05/06/2026
✍ K**a Alivyoniambia [10]
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 Mwanzo 28:3-4 SRUV
[3] Na Mungu Mwenyezi, akubariki, akuzidishe, na kukuongeza, ili uwe mtu wa watu wengi. [4] Akupe baraka ya Abrahamu, wewe na uzao wako pamoja nawe, upate kuirithi nchi ya kusafiri kwako, Mungu aliyompa Abrahamu.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Hakuna kitu ambacho Mungu anakisema au kuahidi na asikifanye, kabla hajakisema anakuwa ameshamaliza kukiandaa ndipo anakupa taarifa. Mungu ni mwaminifu.
Kabla wana wa Israeli hawajaenda utumwani, Mungu alimwambia Abraham kwamba kizazi chake kitaenda utumwani na kizazi cha nne kitarudi kumiliki eneo ambalo BWANA alimuonyesha.
Mwanzo 13:15-16 BHN
[15] Nchi hii yote unayoiona nitakupa wewe na wazawa wako iwe yenu milele. [16] Wazawa wako nitawafanya wawe wengi wasiohesabika, k**a vile mavumbi ya nchi yasivyoweza kuhesabika!
Pamoja na kwamba Mungu alimpa Abraham ahadi kwamba nchi atawapa uzao wake, lakini pia alimwambia watakuwa wengi k**a mavumbi ya ardhini. Kitu ambacho Mungu alikifanya pia.
Kutoka 1:7 SRUV
[7] Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao.
Yakobo alishuka kwenda Misri yeye na familia yake, lakini baada ya miaka mia nne na thelathini, wamekuwa wengi k**a alivyosema Mungu kupitia Isaka, kwamba Yakobo ataongezeka na atakuwa mtu wa watu wengi.
Wewe pia, neno lolote la Mungu unaloamini, litafanyika kwako kwa Jina la Yesu. Amen
🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Baba Yangu wa Mbinguni, K**a Ulimuahidi Abraham na Ukatenda, Basi Hata Mimi Ninajua Utanitendea K**a Ulivyosema Kwenye Neno Lako Kuhusu Afya Yangu, Kazi Zangu, Uchumi Wangu na Kila Kitu. Amen
🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Kutoka 1:8-9 BHN
[8] Basi, akatokea mfalme mwingine huko Misri ambaye hakumjua Yosefu. [9] Naye akawaambia watu wake, “Tazameni jinsi Waisraeli walivyo wengi na wenye nguvu kuliko sisi.
✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Karibu Tujifunze Neno Kwa Njia Whatsapp na Telegram LIVE Saa Nne Kamili Usiku (4:00),
Karibu Pia Ushiriki Na Maombi Saa Kumi Na Moja Na Nusu Alfajiri (11:30).
Unaweza Kujiunga Kwenye Group Kwa Kubonyeza Link Ya Whatsapp au Telegram.
- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm
- Telegram:
https://t.me/+kVDJ2ssIox84ZmU0
- page:
https://www.facebook.com/aganojipyasociety
- Instagram:
https://www.instagram.com/invites/contact/?i=194gcl43r688e&utm_content=mv6ciwm
- TikTok
https://www.tiktok.com/.emmanuel_cliff?_r=1&_t=ZS-9465dMbTBnY
- X (Twitter):
https://twitter.com/AganoSociety?t=SejAk4faxnqppJI8ppfnOA&s=09
- YouTube:
https://youtube.com/?si=ecWrgqiv5_IgXMM1