16/03/2021
KWA HABARI
YA AFYA YA
Kwa namna rahisi kabisa kuelewa na ambayo inaweza kuingia ndani yako na kukupa matokeo
01
KINACHOFANYA
Mtu aitwe baba wa familia, kiongozi wa familia NI MAJUKUMU [ Ili awe Bwana wa Familia, baba wa familia - Lazima awajibike , majukumu ndiyo yanayomfanya kuwa baba ]
K**a wewe hauwezi kukaa kwenye nyumba iliyo na ufa, iliyotoboka kwenye paa, k**a hauwezi kukaa na nyumba chafu iliyo na takataka na harufu mbaya ndani , huwezi kukubali mchwa wajenge kichuguu sebuleni
BASI Bwana Yesu K**a anakaa ndani yako na uhalali wa kukaa ndani yako Ni Kwasababu unao mwili [ Basi huo mwili Ni wa muhimu kwake , na Kwasababu hiyo Ni Bwana Pia katika mwili wako ] He is the Lord over your body Also | Kwahiyo k**a Ni Bwana wa mwili wako , Basi anakazi ya Kufanya , hawezi kuacha uvimbe ukajiibukia tu kiunoni, ana wajibu wa kuutoa
K**a Mwili wako Ni hekalu la Roho Mtakatifu , Basi Hawezi kukaa na eneo lililoharibika , vidonda vya tumbo, pressure , kisukari, ROHO MTAKATIFU ANA KAZI YA KUFANYA
Biblia Inasema
8:11
[11]Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu.
Kazi yake kila siku Ni kuhakikisha , figo iko sawasawa, ini linafanya kazi vizuri , moyo unafanya kazi sawasawa [ hata k**a kulikuwa na uharibifu , anahakikisha anafanya marekebisho kila siku [ anahuisha kila kiungo Cha mwili ]
Na maadam Bwana Yesu Ni Bwana Juu ya mwili wako Pia , Basi anahakikisha kila kitu kinanyenyekea na kuanguka mbele yako [ kansa lazima ipige magoti mbele yako k**a Bwana Yesu anakaa ndani yako ] Every knee should bow
SWALI NI JE | unaamini na uko tayari Kweli hii ifanye kazi kwenye maisha yako , unakubali ufahamu huu ukuweke huru mbali na uonevu wa magonjwa - kazi kwako
UFAHAMU 02
K**a Biblia Inasema | 1 6:20[20]maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu
Ulinunuliwa [ Wewe sio Mali yako, hauishi kwa ajili yako, mwili wako sio wako ] mwili wako ulishanunuliwa
Aliyeununua, alilipa gharama ngumu , alipigwa na kuumizwa vibaya hata kufa, hiyo ndiyo gharama aliyolipa kwa ajili ya mwili wako NA BIBLIA INASEMA
1 Petro 2:24
[24]Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kwake mliponywa.
Aliyeununua mwili wako, aliyegharamikia , aligharamikia Damu yake na mwili wake [ ambaye Ni Yesu ] na kutokana na hayo aliununua kwa thamani ya damu yake [ Damu ya mwana wa Mungu ]
K**a ndivyo ilivyo Basi mwili wako ulinunuliwa ili usipate mashambulizi Tena ya kiafya kila wiki, ulinunuliwa ili usiteswe na magonjwa , ulinunuliwa ili umtukuze Mungu katika mwili huo
SASA BAADA YA KUELEWA HIVYO
Kansa inapokuja kwenye mwili wako na kukutishia kukuua , Kisukari kinapokuja kukutishia kukuua [ Kiulize swali, K**a Nilinunuliwa kwa thamani ambayo hailingani na kitu chochote hapa Duniani ili niwe na Afya " Wewe kisukari umeenda lini kwa Mungu ukawa na Dau kubwa kuliko Damu ya mwana wa Mungu na ukapewa Ruhusa Kuja kwenye mwili wangu ]
Utagundua kuwa Haiwezekani na K**a Haitawezekani kansa kuwa na Dau kubwa kiasi cha kununua mwili wako na kuuanza Kufanya uoze [ Basi Kansa haiwezi kukuua kwasababu ulinunuliwa kwa thamani ili umtukuze Mungu katika mwili huo na sio uoze ]
SWALI NI JE | Mambo haya yatakuelea na utayakubali - ili yaanze kukupa matokeo ya Baraka na ya utukufu kwenye eneo la Afya
Ninakuombea Uk**ate ufahamu huu, utumie kusema mbeze za Shetani | Utaishi maisha huru mbali na kila uonevu wa Shetani
Hii ni Kweli | na ukiifahamu
Inakuweka Huru
God bless you
Pastor Ibrahim Amasi
ABC KAHAMA
LivingWord|2021
Make a Living