15/03/2026
SOMO LA LEO : UWANAFUNZI.
MHUBURI : Mr. Christopher Kombe.
Yesu alisema, Enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi. (Mathayo 28:19–20). Hii ni wito wa kila Mkristo, sio tu kwa wachungaji au viongozi wa kanisa, bali kwa kila mmoja wetu aliyeokolewa. Ukristo sio kukaa kanisani tu, bali ni kuishi maisha yanayoangaza ulimwengu kwa matendo, upendo, na ushuhuda wa kweli. Uwanafunzi ni safari ya kumfuata Kristo kwa uaminifu, kujifunza kutoka kwake, na kuwafundisha wengine kufanya vivyo hivyo. Tunapoitwa kuwa wanafunzi, tunaitwa pia kuwa walimu wa mataifa, tukiwavuta kwa nuru ya injili. Leo tunakumbushwa kwamba jukumu letu ni kueneza mwanga wa Kristo, kuonyesha mfano wa maisha ya kiroho, na kushirikisha ulimwengu tumaini lililo ndani yetu. Hii ndiyo agizo kuu ambalo halina kikomo cha muda, bali ni wajibu wa kila siku kwa kila aliyeamini.