Efatha Church Jerusalem

Efatha Church Jerusalem Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Efatha Church Jerusalem, Pentecostal Church, mbauda, Arusha.

02/06/2026
MEZA YA BWANAMungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yak...
02/06/2026

MEZA YA BWANA

Mungu hadharau mwanzo mdogo, anza unapoanzia imani yako iwe k**a mbegu linda imani yako, ukilinda imani yako ndipo dhambi, magonjwa, shetani wachawi, njaa na hata dhiki zitakukimbia na ndipo utakapoona mema yakikujilia. Ayubu anasema utakusudia neno nao litatimia. Ukilinda imani yako isiyumbe hautasikia njaa wala kiu, maana yake mahitaji yako yatatimizwa.

Haya yote yatatokea kwako k**a utalinda imani yako. Tunapomega mkate na kunywa mvinyo, yale yaliyoshindikana yakawezekane, Biblia inasema “Imani huja kwa kusikia na kusikia huja kwa Neno la Kristo” mwana wa Mungu Neno hili litatimia kwako, hutaona kiu wala njaa maana mahitaji yako yatatimilizwa, unaenda kula na kunywa vile vitamanikavyo.

Biblia inasema Mungu ndiye uzima wako, baada ya kula na kunywa (meza ya Bwana) ule ugonjwa uliyokukandamiza utaondoka. Kwa mamlaka niliyonayo utaenda kutamka Neno leo na litakwenda kutimia, yule mgonjwa aliyekuwa kitandani kwamba ni mkubwa au mdogo anakwenda kuinuka, kwamba ulikuwa unaumwa na kansa, TB, presha, kisukari au aina yoyote ya ugonjwa leo huo ugonjwa umeondolea maana Bwana amesema amekuja ili sisi tuwe na uzima tele, leo unakwenda kuwa na uzima tele. K**a umekuja hapa ulikuwa na maswali yanayokusumbua umepata majibu yake. Mwanangu wacha ikawe hivyo kwako.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

MEZA YA BWANAYohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.  B...
02/06/2026

MEZA YA BWANA

Yohana 6:33-35 “Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima. Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.”

Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.”

Yohana 1:1-5 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.”

Tunapokubaliana na neno tunakuwa tunapata uzima wa milele, tunaporuhusu Neno ndani yetu tunaruhusu Yesu akae ndani yetu, kwa maana Yesu ndiye uzima wetu. Tukikubali Neno tumemkubali Yesu, na hapo ndipo tunalinda imani yetu, ukiilinda imani yako itakupa kuponyeka, ukiamini kile unachokiamini mtu asikiondoe wala kukiharibu ndipo uponyaji unatokea kwako, Yusufu alilinda imani yake japokuwa alitupwa gereani lakini akaishia kuwa mtu mkuu, Daudi pia alilinda imani yake na akaishia kuwa mfalme. Imani ukiilinda unakuwa salama na kwako kunakuwa kwema.

Zaburi 128:1-4 “Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake, Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema…”

Yule amchaye Bwana atabarikiwa. Kumcha Bwana ni kulinda kile unachokiamini, unapolinda unachokiamini maisha yako yanaonekana yana mpangilio na ndipo Mungu anakufurahia, kwa maana unapolinda hicho unajiponya na mambo au ulimwengu huu na ndipo Mungu anakufurahia na kuruhusu mema yakujilie na kwako kunakuwa kwema.

Zaburi 126:6 “Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”

Tunapolinda imani kuna magumu, machungu kudharauliwa na kusukumwa lakini usiangalie yale yanayoendelea bali angalia kile unachokiamini ili kikupe kile unachokitaka, hakikisha unalinda kile unachokiamini na ndipo kwako kutakuwa kwema na Mungu atakushangaza na kila mtu atakushangaa.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Mwovu hataweza kukugusa mpaka pale utakapoilinda imani yako, ni lazima ujue umeipataje imani yako, watu wengi wanalinda ...
31/05/2026

Mwovu hataweza kukugusa mpaka pale utakapoilinda imani yako, ni lazima ujue umeipataje imani yako, watu wengi wanalinda magari yao, nyumba zao, wake au watoto wao lakini hawalindi imani zao, uko sawa wewe? Linda imani yako kuliko chochote ukilindacho maana ndipo ilipo chemchemi ya uzima wako, linda yale yaliyofanya wewe uitwe mlokole na uwe na nguvu za Mungu linda hicho usiku na mchana.

Waefeso 4:27 “wala msimpe Ibilisi nafasi.”

Wala msimpe Ibilisi nafasi.” tambua kuwa ukimpa tu ibilisi nafasi amekumaliza, unawezaje kumzuia ibilisi asipate nafasi kwako? Kwa kulinda imani yako.

Warumi 8:28 “ Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.”

Watu gani wanampenda? Ni hao wenye imani, hauwezi kumpendeza Mungu k**a hauna imani na imani ni kujua kuwa ulikuwa mwenye dhambi na sasa umeokoka na Je! umeokokaje? Hicho ndicho unapaswa kukilinda. Mungu anafanya kazi na hao wanaompenda ili nini? Ili awape mema.

TANGAZO: Nakutangazia Mungu akakupe mema.

Ukishajua wewe ni nani na uko tayari kufanya kazi na YEYE; ndipo anakuwa tayari kukupa wewe mali.

1 Petro 2:9 “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;”

Lazima uelewe kuwa wewe umechaguliwa na siyo umekataliwa, la! Hata watu wakikusengenya wala usiumie bali jipongeze kwa maana wameona kuna kitu cha tofauti kwako. Mwana wa Mungu wewe umeandaliwa kumiliki yaliyo ya Bwana.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Waamini walio wengi hawaelewi wokovu wao; kwa nini wameokoka? Ni k**a vile umemuajiri mtu katika nafasi fulani na huyo m...
31/05/2026

Waamini walio wengi hawaelewi wokovu wao; kwa nini wameokoka? Ni k**a vile umemuajiri mtu katika nafasi fulani na huyo mtu haelewi wajibu wa hiyo nafasi, ingawa anafanya kazi kila siku. Hiki ndicho kinachowakuta watu wengi ambao wameokoka; ibilisi anawapiga huku na kule maana hawaelewi nafasi zao, kwa nini wameokoka.

1 Yohana 5:18 “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.”

Yohana 16:8 “Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi;”

Dhambi ni nini? Ni kutokumwamini YEYE, tendo lolote linaloitwa dhambi ni matokeo ya kutokujua chanzo cha imani. Ukiwa na imani hata dhambi yoyote itakayokutokea kwa sababu una imani ni rahisi kuiondoa hiyo dhambi pasipo mtu yeyote kuja kukwambie tubu maana unajua umekosea, lakini k**a haujui utaendelea kuitenda hiyo dhambi.

Biblia inasema “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.” Ilinde imani yako kuliko unavyoilinda afya, fedha zako au kuliko kitu kingine unachokijua kwa sababu imani yako ndiyo kila kitu. Ibilisi hana haja na nyumba yako wala fedha zako maana anazo nyingi, bali anashida na imani yako kuliko kitu kingine chochote kile, maana akifanikiwa kuitoa imani yako amekushinda wewe. Yesu alikuja na akafa msalabani kwa ajili yetu, usisahau hilo.

1 Yohana 5:18 “Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi.”

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa...
31/05/2026

Isaya 53:5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

Baba anabeba mizigo yote inayohusu watoto, maumivu yote ya watoto, huu ndiyo ubaba; anasimama kwa ajili ya familia yake. Yesu aliye baba wa milele kwetu, alichukua mizigo yetu, maumivu yetu na changamoto zetu zote na akafa nazo msalabani na huu ndiyo ubaba.

Wakolosai 2:14-15 “akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutush*taki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani; akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.”

Yesu k**a baba aliyabeba haya yote kwa ajili yetu mimi na wewe, halafu kuna mtu anasahau kile Yesu Kristo amefanya pale msalabani? Aliyoyafanya Yesu ni kwa ajili yetu.

Wakolosai 2:13 “Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;”
Tulikuwa tumekufa lakini kwa ajili yake leo hii tupo hai.

Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Pasipo Imani hauwezi kumpendeza Mungu, k**a haumpendezi YEYE inamaana kuwa unamkosea; utajuaje hivyo? Kwa maana Biblia inasema “huwapa thawabu wale wamtafutao.”

Wale wanaompendeza Mungu YEYE huwapa mahitaji yao, hii ina maana kuwa wale wasiyompendeza wanateseka na kuzunguka sana, wanaishi na njaa na katika uhitaji ingawa wamezaliwa mara ya pili (wameokoka) kwa nini wanaishi hivyo? Ni kwa sababu hawampendezi YEYE.

Biblia inasema “Kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Hivyo kwanza unapaswa kuelewa kuwa YEYE yupo hai, anakuona na kukutazama, hivyo atatazama kila unachofanya, kile unachokifanya kikimpendeza YEYE anakupa mahitaji ili kukufanya wewe uende mbele, k**a ukifanya vizuri anakupa uzuri ili aweze kukushawishi wewe uende mbele. Vile unavyofanya vizuri inamfurahisha YEYE na YEYE akifurahi anakupa wewe zaidi na zaidi na ndivyo unavyozidi kuwa na kila kitu katika maisha yako, yaani (unakuwa tajiri).

Mwanamke muombe Mungu akupe kuolewa na mwanaume mwenye akili nzuri maana mtu mwenye akili nzuri mara zote anatafuta kumpendeza Mungu. Anaweza kuwa leo hii hana kitu lakini k**a akili yake ni nzuri basi utajua kuwa huyu ana uhakika na anajua wapi anaenda. Mwanaume mwenye imani hata k**a ataanguka lakini Bwana Yesu atamuinua na atampa kusonga mbele.

Wewe mama muangalie mumeo Je! Akianguka anainuka? Ukimuona anaamka na kwenda kanisani usiangalie alichokosea lakini angalia nia aliyonayo, biblia inasema “ataanguka mara saba lakini atainuka,” mwanamke usimkatishe mumeo tamaa maana ana safari na atafika. Mimi k**a baba yao nimeamua kusimama na wababa na sitakaa kimya mpaka wafike wanakotakiwa kufika.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Nay...
31/05/2026

Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Ndiyo maana hata unaposoma biblia Waebrania wote walikuwa wanamuita Ibrahimu baba, kwa nini? Kwa sababu ubaba wa Ibrahimu hautakaa uishe japokuwa yeye amekufa lakini ubaba upo maana huo ubaba ni agano kati ya Mungu na Ibrahimu na huo ubaba utaendelea kuwepo milele. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio yako. Yesu alizaliwa katika ushindi wa namna hii akibeba majina haya, kwa nini? Kwa sababu alikuwa kwa ajili yetu.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGUIsaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kif...
31/05/2026

SOMO: KUFANYA MAPENZI YA MUNGU

Isaya 9:6
“Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.”

Kwa ajili yetu, na kwa faida yetu na kwa ajili ya maisha yetu mtoto amezaliwa, siyo kwa ajili ya Mungu, la! bali ni kwa ajili yetu, usisahau hilo. Watu wanaishi maisha haya ya wokovu k**a vile kamwe hawatakaa wafe, kwamba wataishi duniani milele, la! Lazima ufe, labda tu Yesu aje mapema, lakini k**a sivyo kufa utakufa tu, lakini lazima uelewe unakufaje, kwamba unakufa na utukufu au laana.

Biblia inasema “Tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani” tulipewa mtoto mwanaume ambaye alikuwa na majina manne:-

Mshauri wa ajabu; akikushauri, akikusaidia na kukuongoza wewe, akikunyoosha ili uende kule Mungu anataka uwe.

Mungu mwenye nguvu; hii ina maana kuwa kuna miungu mingine lakini Mungu huyu ni Mungu mwenye nguvu, kwa nini mwenye nguvu? Ili kukusababisha wewe uweze kushinda, ili aweze kushinda miungu mingine yote kwa ajili yako. Mungu anapokupa mtu kusimama kwa ajili yako kumbuka anampa huo uweza ili akukomboe kutoka kwenye miungu mingine.

Baba wa milele: hii ina maana kuwa ubaba wake hauna mwisho, Mungu anapokupa baba wa kiroho huo ubaba kamwe hautakaa uishe, kwamba amekufa au yupo hai. Ndiyo maana hata unaposoma biblia Waebrania wote walikuwa wanamuita Ibrahimu baba, kwa nini? Kwa sababu ubaba wa Ibrahimu hautakaa uishe japokuwa yeye amekufa lakini ubaba upo maana huo ubaba ni agano kati ya Mungu na Ibrahimu na huo ubaba utaendelea kuwepo milele. Mungu anapokupa baba wa kiroho unapaswa kujua kuwa huo wajibu hautakaa uishe kwa maana siku tutakapofika mbinguni ni Yeye baba wa kiroho atakayesimama kwa ajili yako.

Mfalme wa Amani: Yeye amebeba mambo yote yanayohusu amani, maana yake ni pamoja na mafanikio yako. Yesu alizaliwa katika ushindi wa namna hii akibeba majina haya, kwa nini? Kwa sababu alikuwa kwa ajili yetu.

@ MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

Address

Mbauda
Arusha

Telephone

+255768588885

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Efatha Church Jerusalem posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share