaye ni mwenye uhitaji hasa kwa aliye ndugu yako katika kanisa au Familia.

Achana na kusema, Nimekwisha kutoa fungu la Kumi au zaka hivyo nasubiri baraka za Mungu’. Hatuna sheria hiyo kwa sasa ila Sheria ya kuwajali masikini na wenye njaa na walio dhaifu. Acha kuweka nguvu katika sadaka za bahasha zisizolenga kuwainua walio dhaifu katika Kanisa na Familia.

Fungu la Kumi na Sadaka za Zaka Madhabahuni tutatoa ikiwa ni kwaajili ya kuwajali watumishi k**a sehemu ya kuwapenda kwa huduma zao ili nao wapate vya mwilini. Lakini hatutoi ili kutimiza sheria ya zamani au kutimiza mapokeo.

Katika Agano Jipya Tumeitwa kwa Amri Moja tu ya UPENDANO WA KINDUGU wala hatukiutwa kwa Amri ya Sadaka za Mapokeo katika Madhehebu yetu.

“Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.” Yakobo 1:27

HAKUNA THAWABU KUTOA FEDHA MADHABAHUNI IKIWA NDUGU ZAKO NI WAHITAJINaomba Mnisamehe ikiwa kauli yangu ni kwazo!Watu huse...
05/12/2023

HAKUNA THAWABU KUTOA FEDHA MADHABAHUNI IKIWA NDUGU ZAKO NI WAHITAJI

Naomba Mnisamehe ikiwa kauli yangu ni kwazo!

Watu husema “Fedha hizi zafaa kumtolea Bwana kanisani (madhabahuni) ili nitimize sheria ya Bwana”

Watu hudhani tu kumtolea Mungu Sadaka ni kwa njia ya kwenda Kanisani na kutoa fedha za uwiano, michango ya maendeleo au Shukrani kwa Bwana. Hayo ni Mapokeo ya Kanisa kwa maana ya desturi inayorithiwa katika madhehebu. Sisemi ni mbaya kuwa na mapokeo lakini Nahitaji kukumbusha Neno la Bwana lisiachwe kwa sababu ya Mapokeo hayo.

Mapokeo huja kwa sababu ya kulishika Neno fulani lenye manufaa binafsi ya dhehebu au Kanisa na kiliacha Neno lenye manufaa kwa waliokusudiwa na Bwana.

“Lakini k**a mngalijua maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka..”Mathayo 12:7

Rehema maana yake ni kuwa na moyo wa kusaidia wenye udhaifu na wahitaji kwa kutoa nguvu au uwezo wako kwa ajili yao. Hilo ndilo Neno la Bwana katika kumtolea Bwana.

Hebu fikiri, kutoa fedha kwaajili ya Maendeleo ya Mtaa wa Kanisa au Dhehebu kwa kutumia Neno la kusema “Mheshimu Bwana kwa Mali zako” au “Leteni zako kamili ghalani mwa Bwana”, Na katika kutoa huko hakuna rehema kwa waliokusudiwa.

Nini maana ya Maneno haya? “Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao...”

Hebu fikiri, Umetoa fedha nyingi na ahadi nyingi kwa ajili ya Shukrani kwa Bwana Kanisani au kwa ajili ya maendeleo ya Mtaa, huku unayo ndugu wengi wenyi uhitaji wa chakula na mavazi au wengine kuhitaji fedha kidogo kwa ajili ya matibabu. Au natamani kujua Je, ni dhehebu lako ndilo lenye uhitaji zaidi ya ndugu zako?

Je, mwadhani kumtolea Bwana ni kwa Sadaka za sheria za Mapokeo au kwa kuwa na Rehema? Na Lipi ndilo Neno la Bwana kati ya kutoa Sadaka na kutoa Rehema?

“Heri wenye Rehema maana hao watapata rehema”

Kumbuka habari za Kornelio “Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia, 2 mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima.” Matendo 10:1-2.

Kumbuka habari za Tajiri “Yesu akamwambia, Ukitaka kuwa mkamilifu, enenda ukauze ulivyo navyo, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate.”

Habari hizi ni za utoaji kwa Bwana lakini ikiwa kwa Rehema; kwa ajili ya hao waliokusudiwa katika Neno la Bwana na wala si katika Mapokeo. Kwa maana Kumpenda jirani yako ndio bora kuliko kutoa sadaka nyingi madhabahuni. K**a vile Kornelio alitoa sadaka nyingi kwa watu na kumcha Mungu na kumcha Mungu ndiyo bora kuliko Mapokeo.

“Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.” Mithali 19:17 “Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini, Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.” Mithali 21:13.

Mniwie radhi kwa kwazo lolote.. ila Naomba kila mmoja wetu kujali rehema kuliko sadaka. Ndugu zako ni wahitaji na wanahitaji rehema kwa kile wanachokihitaji. Maskini tunao sasa kwa mapenzi ya Mungu na Madhehebu tunayo kwa Mapokeo yetu. Tulijali lile la Bwana kuliko lile la Wanadamu.

🙏

ALIYEACHA VYOTE NDIYE APEWAYE ZAIDI KATIKA UFALME WA MUNGUKuna wakati watu wanaogopa kuacha vitu au watu walio nao ili  ...
22/11/2023

ALIYEACHA VYOTE NDIYE APEWAYE ZAIDI KATIKA UFALME WA MUNGU

Kuna wakati watu wanaogopa kuacha vitu au watu walio nao ili wapate nafasi kwa ajili ya Mungu. Yawezekana watu hao ni marafiki wa karibu sana, au ndugu, mke au mume na hata nafasi za kazi (vyeo).

Hofu ya kutengana nao ndiyo inayokuwa kifungo cha utumwa wao wasiwe huru kutenda haki, na kusimama katika kusudi la Mungu.

Inawezekana kuna rafiki au ndugu ambaye amekuwa msaada sana, na alionesha upendo wakati wote wa dhiki yako, na hivyo huwezi kutengana naye japo inakupasa utengane naye ili upate kutenda haki na kulitimiza kusudi la Mungu.

Inawezekana pia ni nafasi (cheo) ambayo imekuwa ni mlango wa kupata riziki kwaajili ya maisha, na hivyo huwezi kutengana nayo japo inakupasa ili uweze kutenda haki na kulitimiza kusudi la Mungu.

Ndugu yangu, Neno la Kristo linasema;

“Hakika nawaambia, hakuna mtu aliyeacha nyumba, au mke, au ndugu, au wazazi, au wana, kwa ajili ya ufalme wa Mungu, asiyepokea zaidi mara nyingi katika zamani hizi, na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.” Luka 18:29-30

Ndugu yangu, fahamu kuwa mtu asikiaye Neno la Kristo na kulifanya, huyo ndiye mtu mwenye akili katika ufalme wa Mungu.

Neno la Kristo limeweka wazi kuwa hakuna mtu aliyeacha vyote kwaajili ya Ufalme wa Mungu kisha akapungukiwa katika maisha kwa maana ahadi katika hilo Neno ni kwamba, Mtu huyo aliyeacha vyote atapewa zaidi ya alivyokuwanavyo na kisha kupokea ahadi kuu ya Uzima wa Milele.

Ndugu yangu Uwe hodari katika kutenda yaliyo mapenzi ya Mungu, chagua lile lililo jema lenye ahadi ya Mungu.

Achana na kile ambacho kimekua kufungo chako cha kutokamilika katika Ufalme wa Mungu, ikiwa ni mtu au vitu. Kwa maana Mungu ametoa ahadi ya kuzidishwa zaidi na kisha ahadi ya Uzima wa Milele.

Usiache Mtu au Kitu chochote kikutenge na kusudi la Mungu kwa sababu ya kuogopa kupeteza. Fanya kwaajili ya Utukufu wa Mungu.

Mungu atusaidie.

ROHO MTAKATIFU NDANI YANGU“Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yak...
08/11/2023

ROHO MTAKATIFU NDANI YANGU

“Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu.

12 Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.”

2 Wakorintho 2:11-12

Address

Arusha
123

Telephone

+255758857317

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwl. Daniel Piniel posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Mwl. Daniel Piniel:

Share