Ps. Emmanuel Cliff

Ps. Emmanuel Cliff Turning People to Become God's Sons. Galatians 4:7

✍ K**a Alivyoniambia [10]━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━🪙 Mwanzo 28:3-4 SRUV[3]  Na Mungu Mwenyezi, akubariki, akuzidishe, na kukuo...
05/06/2026

✍ K**a Alivyoniambia [10]
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 Mwanzo 28:3-4 SRUV
[3] Na Mungu Mwenyezi, akubariki, akuzidishe, na kukuongeza, ili uwe mtu wa watu wengi. [4] Akupe baraka ya Abrahamu, wewe na uzao wako pamoja nawe, upate kuirithi nchi ya kusafiri kwako, Mungu aliyompa Abrahamu.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Hakuna kitu ambacho Mungu anakisema au kuahidi na asikifanye, kabla hajakisema anakuwa ameshamaliza kukiandaa ndipo anakupa taarifa. Mungu ni mwaminifu.

Kabla wana wa Israeli hawajaenda utumwani, Mungu alimwambia Abraham kwamba kizazi chake kitaenda utumwani na kizazi cha nne kitarudi kumiliki eneo ambalo BWANA alimuonyesha.

Mwanzo 13:15-16 BHN
[15] Nchi hii yote unayoiona nitakupa wewe na wazawa wako iwe yenu milele. [16] Wazawa wako nitawafanya wawe wengi wasiohesabika, k**a vile mavumbi ya nchi yasivyoweza kuhesabika!

Pamoja na kwamba Mungu alimpa Abraham ahadi kwamba nchi atawapa uzao wake, lakini pia alimwambia watakuwa wengi k**a mavumbi ya ardhini. Kitu ambacho Mungu alikifanya pia.

Kutoka 1:7 SRUV
[7] Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao.

Yakobo alishuka kwenda Misri yeye na familia yake, lakini baada ya miaka mia nne na thelathini, wamekuwa wengi k**a alivyosema Mungu kupitia Isaka, kwamba Yakobo ataongezeka na atakuwa mtu wa watu wengi.

Wewe pia, neno lolote la Mungu unaloamini, litafanyika kwako kwa Jina la Yesu. Amen

🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Baba Yangu wa Mbinguni, K**a Ulimuahidi Abraham na Ukatenda, Basi Hata Mimi Ninajua Utanitendea K**a Ulivyosema Kwenye Neno Lako Kuhusu Afya Yangu, Kazi Zangu, Uchumi Wangu na Kila Kitu. Amen

🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Kutoka 1:8-9 BHN
[8] Basi, akatokea mfalme mwingine huko Misri ambaye hakumjua Yosefu. [9] Naye akawaambia watu wake, “Tazameni jinsi Waisraeli walivyo wengi na wenye nguvu kuliko sisi.

✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Karibu Tujifunze Neno Kwa Njia Whatsapp na Telegram LIVE Saa Nne Kamili Usiku (4:00),
Karibu Pia Ushiriki Na Maombi Saa Kumi Na Moja Na Nusu Alfajiri (11:30).
Unaweza Kujiunga Kwenye Group Kwa Kubonyeza Link Ya Whatsapp au Telegram.

- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm

- Telegram:
https://t.me/+kVDJ2ssIox84ZmU0

- page:
https://www.facebook.com/aganojipyasociety

- Instagram:
https://www.instagram.com/invites/contact/?i=194gcl43r688e&utm_content=mv6ciwm

- TikTok
https://www.tiktok.com/.emmanuel_cliff?_r=1&_t=ZS-9465dMbTBnY

- X (Twitter):
https://twitter.com/AganoSociety?t=SejAk4faxnqppJI8ppfnOA&s=09

- YouTube:
https://youtube.com/?si=ecWrgqiv5_IgXMM1

✍ K**a Alivyoniambia [9]━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━🪙 Mwanzo 26:3 SRUV[3]  Kaa ugenini katika nchi hiyo, nami nitakuwa pamoja na...
04/06/2026

✍ K**a Alivyoniambia [9]
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 Mwanzo 26:3 SRUV
[3] Kaa ugenini katika nchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe, na kukubariki, maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote. Nami nitakifanya imara kiapo nilichomwapia Abrahamu baba yako.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Ulishawahi kujiuliza kwamba ni nini ufanye ili kutoka kwenye changamoto uliyonayo? Umejaribu kila njia lakini imeshindikana, sasa ni wakati wa kumuuliza Mungu kwamba ufanye nini ili uwe huru.

Isaka alijikuta kwenye changamoto ya ukame mahali alipokaa. Na k**a ilivyokuwa kwa watu wote, hata yeye alitaka kufanya kile ambacho watu wengine wanafanya; kukimbilia Misri.

Mungu akamtokea na kumwambia kwamba asiende Misri kujitafutia chakula, abaki hapo hapo kwenye eneo la ukame kwa sababu Mungu atakuwa pamoja nae na kumbariki.

Mungu aliposema kumbariki alimaanisha kumtajirisha, sawasawa na Mithali 10:22. Isaka alimtii Mungu, akabaki kwenye ukame, na kwa kuwa alitaka chakula, Isaka alipanda mbegu kwenye ukame huo.

Kwa kuwa ni Mungu amesema abaki asiondoke, basi Mungu alikuwa na jukumu la kuhakikisha kwamba anakuwa mwaminifu; Isaka alipopanda mbegu ni jambo gani lilitokea?

Mwanzo 26:12-13 BHN
[12] Mwaka huo Isaka alipanda mbegu katika nchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Mwenyezi-Mungu alimbariki, [13] naye akatajirika. Alizidi kupata mali hadi akawa tajiri sana.

Baraka ya Mungu ilisababisha mbegu kuota, kukua na kumpa mavuno mengi pasipo mvua kunyeesha. Hivi ndivyo ambavyo Mungu anafanya kazi, ukimtii, baraka zake zitakusaidia na kukupatia unachotaka.

Wewe Mungu amekwambia nini? Neno lake linakwambia ufanye nini? Fanya chochote ambacho Mungu amekwambia utaona nguvu zake zitakavyokusaidia. Hallelujah!

🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Mungu Wangu na Baba Yangu Ninakushukuru Kwa Neno Lako La Baraka, Ninaomba Unisaidie Kufahamu ni Jambo Gani Unalotaka Mimi Nifanye, Ni Hatua Gani Nichukue Ili Kwamba Uchumi Wangu Uimarike. Roho Mtakatifu, Ninaomba Unifunulie Jambo Hilo Kwa Sababu Wewe Unayajua Mafumbo ya Mungu. Amen

🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Mwanzo 30:43 BHN
[43] Basi, Yakobo akatajirika sana, akawa na makundi makubwa ya wanyama, watumishi wa k**e na wa kiume, ngamia na punda.

Mwanzo 31:1 NEN
[1] Yakobo akawasikia wana wa Labani wakisema, “Yakobo amechukua mali yote ya baba yetu, naye amepata utajiri huu wote kutokana na mali ya baba yetu.”

✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Karibu Tujifunze Neno Kwa Njia Whatsapp na Telegram LIVE Saa Nne Kamili Usiku (4:00),
Karibu Pia Ushiriki Na Maombi Saa Kumi Na Moja Na Nusu Alfajiri (11:30).
Unaweza Kujiunga Kwenye Group Kwa Kubonyeza Link Ya Whatsapp au Telegram.

- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm

- Telegram:
https://t.me/+kVDJ2ssIox84ZmU0

- page:
https://www.facebook.com/aganojipyasociety

- Instagram:
https://www.instagram.com/invites/contact/?i=194gcl43r688e&utm_content=mv6ciwm

- TikTok
https://www.tiktok.com/.emmanuel_cliff?_r=1&_t=ZS-9465dMbTBnY

- X (Twitter):
https://twitter.com/AganoSociety?t=SejAk4faxnqppJI8ppfnOA&s=09

- YouTube:
https://youtube.com/?si=ecWrgqiv5_IgXMM1

04/06/2026

Hampati Kwa Sababu Hamuombi.

✍ K**a Alivyoniambia [8]━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━🪙 Luka 1:38 SRUV[38] Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na i...
04/06/2026

✍ K**a Alivyoniambia [8]
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 Luka 1:38 SRUV
[38] Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu k**a ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Mariamu alijua nini cha kufanya pale ambapo unapewa neno na Mungu; unatakiwa kulipokea kwa imani ili liweze kufanyika maishani mwako. Sio k**a Zakaria alivyodai ishara, unatakiwa kuamini.

Usikubali kuishi kwa kuona, kuangalia mazingira, kuamini yanayonekana, unayoyasikia, unayoyahisi nk; usiishi kwa mwili, ishi kwa imani kwa sababu wewe ni mzao wa Abraham.

Baraka zote za Mungu zinapokelewa kwa imani sio kwa kuona. Huwezi kuona kitu halafu ukasema nina amani, utaaminije kitu kinachoonekana. K**a kitu kinaonekana huhitaji imani, unahitaji macho.

Imani ni kuwa na uhakika wa mambo unayoyatarajia, mambo ambayo huyaoni; ukishaona huwezi kutarajia tena kwa hivyo huhitaji kuamini kitu ambacho unakiona.

Neno linasema kwamba Bwana Yesu alifanyika maskini ili mimi na wewe tuwe matajiri, unatakiwa kuamini kwamba wewe ni tajiri. Usisubiri kuwa tajiri ndipo ukubali, kubali sasa hivi ndipo utaona.

Neno linasema kwamba Bwana Yesu alichukua madhaifu yako na kuyatwaa magonjwa yako. Amini kuwa wewe ni mzima hata k**a unaumwa. Usisubiri upone ndipo ukubali, kubali umepona ndipo utapona.

Siri ipo katika kukubaliana na kile ambacho amesema Mungu pasipo kuangalia k**a tayari kinaonekana au hakionekani. Kubaliana na Neno la Mungu, amini ndivyo lilivyo maishani mwako, kisha litakuwa.

🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Baba Mpendwa Ninakushukuru Kwa Neema Yako, Umenipa Kila Kitu Kabla Hata Sijaomba na Kabla Sijazaliwa Umeshanitendea. Nina Amini Nimepokea Uponyaji na Baraka Inayotajirisha Kwa Jina la Yesu. Amen

🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Mwanzo 28:3-4 SRUV
[3] Na Mungu Mwenyezi, akubariki, akuzidishe, na kukuongeza, ili uwe mtu wa watu wengi. [4] Akupe baraka ya Abrahamu, wewe na uzao wako pamoja nawe, upate kuirithi nchi ya kusafiri kwako, Mungu aliyompa Abrahamu.

✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Karibu Tujifunze Neno Kwa Njia Whatsapp na Telegram LIVE Saa Nne Kamili Usiku (4:00),
Karibu Pia Ushiriki Na Maombi Saa Kumi Na Moja Na Nusu Alfajiri (11:30).
Unaweza Kujiunga Kwenye Group Kwa Kubonyeza Link Ya Whatsapp au Telegram.

- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm

- Telegram:
https://t.me/+kVDJ2ssIox84ZmU0

- page:
https://www.facebook.com/aganojipyasociety

- Instagram:
https://www.instagram.com/invites/contact/?i=194gcl43r688e&utm_content=mv6ciwm

- TikTok
https://www.tiktok.com/.emmanuel_cliff?_r=1&_t=ZS-9465dMbTBnY

- X (Twitter):
https://twitter.com/AganoSociety?t=SejAk4faxnqppJI8ppfnOA&s=09

- YouTube:
https://youtube.com/?si=ecWrgqiv5_IgXMM1

✍ K**a Alivyoniambia [7]━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━🪙 Luka 1:18, 20 SRUV[18]  Zakaria akamwambia malaika, Nitajuaje neno hilo? M...
03/06/2026

✍ K**a Alivyoniambia [7]
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 Luka 1:18, 20 SRUV
[18] Zakaria akamwambia malaika, Nitajuaje neno hilo? Maana mimi ni mzee, na mke wangu ni mkongwe wa siku nyingi.
[20] Na tazama! Utakuwa bubu, usiweze kusema, mpaka siku ile yatakapotukia hayo, kwa sababu hukuyasadiki maneno yangu; nayo yatatimizwa kwa wakati wake.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Sio ajabu kuona mtu anajiuliza kwamba "Mungu atanipaje, ataniponyaje, atawezaje nk;" ni maneno yasiyo ya imani na wetu wengi wanadhani ni sahihi kujiuliza maswali hayo.

Maswali k**a hayo yanaletwa na adui, sio wewe unayewaza hivyo wala sio Mungu, ni shetani kwa sababu anajua akifanikiwa kukupa mawazo hayo atakutoa kwenye imani.

Zakaria alipopewa ahadi na Mungu kupitia Malaika, hakuamini kwamba inawezekana kwa kuangalia uzee aliokuwa anao; alitaka uhakika kuwa Mungu atampa mtoto. Uhakika gani zaidi ya neno la Mungu?

"Na tazama! Utakuwa bubu, usiweze kusema, mpaka siku ile yatakapotukia hayo, kwa sababu hukuyasadiki maneno yangu....."

Malaika amekutokea, anakwambia neno la Mungu, hutaki neno la Mungu unataka uhakika. Kilicho sababisha Zakaria kuwa bubu ni kwa sababu hakuamini, alitafuta ishara ya macho.

Alitaka Mungu afanye jambo mbele ya macho yake ndio aweze kuamini, hakuamini neno la Mungu aliloleta Malaika. Alikuwa bubu ili asizungumze maneno yasiyo ya imani.

Kwa nini kila unachoomba unakosa? Ni kwa sababu unatafuta ushahidi wa macho ili uweze kuamini kwamba ni kweli Mungu atatenda ulichomuomba. Neno linasema;

Rum 8:8 SUV
[8] Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.

Waebrania 11:6 BHN
[6] Basi, pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu....

Mwili wako unaishi kwa kuona sio kwa imani, Mungu hapendi. Mungu anaishi na kufanya mambo yote kwa imani, k**a wewe unaishi kwa kuona basi unaishi kwa kufuata mwili. Mungu hapendezwi na hilo!

Amua Kuamini, Utampendeza Mungu na Utapata Unachotaka. Amen

🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Ninakataa Kuwa na Mashaka Kuhusu Neno Alilosema Mungu Kuhusu Mimi, Maisha Yangu na Kile Ambacho Mungu Anataka Nifanye. Kwa Jina la Yesu Nimeamua Kuishi Kwa Kushika na Kutenda Neno la Mungu Tu, Nikijua Kuwa Mungu ni Mwaminifu Kulitimiza Kwangu. Amen

🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Mwanzo 26:3 SRUV
[3] Kaa ugenini katika nchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe, na kukubariki, maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote. Nami nitakifanya imara kiapo nilichomwapia Abrahamu baba yako.

Mwanzo 26:12-13 BHN
[12] Mwaka huo Isaka alipanda mbegu katika nchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Mwenyezi-Mungu alimbariki, [13] naye akatajirika. Alizidi kupata mali hadi akawa tajiri sana.

✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Karibu Tujifunze Neno Kwa Njia Whatsapp na Telegram LIVE Saa Nne Kamili Usiku (4:00),
Karibu Pia Ushiriki Na Maombi Saa Kumi Na Moja Na Nusu Alfajiri (11:30).
Unaweza Kujiunga Kwenye Group Kwa Kubonyeza Link Ya Whatsapp au Telegram.

- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm

- Telegram:
https://t.me/+kVDJ2ssIox84ZmU0

- page:
https://www.facebook.com/aganojipyasociety

- Instagram:
https://www.instagram.com/invites/contact/?i=194gcl43r688e&utm_content=mv6ciwm

- TikTok
https://www.tiktok.com/.emmanuel_cliff?_r=1&_t=ZS-9465dMbTBnY

- X (Twitter):
https://twitter.com/AganoSociety?t=SejAk4faxnqppJI8ppfnOA&s=09

- YouTube:
https://youtube.com/?si=ecWrgqiv5_IgXMM1

✍ K**a Alivyoniambia [6]━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━🪙 2 Wafalme 4:16-17 SRUV[16]  Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbat...
03/06/2026

✍ K**a Alivyoniambia [6]
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 2 Wafalme 4:16-17 SRUV
[16] Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana. Akasema, La! Bwana wangu, wewe mtu wa Mungu, usiniambie mimi mjakazi wako uongo. [17] Yule mwanamke akachukua mimba, akazaa mtoto wa kiume wakati uo huo mwakani, k**a Elisha alivyomwambia.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Wakati mwingine tunapowaambia watu neno la Mungu, au tunapotoa utabiri juu ya maisha yao wanadhani ni kitu ambacho hakiwezekani. Jambo wasilolijua ni hili, Mungu hashindwi kitu.

Kitu kimoja tu kinahitajika siku zote, "KUBALI" kile ambacho unaambiwa au kile ambacho Neno limesema. Hiyo ndio siri ya mafanikio na ndio siri ya kufanya ahadi ya Mungu kutimia kwako.

Mwanamke Mshunami alipewa ahadi ya kupata mtoto, sasa kwa sababu mume wake alikuwa mzee, huyu mwanamke akasema "Bwana wangu, wewe mtu wa Mungu, usiniambie mimi mjakazi wako uongo."

Alichokuwa anaona ni uzee wa mume wake na sio Nguvu za Mungu. Wewe unaangalia pochi yako kwamba haina hela au unamuangalia Mungu ambaye anaweza kukupatia hela? Jibu unalijua mwenyewe.

Huwezi kujifanya huoni kwamba unaumwa, kwamba huna fedha, kwamba huna amani, huna furaha, huna kazi nk; unachoweza kufanya ni kumwamini Mungu kwamba nguvu zake zitabadilisha hali uliyonayo.

Pokea chochote ambacho Mungu amekisema, amini kwamba itakuwa kwako k**a alivyosema na endelea kumtukuza kila siku mpaka utakapoona jambo lako limetokea, hali yako imebadilika nk.

🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Mungu na Baba Yangu wa Mbinguni, Hakika Hakuna Neno Gumu Kwako. Ni Wewe Ulifanya Njia Kwenye Bahari, Ukanyeesha Chakula Kutoka Mbinguni na Kwa Njia ya Kristo Ukafanya Kila Ishara, Ajabu na Miujiza Katika Watu. Ninajua Unandaa Muujiza Wangu Pia Kwa Jina La Yesu. Amen

🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Luka 1:18, 20 SRUV
[18] Zakaria akamwambia malaika, Nitajuaje neno hilo? Maana mimi ni mzee, na mke wangu ni mkongwe wa siku nyingi.
[20] Na tazama! Utakuwa bubu, usiweze kusema, mpaka siku ile yatakapotukia hayo, kwa sababu hukuyasadiki maneno yangu; nayo yatatimizwa kwa wakati wake.

✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Karibu Tujifunze Neno Kwa Njia Whatsapp na Telegram LIVE Saa Nne Kamili Usiku (4:00),
Karibu Pia Ushiriki Na Maombi Saa Kumi Na Moja Na Nusu Alfajiri (11:30).
Unaweza Kujiunga Kwenye Group Kwa Kubonyeza Link Ya Whatsapp au Telegram.

- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm

- Telegram:
https://t.me/+kVDJ2ssIox84ZmU0

- page:
https://www.facebook.com/aganojipyasociety

- Instagram:
https://www.instagram.com/invites/contact/?i=194gcl43r688e&utm_content=mv6ciwm

- TikTok
https://www.tiktok.com/.emmanuel_cliff?_r=1&_t=ZS-9465dMbTBnY

- X (Twitter):
https://twitter.com/AganoSociety?t=SejAk4faxnqppJI8ppfnOA&s=09

- YouTube:
https://youtube.com/?si=ecWrgqiv5_IgXMM1

✍ K**a Alivyoniambia [5]━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━🪙 Mwanzo 18:14 SRUV[14]  Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa ...
02/06/2026

✍ K**a Alivyoniambia [5]
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 Mwanzo 18:14 SRUV
[14] Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Mungu hajasema tumsifu kwa sababu hakuna kinachoshindikana kwake, anataka tukubali, tuamini na kuishi katika kweli hiyo kwamba mambo yote yanawezekana kwake.

Kumwimbia au kumwabudu na kumsifu pasipo kuonyesha kwa matendo kwamba Mungu anaweza mambo yote haibadilishi maisha yetu. Ili Mungu adhihirishe nguvu zake, anataka imani yetu.

K**a vile ilivyokuwa kwa Sara ambaye ni mama yetu kwa imani, aliangalia hali ya uzee wake na wa Abraham, akaona kwamba hakuna namna ambayo anaweza akapata mtoto.

Pamoja na kwamba ni Mungu amesema lakini hakukubali kwamba inawezekana katika uzee kupata mtoto. Kwa maana nyingine hakukubali kwamba Mungu anaweza kumpa mtoto uzeeni.

Ashukuriwe Mungu kwamba Ahadi ya mtoto alipewa Abraham mwenye imani, angepewa Sara basi Isaka asingezaliwa. Abraham aliamini kabisa kwamba pamoja na uzee wake atapata mtoto.

Abraham hakuyumbishwa na hali aliyokuwa anaiona ya uzee, alikubali bila shaka yoyote kwamba kwa Mungu mambo yote yanawezekana. Hakujua itakuwaje, lakini, alijua Mungu anaweza kufanya.

Nguvu za Mungu hazipungui kwa namna yoyote, ila mawazo yetu yanaweza kufanya nguvu za Mungu zisitusaidie. Pale ambapo tunawaza kwamba Mungu anaweza hili lakini hawezi lile.

K**a una amini Kwamba Mungu anaweza mambo yote, basi nguvu zake zitakupatia kila kitu ambacho unahitaji, neno lake la Ahadi litafanyika kwenye maisha yako. Usikubali mtu akutoe kwenye imani.

🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Hakuna Jambo Gumu Kwa Mungu Baba Yangu wa Mbinguni. Kila Kitu Kimeumbwa na Yeye, Kwake Kila Kitu Kinamtii, Viumbe Vyote Vipo Chini ya Mamlaka Yake na Hakuna Kilicho Juu Yake. Nina Amini Kila Alichosema Kuhusu Mimi Kitafanyika K**a Alivyosema. Amen

🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Luka 1:36-37 SRUV
[36] Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto wa kiume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa; [37] kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.

Luka 1:38 SRUV
[38] Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu k**a ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.

✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Karibu Tujifunze Neno Kwa Njia Whatsapp na Telegram LIVE Saa Nne Kamili Usiku (4:00),
Karibu Pia Ushiriki Na Maombi Saa Kumi Na Moja Na Nusu Alfajiri (11:30).
Unaweza Kujiunga Kwenye Group Kwa Kubonyeza Link Ya Whatsapp au Telegram.

- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm

- Telegram:
https://t.me/+kVDJ2ssIox84ZmU0

- page:
https://www.facebook.com/aganojipyasociety

- Instagram:
https://www.instagram.com/invites/contact/?i=194gcl43r688e&utm_content=mv6ciwm

- TikTok
https://www.tiktok.com/.emmanuel_cliff?_r=1&_t=ZS-9465dMbTBnY

- X (Twitter):
https://twitter.com/AganoSociety?t=SejAk4faxnqppJI8ppfnOA&s=09

- YouTube:
https://youtube.com/?si=ecWrgqiv5_IgXMM1

02/06/2026

Bathimayo Kipofu [2]

✍ K**a Alivyoniambia [4]━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━🪙 Mwanzo 21:1-2 SRUV[1]  BWANA akamjia Sara k**a alivyonena, na BWANA akamfa...
02/06/2026

✍ K**a Alivyoniambia [4]
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 Mwanzo 21:1-2 SRUV
[1] BWANA akamjia Sara k**a alivyonena, na BWANA akamfanyia k**a alivyosema. [2] Sara akapata mimba akamzalia Abrahamu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Abraham na Sara walipewa habari njema kwamba watapata mtoto wa kiume mwaka ambao ungefuata, lakini, Sara hakuamini bali alicheka akijua kwamba jambo hilo haliwezekani.

Wote walikuwa wazee sana na Sara aliona hilo ni kigezo tosha cha wao kutokupata watoto; hakujua kwamba Mungu hazuiliwi na jambo lolote. Sara aliangalia mazingira na hali ilivyo, hakuamini.

Lakini kutokuoamini kwa Sara hakufanya Mungu ashindwe kutenda jambo alilosema kwa Abraham, Mungu alimpa Abraham nguvu za kiume katika uzee wake, akafungua tumbo la Sara aliyekuwa tasa.

Neno la Mungu likadhihirika k**a vile ambavyo alikuwa amesema, na kwa wakati uleule ambao alikuwa amepanga Mungu. Hatimaye Sara akawa na mtoto k**a Mungu alivyosema.

Mungu hashindwi na jambo lolote, hitaji lako ni jepesi sana mikononi mwake; anahitaji imani yako na msimamo wako usioyumba pamoja na subira. Mungu yupo tayari kufanya kila kitu k**a utaamini.

Kuna neno gani gumu kwake? Mimi na wewe tunakubaliana kwamba hakuna. K**a hakuna, kwa nini tunaanza kuamini kisha tunaacha? Kwa nini hatusibiri k**a Abraham ili tupate tunachotaka?

Usitishiwe na mambo unayoyaona, aliye ndani yako ni mkuu kuliko changamoto unazoziona. Itakuwa kwako k**a neno linavyosema na k**a ulivyoomba, usiogope kuwa na subira. Hallelujah.

🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Baba Kwa Jina la Yesu Kristo, Ninaamini Kila Neno Ambalo Umeniambia Kwamba Litakuwa K**a Ulivyoniambia. Kuhusu Afya Yako, Kuhusu Uchumi Wangu na Mafanikio Yangu Yote, Naamini Itakuwa Hivyo K**a Ulivyoniambia. Amen

🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Mwanzo 18:14 SRUV
[14] Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.

2 Wafalme 4:16-17 SRUV
[16] Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana. Akasema, La! Bwana wangu, wewe mtu wa Mungu, usiniambie mimi mjakazi wako uongo. [17] Yule mwanamke akachukua mimba, akazaa mtoto wa kiume wakati uo huo mwakani, k**a Elisha alivyomwambia.

✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm

- Telegram:
https://t.me/+kVDJ2ssIox84ZmU0

- page:
https://www.facebook.com/aganojipyasociety

- Instagram:
https://www.instagram.com/invites/contact/?i=194gcl43r688e&utm_content=mv6ciwm

- TikTok
https://www.tiktok.com/.emmanuel_cliff?_r=1&_t=ZS-9465dMbTBnY

- X (Twitter):
https://twitter.com/AganoSociety?t=SejAk4faxnqppJI8ppfnOA&s=09

- YouTube:
https://youtube.com/?si=ecWrgqiv5_IgXMM1

✍ K**a Alivyoniambia [3]━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━🪙 1 Wafalme 17:16 SRUV[16]  Lile p**a la unga halikupunguka, wala ile chupa ...
01/06/2026

✍ K**a Alivyoniambia [3]
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
🪙 1 Wafalme 17:16 SRUV
[16] Lile p**a la unga halikupunguka, wala ile chupa ya mafuta haikuisha, sawasawa na neno la BWANA alilolinena kwa kinywa cha Eliya.
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Kwa nini katika kizazi cha sasa cha Wakristo hatuoni matendo makuu ya Mungu, ni kwa sababu hakuna watu ambao wanataka kumtii Mungu ili aweze kuwatendea maajabu.

Mungu anazungumza na kila mtu katika kila hali, hata k**a kuna namna unapitia hali mbaya ya maisha lakini bado Mungu anaongea na wewe jinsi ya kutoka kwenye tatizo ulilonalo. Tulia utasikia!

Mwanamke mjane na mtoto wake walikuwa katika hali ya kufa kwa njaa, huyu hakuwa mtu wa taifa la Israeli, lakini Mungu alimsikia kilio chake na kumtuma Eliya kwenda kusababisha muujiza kwake.

Ili aweze kupata chakula alichomuomba Mungu, ilibidi akubali kumwamini Mungu kwa chochote atakacho ambiwa. Eliya alimkuta huyu mwanamke akifanya maandalizi ya chakula cha mwisho.

Chakula ambacho angekula cha mwisho, Eliya alimwambia akitoe ili Mungu akitumie kusababisha muujiza wa chakula. Sasa huyu mwanamke alikuwa na machaguo mawili, amuamini Mungu au asiamini.

Kwanza ana njaa ndio maana Eliya alimkuta alikusanya kuni za kwenda kupika, halafu hana chakula kingine tena; sasa aamue kula kisha asipate kingine au kukitoa kisha Mungu amtunze.

Tunajua kwamba alipoamua kutii neno la Mungu, Mungu alikuwa mwaminifu kutenda kile ambacho alikisema kupitia Eliya. Mwanamke mjane, na mtoto wake pamoja na Eliya walikula kwa miaka mitatu.

Tuna neno la Mungu kwenye Biblia zetu, neno zuri la baraka, afya na mafanikio; tunapaswa kuchagua, tuamue kuamini ili Mungu atutendee au tuache tusiamini tuendelee kuteseka.

Jambo moja muhimu kujua ni hili, Mungu ni muaminifu siku zote na hawezi kubadilika. Ukiamua kusimama katika neno alilosema, itakuwa kwako k**a ambavyo amesema. Hallelujah!

🔑 Sala:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
Nimuamini Mungu Kuliko Mazingira Yangu, Yeye ni Mwaminifu na Atafanya Sawasawa na Neno Lake. Ninadumu Katika Ahadi Siku Zote Mpaka Nione Matendo Ya BWANA Mungu Wangu. Amen

🪙 Soma:
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
1 Wafalme 17:14 SRUV
[14] Kwa kuwa BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Lile p**a la unga halitapunguka, wala ile chupa ya mafuta haitaisha, hata siku ile BWANA atakapoleta mvua juu ya nchi.

Mwanzo 18:10, 13 SRUV
[10] Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake.
[13] BWANA akamwambia Abrahamu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee?

✍ ps_emmanuel_cliff
━━━━━━━━━━━━━━━━━━━━
- Whatsapp:
https://chat.whatsapp.com/KnrRt1D9CtIIiaCI7nlODm

- Telegram:
https://t.me/+kVDJ2ssIox84ZmU0

- page:
https://www.facebook.com/aganojipyasociety

- Instagram:
https://www.instagram.com/invites/contact/?i=194gcl43r688e&utm_content=mv6ciwm

- TikTok
https://www.tiktok.com/.emmanuel_cliff?_r=1&_t=ZS-9465dMbTBnY

- X (Twitter):
https://twitter.com/AganoSociety?t=SejAk4faxnqppJI8ppfnOA&s=09

- YouTube:
https://youtube.com/?si=ecWrgqiv5_IgXMM1

Address

Arusha
23306

Telephone

+255787131824

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ps. Emmanuel Cliff posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share