Mnamo mwaka 1980, kikundi kidogo cha wanachuo wapentekoste kilijitenga kutoka kwenye jumuiya ya wakati huo ya Umoja wa kikristo wa wanafunzi Tanzania (UKWATA) na kuunda ushirika mpya ulio julikana k**a Christian Fellowship (CF) na kuanza kufanya ibada katika chumba namba 06 (Ukumbi wa Bunge - Arusha Technical College) kwa kuanza na wanafunzi wachache wasiozidi 15 chini ya aliyekuwa mwenyekiti wa t
awi wakati huo, ambaye kwasasa ni Mchungaji na Askofu Lawrance Kameta. Tangu wakati huo Christian Fellowship (CF) bila kujali uchache waliokuwa nao iliendelea kukua na kuleta UAMSHO katikati ya chuo hivyo kusababisha baadhi ya wanafunzi kumpokea YESU kuwa BWANA na MWOKOZI wa maisha yao. Christian Fellowship (CF) iliendelea kukua na kuongezeka mwaka hadi mwaka chini ya viongozi mbalimbali, na yafuatayo ni majina machache tu ya baadhi ya viongozi walio ongoza kundi chini ya Christian Fellowship(CF) ambao ni Eng.Kalembo(1980), Mchungaji na Askofu Lawrance Kameta(1981), Mchungaji na Muhandisi Rodgers Namwenje(1982), Mchungaji na Muhandisi Joseph Kotini(1983), Mchungaji Raphael, Eng.Simon Mbaga(1997), Mkufunzi wa Elimu Ya Juu na Mzee wa Kanisa Nicolaus Stanslaus (1998), Mzee wa Kanisa na Muhandisi Seba Maginga(1999), Eng.Huruma Kidenya(2000), Eng.Wilfred Ntandu Mkese(2001), Eng.Hosea Nango(2002). Mnamo mwaka 2006 Uongozi wa CASFETA TAYOMI mkoa wa Arusha pamoja na Mkurugenzi wa kwanza wa CASFETA nchini; Mch. JOSEPH JUSTINE kwa kushirikiana na Christian Fellowship(CF) uongozi wa tawi pamoja na mlezi wa Christian Fellowship Mchungaji na Muhandisi Joseph M. Kotini (ambaye amekuwa Mwalimu mlezi kwa miaka 32 kuanzia 1989 - 2021, kisha Kuwa Mchungaji Mlezi wa tawi) walikubaliana kubadilisha jina la ushirika kutoka Christian Fellowship kwenda CASFETA TAYOMI ATC. Kuanzia wakati huo hata sasa tawi hili limekuwa chini ya TANZANIA YOUTH MINISTRIES (TAYOMI). IFUATAYO NI ORODHA YA BAADHI YA WALIOWAHI KUTUMIKA K**A WENYEVITI :-
01. Erick Longino - 2011/2012
03. Florian Kamala - 2012/2013
04. Christover Mahenge - 2013/2014
05. Emmanuel Nobert - 2014/2015
06. Lazaro Mollel - 2015/2016
07. Onorasco Daudi - 2016
08. Jeremiah Samson •2016/2017 •2017/2018 •2018/2019
09. Mwemezi William Kato - 2019/2020
10. Maiko Elisha Haonga - 2020/2021
11. Ramson G. Weston - 2021/2022
Pia mchango wa wateule wengine k**a Rhoda Kephas(2019), Joseph Makindi(2020), Ivan Kameka(2021), Emmanuel Macha(2022). Sifa na utukufu apewe Mfalme Yesu. BAADHI YA MIKUTANO YA INJILI TULIYOIFANYA MPAKA SASA:-
•Kilimanjaro, MOSHI (2012).
•SINGIDA (2014).
•Kilimanjaro, OldMoshi - KIKARARA (2015).
•Tanga, Handeni - KABUKU (2016).
•Manyara, Simanjiro - NABERELA (2017).
•Kimanjaro, Moshi - HIMO (2018).
•Pwani, Kibaha - MLANDIZI (2019).
•Tanga, LUSHOTO (2020).
•Kilimanjaro, Rombo - TARAKEA (2021).
•Manyara, Hanang - KATESH (2022). Casfeta Tayomi Atc, familia hii imekuwa ya muhimu sana katika kukuza na kuvilea vipawa na huduma zetu mbalimbali k**a watumishi wa Mungu lakini pia k**a wasafiri wa kwenda mbinguni. "Kwa hiyo nampigia Baba magoti, ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa" - Waefeso 3:14-15.