Ev.John Judas

Ev.John Judas KRISTO TU. USIOGOPE Bwana yupo nawe................''

KARIBU, Mpendwa msomaji na mtazamaji pamoja na mfuatiliaji wa page hii,endelea kufurahia mafundisho mbalimbali yanayotolewa na watumishi wa Mungu lakini pia mafundisho ya imani yetu Wakristo kwa mlengo wa KILUTHERI, Bwana akubariki.

20/01/2026
Big shout out to my newest top fans! 💎 Poa MaxDrop a comment to welcome them to our community,
16/08/2025

Big shout out to my newest top fans! 💎 Poa Max

Drop a comment to welcome them to our community,

Jumatano 17 July 2019Somo:TAMBUA ZAMU YAKOF/kuu:Habakuki2;1____________________________________     "Mimi nitasimama kat...
15/01/2025

Jumatano 17 July 2019
Somo:TAMBUA ZAMU YAKO
F/kuu:Habakuki2;1
____________________________________
"Mimi nitasimama katika zamu yangu,nitajiweka juu ya mnara nitaangalia ili nione atakaloniambia,na jinsi nitakavyo mjibu..."
_____________________________________ ✍ katika maisha ya ukristo watu wengi sana ni wakristo ambao hawa tambui zamu zao mbele ya Mungu nambele ya kanisa pamoja na nchi na ndio maana tumekuwa tukipishana na baraka za Mungu sio mara moja ni mara nyingi na half nafika hatua mkristo anakuambia Mungu hayupo kwasababu sijaona utendaji kazi wake kwangu
Swali:Je? ni mara ngapi umetambua utendaji kazi wake Mungu maishani mwako? na k**a hujawahi ona je? umeshawahi jiuliza kwanini hufanikiwi katka mambo kadhaa? ukisha lijua Hilo jiulize upo kwenye ZAMU yako.?
✍ Tukilejea kwenye maandiko ya Habbakuki2;1
tunaona habakuki alikuwa hata mbui zamu yake mbele ya Mungu na mbele ya wanawaisrael kutokana na mambo alio kuwa akiyafanya akawa anapishana na baraka za Mungu lakini katika sura ya2:1 tunaona anakiri kwa kinywa chake kuwa atasimama kwenye ZAMU yake kwasababu hapo ndipo baraka za Mungu hushuka na ndipo Mungu anaposema na watumishi wake.
✍ Kupitia mstari huu tunatambua kuwa tukiwa katika nafasi ya kumwabudu Mungu inatupasa tujiweke juu ya kinara yaani rohoni na ndipo tumsikilize Mungu anasema nini na maisha yetu na namna ambapo tutamjibu dhahiri kwa matendo kwa habari ya maisha yetu.
✍Wakristo wengi wakarne hii Mungu hasemi nasisi nikwasababu hatuja kaa kwenye ZAMU ama Nafasi ambayo Mungu anaweza kusema nasi nandio maana utashangaa mkristo naondolewa kwenye uwepo wa Mungu kirahisi nakuingia kwenye uovu.
✍MWISHO nikushauri ndugu mpendwa wa kristo jaribu kubadili mwenendo wa maisha yako na uitambue zamu yako mbele za Mungu naye atakupa haja ya Moyo wako k**a habakuki alivyo tambua. ______________________________________
Kwa Maswali,Maoni,Ushauri na Maombi na msaada wa kiroho na maisha kwa ujumla karibu kwenye page andika Ev.John Judas
Uwemba parish
MWISHO

ASANTENI SANA NYOTE MLIO LIKE NA KUFOLLOW PAGE YANGU Tupo 2500 kwasasa,Mungu awabarikini sanaI have reached 2.5K followe...
15/01/2025

ASANTENI SANA NYOTE MLIO LIKE NA KUFOLLOW PAGE YANGU
Tupo 2500 kwasasa,Mungu awabarikini sana

I have reached 2.5K followers! Thank you for your continued support. I could not have done it without each of you. 🙏🤗🎉

HILI NI PIGO KWA KANISA LA LETU ZURI LA KKKT BWANA UTUSAIDIE😭😭😭😭😭😭  Watu watano ambao ni wanakwaya wa Kanisa la Kiinjili...
22/10/2024

HILI NI PIGO KWA KANISA LA LETU ZURI LA KKKT BWANA UTUSAIDIE😭😭😭😭😭😭

Watu watano ambao ni wanakwaya wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)
wamefariki Dunia na wengine 20 kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuacha njia na kuingia kwenye daraja.

Kwa mujibu wa Mkuu wa wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni (Pichani) amesema usiku wa kuamkia leo majira ya saa tisa usiku gari aina ya Costa iliyokuwa imebeba Wanakwaya wakitokea jijini Dar es salaam kuelekea Machame ilipofika eneo la Kirinjiko wilayani Same liliacha njia na kusababisha vifo hivo.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa, uchunguzi wa awali unabainisha kuwa Dereva wa gari hilo alisinzia na kupelekea gari hilo kuacha njia na kuingia kwenye daraja.

Alisema kuwa, kwa sasa majeruhi wanatibiwa katika hospitali ya wilaya ya Same.
KKKT - Dmp Usharika Wa Kimara
KKKT
EATV

wakati wa maombi kwa watoto shule ya jumapili KKKT-DKU USHARIKA WA UWEMBA
07/10/2024

wakati wa maombi kwa watoto shule ya jumapili KKKT-DKU USHARIKA WA UWEMBA

vimepangiliwa kwa kufuata mitindi ya kiuandishi. Vitabu vyenye muundo mmoja wa kiandishi vimewekwa katika fungu moja mfa...
30/08/2024

vimepangiliwa kwa kufuata mitindi ya kiuandishi. Vitabu vyenye muundo mmoja wa kiandishi vimewekwa katika fungu moja mfano vitabu vya torati, Historia, Ushahiri na unabii. CHATI YA MPANGILIO WA BIBLIA MPANGILIO WA VITABU VYA AGANO LA KALE Mtindo wa kiuandishi Majina ya vitabu Jumla Sheria Mwanzo – kumbukumbu la torati 5 Historia Yoshua – Esta 12 Mashairi Ayubu – Wimbo uliobora 5 Kinabii / manabii Isaya - malaki 17 Jumla ya vitabu vy agano la kale 39 Mtindo kiuandishi Majina ya vitabu Jumla Injili Mathayo – Luka 4 Historia Matendo ya Mitume 1 Barua Warumi – Yuda 21 Unabii Ufunuo wa Yohana 1 Jumla ya vitabu agano jipya 27 UANDISHI WA BIBLIA LA KALE Wanadamu walianza kuandika k**a mwaka 3200k.k. Kuandikwa kwa kwanza kulifanywa katika mabamba ya towe nyororo katika mawe na katika ngozi waliziunganisha ngozi na kuandika ngozi hizo ziliitwa “Parchment” kisha ngozi hizo baada ya kuziandika walizivingisha na kuitwa magombo “Scrolls’. Katika Biblia neno kuandika lilitajwa kwanza katika Kutoka 17:14 Mungu alipomwambia Musa kuandika mambo ya ushindi wa Israeli juu ya waamaleki k**a mwaka 1440k.k BIBLIA NA MIAKA Zamani za kale watu hawakuandika tarehe na miaka k**a tufanyavyo sasa hivi walikuwa wakitaja nyakati za wafalme wa zama zao wenyewe tu. Mfano katika Isaya 6:1 katika mwaka aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi kilicho juu sana na kuinuliwa na pindo la vazi lake vikalijaza hekalu.” Luka 3:1 – 2 “Mwaka wa kumi na tano wa kutawala kwake kaisari Teberio Pontio Pilato alipoalipokuwa liwali wa Uyahudi na Herode Mfalme wa Galilaya na Filipo ndugu yake Mfalme wa Itulea na nchi ya Trakoniti Lisania Mfalme wa Abilene wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa.Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria jangwani.” Hivi ndivyo ilivyokuwa katika nchi zote na nyakati zote za zamani hawakutaja miaka k**a tunavyotaja sasa. Lakini iliandikwa hivi katika mwaka Fulani wa kutwala kwake Mfalme Sulemani. Hivyo wataalamu wa Biblia hufanya kazi ya kuchunguza na kuunganisha miaka na nyakati ya wafalme wanchi mbalimbali. Hii ni kutokana kwamba kila nchi ina hesabu yake yenyewe ya miaka. Hivyo wataalamu wa Biblia na Theologia hawakubaliani katika mambo yote kuhusu miaka, hivyo katika kutaja miaka tunatumia neno “Kama” kwa sababu hakuna anaejua mwaka kamili ila tunafanya makisio baada ya kufanya utafiti kwa kina. Kalenda tunayotumia sasa iligunduliwa na mtaalamu mmoja mtawa anaeitwa Dionysius Exiguus. Warumi walihesabu miaka tangu kujengwa kwa Rumi. Miaka kabla ya kuzaliwa kwa Kikristo huhesabiwa kwa kurudi nyuma toka kwa Yesu Kristo kurudi nyuma na inaitwa K.K / BC na baada ya kuzaliwa kwa Yesu huhesabiwa toka kwa Yesu kwenda mbele na inajulikana k**a BK/AD. TAFSIRI ZA BIBLIA ZA ZAMANI SANA Kutokana na kufifia kwa lugha ya kiebrania mpaka kufikia mwaka 200 K.K na lugha hii kusahaulika na wengi na kutotumiwa na wengi ndipo ilibidi Agano la kale litafsiriwe katika lugha za mataifa mengi k**a vile Kiaramu, Kisuria, Kigiriki, Kiarabu, Kimisri n.k. SEPTUAGINTI YA KIGIRIKI Mwaka 300 – 200 K.K. Agano la kale lilitafsiriwa k**a lugha ya Kigiriki iliitwa Septuaginti. kwa sababu inasemekana ilitafsiriwa na watu 70. Septuagintu haiwezi kufaa kutumika k**a asili ya kutafsiri Biblia tena katika lugha zingine kwa sababu tafsiri yake inajichanganya kunasehemu imetafsiriwa neno kwa neno na kupoteza mantiki{ maana} halisi na sehemu zingine hazifahaamiki vema. Ila inasaidia wataalamu wa Biblia na Theolojia kujua maana ya maneno ya kiebrania cha zamani zile. Septuaginti ilikuwa Biblia ya wakristo wa kwanza na ilisomwa siku za Bwana Yesu ilisaidia sana watu wengi kulielewa Neno la Mungu wale ambao hawakuweza kusoma kiebrania. TARGUMU ZA KIARAMU Ni Agano la kale ambalo lilitafsiriwa kwa kiaramu baada ya lugha ya kiebrania kupoteza mashiko na kufifia watu walianza kutafsiri maneno yake katika masinagogi ya wayahudi walisoma kwa kiebrania na mtumwingine alitafsiri kwa kiaramu. Baadae tafsiri hizo ndipo zilipoandikwa na kusomwa na zilipewa jina la Targumu lenye maana ya tafsiri k**a Kiaramu. KISHAMU (KISURIA) ni tafsiri za Biblia ambazo zilitafsiriwa kwa lugha ya kishamu. Wakristo walipoongezeka katika nchi ya Shamu walihitaji kuwa na Biblia katika lugha yao ya kishamu na hivyo Biblia ilitafsiriwa kwa Kishamu. VULGALE ZA KITATIRI Ni Biblia iliyokuwa imetafsiriwa kwa kilatini. Mwaka 329 alizaliwa mtu mmoja aliyeitwa Jerome alikuwa ni mtaalamu alitafsiri Biblia nzima kwa lugha ya kirumi ambay o ni kilatini tafsiri hiyo iliitwa Vulgate. Vulgate ni tafsiri nzuri na imefwatwa na watu wengi katika kutafsiri maandiko. KASORO NDOGO NDOGO ZA KIUANDISHI Kabla ya kuangalia kasoro ndogo ndogo za kiuandishi zilizopo katika Biblia tuna budi kutambua namna ya uandishi uliotumika katika kuandika Biblia zamani za kale na hata vitabu vinginevyo vya kawaida. Ni vyema kutambua kwamba mashine za kuchapia vitabu hazikuwepo wakati wa kale mpaka mwaka wa 1450 BK ndipo zilipogunduliwa kwa hiyo kwa muda wa miaka 2730.........inaendelea

Namshukuru Mungu kwa neema yake ananitunza.
19/08/2024

Namshukuru Mungu kwa neema yake ananitunza.

24/07/2024

Big shout-out to my newest top fans! Poa Max

Address

Arusha
0000

Telephone

+255768386606

Website

https://www.youtube.com/@evjohnshalom419

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ev.John Judas posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Place Of Worship

Send a message to Ev.John Judas:

Share