22/07/2024
Huduma ya Kijamii kwa Wazee Tanzania
Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu wetu kwa kutupa nafasi na kibali cha kumtumikia kwa njia nyingine tena.
Neno la Mungu linasema ufalme wa Mungu unatekwa na wenye nguvu ndio maana tumeona bado kwetu sisi hii ni fursa ya pekee katika kugusa maisha ya wazee tukiwa na nguvu ya ufalme wa Mungu.
Huduma ya Woman Of Purpose iliyo chini ya The Worhiperz Intl, Inayoongozwa na mbeba maono Pastor Grace Hango tulipata neema na kibali cha kuweza kuwagusa na kuwahudumia wazee 81 walioko kijiji cha Orkesumet simanjiro kwa kuwapa vitu k**a mchele,maharage, mafuta ya kupikia, sukari , majani ya chai na sabuni.
Wazee ni hazina kubwa Lakini kuna namna tumewasahau hasa katika ulimwengu huu wa teknolojia, tumewasahau wazee saana kwa kule kutokujali na kutaka hekima zao.
Katika huduma hii tumekumbushwa kuthamini mchango wao, tuwatambue k**a wapo katikati yetu. Tusiwapite wana kitu kikubwa cha Mungu kwa ajili yetu…Kutoka 4:29 “Musa na Haruni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa watu wa Israeli.”
Bwana alitukumbusha kuwa wazee ni hazina ya THAMANI tuitunze.
MUNGU NI PENDO ALITUPENDA HIVYO NASI TUWAPENDE WATU.
Sambamba na hapo tulipata neema kumjengea Mungu nyumba kwa kununua zaidi ya bati 30 za huduma ya Bonde la Baraka lililopo chini ya Mtumishi wa Mungu aka mch wa Zamu Danny Kiungai ambaye ndiye alikuwa mwenyeji wa tukio letu la kihuduma kwa wazee wa Orkesumet.
Mungu awabariki saana k**ati yetu nzuri chini ya Mwenyekiti Mr Godfrey Nangoma na Katibu Florah Evarist na washirika na marafiki wa huduma ya Woman Of purpose na The WZ Intl kwa kujizoea baraka kupitia tukio hili.
“Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.”
Gal 6:9 SUV
youtu.be/H0__hRDTz0E…
Huduma ya Kijamii kwa Wazee TanzaniaTuna kila sababu ya kumshukuru Mungu wetu kwa kutupa nafasi na kibali cha kumtumikia kwa njia nyingine tena. Neno la M...