07/09/2026
✍ Nyenyekea
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 1 Petro 5:6-7 SRUV
[6] Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; [7] huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Kunyenyekea chini ya mkono wa Mungu ulio hodari ina maana kwamba kumpa Mungu mambo yote yanayokusumbua ili kwamba Yeye aweze kukusaidia, ashuhulikie.
Neno linasema "mkono wa Mungu ulio hodari," ina maana kwamba tujitiishe chini ya nguvu za Mungu ambazo ni Kuu kuliko jambo lolote au kitu chochote. Yaani, ni Kuu kuliko magumu uliyonayo.
"mkimtwika yeye fadhaa zenu zote." Fikiria una mahali ambapo ukiwa na tatizo unaweza kwenda na pasipo kutumia nguvu zako ukasaidiwa; Mungu hakudai chochote ili kukusaidia.
Unapompa mambo yanayokusumbua yote, huo ndio unyenyekevu wenyewe, unamuonyesha Mungu kwamba hujitegemei bali unamtegemea Yeye. Kwa kufanya hivyo atashuhulikia mambo yako yote.
Wewe kupambana mwenyewe na mambo ya maisha ambayo yanakushinda ni ishara kwamba una kiburi, na Mungu hapendezwi na mtu mwenye kiburi. Mpe Mungu akusaidie na kukuinua kimaisha.
"nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake" Aina ya maisha unayoishi huyapendi, huna uwezo wakubadilisha lakini Mungu anaweza kuyabadilisha.
Badala ya kuhangaika na kukosa usingizi, mpe Mungu akusaidie na kukuinua pasipo wewe kuteseka. Atakuinua, atakupumzisha na utayafurahia maisha siku zote ndani ya Kristo. Hallelujah!
🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Bwana Yesu Nakupa Kila Jambo Gumu Kwenye Maisha Yangu Unisaidie. Kazi Yangu Ninayofanya Kila Siku Naiacha Mikononi Mwako, Ukanisaidie Wewe Mungu Wangu. Amen
🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Yakobo 4:10 BHN
[10] Nyenyekeeni mbele ya Bwana, naye atawainueni.
Ayubu 22:29 SRUV
[29] Hapo watakapokuangusha, utasema, Kuna kuinuka tena; Naye mnyenyekevu Mungu atamwokoa.
Luka 14:11 BHN
[11] Kwa maana yeyote anayejikweza atashushwa na anayejishusha, atakwezwa.”
✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Karibu Tujifunze Neno Kwa Njia Whatsapp na Telegram LIVE Saa Nne Kamili Usiku (4:00),
Karibu Pia Ushiriki Na Maombi Saa Kumi Na Moja Na Nusu Alfajiri (11:30).
Unaweza Kujiunga Kwenye Group Kwa Kubonyeza Link Ya Whatsapp au Telegram.
- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm