SIRI YA INJILI

SIRI YA INJILI injili kwa watu wote
Kusudio kubwa la ukurasa huu ni kufikisha injili kwa watu wote huduma hii ni kwa ajili ya watu wote

SIMAMA TENA UUONE WOKOVU WA MUNGU. “Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowaonyesha leo”. (Mwa 14:12), Ms...
05/11/2024

SIMAMA TENA UUONE WOKOVU WA MUNGU.

“Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowaonyesha leo”. (Mwa 14:12), Mstari huu mara nyingi hutumiwa kutia moyo mtu anapopitia jaribu zito.

Sura hii ina muujiza wa kufunguliwa kwa Bahari ya Shamu ili taifa liweze kuvuka salama na kisha kuendelea hadi Nchi ya Ahadi. Paulo anafundisha kwamba mambo yaliyotokea kwa taifa la Israeli katika Agano la Kale yaliandikwa kwa ajili ya kutuonya kwa sababu miisho ya dunia iko juu yetu (1Kor 10:11). Neno “mwisho” hurejelea mwisho wa kusudi la kinabii. Neno "ulimwengu" linamaanisha umri. Tunaishi kwenye mwisho wa mojawapo ya makusudi ya Mungu ya kiunabii, na, kwa kuja kwa Kristo, kusudi jipya na jipya la kinabii linaanza.

Mistari 2-3… Bwana alimwagiza Musa kupiga kambi ya taifa mbele ya Bahari ya Shamu. Kulikuwa na milima kila upande na jeshi lenye uadui nyuma yao. Mungu alikuwa amewaweka mahali ambapo hapakuwa na njia ya kuepuka katika hali ya asili. Watu wengi wa siku hizi tungesema, “Ni ya Ibilisi.” Lakini, ni Mungu ndiye aliyewaweka katika hali hii na si shetani.

“Wametatanishwa na nchi na nyika imewafunga.” Neno “kunaswa” linamaanisha “kuchanganyikiwa,” na maneno “nyamaza” yanamaanisha kuzuiwa na kuwa tayari kukata tamaa. Watu wengi hujikuta wamenasa katika ardhi na njia ya kutoka imezuiwa.

Wakati ujao unaonekana kuwa mbaya. Wengi wamenaswa na matatizo ya kifedha, wengine katika misukosuko ya ndoa, wengine katika mazoea ya uasherati, na wengine katika mabishano ya kujifunza Biblia, na kujikuta wamenaswa na masuala ya mafundisho yanayozuia mtiririko wa Roho wa Mungu.

Israeli walikuwa wamejua uwezo wa Mungu, lakini kumbukumbu ni fupi wakati shida mpya inapokuja. Ukombozi uliopita umesahaulika. Yesu hakusema kamwe kwamba njia ya imani itakuwa rahisi.

Imani yetu itakuja kujaribiwa tena na tena. Tunaonekana kutatizika inapokuja katika kujifunza kwamba Mungu ana uwezo wa kukabiliana na kila jaribu jipya. Katika Bahari ya Shamu ilionekana kwamba Mungu alikuwa amewaacha.

Kuonekana mara nyingi ni udanganyifu. Kile kinachoonekana k**a kifo kwetu kinaonekana k**a ushindi kwa Mungu.

Mistari 13-14… Bwana kupitia Musa anatoa unabii wa maneno hamsini. Hamsini ni idadi ya Pentekoste.

Neno la kwanza lilikuwa, "Usiogope." Imani haiwezi kupanda katika moyo wenye hasira au katika moyo wa wasiwasi. Taifa lilikuwa katika hofu kubwa ya kutojulikana au ya majeshi yanayowafuatia. Bwana anaweza kufanya miujiza mikubwa wakati moyo ukiwa umetulia. Abrahamu alihitaji “usiogope” ya Mungu (Mwa 15:1), Yoshua alihitaji “usiogope” ya Mungu (Yoshua 8:1), Gideoni alihitaji “usiogope” ya Mungu ( Waamuzi 6:23 ), Danieli alihitaji “usiogope” ya Mungu ( Waamuzi 6:23 ) Danieli 10:12), mitume walihitaji “msiogope” Yesu (Luka 12:32), na tunahitaji “msiogope” Yake pia.

Neno, “Simama.” Bwana sasa alikuwa anashughulika na roho isiyotulia ndani ya Waisraeli. Kutokuwa na utulivu husababisha kutojali, shida. Tunafanya mambo yetu wenyewe tunapokosa utulivu. Imani lazima ijifunze kuwa na subira. Wakati ujao wetu unapokuwa hatarini mara nyingi tunakuwa na haraka. Simama tu.

Epuka kufanya mambo ya kipumbavu. Mwache Mungu akufanyie kazi kesho yako. Maneno “simama tu” yanamaanisha “kujiweka, na kuwa tayari kusonga mbele.” Wazo ni, jitayarishe kuvuta vigingi vya hema na uwe tayari kusonga.

Mara nyingi Mungu anataka tusonge mbele lakini hatutaki kusonga mbele. Kuvuta vigingi vya hema kunahitaji imani na matendo.

Amen.

©Gideon Lulabuka

25/10/2024
UBATIZOUbatizo ni tendo la agano, linalowakilishwa kwa ISHARA ya kuzamisha mwili majini au kunyunyiza maji kichwani.Utar...
21/10/2024

UBATIZO

Ubatizo ni tendo la agano, linalowakilishwa kwa ISHARA ya kuzamisha mwili majini au kunyunyiza maji kichwani.Utaratibu huu wa kubatiza ulitumika toka karne ya kwanza.Ingawa Waisraeli waliutumia kabla ya hapo kwa wamataifa waliojiunga kuwa raia wao. Kwa mujibu wa desturi wakati wa karne ya kwanza baba wa familia alipojiunga na Ukristo familia nzima ilipaswa kubatizwa wakiwemo watoto wao.Ukwepli kiroho ubatizo halisi ni ule aubatizao Yesu mwenyewe kwa Roho Mtakatifu.(Mt. 3:11. na Mdo.1:4-5).Batizo zote ni ishara tu.Isivyo bahati madhehebu yetu yanabishania ishara toka enzi za karne ya kwanza ubishi uliosababisha mfumuko wa madhehebu.

Ushauri

Mzazi,mpe mtoto wako kila kilicho chema.Ingiza mtoto wako kwenye agano la uzima.Wapagani wanawaingiza watoto wao kwenye agano la mizimu.

I found a great domain name for sale on Dan.com. Check it out!

16/10/2024

UJUMBE WA LEO

Basi roho ikaniinua, ikanichukua mahali pengine; nami nikaenda kwa uchungu, na hasira kali rohoni mwangu, na mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu kwa nguvu.
Ezekieli 3:14

Uchungu unarudisha nyuma kufikiri kwako

Uchungu unarudisha nyuma kuamua kwako

Uchungu unafanya usifanye kitu.

Neema ya Mungu inapotukumbuka wakati tukiwa katika hali ya uchungu, anatushushia Roho ya kutafuta uso wake, ili katikati ya huzuni na uchungu namna hiyo, nguvu za Mungu zilizo mshukia Yesu kuomba zipate kushuka na kwako

Haijalishi upo peke yako kiasi gani,

Haijalishi wakina Petro wako wanalala

Haijalishi hueleweki kwa wengine

Haijalishi!

Nguvu za kuomba zinakuja kwako kwa sababu unapo omba una waokoa wengine katika familia na mazingira yako. Utavuka wewe na watu wengine

Walio ofisini, nyumbani na ndugu zako.

Ukiwa na uchungu usiache kuomba
Usiache kumsifu Mungu
Usiache! Kwa sababu utatoa na wengine katika uchungu huo
Nguvu za Mungu zitakuwa juu yako ili uwatoe wengine kwa maombi katikati ya uchungu
Unakua kibebeo kwa wengine

Mungu akubariki sana

©GIDEON LULABUKA

16/09/2024

Page yetu imeongezeka. Mungu awabariki sana washirika mlio ongezeka.
Wiku hii nitaanza kufundisha
Hakikisha una mkaribisha mwenzako.

31/05/2024

MWISHO WA MZUNGUKO

K**a ukitokea katika familia ya walevi, zuia huo ulevi usifike kwako. Na ulevi huo usipite kwenda kwa kizazi kinacho fuata.

K**a umetoka familia ambayo watoto wanakatiza masomo yaani hakuna anaye maliza au kwenda chuo kikuu, zuia huo mzunguko na wewe usome ufike mbali katika ngazi ya juu na uthibitishe kuwa hata katika familia yenu inawezekana akatoka mtu wa kuleta maajabu kimasomo

K**a ndugu zako katika ndoa zao haziendelei na hata wazazi wako ndoa yao ilikuwa ngumu hadi kuachana, wewe zuia huo mzunguko usiendelee, na ukioa au kuolewa ndoa yako idumu zaidi hata mmalize mwendo salama

K**a wewe ni mwanaume na baba yako alizoea kumpiga mama yako, wewe zuia huo mzunguko, uwe tofauti na baba yako na umpende mkeo k**a mwanaume mkamilifu anavyo takiwa kuonesha upendo

K**a wewe umetoka familia ya kikabila ambayo maamuzi yanafanywa kwa wazee wa mila, wewe zuia huo mzunguko na uoneshe familia yako kuwa yupo Mungu wa kweli na sio mizimu ya kabila lenu

K**a ulipo zaliwa familia yako ni masikini na mmeishi katika umasikini, zuia mzunguko huo hakikisha unapata pesa na unyanyue familia yako kuwa na ukwasi mkubwa

K**a wanafamilia wa kwenu wanajulikana kwa vitu viovu na hovyo, wewe zuia huo mzunguko wewe uwe wa tofauti na wao na ufanikiwe kuleta heshima kwa familia yako na kwa jina la familia kwa ujumla

K**a watu wa kutoka familia yako wanajulikana kuwa ni watu wa hasira, wewe zuia huo mzunguko kwa kuwa rafiki na mpole na mtu mwenye ushawishi katika maisha na familia yako

K**a familia yako imekuwa ikihusika na uchawi na mauaji na kila aina ya ulozi na kuto kupendwa, zuia mzunguko huo kwa kumtambulisha Mungu kwa njia ya Kristo katika familia yako na kisha weka agano kuwa kuanzia wewe na nyumba yako utamtumikia Mungu aliye hai!

Uhitaji kubeba na kuendeleza mapungufu ya familia yako hadi kufika kizazi kingine. Penda familia yako lakini jifunze kwa makosa yao. Hutakiwi kuwa na maono kutokana na familia uliyo zaliwa, lakini unaweza kujipanga na kuwa na maono wewe utakuwa nani na namna ya hatima ya familia yako uliyo nayo au itakayo kuja. Maamuzi yako yanaleta matokeo kwa kizazi kijacho huko mbeleni

© Gideon Lulabuka

Karibu tujifunze kila siku

Karibu kusikiliza semina ya pasaka kwa njia ya You Tube leo siku ya tatu. Karibu shirikisha na mwingine na usiache ku su...
26/03/2024

Karibu kusikiliza semina ya pasaka kwa njia ya You Tube leo siku ya tatu. Karibu shirikisha na mwingine na usiache ku subscribe katika channel hiyo

Address

Arusha
P.O.BOX12205

Telephone

+255768612970

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SIRI YA INJILI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share