Efatha Church Sharoni - Arusha

Efatha Church Sharoni - Arusha KANISA LA EFATHA ARUSHA. Uponyaji na Ukombozi kwa damu ya YESU KRISTO. Mark7:34

MCHUNGAJI KIONGOZI JOSSY DUFFYZiara ya kanisa la Efatha Tengeru.
28/07/2026

MCHUNGAJI KIONGOZI JOSSY DUFFY

Ziara ya kanisa la Efatha Tengeru.

MCHUNGAJI KIONGOZI JOSSY DUFFYZiara ya kanisa la Efatha Arusha kituo cha Sayuni Kilala.
28/07/2026

MCHUNGAJI KIONGOZI JOSSY DUFFY

Ziara ya kanisa la Efatha Arusha kituo cha Sayuni Kilala.

IBADA YA JUMAPILI: TAREHE 26/07/2026MAMA MCHUNGAJI: MERCY KOMBASOMO: UTAMBULISHO WAKO UPO KATIKA MUNGUMambo ya walawi 9:...
26/07/2026

IBADA YA JUMAPILI: TAREHE 26/07/2026
MAMA MCHUNGAJI: MERCY KOMBA
SOMO: UTAMBULISHO WAKO UPO KATIKA MUNGU

Mambo ya walawi 9:2
Mungu ameniumba k**a yeye kwanini nifanye dhambi
Utakatifu ni tabia ya Mungu yatupasa kutembea katika IBADA YA JUMAPILI: TAREHE 26/07/2026
MCHUNGAJI: MERCY KOMBA
SOMO: UTAMBULISHO WAKO UPO KATIKA MUNGU

Asili ni nini?

Asili ni sura na mfanano na Mungu.
Mungu kwa upendo wake bado aliupenda ulimwengu akamtoa mwanae ii kila mmoja asipotee, rudi kwenye chanzo chako

ZABURI 82:6
Tusipokaa kunako nafasi na kujitambua na kuelewa utambulisho wetu hutateseka k**a wanavyoteseka wengine.

Mtu ili aweze kufika mahali pakutawala lazima uwe mfano na sura ya Mungu lazima ukubali kutawaliwa na Mungu na ukikubali inamaana uko chini ya mamlaka yake

Mungu akinitazama anaona ni ubora wa kazi yake. Mungu anataka akitutazama auone utendaji wake, akili ake na ukamilifu wake.

Ni nini kinachotufanya tusiwe k**a Mungu ni dhambi ndiyo imetufanya tukatoka kwenye nafasi yetu.
Kuna mambo tunayofanya hayamwakisi Mungu
Mungu anataka kujiona katika kile tunachoongea ajione yeye anaongea wa Mungu maana nje ya utakatifu wa Mungu hakuna kitu kinatokea.

c).Upendo
1Yohana 4:8
Asiyependa akujua asili yake k**a haupendi wengine haujamjua Mungu, uwezi kupenda k**a uwezi kutoa.

Mungu alipomaliza kuumba udongo alipulizia pumzi hai, akatupa sura yake na mfano wake akatupa utambulisho wake popote tunapoonekana tuonekane k**a yeye ni upendo tu wa Mungu kwetu.

Upendo una gharama, uwezi kupenda bila kuingia gharama. Katika kutoa ndiyo kunadhihirisha pendo, hakuna upendo ambao hauna gharama na hii tunajifunza kwa Mungu mwenyewe kumtowa mwanae kwa ajili yetu.

Kila kitu kilichoopo ulimwenguni kinahitaji kuona pendo lako

d).Huruma na rehema
Zaburi 103:8
Luka 6:33

Mungu ni wa huruma na rehema na hii ndiyo sifa yake,
Sisi kwa sisi tuhurumiane tuwahurumie wenye dhambi, lazima uwe na huruma unapoona wenye dhambi wanateseka, katika kanisa tunapaswa kukaa katika pendo ili tuhurumiane na tkae katika fadhili.

Matendo yetu mema tutakayofanya kwetu sisi kwa sisi ndiyo yatavuta wa nje na walioko nje wanatazamia kuvutwa kutoka kwetu wanapoona pendo na huruma yetu.

Tunapojaliana sisi kwa sisi itaonekana ni mahali pa kimbilio na kukaa tunapaswa kuvaa sifa za Mungu ili Mungu ajione ndani yetu.

e). Mwaminifu
2Timotheo 2:13

Mungu ni mwaminifu siku zote
Chochote unachotaka kuona kinatokea simama kwenye nafasi yako.

IBADA YA JUMAPILI: TAREHE 26/07/2026MCHUNGAJI: MERCY KOMBASOMO: UTAMBULISHO WAKO UPO KATIKA MUNGU5.MUAMINIFU2 Timotheo 2...
26/07/2026

IBADA YA JUMAPILI: TAREHE 26/07/2026
MCHUNGAJI: MERCY KOMBA
SOMO: UTAMBULISHO WAKO UPO KATIKA MUNGU

5.MUAMINIFU
2 Timotheo 2:13
Unapokosa uaminifu unakuwa unajikana mwenyewe. Mungu hudumu wa kuaminiwa sababu ni muaminifu. Nawe kawe mwaminifu kwa kila jambo ndio yako iwe ndio na hapana iwe hapana,amua kunyooka pasipo kuwa na kigeugeu. Mungu ni mwaminifu

Kumbukumbu 7:9 Akisema nimekuponya, Nimekubariki n.k. ndivyo itakavyokua ikiwa hautakengeuka.

Hizi ni baadhi ya sifa za Mungu ambazo kila mtu alieumbwa kwa sura na mfano wa Mungu anatakiwa kuwa nazo ikiwa anataka kutembea ktk Utambulisho wa Mungu.

IBADA YA JUMAPILI: TAREHE 26/07/2026MCHUNGAJI: MERCY KOMBASOMO: UTAMBULISHO WAKO UPO KATIKA MUNGUUtambulisho ni hali, si...
26/07/2026

IBADA YA JUMAPILI: TAREHE 26/07/2026
MCHUNGAJI: MERCY KOMBA
SOMO: UTAMBULISHO WAKO UPO KATIKA MUNGU

Utambulisho ni hali, sifa ya vitu vinavyomfanya mtu , kitu au Kundi litambulike au lijulikane.

Mwanzo 1:26-27

Huu ndio utambulisho wetu na asili yetu na ndiyo sababu iliyopelekea Yesu kuja kufa Msalabani, sababu huyu ni mtu alipoteza asili yake pale dhambi ilipoingia kwake kupitia Kusikia. Yesu hakuja kwa Kusudi la sisi kuondolewa magonjwa na taabu bali alikuja ili kuturudisha ktk nafasi yetu ya kwanza ambayo tulikuwa tumeumbiwa kwayo ambayo ni mfano na sura ya Mungu. Watu leo wanamtafuta Mungu ili wapate kuponywa badala ya kumpata Mungu.

Zaburi 82:6
Mwanadamu ni akili ya Mungu, Ubunifu wa Mungu anataka akikuona wewe ajione yeye kwako, mahali popote ulipo aone ukiwa k**a Mungu. Kwa kutokuwa kwenye nafasi yetu ya asili ambayo tumeumbiwa.

Fika mahali jua kuwa wewe sio mtu wa kawaida wala wa hovyo tena mshukuru Mungu kwa jinsi ya ajabu k**a Daudi alivyosema.
Zaburi 139:14
Je umeshawahi Kumshukuru Mungu kwa jinsi alivyokuumba?

Ikiwa Mungu ametuumba tutembee ktk Utambulisho wake je yeye yupoje ?

Sifa za Mungu
1. MUUMBAJI
Mwanzo 1:1...
Mungu aliumba kila kitu kinachoonekana leo kutoka mahali pasipokuwa na kitu.
-Ili uweze kuona vitu vikioneka ktk maisha yako,familia, kazi n.k anza kuumba kwa kutamka kile unataka kitokee. Unapotamka tamka kwa Imani.
Waebrania 11:3
-Usiruhusu kinywa chako kuongea hasi bali ongea vema. Baada ya kutamka chukua hatua maana hata Mungu baada ya kutamka alikuja kufanya. Hivyo fanya kazi pia.

2.MTAKATIFU
1 Petro 1:15-16
Ikiwa aliyetuumba ni Mtakatifu basi na sisi tuwe watakatifu, dhambi na uovu visionekane ndani yako.

3.UPENDO
1Yohana 4:8
Mungu ana upendo, Yeye ndiye Pendo. Ikiwa huna upendo hujamjua Mungu bado.
-Hakuna Upendo pasipo kutoa, ndiomaana kwa upendo wake kwetu alimtoa mwanae wa pekee. Huwezi kusema unampenda mtu usiekubali kujitoa kwake.
Waefeso 5:1-2

4.HURUMA
Zaburi 103:8
Tuwe na huruma na wengine, hurumia wenye dhambi k**a yeye anavyohurumia maana ni tabia yake.
Luka 6:36

Inaendelea...........

KANISA LA EFATHA SHARON ARUSHA IBADA YA KUSIFU Zaburi : 34 : 1 - Nitamhimidi Bwana kila wakati, Sifa zake zi kinywani mw...
26/07/2026

KANISA LA EFATHA SHARON ARUSHA

IBADA YA KUSIFU

Zaburi : 34 : 1 - Nitamhimidi Bwana kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima.

KANISA LA EFATHA SHARON ARUSHAIBADA YA KUABUDU Zaburi : 23 : 1 - Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
26/07/2026

KANISA LA EFATHA SHARON ARUSHA

IBADA YA KUABUDU

Zaburi : 23 : 1 - Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

KANISA LA EFATHA SHARON ARUSHATAREHE 26/07/2026IBADA YA UFUNGUZIZaburi : 12 : 6 - Maneno ya Bwana ni maneno safi, Ni fed...
26/07/2026

KANISA LA EFATHA SHARON ARUSHA

TAREHE 26/07/2026

IBADA YA UFUNGUZI

Zaburi : 12 : 6 - Maneno ya Bwana ni maneno safi, Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi; Iliyosafishwa mara saba.

26/07/2026

KARIBU KATIKA IBADA YA JUMAPILI 26.07.2026

Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.”Sisi watu tu...
19/07/2026

Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.”

Sisi watu tuliookoka tunapaswa kupita katika njia ya Yesu, njia ya Yesu imesonga sana, imejaa upendo na mapatano imejaa utakatifu kwaajili ya wasafirio. Lazima tuangalie tunavyoenenda sio kila njia tutapita.

Katika safari ya wokovu beba kweli ya Mungu, beba ule uhalisia wa Mungu na sio unafiki tembea na kweli ya Mungu, wala usiungane na wabeba uovu.

Maombi
1. Omba Mungu akuondolee vitu vyote vitakavyofanya tusiuone ufalme wa Mbinguni.

2. Msii Mungu akusaidie kuingia mbinguni wala mazingira yasikuziulie kuingia Mbinguni.

Address

Kimandolu
Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Sharoni - Arusha posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category