Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania - KKKT.

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania - KKKT. Kristo tu, Neno tu, Neema tu. Umoja wetu ndiyo nguvu yetu kwakuwa Kristo yu ndani yetu daima.

02/01/2026

Jukumu la Kanisa ni kugusa Roho na mioyo ya waumini wake na wasio waumini ili kuwafanya wausikie na kuuhisi Upendo wa Yesu Kristo kwenye maisha yao ya kila siku.

Tutaanza program ya kuwachangia watu wenye mahitaji maalum hapa ili wakutane na upendo wa Yesu Kristo.

Je, nini maoni yako katika hili??
0712401880

Heri ya Mwaka mpya kwa Ndugu wote katika Kristo Yesu.
02/01/2026

Heri ya Mwaka mpya kwa Ndugu wote katika Kristo Yesu.

Askofu Msaafu Wa Dayosisi ya kaskazini Dk Erasto N kweka amefariki Dunia jijini Dar Es SalaamMungu ampumzishe mahali pem...
27/11/2023

Askofu Msaafu Wa Dayosisi ya kaskazini Dk Erasto N kweka amefariki Dunia jijini Dar Es Salaam

Mungu ampumzishe mahali pema Mtumishi Wake Askofu Erasto Kweka

*AMEN*🕯️

02/10/2023

Mungu awabariki sana

07/03/2023
11/02/2023

Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila alimpokea Askofu Dkt. Fredrick Shoo, Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, anayefanya ziara katika KKKT Dayosisi ya Kaskazini Magharibi, Bukoba.

Askofu Dkt. Shoo alianza ziara hiyo Februari 8, 2023na ameambatana na mwenyeji wake, Askofu Dkt. Abednego Keshomshahara wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Magharibi. Katika mazungumzo yao Mhe. Chalamila alimweleza Askofu Dkt. Shoo juu ya mazingira mazuri ya uwekezaji, ikiwa ni pamoja na kupata mvua za uhakika misimu miwili kwa mwaka.

Mhe. Chalamila alimweleza Askofu Dkt. Shoo kwamba pamoja na Mkoa wa Kagera kuwa na wasomi wengi na mazingira mazuri ya uwekezaji, bado hali hiyo haijatafsirika vizuri katika vitendo ili kuweza kuinua uchumi wa Mkoa. Mhe. Chalamila alieleza kwamba ofisi ya Mkuu wa Mkoa inaendelea kushirikiana na wadau wengine kuhakikisha watu wengi zaidi wanawekeza na kuongeza uzalishaji katika nyanja mbalimbali ili kuinua kipato binafsi na uchumi wa jumla katika Mkoa.

GROUP JIPYA KABISA LA NYIMBO ZA MWIMBIENI BWANA TANZANIA.Hizi ni sauti za nyimbo zilizoimbwa na Walimu wetu mbalimbali w...
05/01/2023

GROUP JIPYA KABISA LA NYIMBO ZA MWIMBIENI BWANA TANZANIA.

Hizi ni sauti za nyimbo zilizoimbwa na Walimu wetu mbalimbali wa Muziki toka Makanisa tofauti ya Kilutheri ndani ya Tanzania na nje ya Tanzania kisha kuchanganywa na ala za Kinanda.

Sote tuwe na Umoja K**a Kristo alivyo pamoja na Baba.
Karibuni sana kujiunga.

WhatsApp Group Invite

05/01/2023

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania tunakutakia HERI YA MWAKA MPYA wenye mafanikio.

Mtaa wa Kiwengwa Zanzibar umetimiza Mwaka mmoja tangu kuanzishwa. Leo ni ibada maalumu ikiwa ni pamoja na kukusanya fedh...
25/09/2022

Mtaa wa Kiwengwa Zanzibar umetimiza Mwaka mmoja tangu kuanzishwa. Leo ni ibada maalumu ikiwa ni pamoja na kukusanya fedha kwa ujenzi wa nyumba ya Bwana.

21/09/2022

Suala la Kanisa kuwasaidia Waumini wake Kiuchumi ni sehemu ya Mapinduzi kifikra.
Si jambo la heri Kanisa kuwa na account yenye Billions of money halafu waumini wanateseka Kiuchumi.
Vijana hawana ajira
Wamama wanakuwa ombaomba
Biashara za waumini zinayumba

Kanisa liwakopeshe vijana
Watengeneze miradi
Elimu itolewe wapate ajira.
Watumishi watazameni vijana
Fungueni milango ya utume

Kisha waliumega mkate pamoja
Wakagawana kila walichopata
Walikula Kwa shirika
Mwili wa Kristo ukakuwa.

Address

Arusha

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania - KKKT. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share