13/02/2021
Jipatie BURE Nakala yako ya mwezi FEBRUARI kwa LUGHA YA KISWAHILI na nyingine nyingi ikusaidie kukua kiroho: http://distribution.rhapsodyofrealities.org/dept/?team=center1
FANYA NGUVU IWEPO KWANZA
Jumamosi, 13
```Mchungaji Chris Oyakhilome, PhD```
*…Sala ya bidii (ya moyoni, endelevu) ya mwenye haki hufanya nguvu kuu kuwapo [ijizalishayo katika utendaji wake] ```Yakobo 5:16 toleo la “AMPC”```
Wengi hawaelewi umuhimu wa sala ya moyoni, na endelevu. Wanatamka maneno kabla ya kutumia muda wa kutosha katika sala na kujiuliza ni kwa nini ukiri wao hauna matokeo. Unapaswa kujifunza namna ya kusababisha nguvu iwepo kwanza!
Pindi unapokuwa umeshafanya nguvu iwepo, na kisha kufanya ukiri wa imani, kwamba lile badiliko ulilo na shauku nalo litathibitika (litasimama). Soma habari ya Eliya katika 1 Wafalme 17-18. Aliomba ukame uje katika nchi—na mvua haikunyesha—hakukuwa hata na tone kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu.
Wakati ulipofika wa ukame kukoma, Eliya alimwomba Bwana kwa ajili ya mvua. Haikuwa tu maombi mafupi, maneno ya kawaida ya haraka-haraka katika sala; hapana! Yalikuwa ni ya msukumo mkubwa, ya moyoni, endelevu na ya bidii!
Alimtuma mtumishi wake mara sita kuona k**a kulikuwa na ishara kwa alivyokuwa anaendelea katika sala, akitarajia jibu (badiliko). Mtumishi alirudi mara ya saba na kusema, “Ninaona wingu dogo; nalo ni dogo sana k**a mkono wa mtu.” Hilo ndilo lilikuwa kila kitu Eliya alichohitaji; alitambua kuwa ameshinda!
Alimwambia mtumishi wake, *“Upesi, shika njia. Mwambie Ahabu, ‘Tandika kiti cha farasi na uteremke upesi kutoka mlimani kabla mvua haijakuzuia’”* (1 Wafalme 18:44 toleo la “MSG”). Angalia mlolongo, Eliya alifanya nguvu kuu kuwepo kwanza kupitia sala ya bidii ya moyoni, na kisha akatoa neno.
Kwa njia iyo hiyo, baada ya kuchochea dhoruba ya Roho Mtakatifu katika chumba chako cha siri, hapo ndipo unapotamka “rhema” (Neno). Hiyo ndiyo njia ya uhakika ambayo kwa ufanisi unaweza kubadilisha hali ziende sanjari na mpango wa Kiungu wa Mungu, makusudi na mapenzi Yake katika maisha yako, familia, mji, taifa na kote duniani.
*| SALA
Mpendwa Baba, ninaomba kwa ajili ya mataifa ya ulimwenguni leo, kwamba mapenzi Yako na madhumuni Yako yasimamishwe kila mahali. Mioyo ya viongozi na wale walio katika mamlaka watekeleze na kufuata lile lililo sahihi. Na ninatamka kwamba nguvu na ushawishi wa wale waliodhamiria mioyoni mwao kutenda uovu kuondolewa, na shauku zao hazitotimia wala kutekelezeka katika Jina la Yesu! Kanisa linashinda na kutawala kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
Jifunze Zaidi:
*||* Yakobo 5:16-18 AMPC; 1 Wafalme 18:41-44 *||*
SOMA MAANDIKO KILA SIKU
MPANGO WA KUSOMA BIBLIA MWAKA-1:
Matayo 28 & Walawi 4-5
MPANGO WA KUSOMA BIBLIA MIAKA-2:
Matayo 14:1-10 & Mwanzo 44
Imetolewa kutoka: Rhapsody of Realities Daily Devotional
Weka maoni kuhusu Rhapsodi ya leo kwenye www.rhapsodyofrealities.org
Improving your life each day, one article at a time